Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Ukweli kuhusu kikundi cha “Pussy Riot” na kuvuruga fainali ya kombe la dunia

$
0
0

Jana fainali za kombe la dunia zilipigwa, bao la kujifunga la Mario Mandzukic, lingine la Paul Pogba, Antoine Griezman na lile la Kylian Mbappe yakwapa ubingwa wa dunia timu ya taifa ya Ufaransa.

Kwa wale ambao hatukwenda Urusi kama bwana Shaffih Dauda tulishuhudia mchezo huu pale Escape One, katika mechi ile kuna tukio lilikuea likiendelea japo wengi tuliona kama linakatwa katwa na kujiuliza ni nini hiki.

Kulikuwa na kikundi cha mashabiki ambao kwa muonekano wa kawaida unaweza ukadhania ni scout ama ni askari lakini walikuwa wakiingia uwanjani na kutolewa kwa nguvu na maafisa usalama waliokuwepo uwanjani.

Moja kati ya picha iliyosambaa sana mtandaoni ni picha inayomuonesha mlinzi wa Liverpool Dejan Lovren akionekana kumkamata kijana mmoja kama anataka kumpiga, picha ambayo kila mtu alikuwa na maoni yake.

Wengi walimuona Lovren hana utu haswa kutokana na kijana huyo kuonekana akimpa mkono Mbappe na Mbappe akakubali, lakini kwanza kijana aliyekunjwa na Lovren na aliyempa Mbappe ni waawili tofauti, kuhusu Lovren alikuwa ana hasira, tuachane na hayo ni kwa nini haswa vijana wale walikuwa wakiingia uwanjani?

PUSSY RIOT. Ni nini hiki? Hili ni kundi la vijana ambao umri wao unatajwa kuanzia miaka 20-33 ambalo liliundwa mnamo mwaka 2011 na nia yao haswa ni kupingana na sera za raisi wa Urusi Vladmir Puttin wanayemuona kama gaidi, wamekuwa wanampinga haswa kwa kutumia sanaa na makongamano mtaani.

Inadaiwa kwamba kikundi hiki tangu wakati Urusi wakitangazwa kwamba watakuwa wenyeji wa kombe la dunia, wenyewe walijipanga kutumia fainali ya kombe la dunia kupeleka ujumbe wao kwa Puttin na serikali yake, bila kujali mechi ya fainali atacheza nani.

Walichoamua kufanya ni kuingia uwanjani ili iipe attention dunia kufahamu hawa ni wakina nani na kupitia jambo hilo dunia itafahamu ujumbe wao, na jana wakafanya hivyo mara nne wakaingia uwanjani.

Baada ya tukio hilo kutokea kikundi hicho kimetuma ujumbe sasa kuonesha nini wanakitaka na nini sababu haswa ya wao kuingia uwanjani na kufanya tukio kama lile katika mechi kubwa kama ile.

Kwanza wanataka wafungwa wote wa kisias walioko gerezani waachiliwe, hasa Oleg Senstov ambaye ni mtengeneza filamu wa kutoka Ufaransa ambaye amekamatwa nchini Urusi tangu mwaka 2014 kutokana na kupinga siasa za Putin.

Lakini  pili serikali ya Urusi iache kamata kamata inayoendelea ya watu wanaojihusisha na siasa nchini humo, tatu kuacha kufunga jela watu kwa mapenzi na chuki lakini nne wanasisitiza kuwepo na ushindani wa kisiasa nchini humo.


Ronaldo alivyokibadili kibibi kizee, sasa mambo saaafi

$
0
0

Watu walikuwa wanasubiri vipimo tu na hatimaye hii leo klabu ya soka ya Juventus imekamilisha vipimo vya mwanasoka Cristiano Ronaldo tayari kuwatukimikia.

Ronaldo amepewa jezi namba 7 kama kawaida ambayo alikuwa akiitunia Curdado na mwenyewe amekubali kuiachia jezi hiyo kwa heshima ya nyota huyo wa Ureno.

Tangu Juventus na Real Madrid kukubaliana kuhusu uhamisho wa Cristiano Ronaldo mambo yamebadilika kwa kibibi kizee cha Turin(Juventus) kuanzia mitandaoni hadi thamani ya klabu.

Unaambiwa siku sita tu baada ya Juve kutangaza kumpata Ronaldo thamani ya klabu hiyo katika soko la hisa imepanda kwa asilimia zaidi ya 20 tofauti na ilipokuwa mwanzo.

Huko katika social media ambapo ndio uwanja wa nyumbani wa Ronaldo mambo yamebadilika sana kuanzia Twitter, Face Book mpaka Instagram kuna mabadiliko katika kipindi kifupi sana.

Katika mtandao wa kijamii wa Instagram klabu ya Juventus imepata followers wapya zaidi ya milioni 1.5 katika siku hizi chache, Twitter nako Juventus wana followers wapya milioni 1.7 huku facebook wakiongezeka zaidi ya laki 7.

Madrid wakasirika. Ramon Calderon ambaye ni raisi mstaafu wa Real Madrid ametoa hisia zake kuhusu Ronaldo kutimkia Juventus akisisitiza kwamba hii ni mistake kubwa ambayo amewahi ona Madrid wakifanya.

Calderon alikuwepo Madrid wakati wakimnunua toka Manchester United 2009 na anasema kwa tabu waliyopata kumshawishi Ronaldo aliamini kwa uwezo wake wangemuacha acheze Madrid hadi achoke.

Amesisitiza kwamba duniani hakuna kama Ronaldo na hata auzwe kwa £100m au £1b sii lolote kwani ubora wa Ronaldo ni zaidi ya kitu chohote kile duniani 

Picha, huko Croatia leo usipime jinsi timu ilivyopokelewa

$
0
0

Croatia wamerudi nyumbani hii leo baada ya kuushangaza ulimwengu kwa namna walivyopenya hadi fainali huku vigogo wengi wakiangula katika kombe la dunia.

Pamoja na kufungwa katika mchezo wa nusu fainali kwa bao 4-2 lakini hiyo haikuzuia wao kupokea kifalme wakato wanarejea nchini kwao hii leo na inasemekana zaidi ya 5% ya wananchi walikuwa jijini Zagreb kuwapokea. 

Kwa namna ambavyo watu walikuwa wengi, baadhi ya wananchi walilazimika kupanda juu ya mito na kuchungulia kutoka madirishani.

Huyu hapa ni Mario Mandzukic akisaini kofia la askari polisi ambaye hii leo alikuwep wakati Croatia wakiwasili nchini kwao.

Hadi jioni watu walikuwa bado wako mtaani kuishangilia timu yao huku fataki zikipigwa kama heshima kwa nyota wao.

Picha 17 namna mabingwa wa dunia walivyopokelewa nyumbani kifalme

$
0
0

Baada ya kusubiri kwa takiribani miaka 20 hatimaye hii leo kwa mara ya pili wananchi wa Ufaransa wamepata kuliona kombe la dunia likipita nchini mwao baada ya Ufaransa kushinda kombe hilo nchini Urusi, hapa nia matukio ya namna Ufaransa ilivyokuwa hii leo.

Hapa ni wakati wachezaji wanashuka kwenye ndege, tayari kupita na kombe mitaa ya Paris kwa ajili ya wananchi kuliona kombe.

Paul Pogba akishuka kwenye ndege na kuusalimia umati uliokuja kuwapokea uwanja wa ndege.

Hii ni Paris ambapo maelfu ya mashabiki walijipanga pembezoni mwa bara bara wakishangilia mashujaa wao.

Ulinzi nao asikuambie mtu, askari walizunguka basi la wachezaji huku na huku kuhakikisha hakiharibiki kitu.

Hugo Lloris ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa akishuka na kombr kwenye ndege na hapo chini akifurahia kombe pamoja na raisi Emmanuel Macron.

Blue, nyeupe na nyekundu rangi ya bendera ya Ufaransa ilitawala hii leo na fataki zilipigwa zikitoa rangi hiyo.

Mji mzima wa Paris leo kulikuwa hakuna kazi na wananchi waliungana barabarani kushuhudia zawadi kubwa zaidi katika soka Ulimwenguni ikipita nchini kwao.

Sio ya kukosa: Takwimu zote za kombe la dunia hizi hapa

$
0
0

Tunafunga kombe la dunia kama ifuatavyo.

Jumla ya Mechi= 64

Idadi ya – 169 (2.64 kwa mechi)
Wafungaji bora:⚽⚽⚽

1. H. Kane (England) – 6
2. K. Mbappé (France) – 4
3. Griezmann (France) – 4
4. C. Ronaldo (Portugal) – 4
5. R. Lukaku (Belgium) – 4
6. D. Cheryshev (Russia) – 4
7. Ivan Perišić (Croatia) – 3
8. M. Mandžukić (Croatia) – 3
9. E. Hazard (Belgium) – 3
10. D. Costa (Spain) – 3
11. E. Cavani (Uruguay) – 3
12. A. Dzyuba (Russia) – 3
13. Y. Mina (Colombia) – 3
14. P. Coutinho (Brazil) – 2
15. J. Stones (England) – 2
16. M. Salah (Egypt) – 2
17. L. Suárez (Uruguay) – 2
18. A. Granqvist (Sweden) – 2
19. L. Modric (Croatia) – 2
20. D. Neymar Jr. (Brazil) – 2
21. S. Agüero (Argentina) – 2
22. A. Musa (Nigeria) – 2
23. M. Jedinak (Australia) – 2
24. S. Heung-min (South Korea) – 2
25. W. Khazri (Tunisia) – 2
26. T. Inui (Japan) – 2

27. Goli 1 – Wachezaji 84

Magoli yaliyofungwa nje ya 18.

🇵🇹 Cristiano Ronaldo (faulo)
🇧🇷 Philippe Coutinho
🇪🇸 Nacho
🇭🇷 Luka Modrić
🇷🇺 Aleksandr Golovin (faulo)
🇷🇸 Aleksandar Kolarov (faulo)
🇨🇴 Juan Quintero (faulo)
🇨🇭 Granit Xhaka
🇰🇷 Son Heung-min
🇩🇪 Toni Kroos (faulo)
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Jesse Lingard
🇺🇾 Luis Suárez (faulo)
🇪🇬 Mohamed Salah
🇵🇹 Ricardo Quaresma
🇦🇷 Angel Di Maria
🇫🇷 Benjamin Pavard
🇷🇺 Denis Cheryshev
🏴 Kieran Trippier (faulo)
🇫🇷 Paul Pogba
🇫🇷 Kylian Mbappé

Magoli ya kujifunga- 12

Aziz Behich (dhidi ya France)
Fernandinho (dhidi ya Belgium)
Ahmed Fathy (dhidi ya Russia)
Edson Álvarez (dhidi ya Sweden)
Aziz Bouhaddouz (dhidi ya Iran)
Oghenekaro Etebo (dhidi ya Croatia)
Thiago Cionek (dhidi ya Senegal)
Denis Cheryshev (dhidi ya Uruguay)
Sergei Ignashevich (dhidi ya Spain)
Yann Sommer (dhidi ya Costa Rica)
Yassine Meriah (dhidi ya Panama)
Mario Mandžukić (dhidi ya France)

Idadi ya matuta- 29

Zilizofungwa – 22

Wafungaji wa mikwaju ya penati

☑ Griezmann (3)
☑Kane (3)
☑ Jedinak (2)
☑ Granqvist (2)
☑ Hazard
☑ Kagawa
☑ Modric
☑ Salah
☑ Sassi
☑ Ronaldo
☑ Vela
☑ Al-Faraj
☑ Ansarifard
☑ Sigurdsson
☑ Moses
☑ Dzyuba

Zilizopotea – 7

✖ Ronaldo
✖ Sigurdsson
✖ Cueva
✖ Messi
✖ Al-Muwallad
✖ Modrić
✖ Ruiz

Mipira ya adhabu iliyofungwa- 7

Wafungaji wa faulo
🇷🇺 Aleksandr Golovin
🇵🇹 Cristiano Ronaldo
🇷🇸 Aleksandar Kolarov
🇨🇴 Juan Quintero
🇩🇪 Toni Kroos
🇺🇾 Luis Suárez
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Kieran Trippier

Idadiya kadi nyekundu- 4

Idadi ya kadi za Njano- 219

Zawadi:

Mchezaji bora: Luka Modric (Croatia)

Mchezaji bora chipukizi: Kylian Mbappé (France)

Mfungaji bora: Harry Kane (England)

Mlinda lango bora: Thibaut Courtois (Belgium)

Walinda lango waliofanya uzembe uliozaa mabao(10):

🇵🇱 Wojciech Szczesny
🇩🇪 Manuel Neuer
🇦🇷 Willy Caballero
🇺🇾 Fernando Muslera
🇭🇷 Danijel Subasic
🇸🇦 Mohammed Al Owais
🇪🇸 David De Gea
🇦🇷 Franco Armani
🇯🇵 Eiji Kawashima
🇫🇷 Hugo Llloris

Wachezaji walionyakua tuzo ya mchezaji bora wa mechi mara nyini zaidi:

Griezmann (3)
Modric (3)
Hazard (3)
Kane (3)
Ronaldo (2)
Cheryshev (2)
Coutinho (2)
Mbappé (2)
Suárez (2)

Mgawanyo wa zawadi kwa njia fedha!

<Bingwa> – $38m
Mshindi wa pili – $28m
Mshindi watatu – $24m
Nafasiya nne – $22m
Timu zilizoishia robo fainali- $16m
Timu zilizoishia nafasi ya 16 bora- $12m
Timu zilizoishia makundi- $8M

Timu iliyoonesha nidhamu na utu zaidi: Spain

Orodha ya timu bora:

1. France
2. Croatia
3. Belgium
4. England
5. Russia
6. Sweden
7. Brazil
8. Uruguay
9. Colombia
10. Switzerland
11. Japan
12. Mexico
13. Denmark
14. Spain
15. Portugal
16. Argentina
17. Senegal
18. Poland
19. Tunisia
20. Panama
21. Korea Republic
22. Germany
23. Serbia
24. Costa Rica
25. Nigeria
26. Iceland
27. Peru
28. Australia
29. Iran
30. Morocco
31. Saudi Arabia
32. Egypt

MABINGWA WA HAPO AWALI:

1930 – Uruguay 🇺🇾
1934 – Italy 🇮🇹
1938 – Italy 🇮🇹
1950 – Uruguay 🇺🇾
1954 – Germany 🇩🇪
1958 – Brazil 🇧🇷
1962 – Brazil 🇧🇷
1966 – England 🏴
1970 – Brazil 🇧🇷
1974 – Germany 🇩🇪
1978 – Argentina 🇦🇷
1982 – Italy 🇮🇹
1986 – Argentina 🇦🇷
1990 – Germany 🇩🇪
1994 – Brazil 🇧🇷
1998 – France 🇫🇷
2002 – Brazil 🇧🇷
2006 – Italy 🇮🇹
2010 – Spain 🇪🇸
2014 – Germany 🇩🇪

2018 – France 🇫🇷

Mataifa yenye idadi kubwa ya Makombe.

Brazil 🇧🇷 – 5
Germany 🇩🇪 – 4
Italy 🇮🇹 – 4
Argentina 🇦🇷 – 2
France 🇫🇷 – 2
Uruguay 🇺🇾 – 2
England 🏴 – 1
Spain 🇪🇸 – 1

Wanadamu waliowahi kutwaa kombe la dunia kama mchezaji na pia kama kocha:

1958 & 1970: 🇧🇷 Mario Zagallo
1974 & 1990: 🇩🇪 Franz Beckenbauer
1998 & 2018: 🇫🇷 Didier Deschamps

Mengineyo.

Wachezaji waliojiuzulu timu zao za taifa kufikia sasa baada ya kombe la dunia.

Javier Mascherano (Argentina)
Lucas Biglia (Argentina)
Andres Iniesta (Spain)
Keisuke Honda (Japan)
Sardar Azmoun (Iran)
Sergei Ignashevich (Russia)

Timu zilizoshiriki kombe la dunia mara nyingi zaidi.

🇧🇷 Brazil – 21
🇩🇪 Germany – 19
🇮🇹 Italy – 17
🇦🇷 Argentina – 17
🇲🇽 Mexico – 16
🇫🇷 France – 15
🇪🇸 Spain – 15
🏴 England – 15
🇧🇪 Belgium – 13
🇺🇾 Uruguay – 13
🇷🇸 Serbia – 12
🇸🇪 Sweden – 12
🇨🇭 Switzerland – 11
🇷🇺 Russia – 11
🇺🇸 USA – 10
🇳🇱 Netherlands – 10
🇰🇷 South Korea – 11
🇭🇺 Hungary – 10
🇨🇿 Czech Republic – 9
🇨🇱 Chile – 9
🏴 Scotland – 9
🇵🇱 Poland – 8
🇵🇾 Paraguay – 8
🇵🇹 Portugal – 7
🇧🇬 Bulgaria – 7
🇨🇲 Cameroon – 7
🇷🇴 Romania – 7
🇦🇹 Austria – 7
🇯🇵 Japan – 6
🇳🇬 Nigeria – 6
🇨🇴 Colombia – 5
🇸🇦 Saudi Arabia – 5
🇳🇿 Australia – 5
🇭🇷 Croatia – 5
🇹🇳 Tunisia – 5
🇮🇷 Iran – 5
🇨🇷 Costa Rica – 5
🇵🇪 Peru – 5
🇲🇦 Morocco – 5
🇩🇰 Denmark – 5
🇩🇿 Algeria – 4
🇬🇭 Ghana – 3
🇮🇪 Ivory Coast – 3
🇹🇿 Tanzania – 0

Wafungaji bora wa kombe la dunia muda wote:

1. M. Klose 🇩🇪 (16)
2. Ronaldo 🇧🇷 (15)
3. G. Muller 🇩🇪 (14)
4. J. Fontaine 🇫🇷 (13)
5. Pele 🇧🇷 (12)
6. S. Kocsis (11)
7. J. Klinsman 🇩🇪 (11)
8. T. Muller 🇩🇪 (10)
9. H. Rahn 🇩🇪 (10)
10. G. Batistuta 🇦🇷 (10)
11.G. Lineker 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 (10)
12. Hakuna mtanzania yeyote

Vilabu ambavyo wachezaji wake wamefunga mabao mengi:

PSG – 12
Barcelona – 11
Tottenham – 11
Real Madrid – 10
Manchester United – 8
Atletico Madrid – 8
Manchester City – 5
Chelsea – 4
Liverpool – 4
Dortmund – 3
Inter Milan – 3
Juventus – 3
West Brom – 2

Imeandaliwa na Privaldinho (Instagram)

Manchester United wamuacha Alexis Sanchez kutokana na uhalifu

$
0
0

Tayari wachezaji wa Manchester United ambao hawakuwepo katika michuano ya kombe la dunia pale nchini Urusi wametua Marekani kwa ajili ya ziara ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi.

Juan Mata, Ander Herrera, Eric Bailly na Anthony Martial ni moja kati ya nyota ambao wameongozana na kikosi hicho kilichoweka kambi mjini Los Angeles.

Lakini katika hali ambayo imewashangaza wengi nyota wa Manchester United Alexis Sanchez hajasafiri na timu licha ya kwamba alionekana akiwa katika mazoezi ya timu hiyo mjini Manchester siku chache zilizopita.

Sanchez amenyimwa Visa ya kwenda nchini Marekani kutokana na taifa hilo kutoruhusu mtu yeyote mwenye makosa ikiwemo ukwepaji wa kodi au anayetumikia adhabu yeyote kuingia katika nchi hiyo kabla adhabu yake haijaisha.

Hii ilisababisha United wamuache nchini Uingereza na wao wakatangulia Marekani huku Sanchez akiwa anashughulikia suala hilo pamoja na mwanasheria wake ili kuona namna gani anaweza kusafiri.

Ikumbukwe Alexis Sanchez bado anatumikia adhabu ya kifungo cha nje ya miezi 16 ambayo aliipewa mwezi February na mahakama ya nchini Hispania baada ya nyota huyo kudaiwa kukwepa kodi akiwa nchini Hispania.

United wanaanza michezo yao ya kujiandaa na msimu mpya wa Epl kwa kucheza mechi ya kwanza Ijumaa dhidi ya Club America ya Mexico lakini pia watacheza na Liverpool, Ac Milan na Real Madrid wakiwa nchini humo.

Chilunda anaondoka lini kwenda Hispania?

$
0
0

Chilunda ameshaingia mkataba wa miaka miwili na Tenerife inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Hispania.

Kilichobaki ni kuondoka kwenda Hispania kuanza maisha mapya, kuhusu anaondoka lini ndio swali ambalo kila mtu angependa kujibiwa maana isijekuwa amesaini mkataba ambao ataanza kuutumikia mwaka ujao.

“Kuhusu suala la kuondoka nasubiri kibali cha kazi kitoke kule (Hispania), wameshakifatilia hakitachukua muda mrefu kitatumwa huku ili nifatilie visa kwa ajili ya kuondoka”-Shabani Chilunda.

“Nimesaini mkataba wa miaka miwili lakini wakati wowote timu ikitokea kunihitaji wataniuza.”

“Ukiifatilia Tenerife ni timu nzuri ambayo inauza wachezaji kwenda timu kubwa lakini ni timu ambayo inafanya vizuri, kwangu mimi ni level kubwa kwa sababu kutoka ligi ya Tanzania hadi  Segunda ni maendeleo makubwa na naamini ntacheza na kupata timu kubwa zaidi ya pale.”

Chilunda anaondoka Azam huku akiamini timu hiyo itafanya vizuri msimu ujao kutokana na uboreshaji uliofanywa kwenye benchi la ufundi.

“Kila mwalimu ana plan yake, mwalimu kafika kaangalia wachezaji anaowataka anaweza kufanya nao kazi, naamini wachezaji ambao kawasajili mwenyewe atawapa nafasi na watafanya vizuri”

Baada ya kufanya vizuri kwenye mashindano ya Kagame Cup 2018 Shabani Idd Chilunda ameushukuru Azam kwa kuwa naye kwa kipindi chote walichomlea kama mchezaji.

Wachezaji wa kigeni wataidhoofisha Stars

$
0
0

Kamati ya utendaji ya shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) imepitisha kanuni kuruhusu timu moja kusajili idadi ya wachezaji 10 wa kigeni kucheza ligi kuu Tanzania bara kuanzia msimu ujao.

Wachezaji hao wanaweza kutumika wote kwa pamoja katika mchezo mmoja. Kikao kikao hicho kilifanyika July 12, 2018 makao makuu ya TFF Dar.

Kocha wa Lipuli FC Selemani Matola amesema kuruhusu vilabu kusajili wachezaji 10 na wacheze kwa wakati kutaiathiri timu ya taifa.

“Unapomchukua mchezaji wa kigeni siku zote anatakiwa kuwa na kitu cha ziada na acheze, maana yake kama kuna timu zitaweza kusajili wachezaji 10 wenye vitu vya ziada na wote wakapata nafasi ya kucheza maana yake ni mchezaji mmoja wa kitanzania ndio atapata nafasi ya kucheza kwenye timu hizo”- Selemani Matola.

“Vilabu ambavyo vinaweza kuwa na wachezaji 10 wa kigeni kwa msimu ni Simba, Yanga na Azam lakini vilabu vingine vinauwezo wa kuwa na wachezaji wa kigeni watatu au wawili lakini haviwezi kusajili wachezaji wote 10.”

“Kwa upande wa Simba, Yanga na Azam inaweza kuwa faida kwao kwa sababu wanaweza kuwasaidia kwenye mashindano ya kimataifa lakini athari yake ni kuua timu ya taifa vilabu hivyo (Simba, Yanga na Azam) ndio vinatengeneza timu ya taifa.”

“Vilabu hivi vinaweza kuwahudumia wachezaji vizuri kwa ajili ya mahitaji ya kimpira tofauti na vilabu vya mikoani. Wanaweza kulipa mishahara vizuri, kambi nzuri na mambo mengine lakini kama wachezaji wazawa hawatatumika kwenye vilabu hivi huko mikoani hakuna timu inayoweza kutoa wachezaji wa kutosha wenye ubora kucheza timu ya taifa.”

Watu wanatolea mfano ligi ya Congo DR kwamba ina wachezaji wengi wa kigeni lakini timu yao ya taifa inafanya vizuri, wanasahau Congo wakiita timu ya taifa hawategemei wachezaji wa ndani wachezaji wao wengi wa timu ya taifa wanatoka nje sisi bado tunategemea wachezaji kutoka kwenye ligi yetu.”


Mfahamu Mbappe mchezaji tishio zaidi kombe la dunia 2018

$
0
0

Katika umri wako wa miaka 19 una nini? au uliwahi kumiliki nini? au una mpango wa kumiliki nini? Hapo baadae utajivunia kipi kwa wanao hapo baadae? Utaelezea kitu gani? Unadhani wewe na Mbappe yupi hadithi yake kwa wanae na wajukuu zake itawavutia zaidi? Kila mtu hapa duniani amezaliwa na bahati yake.

Kylian Mbappé alizaliwa kaskazini mwa Paris kule Bondy umbali wa kilometa 11. Mbappe Lottin alizaliwa miezi sita baada ya tu kombe la dunia kukamilika kule Ufaransa.

Hakukulia kwenye kilimo cha korosho! la hasha! wala hajui jembe ni nini, yeye alikulia kwenye akademi ya soka.

Kylian Mbappé ameisaidia “Les Bleus” kutwaa taji lao ya 2 la dunia. Ameisadia timu yake kupata ushindi wa 4-2 Croatia kule Moscow ndani Luzhniki Stadium na kuwa mabingwa wapya mbele ya mabingwa wa soka duniani Messi na Ronaldo.

Wakati dunia inamjadili kijana huyu mwenye miaka 19 tu, tuna mengi ya kufahamu kutoka kwake. Mbappé aliipatia France ushindi dhidi ya Peru, 1-0, na kumuondosha Leo Messi na Argentina yake kwa kutia kimyani mabao mawili kwenye ushindi wa mabao manne.

Baba yake alikuwa kocha na mchezaji wa klabu ya AS Bondy iliyokuwa chini ya raisi Atmane Airouche. Nyakati hizo ndo kwanza Mbappe aliachishwa maziwa. Raisi huyo anasema Mbappe alikuwa akipenda sana mpira kuliko hata kula.

Baba yake Mbappé bwana Wilfried ni mzaliwa wa Cameroon.

Mwandishi mmoja kutoka Nigeria ajulikane kama Tana Aiyejina nae alikuja na hoja kwamba Mbappe ana asili ya Nigeria na sio Cameroon pekee.

Mama yake Mbappé’s ni mzaliwa wa Algerian na anajulikana kama Fayza Lamari, ambaye iia alicheza mpira wa mkono ligi daraja la kwanza katika klabu ya Bondy miaka ya 1990 mpaka 2000. Hata hivyo mama yake aliwahi kuingia kwenye kasheshe akiwatuhumu sana wachezaji wa PSG akiwataja Neymar, Alves na Silva kumtania mwanae kwa kumtumia vinyago vya ajabu.

Mwezi februari mwaka huu Neymar na Mbappe hawakuwa kwenye mahusiano mazuri mara baada ya taarifa kudai kwamba Mbappe aligoma kwa makusudi kumpa pasi Neymar. Mama yake akadai kuwa utani wanaomfanyia mwanae sio mzuri na hauna tija kwemye nidhamu ya soka bali ni masikhara yasiyo na manufaa kwa mwanae.

Taarifa zinasema kwamba mzee Wilfred Mbappe, alikuwa mkimbizi hapo awali na aliamua kutimkia France kutafuta maisha. Ili kupata uraia wa kudumu kule France ilibidi amuoe mwanamke mzaliwa Algeria mwenye asili ya France Fayza.

Kylian alipewa jina la KiYoruba kabila la huko Nigeria akaitwa Adesanmi maanake “Nafaa kuwa mtawala” Mzee Wilfred, pia alikuwa baba mlezi wa Jirès Kembo Ekoko, mwenye asili ya Congo. Kylian pia ana mdogo wake anayejulikana kama Adeyemi Mbappe,

Adeyemi manake Yoruba ni “uvikwe taji.” Mara nyingi Mbappe anaposhangilia kwa kubana mikono makwapani huwa anafanya hivyo ikiwa ni ishara ambayo mdogo wake hupenda kufanya kila mara wanapocheza michezo ya game, mdogo wake akimfunga huwa anashangilia kwa aina hiyo.

Hapo mwanzoni palikuwepo na fununu kwamba Mbappe huenda akawa mjukuu wa Samuel Mbappe Leppe. Leppe, aliichezea Oryx Douala miaka 1950s na 1960s, akashinda makombe matano ya ligi na vikombe vingine vitatu (1963, 1968 na 1970) Alikuwa nahodha wa kwanza kubeba kombe la African Champions Clubs’ Cup mwaka 1964/65 lakini fununu hizo hazikuwahi kuthibitishwa na upande wowote.

Kaka yao Mbappé , Jirès Kembo-Ekoko anacheza huko uturuki kunako klabu ya Bursaspor, na mdogo wake Ethan, mwenye miaka 12, yupo kwenye kikosi cha U-12 cha Paris Saint-Germain (PSG).

Mashindano mechi Magoli asisti Njano N/R Nye dakika
Jumla : 105 48 33 6 1 6.713′
68 29 20 5 3.959′
17 10 3 1 1.194′
9 6 6 812′
8 3 2 1 613′
1 1 34′
1 1 30′
1 71′
Mwalimu wake wa zamani bwana Antonio Riccardi anasema Mbappé akiwa na miaka 6 tayari alikuwa kiongozi na mchezaji tegemezi wa klabu ya umri wa miaka 10.Alipofikisha umri wa 12, Mbappé alikwenda kufanya maajaribio katika kituo cha kulea vipaji cha Clairefontaine football centre.

Katika umri wa miaka 14, alipata nafasi ya kufanya mazoezi na kikosi cha wakubwa cha Monaco. Alifanya hivyo kwa kipindi kirefu kabla hata hajamaliza elimu ya juu ya sekondari. Alicheza mchezo wake wa kwanza kwa Monaco akiwa na umri wa 16 na siku 347 na kuvunja rekodi iliyowekwa hapo awali na Henry, alipokuwa na miaka 17 na siku 14 takribani miaka 20 iliyopita.

Mbappe akiwa na umri wa miaka 18 alifunga mabao 26 kwenye msimu wake wa kwanza pale Monaco. Kwa kiwango kile Real Madrid Waliingia mfukoni kutoa kitita cha £161m kabla ya PSG kumnasa.

Mbappé alipojiunga na PSG aliweka rekodi ya kuwa kijana mchanga zaidi duniani kuwahi kulipwa mshahara mkubwa. Monaco walikubaliana na PSG kuuziana mchezaji huyo kitita cha €180 million (zaidi US$210.4 million) baada ya mkopo wake kukamilika.

Ameweka rekodi kubwa katika fainali za kombe la dunia kwa kuwa kijana mdogo zaido kuwahi kufunga bao katika fainali za kombe la dunia tokea Pele kufanya hivyo mwaka 1958.

Timu ya Taifa
2014 France U17 2 (0)
2016 France U19 11 (7)
2017– France 22 (8)

Tuzo zake Binafsi

Kikosi bora cha UEFA European U-19 Championship : 2016
Chezaji chipukizi wa ligi kuu Ufransa kupitia UNFP Ligue 1 : 2016–17, 2017–18
Kikosi bora cha UNFP Ligue 1: 2016–17, 2017–18
Mchezaji bora wa mwezi kupitia UNFP: April 2017, March 2018
Kikosi bora cha UEFA Champions League : 2016–17
Kikosi bora cha tatu ch FIFPro World XI: 2017
Golden Boy: 2017
Mchezaji bora chipukizi wa kombe la dunia:2018

Yanga mkao wa kula Kenya

$
0
0

Wawakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ngazi ya vilabu Yanga kesho wanatarajia kukiwasha dhidi ya Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa kombe la shirikisho Afrika.

Meneja wa Yanga Hafidh Saleh amesema kila kitu kimekamilika na wamejipanga vyema dhidi ya wapinzani wao.

“Tumefanya mazoezi usiku (saa 1 usiku) kwa sababu mechi itakuwa saa 1:00 jioni kwenye uwanjannkubwa wa Kasarani hapa Nairobi”-Hafidh Saleh.

“Hali ya wachezaji wote iko vizuri hakuna majeruhi yoyote, kuna kibaridi kidogo lakini hakiathiri hali ya wachezaji kimchezo.”

Dismas Ten kakwamisha usajili wa Ngasa, Kaseke Caf?

$
0
0

Kumekuwa na taarifa kutoka kwa wapenzi na wanachama wa Yanga kumshutumu ofisa habari wa klabu hiyo Dismas Ten kwamba amekwamisha usajili wa wachezaji watatu kwenda Caf ambao klabu hiyo ingeweza kuwatumia kwenye kombe la shirikisho Afrika.

Dismas amemwambia Prisca Kishamba kilichotokea hadi wachezaji hao wakashindwa kusajiliwa Caf ni wachezaji hao kuchelewa kusaini mikataba pamoja na kutokidhi baadhi ya vigezo.

“Zimekuwepo taarifa za Kaseke kuja Yanganmuda mrefu kidogo kama wiki mbili au tatu zilizopita lakini taratibu zake za usajili zimechelewa kukamilika, amesaini mkataba Jumamosi iliyopita. Ni vipi utatuma taarifa za mchezaji Caf wakati taratibu zake za kusajiliwa zilikuwa hazijakamikika?

“Mbali na mkataba mchezaji anatakiwa kuwa na  documents nyingine (local licence, medical report) kuchelewa wao kusaini mkataba pengine kulichelewesha na mambo mengine kufanyika.

“Kupitia ofisi ya Katibu Mkuu, baada ya kuwepo taarifa za kusajiliwa Deus Kaseke, Mrisho Ngasa na Haritie Makambo tuliandika barua kwenda kwa Katibu Kuu wa TFF kumuomba atusaidie wachezaji hawa wapate local licence haraka ili tuwaingize kwenye mfumo wa Caf.

“Majibu yalikuja kwamba, hawa wachezaji bado hawajasajiliwa maana yake hawapo kwenye mfumo wa usajili wa ndani kwa sababu walikuwa bado hawajatimiza taratibu zinazotakiwa kwa klabu.

“Jumamosi iliyopita ndio walisaini mikataba na baada ya hapo taratibu nyingine zikaanza ili kuhakikisha wanaingia kwenye mfumo wa Caf, bahati mbaya muda ulikuwa umepita (kwa mchezo huu Yanga vs Gor Mahia).

“Mchezaji kama Makambo ni mchezaji wa kimataifa kwa namna yoyote kwenye uhamisho wake system ya usajili inaelekeza ni lazima awe na work permit, residence permit, ITC na medical report ili kukamilisha taratibu zote za kumtambulisha yeye ni mchezaji halali wa Yanga.”

Jibu la Masoud Djuma kuhusu Yondani kusajiliwa Simba

$
0
0

Kuna tetesi zinazomhusisha beki wa kutumainiwa Yanga Kelvin Yondani muda wowote atajiunga na klabu ya Simba kwa ajili ya kuitumikia kwenye ligi kuu na mashindano mengine ikiwemo ya kimataifa.

Yondani hajasafiri na Yanga na inaelezwa kila kitu kinakwenda sawa na dili limefikia hatua za mwisho kabisa.

Kocha msaidizi wa Simba Masoud Djuma amesema karibia asilimia 80 ya wachezaji waliowataka wamewapata, hawezi kusema wamekamilisha usajili kwa sababu kuna baadhi ya wachezaji walikuwa wanawataka lakini hawajawapata.

Kuhusu usajili wa Kelvin Yondani Masoud amesema: “Hapo sina jib” lakini inaashiria kuna vitu vichache bado havijamaliziwa ili Yondani amwage wino Msimbazi.

Leo saa 1:00 usiku Yanga itakuwa kibaruani kupigania pointi tatu dhidi ya Gor Mahia katika mchezo wa kombe la shirikisho Afrika meneja w timu Hafidh Saleh amesema kikosi kipo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

“Tupo tayari kwa ajili ya mchezo, mechi itachezwa saa 1:00 usiku. Tumejipanga vizuri mwalimu amemaliza mazoezi jana kwenye uwanja wa Kasarani (mechi itachezwa hapo) wachezaji wote wapo sawa tupo tayari kwa mchezo.”

Meneja amekataa kuzungumzia wachezaji ambao hawajasafiri na timu akiwepo Kelvin Yondani.

“Kuna wachezaji wengine wapo Dar es Salaam, waliopo hapa wameahidi watapigana kufa nakupona kupata ushindi kwenye mchezo wa leo.”

“Sitaki kusema lolote kuhusu hilo, ninachoweza kusema ni kuhusu waliokuja huku (Kenya). Waliobaki Dar es Salaam kuna wengine wana majeruhi, wengine wana matatizo ya kifamilia na wengine wana matatizo hilo sitaki kuliweka wazi.”

“Yanayosemekana” yote kuhusu usajili wa Arsenal, Chelsea na United yako hapa

$
0
0

Kona ya Inasemekana iko hapa kukuletea tetesi zoote na yanayosemwa na magazeti pamoja na vyanzo mbali mbali vya usajili kutoka barani Ulaya.

Inasemekana Petr Cech anakaribia kurudi katika klabu ya Chelsea, Chelsea wanataka kufanya mpango huo kama Thibaut Courtois atakwenda Madrid lakini Chelsea hao hao inasemekana wanataka kujaribu kuzuia uhamisho wa mlinda lango Allison inayesemekana anakwenda Liverpool.

Pale Anfiled inasemekana kwamba klabu ya Liverpool imekubali kutoa kiasi cha £66m kwa ajili ya kumnunua mlinda lango wa As Roma Allison ambaye wamekuwa wakimuwinda kwa misimu takribani miwili sasa.

Lakini Ujerumani nako inasemekana klabu ya Borussia Dortmund imekata tamaa kumnunua Mitchy Batshuayi kutoka Chelsea na sasa klabu hiyo imejipanga kutuma ofa Juventus kwa ajili ya kumnunua Mario Mandzukic.

Inasemekana hii ni habari ambayo mashabiki wa Chelsea hawataki kuisikia kwani inasemekana Real Madrid bado imewaganda Eden Hazard na Thibaut Courtois na habari za magazeti ya Hispania hii leo zinadai Madrid wako tayari kuwapa Chelsea kiasi cha £150m kuwanasa nyota hao.

Klabu za Manchester United na Paris St German zimejikuta katika vita ya kumnasa mlinzi wa klabu ya Tottenham Hotspur Toby Alderweireld ambaye alikuwa na kiwango kizuri na timu ya taifa ya Ubelgiji.

Inasemekana Real Madrid wameanza chokochoko kwa Manchester United kuhusu Romelu Lukaku, na wanataka kama United wakimtaka Bale baasi Lukaku awe sehemu ya dili hilo.

Na mwisho kwa leo inasemekana bado Manchester United hawajaachana na Ivan Perisic, klabu hiyo inaendela na mchakato wa kumnasa nyota huyo wa Croatia na sasa wanamhitaji yeye pamoja na nyota mwingine wa Croatia Ante Rebic.

Inasemekana klabu ya PSG ina mpango wa kumuongezea mkataba Neymar hadi kufikia kiasi cha €50m kwa mwaka kutoka €35m kwa mwaka ili kujaribu kuzuia ushawishi wa aina yoyote kutoka Real Madrid.

Deus Kaseke pekee amekidhi vigezo vya usajili Yanga

$
0
0

Ofisa habari wa Yanga Dismas Ten amesema mchezaji pekee aliyekidhi vigezo vya usajili ni Deus Kaseke huku Kelvin Yondani na Hassan Kessy wakiwa hawana mikataba na klabu hiyo.

Dismas alizungumza na Prisca Kishamba kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu usajili wa wachezaji wa Yanga.

“Ukiangalia kwenye mfumo wa usajili wa ndani kwa Yanga, mchezaji pekee ambaye amekidhi vitu vyote vinavyotakiwa kuwepo ni Deus Kaseke, tayari usajili wake tumeutuma tunachosubiri ni TFF kuuthibitisha ili apate leseni ya ndani.”

“Wachezaji wengine wote usajili wao bado upo pending kwa sababu baadhi ya documents zao zinakosekana. Hadi sasa nina medical report za wachezaji watatu, (ya Matheo Anthony ina matatizo) inabidi irudishwe kwa daktari ili aweze kuiweka sawa.”

“Medical report zina gharama yake katika kuzitengeneza. Kabla daktari hajaondoka kwenda Kenya aliniambia kuna kipimo ambacho kinakwenda hadi Tsh. 230,000 ukizidisha kwa idadi ya wachezaji tulionao utaona ni kiasi gani cha fedha kina hitajika.”

“Changamoto ipo lakini baada ya daktari kurudi kutoka Kenya atakuja kukamilisha medical report na baadaye usajili uweze kufanyika kwa sababu baadhi ya wachezaji usajili wao upo pending kutokana na baadhi ya vitu kutokamilika.”

“Wapo wachezaji ambao hadi sasa hawana mikataba, Hassan Ramadhani Kessy, Kelvin Yondani hawana mikataba. Jambo jema ni kwamba kamati ya usajili inaendelea kuzungumza nao ili kuweka mambo sawa.”

Manara kamkataa Yondani

$
0
0

Haji Manara amekanusha tetesi za usajili wa beki Kelvin Yondani anayetajwa kukaribia kujiunga na Simba.

Manara amesema Yanga ndio wanatengeneza picha zima la kumhusisha Yondani kutakiwa na Simba ili watakapo malizana nae ionekane kwa mashabiki kwamba viongozi wamefanya kazi yaziada kumbakiza.

“Hiyo ni movie inatengenezwa kwa ajili ya kuwapoza mashabiki wa Yanga, ionekane kwamba Simba ilimtaka ili watakapomalizana nae ionekane walituzidi ujanja.”

“Sisi hatuna mpango wala hatukumuhitaji, jambo wabalitengeneza wenyewe wanajitekenya wenyewe na kucheka wenyewe, hakuna ishu ya Yondani na Simba kabisa.”

Kuna picha ambayo imeesambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha Yondani na Kazimoto wakiwa pamoja ambapo watu wamekuwa wakiihusisha na usajili wa Yondani kuhamia Msimbazi lakini Manara amei-punch pia.

“Mwinyi Kazimoto anahusika vipi na usajili wa wachezaji wa Simba? Mwinyi sio kiongozi wa Simba hajui chochote kuhusu mambo ya usajili kama yeye ni rafiki yake binafsi lakini haihusiani na usimba. Urafiki binafsi ni jambo jingine na Simba ni jambo jingine.”


Sababu 3 kichapo cha Yanga Kenya

$
0
0

Tumeshuhudia Yanga ikipoteza mechi yake ya pili kati ya tatu ilizocheza kwenye kombe la shirikisho Afrika. Yanga imekubali kichapo cha magoli 4-0 ugenini dhidi ya Gor Mahia kwenye uwanja wa Kasarani Nairobi-Kenya.

Imefungwa idadi ya magoli manne ambayo ilifungwa kwenye mechi yake ya kwanza ilipocheza ugenini dhidi ya USM Ulger ya Algeria.

Kuna sababu nyingi kwa Yanga kupoteza mechi yao dhidi ya Gor Mahia lakini www.shaffihdauda.co.tz imeangazia maeneo matatu.

Kiufundi.

Kwa tulichokiona tunaweza kusema Yanga hwakujiandaa lakini Gor Mahia walijiandaa. Kwenye michezo haijalishi ni soka, masumbwi au kikapu, maandalizi ni kufanya majaribio uwanjani sio mazoezi tu bila mechi za kujipima.

Huwezi kuwa umejifungia unafanya mazoezi halafu ukasema unajiandaa, Gor Mahia walikuwa na faida zote, ligi ya Kenya inaendelea, wana kikosi kipana kwa sababu waliweza kukigawanya kuna kikosi kilikuja kwenye Kagame Cup kingine kilibaki Kenya.

Yanga walikaa karibu mwezi na nusu bila mechi za ushindani tangu walipotolewa kwenye michuano ya SportPesa nchini Kenya, kwa hiyo wavhezaji hawawezi kuwa katika hali ya ushindani.

Mechi ilikuwa kati ya timu iliyojiandaa dhidi ya timu ambayo haijajiandaa na kama Gor Mahia wangekuwa makini zaidi wangefunga magoli zaidi ya manne kwa sababu walikosa mabao ya wazi kama mawili au matatu.

Kisaikolojia

Hakuna asiyefahamu kwa sasa Yanga wanapitia kipindi kigumu kuna mambo mengi ambayo alizungumza ofisa habari wa timu Dismas Ten ambayo hayahitaji elimu kubwa kutambua kwamba ndani ya Yanga mambo hayapo sawa.

Kukosekana kwa wachezaji wenye ubora  na uzoefu.

Tambwe amekosekana kwenye kikosi cha kwanza kwa kipindi kirefu sana, Yanga imemkosa Kamusoko mwenye ubora kwa muda mrefu, wamempoteza Chirwa na Ngoma, Yondani, Kessy hawakuwepo.

Ukiangalia profile ya wachezaji ambao wamekosekana na ambao walicheza dhidi ya Gor Mahia unapata picha halisi ya matokeo waliyopata.

Eden Hazard atachezea wapi msimu ujao?

$
0
0

Tayari usajili wa Cristiano Ronaldo kwenda Juventus umekamilika, hii ndio ilikuwa habari kubwa sana ya usajili lakini hivi sasa kuna hili la mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard.

Mashabiki wa Chelsea dunia nzima hii ni habari ambayo hawataki kuisikia lakini waswahili wanasema lisemwalo lipo na kama halipo laja, na lisemwalo ni Eden Hazard anatakiwa Real Madrid na Barcelona.

Mwanzoni Real Madrid walikuwa wakiongoza mbio hizi lakini sasa klabu ya Barcelona imejitokeza katika mbio hizi na habari kutoka ughaibuni zinasema Barcelona hawataki utani katika hili.

Eden Hazard mwenyewe anaonekana yuko katikati, anaonekana kama anataka kuondoka na anaonekana anataka kubaki. Tofauti na Real Madrid ambao walitaka kutoa pesa tu kwa Chelsea, Barca wenyewe wana dili lingine.

Wababe wa La Liga hao wanataka kumtoa nyota wao aliyetoka Borussia Dortmund Osmane Dembele kama sehemu ya dili hilo la kumnasa Hazard aliyekuwa na kiwango cha hali ya juu kombe la dunia.

Kuna tetesi za chini chini ambazo zinasema wakala wa mchezaji huyo amekutana na Barcelona ili kujaribu kuongelea suala la usajili wake kwenda Barcelona.

Lakini ukiacha hayo, wiki hii Hazard alinukuliwa akimsifu kocha aliyepita wa Real Madrid Zinedine Zidane na kusisitiza kwamba “Real Madrid ni ndoto ya kila mtu”

Florentino Perez tayari amempoteza Cr7 na ni wazi kwamba usajili wa Neymar utakuwa mgumu sana hivyo ni wazi kwamba Real Madrid watatumia nguvu kubwa ya pesa kumnasa Hazard kuwa mrithi wa Cr7.

Achana na Madrid achana na Barcelona, kocha mpya wa Chelsea Marizio Sarri amesema kati ya vitu anavihitaji Chelsea ni Eden Hazard na Chelsea wanajipanga kuitolea nje ofa yeyote itakayoletwa, tusubiri kuona vita hii ya mafahari watatu itaishia wapi.

Kocha mpya wa Simba kiboko! ‘watapata tabu sana’

$
0
0

Na Priva Abiud (Privaldinho)

Wakati wa michuano ya Sportpesa kulizuka sintofahamu kuhusu mkuu wa dawati la ufundi la Simba. Ilisemekana kuwa Piere ametupiwa virago vyake. Zikawa ni stori ambazo hazikuwa na kichwa wala mguu. Ghafla zikazuka tena habari za Masoud Djouma kuwa ameshapewa nauli ya kurudi kwao Burundi.

Wanachama wa Simba wameishuhudia timu yao ikiwa chini ya Masoud Djuma kwenye michuano ya Kagame Cup bila kocha mkuu huku Lechantre akiwa tayari katimka zake. Ni kweli hatimaye Mbelgiji kocha Patrick Aussems ametua nchini na tayari amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuwatumikia wekundu wa msimbazi.

Sasa ni wazi Pierre Lenchantre hawezi kurudi tena klabuni hapo licha ya kuwapa ubingwa uliokumbatiwa na wanajangwani kwa kipindi kirefu.

Majina Kamili Patrick Winand J. Aussems
Tarehe ya kuz 6 Februari 1965
Sehemu kuz MoelingenBelgium
Urefu 1.90 m (6 ft 3 in)
Nafasi ya kuch Mlinzi

Ametumia Muda mwingi sana katika klabu ya Standard Liege akiwa kama mlinzi wa kati.

Alichezea Vilabu hivi hapa
1974–1981 RCS Visé
1981–1988 Standard de Liège
1988–1989 K.A.A. Gent
1989–1990 R.F.C. Seraing
1990–1993 ES Troyes AC

Amekuwa kocha wa muda mrefu katika ligi za Afrika kama Cameroon na Congo kabla ya kutimkia Nepal.

Orodha ya Vilabu alivyovifundisha

Patrick Aussems mara ya mwisho amejiunga klabu ya Marbela United maarufu kama MUFC mnamo January 14, 2017 baaa ya miaka 30 ya uzoefu wa soka la Europe, Asia, na Africa. Aussems amecheza ligi daraja la kwanza huko Belgium na France. Pia aliwahi kuitwa timu ya taifa ya Belgium . Aussems’ anamiliki leseni ya UEFA (UEFA Pro License)

Kocha mkuu timu ya taifa ya Nepal

Patrick Aussems aliisaidia Nepal mwaka 2016 kushinda South Asian Games kule India, pia alitwaa kombe la Banganbadhu Gold Cup kule Bangladesh. Aliweza kuisaidia Nepal, kupanda viwango vya FIFA kwa alama 11 kutoka #192 to #181.

Kocha mkuu wa Benin

Aussems aliisaidia Benin kufuzu mashindano ya mwaka CAN 2008 kule Ghana, pia alifanya hivyo mwaka 2010 kule Angola. Pia aliisidia timu ya vijana ya U19 & U16 kushiriki michuano ya African Cup CAF mwaka 2009. Aliweza kuisaidia Benin kwenye viwango vya FIFA kuruka nafasi 55 , kutoka #114 mwaka 2006, hadi nafasi ya #59 mwaka 2009. Huyu anatufaa taifa Star huyu.

Kocha wa Madaraja ya 1st & 2nd huko Europe, Africa na China

Patrick mwaka 2014/15 aliisaidia Al Hilal Omdurman ya Sudan kushinda ubingwa Sudan Super Cup mwaka huo huo alifika fainali African Champions League mwaka 2015. Kabla ya hapo msimu wake 2013/14 Aussems alikuwa kocha mkuu wa AC Leopards Dolisie ya Congo ambapo alifanikiwa kutwa ubingwa wa ligi na alifanikiwa kufika fainali ya African Cup.

Kuanzia mwaka 2010-2012, Patrick Aussems alikuwa kule China kwenye ligi daraja la kkwanzana klabu ya Shenzhen Ruby, kisha akaelekea Chengdu Blades 2012.

Kule nchini Ufaransa Aussems alishinda National Championship akiwa na timu ya daraja la pili iitwayo ETG FC mwaka 2009/10. Hapo awali kuanzia mwaka 1997-2002, alishinda mataji mawili akiwa na SS Capricorne, na Saint-Louisienne.

Takwimu zake kama Mchezaji

Akiwa kama mchezaji amecheza michezo 250 ndani ya Belgium na France ndani ya miaka 17. Aliichezea timu ya taifa ya U23. Aussems amecheza michezo 20 ya UEFA Cup. Pia aliwahi kutwaa Belgian Super Cup na ubingwa wa Belgium.

Kuna mtu kaniambia huyo kocha asije akajichanganya akaja na begi kubwa maana Simba sio wavumilivu.

VPL yaipeleka Simba Uturuki

$
0
0

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji pamoja na benchi la ufundi watasafiri kuelekea Uturuki kwa ajili ya pre-season kwa lengo la kujiandaa na ligi kuu Tanzania bara.

“Siku ya Jumapili  alfajiri klabu ya Simba itasafiri kuelekea Uturuki kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya ligi kuu Tanzania bara inayotarajiwa kuanza August 22, 2018. Ikiwa huko itakaa hadi August 5 kisha itarejea Dar kwa ajili ya tamasha la Simba Day”-🗣Haji Manara.

“Msafara wa wafu 35 (wachezaji wote na benchi la ufundi) utasafiri kwenda Uturuki, tukiwa huko tunatarajia kupata mechi za kirafiki kwa kadiri benchi la ufundi litakavyoona inafaa.”

“Matarajio yetu pre-season hiyo tunayokwenda kufanya Istanbul itatusaidia kwa wachezaji wapya na wazamani kupata muunganiko mzuri kabla ya ligi kuanza.”

Bei za jezi mpya za United na Chelsea hazishikiki, Arsenal na Spurs nao balaa

$
0
0

Unaambiwa jezi mpya ambayo Manchester United wameitambulisha imezua hasira kwa mashabiki wake baada ya bei ya jezi hiyo kuwa juu kupita kawaida.


Kama unaitaka jezi hiyo ni lazima uwe na pesa sii chini ya 541,070, kwa tshirt peke yake inauzwa karibia 320,000 na kama utahitaji kupata full hadi socks itakugharimu kiasi hicho cha laki 450,000+.


Bukta ya timu hiyo inauza pesa ya Kitanzania shilingi 124,000 huku socks za timu zikiuzwa 75,284 na hii ni kwa mujibu wa bei mpya za kampuno inayotengeneza vifaa vya michezo vya klabu hiyo kampuni ya Adidas.


The Blues/Chelsea nao sio kirahisi kama unavyowaza, wenyewe uzi wao ni £195.85 kuipta jezi full ya klabu hiyo ambapo kiasi hicho ni sawa na karibia na 500,000/= kwa bei ya pesa ya madafu.

Wakati mashabiki wa Manchester United na Chelsea wakilia bei za jezi zao. kwa wenzao Arsenal hali ni tofauti na jezi ya klabu hiyo imeendelea kuuzwa kwa bei ya kawaida.


Ukiitaka jezi mpya ya Arsenal unatakiwa uwe na kiasi cha 295,000 tu kwa tshirt na full itakugharimu 464,197/=, kuipata jezi original ya klabu ya Liverpool kwa tshrt tu unapaswa kuwa na sii chini ya 210,000/= hii ni kwa bei ya Liva msimu uliopita.


Tottenham Hotspur nao wametangaza uzi wao mpya kwa ajili ya 2018/2019 na kama unaitaka jezi mpya ya Tottenham Hotspur unatakiwa kuwa na 473,000 kuipata jezi original ya klabu hiyo

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>