Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Kichuya, Mzamiru, waing’arisha Simba

$
0
0

img_4376

Magoli ya Mzamiru Yassin na Shiza Kichuya yameendelea kuiweka Simba kileleni mwa ligi kuu Tanzania bara ikifikisha jumla ya pointi 23 baada ya kucheza mechi 9 hadi sasa.

Mzamiru Yassin alianza kuifungia Simba goli la kwanza dakika ya 43 kipindi cha kwanda akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Shiza Kichuya.

img_4385

Simba ikafanikiwa kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wake Kagera Sugar.

img_4390

Kichuiya akapachika bao la pili dakika 75 kwa mkwaju wa penati baada ya Ibrahim Mohamed kuangushwa kwenye eneo la hatari la Kagera Sugar.

img_4397

Dondoo

  • Simba bado inaendeleza rekodi yake ya kutopoteza mchezo wa VPL msimu katika mechi 9 ilizocheza. Imetoka sare mara mbili na kushinda michezo mingine 7.
  • Kichuya amefikisha magoli 7 katika mechi 9 za VPL mabazo ameitumikia Simba tangu alivyojiunga nayo akitokea Mtibwa SUgar ya Morogoro.
  • Maoli yote ya Simba dhidi ya Kagera Sugar yamefungwa na wacheaji wa zamani wa Mtibwa Sugar (Mzamiru Yassin na Shiza Kichuya).
  • Simba imeshinda mechi 4 kati ya mechi 5 za mwisho ambazo wamekutana na Kagera Sugar, Kagera Sugar wameshinda mechi moja dhidi ya Simba katika mechi 5 zilizopita. (Simba 0-1 Kagera Sugar, Kagera Sugar 1-2 Simba, Simba 3-1 Kagera Sugar, Kagera Sugar 0-1 na Simba 2-0 Kagera Sugar)

Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>