Kijana Farid Musa ameanza vyema maisha yake ya soka nchini Hispania baada ya kufanikiwa kuifungia magoli mawili timu yake ya Tenerife B wakati akicheza mechi yake ya kwanza tangu awasili kwenye klabu hiyo.
Fairid alikuwa aliisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 wakati ikichuana na CF Unionviera.
Nyota huyo ambaye amesajiliwa kwa mkopo amepelekwa timu B kwa ajili ya kufundishwa baadhi ya mambo ikiwemo mfumo unaotumiwa na timu yake kabla ya kuanza kuingia kwenye timu ya kwanza.