Magoli ya Mzamiru Yassin na Shiza Kichuya yameendelea kuiweka Simba kileleni mwa ligi kuu Tanzania bara ikifikisha jumla ya pointi 23 baada ya kucheza mechi 9 hadi sasa.
Mzamiru Yassin alianza kuifungia Simba goli la kwanza dakika ya 43 kipindi cha kwanda akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Shiza Kichuya.
Simba ikafanikiwa kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wake Kagera Sugar.
Kichuiya akapachika bao la pili dakika 75 kwa mkwaju wa penati baada ya Ibrahim Mohamed kuangushwa kwenye eneo la hatari la Kagera Sugar.