Arsenal imelazimishwa sare ya 0-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani dhidi ya Hull City timu inayoshiriki ligi daraja la kwanza England, mchuano huo uliopigwa Jumamosi February 20 ulikuwa ni mchezo wa FA Cup.
The Gunners walionekana kunyimwa penati ya wazi katika kipindi cha kwanza baada ya mchezaji wa Hull kuunawa mpira kwenye box la hatari kabla ya kuondoshwa kwenye hatari.
Baada ya mapumziko walidhani watacheza dhidi ya wachezaji 10 wa Arsenal ambapo Laurent Koscielny alipona kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu mchezaji wa Hull.