Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Barua ya Manji kujiuzulu Yanga

$
0
0

Barua iliyosainiwa na Yusuf Manji Mei 22, 2017 inaonesha kwamba Manji ameachia rasmi nasasi ya uenyekiti wa klabu ya Yanga na makamu mwenyetiki wa klabu hiyo Clement Sanga atakuwa mwenyekiti na kuiongoza klabu hadi hapo uchaguzi utakapofanyika ili kumpata mwenyekiti mpya.

Kwa mujibu wa maelezo ya barua, Manji alifikia uamuzi wa kujiuzulu Mei 20 mwaka huu siku ambayo Yanga ilitangazwa kuwa bingwa wa ligi kuu Tanzania bara 2016/2017.

Katika barua hiyo, Manji amsema ameamua kuachia ngazi ili kutoa nafasi kwa wengine nao kushika uongozi ndani ya klabu hiyo.


Shaffih Dauda kuhusu Serengeti Boys kutolewa AFCON U17

$
0
0

Shaffih Dauda amewapongeza wachezaji na benchi la ufundi la Serengeti Boys kwa hatua waliyofika ya kushiriki michuano ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 licha ya kutolewa hatua ya makundi baada ya kupoteza mchezo wao wa mwisho wa Kundi B dhidi ya Niger.

Dauda amelipongeza pia shirikisho la soka nchini (TFF) kwa kuiandaa timu tangu hatua ya mwanzo kabisa kwa kuwakusanya vijana wadogo na kuwatengenezea mazingira ya kuonesha uwezo wao.

“Wadogo zetu wamepambana sana hadi kufika hatua waliyofanikiwa kupifika, tuwapongeze katika hilo ukilinganisha na maandalizi waliyopewa kabla hata ya kufuzu kwenda Gabon kwa ajili ya michuano ya vijana.”

“TFF pia imepambana sana kuhakikisha vijana hawa wanafanya vizuri na wamefanikiwa, nawapongeza shirikisho kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kuwatafuta hawa vijana kuwatunza na kuwalea kigumu hatimaye wakawafikisha hapo walipofika.”

“Kwenye michuano ya AFCON U17 Wachezaji wan chi nyingine wametoka kwenye academies pamoja na vilabu kwa hio wamejengwa hadi kufika pale, hawajakusanywa tu. Kwetu ni wachache tu ambao wametoka Mtibwa Sugar, Azam na JKT Ruvu. Vilabu tunavyoviita vikubwa havina kabisa strong youth development programs.”

“Sasa kutolewa kwa Serengeti Boys iwe ni changamoto kwetu na tujifunze kwamba hakuna kitu ambacho kinaanzia juu. Tujipange kwa ajili ya mashindano yajayo kwa kuiandaa timu ambayo itafanya vizuri na kufika mbali zaidi kuliko tulipoishia mwaka huu.”

Dauda amevishauri vilabu vya Tanzania kuwekeza katika vijana ili badae wavisaidie vilabu vyao na timu za taifa kuliko kuoa pesa nyingi kununua wachezaji wa kigeni.

Magazeti ya Ulaya yasemavyo leo Jumanne

$
0
0

Daily Star.Jose Mourinho yupo katika mpango wa kumuondoa Chriss Smalling katika timu yake, na huku Newcasttle na West Ham watakumbana na upinzani toka kwa Monaco katika kumnunua Michy Batshuayi kutoka Chelsea na Manchester United wanavutiwa na mpango wa kuwasajili Raphael Varane pamoja na Marquinhos.

Daily Mirror.Phillipe Coutinho amewatoa hofu mashabiki wa Liverpool kwa kuwaambia anaona atakaa klabuni hapo kwa muda mrefu, klabu ya Fc Bournamouth inaweza kukamilisha usajili wa Jermain Defoe wiki ijayo, na baada ya kupanda daraja klabu ya Newcstle iko na mkakati wa kumsajili Michy Batshuayi kutoka Chelsea.

The Sun.Diego Maradona amedai kwamba kwenye maisha yake yote mchezaji bora kumuona alikuwa Franseco Totti, Manchester United wana matumaini kuwasajili Douglas Costa na Renato Sanchez baada ya kukaa benchi msimu huu wa ligi.

The Sun.Chelsea na Bayern wameingia kwenye mpambano wa kumsajili mlinzi wa Tottenham Kyle Walker ambaye Man City nao wanamtaka, Liverpool wameingia katika mpambano wa kumnunua Oxlade Chamberlain.

Daily Telegraph.Liverpool wamepanga kutumia zaidi ya £100m ili kukiimarisha kikosi chao, huku Everton nao wamepanga kumuweka chini Ross Barkley wiki hii ili kujaribu kumshawishi aendelee kubaki klabuni hapo.

 

Madogo watano wanaoweza iangamiza Manchester United

$
0
0

1.Bertand Troure.Alionekana hadi fainali za Afcon akiichezea Burkina Fasso na hapo kabla alikuwa Chelsea, umri wa Troure ni miaka 21 tu ila amekuwa hatari sana msimu huu na hadi sasa ameshafunga mara 13 huku akichangia kuipeleka timu yake fainali baada ya kufunga mara mbili wakati wa nusu fainali.

2.Kasper Dolberg.Mshambuliaji wa Dernamark mwenye umri wa miaka 19 alifunga hatrick dhidi ya NEC, United wanapaswa kumchunga sana kwani hadi sasa ana magoli 15 na anaonekana anaweza kuwa tishio kubwa kwa walinzi wa Manchester United.

3.Davinson Sanchez.Mlinzi wa kati wa Ajax naye ana umri wa miaka 20 tu lakini ana uwezo mkubwa wa kukaba kuliko hata umri wake, anaweza kuwa kizuizi kikubwa kwa mafowadi wa Manchester United.

4.David Neres.Ni ingizo jipya katika klabu ya Ajax, lakini mshambuliaji huyo wa Kibrazil ameshaanza kuwa jina kubwa nchini Uholanzi na wachambuzi wengi nchini humo wameanza kumfananisha na Luis Suarez.

5.Justin Kluivert.Mtoto wa nguli wa zamani wa soka Patrick Kluivert, winga huyu amekuwa akizungumziwa kutokana na uwezo.wake mkubwa na tayari watu wengi wameanza kumfananisha na baba yake, anaweza kuleta madhara kwa mabeki wa pembeni wa Manchester United.

 

Mkuu wa mkoa Dodoma ameizungumzia fainali Simba vs Mbao

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana ameelezea namna serikali ya mkoa ilivyojipanga kuelekea mchezo wa fainali ya Azam Sports Federation Cup kati ya Mbao FC dhidi ya Simba itakayofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Dodoma inauzoefu wa kukaribishabwatu kwa makundi makubwa kutoka nje ya maeneo yetu. Kwa hiyo tumejipanga vizuri tunawakaribisha watu kutoka sehemu mbalimbali za nchi nzima tuna hoteli za kutosha wasiwe na wasiwasi.

Tupo kwenye hatua za mwisho kabisa za ukarabati wa uwanja ili uwe salama kwa matumizi ya siku hiyo lakini pia usalama utakuwa wa kutosha ili kila mmoja aweze kuburudika wakati mchezo unaendelea.

Tunawakaribisha Simba, Mbao hata Yanga waje waone kabumbu inavyosakatwa hapa Dodoma na mambo mengine yatakavyokwenda.

Mchezo wa fainali unatarajia kuchezwa Mei 27, 2017 na mshindi wa mchezo huo atakuwa amefuzu moja kwa kucheza michuano ya kombe la shirikicho (Caf Confederation Cup).

Baada ya shambulio lililotokea Manchester, FA wajipanga.

$
0
0

Mwanamuziki maarufu wa Pop Ariana Grande alitarajiwa kuwapa furaha wakazi wa London usiku wa Jumatatu katika tamasha ambalo lilifanyika katika mji wenye mahasimu wawili wakubwa Manchester United na Manchester City.

Ariana Grande ambaye anatamba na kibao maarufu cha Side to side tamasha lake liligeuka kilio baada ya kutokea shambulio linalohisiwa ni la kigaidi ambapo watu zaidi ya 22 walikufa huku wengine 59 wakijeruhiwa.

Shambulio hilo limewashtua wengi hadi wanasoka, na chama cha soka cha Uingereza ambacho ndio wasimamizi wa fainali ya FA itakayopigwa mwishoni mwa wiki nao pia wameshtushwa na shambulio hilo.

FA wamesema shambulio hilo limewapa somo kuhusu masuala ya ulinzi haswa katika kipindi hiki ambacho fainali ya FA kati ya Arsenal na Chelsea imebakisha siku chache kuweza kupigwa.

Taarifa iliyotolewa na chama hicho cha soka nchini Uingereza imewahakikishia wapenzi na mashabiki wa soka nchini humo usalama wao na kuwatoa hofua kuhusu jambo lililotokea mjini Manchester.

“Usalama wa mashabiki ni jambo muhimu sana na tunawahakikishia usalama wao kwani tutashirikiana na askari wa metropolian ili kuimarisha usalama” ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya FA.

FA imewataka mashabiki kuwahi kufika uwanjani kwani kutakuwa na ukaguzi mkubwa kwa mashabiki lakini pia FA walitumia taarifa hiyo kutoa salamu za rambirambi kwa watu waliopoteza uhai katika tukio la mjini Manchester.

FA wamesema wameshafanya kikao na washauri wao wa mambo ya kiusalama lakini pia kwa kushirikiana na ofisi ya kuzuia masuala ya ugaidi nchini Uingereza (Nactso) wamejiandaa vyema kukabiliana na tukio kama hilo.

 

Ni United vs Ajax leo, lakini wajua Ajax hawajawahi kupata hata suluhu kwa Mourinho?

$
0
0

Leo ni leo katika dimba la Friends Arena nchini Sweden, uwanja ambao hauna bahati ya fainali lakini leo umebahatika kwa fainali kati ya Manchester United na Ajax ya Uholanzi.

Ushindi wa Manchester United leo utawapa tiketi kucheza champions league msimu ujao lakini wakifungwa watacheza tena Europa, wakati macho yote yakielekezwa Friends Arena sii vibaya ukajua mambo muhimu kuelekea mchezo huo.

Ajax inakuwa timu ya kwanza kutoka nchini Uholanzi kufika fainali ya michuano hiyo ya Europa tangia mwaka 2002 ambapo Feynoord walifanya hivyo

Katika misimu mitano ya ligi kuu Uingereza Manchester United inakuwa timu ya 3 kufika fainali hiyo baada ya Liverpool(2016) na Chelsea (2013).

Manchester United na Ajax wameshakutana mara 4 katika michuano ya barani Ulaya lakini hakuna mbabe, kwani kila mmoja amemfunga mwenzie mara mbilimbili wakati walipokutana.

Hii ni fainali ya kwanza ya Ajax katika michuano ya Ulaya baada ya ile ya mwaka 1995 dhidi ya Juventus katika champions league ambapo Ajax alifungwa kwa mikwaju ya penati.

Manchester United wanaingia katika mchezo huu kifua mbele kwani hadi wanafika fainali hawajawahi kupoteza mchezo katika michezo 10 iliyopita, wakisuluhu mara 3 na kushinda mara 7.

Jose Mourinho ni mbabe haswa wa Ajax, hadi sasa Mourinho ameshakutana na Ajax mara 6 na katika mara zote hizo walichezea kichapo kutoka kwa Mreno huyo.

Kasper Dolberg wa Ajax ana mabao 6 hadi sasa na ni Patrick Kluivert na Tin Blanker tu ambao walifunga mabao mengi kuliko yeye katika michuano ya Ulaya, walikuwa na mabao 7.

Katika fainali 16 zilizopita za Europa ni fainali 2 zilamuliwa kwa mikwaju ya penati, fainali 10 ziliamuliwa kwa muda wa nyongeza na huku fainali 4 zikiamuliwa muda wa kawaida.

 

Hofu ya fujo yatanda fainali ya Europa hii leo

$
0
0

Inasemekana hadi sasa mashabiki 9500 wako nchinj Sweden kuiona mechi kati ya Manchester United na Ajax lakini watu hao wamekosa tiketi za kuingia katika dimba la Friends Arena ambako mtanange huo utapigwa usiku wa leo.

Mwaka 2012 mashabiki wa United na Ajax walitaka kuzipiga uwanjani hali iliyopelekea polisi kukaa katikati yao ili kuzuia hilo lisitokee na askari mmoja nchinj Uingereza ameonya kuhusu tukio hilo.

Askari huyo amesema mchezo kati ya United na Ajax ni jambo la ajabu kwa mtu yeyote kuwaza kwamba unaweza kuisha salama bila jambo lolote kutokea kwani hilo ni suala gumu.

Manchester United imeshatuma maofisa wake wa masula ya kiusalama kwenda nchini Sweden ili kuhakikisha hali inakuwa salama kwa mashabiki wote wa United waliosafiri hadi nchinj humo.

John Ohare ambaye anahusika na masuala ya usalama pia ameonya kuhusu njia ya kukabiliana na mashabiki wa Kiingereza na kusisitiza ni vyema askari kutumia njia ambayo itakuwa salama.

Ohara ameonya kuhusu polisi kutumia nguvu kubwa kuwakabili mashabiki kwa hofu ya kile kilichotokea nchini Hispania wakati wa mechi kati ya Leicester City na Real Madrid.

 


Sababu za Juma Abdul kushindwa kutetea tuzo ya mchezaji bora VPL

$
0
0

Mshindi wa tuzo ya mchezaji bora msimu uliopita Juma Abdul amesema majeraha ya muda mrefu yamemfanya ashindwe kutetea tuzo hiyo katika msimu huu kwa sababu muda muda mrefu alikuwa nje ya uwanja.

Abdul ambaye ni beki wa kulia wa Yanga amesema mchezaji anapopata majeraha ya muda mrefu akirudi inabidi aanze kwanza kupambana kupunguza mwili na uzito kabla ya kuanza kupambana kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza.

“Ni kitu ambacho nilikuwa nimejiwekea kwamba kama msimu uliopita niliweza kuchukua tuzo ya mchezaji bora basi nitapambana ili niweze kutetea lakini yale mategemeo yangu hayakuweza kutimia kutokana na kukaa nje kwa muda mrefu.”

“Unapokaa hufanyi mazoezi, mwili unaongezeka uzito unaongezeka kwa hiyo hata ukirudi unaanza kupambana kupunguza mwili kwanza, halafu ligi ilikuwa imebana mechi zipo karibukaribu kwa hiyo sikuweza ku-perform vile nilivyotegemea kwa hiyo hiyo ndio chagamoto niliyokutana nayo.”

Juma Abdul hakucheza mechi nyingi msimu huu ukilinganisha na msimu uliopita hata mechi ambazo alicheza baada ya kupona majeraha, alikuwa akitokea benchi kuchukua nafasi ya Hassan Kessy.

Mambo manne ya kufahamu kuelekea fainali ya Simba vs Mbao

$
0
0

Kuelekea fainali ya kombe la FA Cup (Azam Sports Federation Cup) kuna mambo kadhaa ambayo yanainogesha fainali hiyo ambayo itachezwa kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma siku ya Jumamosi Mei 27, 2017.

Fainali hiyo inazikutanisha Simba SC (Dar) na Mbao FC (Mwanza) baada ya timu hizo kuvitoa vigogo vya VPL (Simba wakiitoa Azam FC kwenye mchezo wa nusu fainali huku Mbao wakiivua ubingwa Yanga)

Fainali ya kwanza kuchezwa nje ya Dar

Mkoa wa Dodoma umepata bahati ya kuwa mwenyeji wa fainali ya FA Cup kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa kombe hilo ambapo fainali zote zilizopita zilichezwa Dar. Timu zote zinazocheza fainali zitasafiri kutoka kwenye mikoa yao Simba (Dar) na Mbao (Mwanza) kisha zitakutana katikati ya nchi ambapo pia ni makao makuu ya Tanzania.

Bingwa atasafiri na kombe lake kurejea nalo mkoani kwake, mashabiki watalazimika kusafiri kutoka mikoa mbalimbali kuungana na wale wa mkoa wa Dodoma kuzishangilia timu zao.

Public viewing Centers

Chama cha mpira mkoa wa Dodoma (DOREFA) kimejipanga vizuri kuhakikisha mashabiki watakao kosa nafasi ya kuingia uwanjani (Jamhuri Stadium) wataweza kuishuhudia mechi hiyo kupitia public viewing centers ambazo tayari zimeshaandaliwa huku tiketi hizo za mechi ya fainali hiyo zikianza kuuzwa siku ya Ijumaa siku mmoja kabla ya mechi ili kupunguza msongamano siku ya mechi.

Ushindani wa Mbao

Mbao waliitoa Yanga ambao ndio mabingwa watetezi kwa kuwafunga goli 1-0 katika mchezo wa nusu fainali iliyochezwa CCM Kirumba, Mwanza. Mbao wameweka rekodi katika historia yao katika soka baada ya kupanda ligi na kufika fainali ya kombe la FA msimu huohuo kwa kuwatoa mabingwa watetezi.

Yanga walifungwa pia na Mbao katika mchezo wa mwisho wa ligi kwenye uwanja huohuo wa CCM Kirumba sikuwaliyokabidhiwa ubingwa wao wa VPL huku kwa Mbao ushindi huo ukawabakiza kwenye ligi.

Simba walipata ushindi wa goli 1-0 uwanja wa Uhuru lililofungwa dakika za mwisho kabisa za mchezo huo lakini wakashinda tena mechi ya raundi ya pili kwa magoli 3-2 kwenye uwanja wa CCM Kirumba. Mechi hiyo Mbao walitangulia kuwa mbele kwa magoli 2-0 hadi dakika ya 87 Simba walipoanza kusawazisha na hatimaye kushinda mchezo huo.

Simba

Simba wanaona kombe la FA Cup ndio njia pekee ya kuwafanya washiriki michuano ya kimataifa kwa sababu mshindi wa fainali hiyo atakata tiketi ya mucheza mashindano ya kombe la shirikisho Afrika msimu ujao na kuiwakilisha nchi.

Kjlabu ya Simba haijashiriki michuano ya kimataifa kwa muda mrefu, kwa hiyo mechi ya fainali wanaitolea macho ili kurejesha heshima ya kulitwaa taji hilo litakalowarudisha kwenye anga za kimataifa na pia kutuliza presha ya mashabiki wa klabu hiyo kwa kushindwa kubeba kombe kubwa kwa muda mrefu zaidi ya lile la mapinduzi Cup walilotwaa hivi karibuni.

‘Manji anatikisa kibiriti’– Mzee Akilimali

$
0
0

Katibu wa baraza la wazee wa Yanga Mzee Ibrahim Akilimali amesema, huenda kujiuzulu kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji ni kutikisa kibiriti tu lakini atarejea tena kwenye nafasi yake kwa sababu tayari alishawahi kutangaza kujiuzulu halafu akarejea baada ya kuombwa na wanachama kufanya hivyo.

Mzee Akilimali amesema mara ya kwanza Manji alipotangaza kujiuzulu alitukanwa na kutishiwa maisha hadi kutaka kuchomewa nyumba yake lakini baadae Manji alirejea kwa hiyo bado haamini kama amejiuzulu jumla au anatikisa kiberiti kama mwanzo.

“Mimi siamini kwa sababu mguu uliomumwa na nyoka ukikanyaga jani unaogopa, aliposema anajiuzulu basi nilitishiwa amani kabisa na kutukanwa matusi ya laana siwezi kuzungumza nikawa naishi kwa kibali cha polisi ili kunipa usalama lakini alikuwa anatishia, pengine na wakati huu anatishia,” amesema Akilimali wakati akihojiwa na kituo cha EFM Radio.

“Wana Yanga wawe wavumilivu wawe na utulivu kwa sababu hatima tutaisikia kwa sababu mimi nashindwa kuamini, kuna wakati kiongozi wetu alitikisa kibiriti iliniletea mimi kutaka kuawa na kuchomewa nyumba moto lakini kumbe alikuwa anatikisa tu kiberiti mkubwa wetu.”

“Alichokifanya ni haki yake kisheria kwa sababu nimesikia ana matatizo ya kiafya kwa hiyo tumepokea kwa huzuni kwakweli. Kama itathibitika afya yake sio nzuri tutabariki maamuzi yake lakini kama afya yake itakuwa inanafuu tutajaribu kuomba aendelee kidogo kwa sababu wakati mgu huu bado tunamuhitaji.”

Mwezi August 2916 Manji alitangaza kujiuzulu nafasi yake kama mwenyekiti wa Yanga huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni baadhi ya watu kupinga juhudi zake za kujaribu kuikodi nembo ya klabu hiyo kwa miaka 10. Mzee Akilimali ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitajwa kupinga utaratibu wa Manji kuikodi Yanga.

Picha5: Mwakyembe alivyoipokea Serengeti Boys ikitokea Gabon

$
0
0

Tumu ya Serengeti Boys imewasili salama jijini Dar es Salaam kutoka Gabon ilipokua ikishiriki michuano ya AFCON U17 kabla ya kutolewa kwenye mchezo wa mwisho wa Kundi B kwa kufungwa na Niger bao 1-0.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe alwaongoza watanzania katika mapokezi hayo kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. J.K Nyerere.

Mwakyembe amewapongeza Serengeti Boys kwa kushiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza na kuwaambia kuondolewa kwao ni mwanzo mpya wa safari ya kuitumikia Ngorongo Horoes.

“Karibuni nyumbani, mmetuwakisha vizuri na kuweka rekodi ya kuwa Tanzania tupo, tukienda kwenye mashindano ya kimataifa hatuendi kama wasindikizaji, tunaenda kama washindani.”

“Tunawategemea nyie ndio mtakua Ngorongoro Heroes, maandalizi yanaanza sasa kuelekea michuano inayokuja ili mwakani mtuwakilishe vizuri.”

Video: Baba wa Tshabalala alivyoipokea tuzo ya mwanae baada ya kutajwa mchezaji bora VPL

$
0
0

Usiku wa Mei 24, 2017 tuzo za VPL zilitolewa kwa wachezaji, timu na waamuzi waliofanya vizuri katika kipindi chote cha msimu wa 2016/2017 ambapo zilitolewa tuzo takribani 15 kwenda kwa watu mbalimbali.

Katika hafla hiyo, tuzo kubwa ambayo ilikua ikisubiriwa kwa hamu ilikuwa ni ya mchezaji bora wa msimu ambao ulimalizika Mei 20 na Yanga kuibuka mabingwa baada ya kuchukua taji la VPL ikiwa ni kwa mara ya tatu mfululizo huku ikiwa ni mara ya 27 kihistoria.

Mshindi wa tuzo ya mchezaji bora ilinyakuliwa na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ beki wa Simba na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’.

Tshabalala amewashinda golikipa wa Azam Aishi Manula, Simon Msuva kutoka Yanga, kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima na Shiza Kichuya wa Simba.

Beki huyo wa kushoto alifanikiwa kucheza mechi zote za ligi kwa dakika 90 za kila mchezo huku akipata kadi mbili tu za njano na kuisaidia timu yake kumaliza katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

Tuzo hiyo ilipokelewa na baba mzazi wa mchezji huyo Mzee Hussein Zimbwe kutokana na mchezaji mwenyewe kutokuwepo kwenye hafla ya utoaji wa tuzo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ambaye ndiyo alikabidhi tuzo hiyo.

Exclusive Video: Niyonzima amezungumzia hatima yake ndani ya Yanga

$
0
0

Kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima amejibu kuhusu tetesi zilizopo mtaani kwamba huenda akaondoka ndani ya kikosi cha Yanga na asiwepo kwenye msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara 2017/2018.

Niyonzima amesema, mkataba wake unamalizika siku chache zijazo hivyo atatangaza kama ataendelea kuwepo Tanzania au ni wakati wake wa kuondoka na kwenda kutafuta maisha mahali pengine.

Niyonzi ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda amesema, katika misimu yote ambayo amefanikiwa kutwaa ubingwa akiwa Yanga, msimu huu ulikuwa mgumu na changamoto nyingi hadi kufikia kushinda taji la VPL kwa tofauti ya magoli.

Video: List ya washindi wa tuzo za VPL 2016/2017

$
0
0

Usiku wa Mei 24, 2017 tuzo za VPL zilitolewa kwa wachezaji, timu na waamuzi waliofanya vizuri katika kipindi chote cha msimu wa 2016/2017 ambapo zilitolewa tuzo takribani 15 kwenda kwa watu mbalimbali.

Washindi wa nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi ni Azam FC ambao wamepewa kiasi cha pesa cha shilingi milioni 24.

Kagera Sugar wakashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi na kujishindia shilingi milioni 30.

Simba imekamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi na kuzawadiwa shilingi milioni 42.

Mabingwa wa ligi guu Tanzania bara ni Yanga ambao wametwaa kitita cha shilingi milioni 84.

Tuzo ya timu yenye nidhamu imekwanda kwa Mwadui FC ya Shinyanga na kuzawadiwa shilingi milioni 17.5

Tuzo ya mfungaji bora imechukuliwa na wachezaji wawili Simon Msuva (Yanga) na Abdulrahman Musa (Ruvu Shooting) ambao kila mmoja alifunga magoli 14 kwenye msiu wa ligi.

Mwamuzi bora wa msimu ameshinda Elly Sassi wa Dar es Salaam akiwashinda Shomari Lawi (Kigoma) na Hans Mabena (Tanga). Mwamuzi bora amezawadiwa shilingi milioni 5.8.

Mecky Maxime ameshinda tuzo ya kocha bora wa msimu baada ya kuisaidia Kagera Sugar kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi. Maxime amewazidi Joseph Omog (Simba) na Etiene Ndayiragije (Mbao FC).

Tuzo ya mchezaji bora kijana (U20) imepewa jina la Ismail Khalfani Mrisho aliyekuwa mchezaji wa Mbao ambaye alifariki uwanjani akiitumikia timu yake kwenye mashindano ya ligi ya vijana, tuzo hii ameshinda Shabani Idd Chilunda wa Azam FC. Mshindi amezawadiwa shilingi milioni 4.

Tuzo ya heshima ikaenda kwa Kitwana Manara mchezaji wa zamani wa Yanga na timu ya taifa ya Tanzania.

Tuzo ya golikipa bora wa msimu imechukuliwa na Aishi Manula wa Azam FC akiwashinda Juma Kaseja (Kagera Sugar) na Chaima (Mbeya City).

Mbaraka Yusuf (Kagera Sugar) ameshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi.

Tuzo ya mchezaji bora wa kigeni anaecheza ligi kuu Tanzania bara imekwenda kwa Haruna Niyonzima kiungo wa Yanga raia wa Rwanda.

Goli bora la msimu ameshinda Shiza Kichuya, goli lake alilifunga wakati Simba ikicheza dhidi ya Yanga.

Mchezaji bora wa VPL 2016/2017 ikaenda kwa Mohamed Hussein Tshabalala mlinzi wa kushoto wa Simba na timu ya taifa.


Manchester United wabeba ubingwa na kukata tiketi ya Champions League

$
0
0

Ilikuwa ni kufa au kupona kwani United wasingeshinda mchezo wao wa fainali dhidi ya Ajax baasi wangepoteza nafasi ya kushiriki michuano ijayo ya champions league.

Japokuwa Ajax walionekana kama wanaweza kufanya jambo la tofauti katika mchezo huo kutokana na walivyoonekana kuwashika Manchester United lakini uzoefu uliwamaliza. United wamechukua kombe hilo na limemfanya Jose Mourinho sasa kuwa na vikombe vinne vikubwa michuano ya Ulaya.

Dakika ya 18 tu mchezaji ghali kwa Manchester United kiungo Paul Pogba alizifumania nyavu za Ajax na kuufanya mchezo huo kwenda half time United wakiongoza kwa bao moja, Pogba hii ni mara yake ya kwanza kufunga mechi mbili mfululizo tangia afanye hivyo mwezi April mwaka jana.

Kipindi cha pili Ajax walionekana kupambana wakijaribu kusawazisha bao hilo lakini dakika ya 48 tu waliruhusu tena nyavu zao kuguswa na Mualmernia Henrikh Mkhtaryan baada ya kuandika bao la pili, Mkhitaryan mabao 6 ya mwisho kuifungia United yote ameyafunga katika michuano hii.

Mchezo huo ulimalizika hivyo na kuifanya United kwa mara ya kwanza kushinda kombe hilo ambalo lilikuwa ndio kombe pekee ambalo hawajawahi kuchukua. Matokeo hayo pia yanaipa Manchester United tiketi ya kushiriki champions league msimu ujao.

 

Video: Jibu la Msuva baada ya kuulizwa kama ataondoka Yanga

$
0
0

Mfungaji bora wa Yanga na VPL Simon Msuva amesema kuna ofa nyingi zinazomtaka kuondoka kwenye klabu hiyo lakini kwa sasa bado anamkataba na Yanga kwa hiyo suala la yeye kuihama klabu yake lipo mikononi mwa viongozi wa timu pamoja na manager wake.

“Ofa nyingi zimekuja lakini mimi bado nina mkataba na Yanga lakini suala hilo nauachia uongozi wangu pamoja wa Yangana manager wangu kama Mungu atakua amepanga niondoke nitaondoka kama itakuwa bado basi nitaendelea kuwepo.”

Msuva pia amesema, jeraha alilopata wakati anaitumikia timu yake ilipocheza na Mbeya City lilimrudisha nyuma na kumpunguza makali ya kumshinda mshindi mwenzake wa tuzo ya ufungaji bora ambaye ni Abdulrahman Musa wa Ruvu Shooting.

“Majeraha yamenifanya nishindwe kufunga zaidi na kumzidi mpinzani wangu, nilikua naumia kukosa mechi lakini mechi mwisho ya mwisho nilifosi kwa sababu ya kutaka kujiweka sehemu nzuri mimi na klabu yangu.”

“Simon Msuva anaangaliwa na watu wengi kwa hiyo sioni kama kilichotokea uwachani wakati tunavheza na Mbao ndio sababu ya mimi kushindwa kupata tuzo ya mchezaji bora, refa hakupigwa zaidi ya sisi kumfuata na kudai haki yetu.”

“Mimi ninamalengo ya kushinda tuzo hadi nje ya nchi kwa hiyo sifikirii tuzo za hapa tu nataka kupambana kama Mbwana Samatta na kushinda tuzo nje ya nchi.”

Mchezo Wa NBA Afrika Kupigwa Tena. Makampuni Yajitokeza

$
0
0

Chama cha mpira wa kikapu chini Marekani (NBA) and pamoja na chama cha wachezaji wa mpira wa kikapu nchini Marekani (NBPA) wametanganza kuwa makampuni ya Kwesé Sports, Ford Motor Company kutoka Afrika Kusini, Castle Lite, General Electric, Solektra International, Marriott International pamoja na 947 kuwa watakuwa sehemu ya NBA Africa Game 2017.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa mchezo wa NBA unaofanyika Afrika maarufu kama NBA Africa game kuwa na idadi hii kubwa ya wenza washiriki tangu uanze kufanyika.

Mchezo huu ambao utakuwa wa pili kufanyika Afrika utafanyika siku ya Jumamosi tarehe 5, aktika uwanja wa Ticketpro Dome huko Johannesburg, South Africa.

NBA Africa Game 2017, ambao utafanyika ikiwa ni baada ya uzindiuzi wa awamu ya 15 ya mpira wa kikapu bila mipaka which [Basketball without Borders (BWB)] kwa Africa, utafanyika tena ukiwahusisha wachezaji watakaogawanywa kwenye timu mbili ambazo Team Africa vs Team World na utachezwa ikiwa ni katika kuwaunga mkono UNICEF, Nelson Mandela Foundation na shirika la SOS Children’s Villages South Africa (SOSCVSA).

Team Africa, ambayo itakuwa na wachezaji Bismack Biyombo (Orlando Magic; Democratic Republic of the Congo) pamoja na Emmanuel Mudiay (Denver Nuggets; Democratic Republic of the Congo), itajumuisha pia wachezaji kutoka Afrika na wale wenye asili ya Afrika. Team World, ambayo itakuwa na CJ McCollum (Portland Trail Blazers; U.S.), itakuwa na ongezeko la wachezaji kutoka nchi nyingine duniani.

Taarifa zaidi juu ya vikosi kamili, makocha na wachezaji wengine wa zamani wa NBA itatangazwa siku nyingine zijazo.

 

Singida United inaendelea kutisha kwenye usajili

$
0
0

Singida United kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram wameripoti kuwa kwenye mazungumzo ya mwisho na mchezaji wa Mbeya City Kenny Ally ili ajiunge na klabu hiyo pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa.

Klabu hiyo ambayo imepanda daraja kucheza VPL msimu ujao ilianza kusajili wachezaji wa mimataifa lakini baada ya ligi kumalizika wameanza kumalizana na wachezaji wa ndani kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.

Kenny Ally ametajwa kwenye kikosi bora cha msimu uliopita 2016/17 baada ya kuonesha kiwango cha juu akiwa na Mbeya City.

Simba acheni “unafiki”, jifunzeni.

$
0
0

Binafsi nilikuwepo katika utoaji wa tuzo za Vodacom Premier League msimu huu na kushuhudia Mohameid Hussein mlinzi wa Simba akitangazwa kama mchezaji bora wa Vpl msimu wa 2016/2017.

Roho yangu ilisononeka baada ya kuona waajiri wake wakiitosa tuzo hiyo kwa kutohudhuria na huku wakiwabana wachezaji wao kutoenda katika usiku huo maalum kwa ajili ya vilabu na wachezaji.

Baba mzazi wa Mohameid Hussein alikuwepo kuonesha mapenzi kwa mwanae na akaenda kumpokelea tuzo, tukio hili lilinigusa moyo wangu na kuamini kweli mzazi ni mzazi na Simba hawana mapenzi na Tshabalala kama baba yake.

Kuna maisha ya mchezaji kama mchezaji, na kuna maisha ya timu kiujumla na pia kuna mambo wazungu wanaita “one time event” yaani hutokea mara moja tu katika maisha na likipita halijirudii.

Tuzo ya Tshablala na Kichuya ni tukio muhimu sana kwao kama wachezaji na vijana wanaokua kisoka, kuwazuia wasiende ni kuwarudisha nyuma kisoka kwani uwepo wao pale tu unawatia hamasa kufanya mambo makubwa zaidi.

Kweli Simba wana madai yao kwa TFF wanaodai wamewaonea lakini hao ni Simba na madai yao na walipaswa gomea zawadi zao wao kama timu lakini wachezaji wao walipaswa kupata ruhusa kwenda kupokea au kushiriki tukio hili muhimu.

Sina uhakika kama mzazi wa Mohameid Hussein amejisikiaje baada ya kuona waajiri wa kijana wake wamemtosa hawajaja hata kumuwakilisha amekuja yeye kama baba utadhani lile ni tukio la kifamilia.

Kuonewa ndio mugomee kila kitu kuhusu soka? Kama ni hivyo wangegomea baasi na michezo ya ligi kuu iliyopigwa baada ya wao kuona wanaonewa,huwezi kukataa kushiriki hafla ya wadhamini wa ligi na chama cha soka na huku ligi yao munacheza ni unafiki mkubwa sana.

Ushauri wangu kwa Simba hata kama munaitwa wa “mchangani” lakini punguzeni hayo mambo ya “umchangani” angalieni wapi mumekosea na tumieni makosa yenu kama changamoto kufika mutakapo.

 

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>