Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Habari mbaya kwa Arsenal kuhusu Hector Bellerin

$
0
0

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amethibitisha kwamba Hector Bellerin anatarajiwa kuwa nje kwa wiki nne baada ya kupata majeraha katika mchezo dhidi ya Tottenham.

Beki huyo wa kulia Mhispania aliumia kifundo cha mguu wakati wa mchezo dhidi ya Spurs uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 kabla ya kupisha mapumziko ya mechi za kimataifa.

Katika mkutano na wanahabari leo Wenger amesema: “Hectoer atakuwa nje kwa wiki nne. Alipata majeraha sekunde kumi tu kabla ya mchezo dhidi ya Spurs kumalizika.”

Kwa hali hiyo Bellerin ataukosa mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Manchester United unaotarajiwa kufanyika Jumapili ya wikiendi hii katika Uwanja wa Old Trafford.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles