Gerard Pique ni miongoni mwa wachezaji wenye mapenzi ya kupindukia kwa klabu ya Barcelona, alikutana na mchezaji mwenzake wa zamani wa Manchester United Rio Ferdinand na kufanya interview kuhusu mambo kadha wa kadha.
Pique ni mmoja wa wachezaji ambao wamewahi kucheza timu moja na Lionel Messi pamoja na Cristiano Ronaldo kwa nyakati tofauti, Rio Ferdinand amemuuliza Pique mchezaji gani ni bora kati ya Messi na Ronaldo?
Jibu alilolitoa Pique kuhusu nani bora kati ya Messi na Ronaldo ni hili: “Messi siyo binadamu, Cristiano ni binadamu bora kuwahi kutokea”.
Angalia kipande cha video wakati Ferdinand alipokutana na Pique na kupiga story kuhusu Messi na Ronaldo.