Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

WADE NA BOSH WAIONGOZA MIAMI NA REKODI IMARA DHIDI YA SACRAMENTO KINGS

$
0
0

BOSH

Wade alifunga pointi 24 na Miami Heat kuwapiga Sacramento Kings 116-109 Alhamisi usiku ,huku wakitumia faida ya Sacramento kumkosa nyota wao DeMarcus Cousins baada kusimamishwa mchezo mmoja.

Chris Bosh alikuwa na pointi 23 na 11 rebounds , na Tyler Johnson alikuwa na pointi 19 na kuisaidia Miami kupata  ushindi kwa mara ya nne katika mechi tano .

“Haikuwa moja ya michezo yetu bora ya kujilinda ndani  ya msimu huu, lakini kuna baadhi ya utekelezaji bora wa baadhi ya mambo ambayo tumekuwa tukijifunza kiushambuliaji , ” kocha wa Miami Heat Erik Spoelstra alisema.

Mchezaji wa Sacramento Kings,  Rajon Rondo alikuwa na takwimu za juu za msimu kwenye pasi kwa kutoa pasi 18, huku pia akimaliza na  pointi 14 na rebounds 9. Hii ikiwa ni baada ya  Triple doubles  katika michezo yake ya awali minne.

“Nadhani mchezo wake ni wenye kutia moyo sana na chanya kwa kila mtu,” kocha wa Sacramento Kings George Karl alisema. ” Yeye hufanya kila mtu kwenye timu yake awe bora . Yeye hufanya mchezo mliopanga kutokea.”

Rondo ana  wastani wa pointi 14.2 , pasi 14.2 na 9.8 rebounds katika michezo yake mitano iliyopita.

TAKWIMU

Sacramento ina matokeo mabovu ya  3-25 katika uwanja wa Miami. Kings ‘ walipata ushindi wa mwisho katika uwanja wa Miami hii  ilikuwa Novemba 10, 2001 .

Wakati Wade akicheza , Miami ina matokeo chanya ya  11-0 katika mechi za nyumbani dhidi ya Wafalme (Kings) hawa wa Sacramento  na 18-1 ujumla dhidi yao.

HIGHLIGHTS


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>