Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

PICHA: SAMATTA AIONGOZA STARS KWENYE MAZOEZI KUIKABILI CHAD

$
0
0
Nahodha wa Stars Mbwana Samatta akiwa kwenye mazoezi kuelekea mchezo dhidi ya Chad
Nahodha wa Stars Mbwana Samatta akiwa kwenye mazoezi kuelekea mchezo dhidi ya Chad

Timu ya taifa ya tanzania ‘Taifa Stars’ imeendelea vyema na maandalizi ya kuwania kufuzu kwa michuano ya Afrika AFCON dhidi ya timu ya taifa ya Chad itakayochezwa March 28 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

MKchezaji wa Tanzania Adi Yusuf anayecheza Mansfield Town inayoshiriki ligi daraja la pili England akimiliki mpira wakati wa mazoezi
MKchezaji wa Tanzania Adi Yusuf anayecheza Mansfield Town inayoshiriki ligi daraja la pili England akimiliki mpira wakati wa mazoezi

Taarifa za ukamilifu wa Stars zimetolewa na afisa habari wa TFF Baraka Kizuguto ambaye pia amesema timu ya Chad inasuasua kuingia nchini huku timu hiyo ikigoma kuzungumzia safari yao licha ya TFF kuiuliza mara kadhaa.

Wachezaji wa Taifa Stars wakisubiri kuambiwa nini cha kufanya na kocha wao Mkwasa wakati wa mazoezi
Wachezaji wa Taifa Stars wakisubiri kuambiwa nini cha kufanya na kocha wao Mkwasa wakati wa mazoezi

Ili kukiimarisha vyema kikosi cha Stars, kocha wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa amemuongeza mchezaji mwingine wa kimataifa kikosini Adi Yusuf mbaye anayecheza Mansfield Town ya England anayeifanya Stars kuwa na wachezaji watatu wa kimataifa akiungana na Samatta pamoja na Thomas Ulimwengu.

Shabani Kado akionesha umahiri wake wakati wa mazoezi
Shabani Kado akionesha umahiri wake wakati wa mazoezi

Stars ipo kundi moja na Nigeria, Misri na Chad ambapo jana Nigeria ilitoka sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Misri na kuifanya Misri kuongoza kundi ikiwa na pointi saba, Nigeria ikifuata ikiwa na pointi tano huku Stars ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi zake nne na Chad ikibuzuza mkia bila ya pointi.

Picha zaidi…

Samatta akifanya yake uwanjani akiwa na timu ya taifa ya Tanzania
Samatta akifanya yake uwanjani akiwa na timu ya taifa ya Tanzania
Mbwana Samatta akichuana na mchezaji mwenzake wa Stars wakati wa mazoezi kwenye uwanja wa taifa
Mbwana Samatta akichuana na mchezaji mwenzake wa Stars wakati wa mazoezi kwenye uwanja wa taifa
Deus Kaseke (mbele) akimwacha Erasto Nyoni wakati Stars ikifanya mazoezi kwenye uwanja wa taifa
Deus Kaseke (mbele) akimwacha Erasto Nyoni wakati Stars ikifanya mazoezi kwenye uwanja wa taifa
Wachezaji, makocha na viongozi wa Stars wakifunga mazoezi
Wachezaji, makocha na viongozi wa Stars wakifunga mazoezi

Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>