Uwanja wa Millenium Stadium umekuwa gumzo sana siku za usoni kwani uwanja huo ndio uwanja ambao mtanange mkubwa fainali ya UEFA kati ya Juventus na Real Madrid.
Millenium Stadium ambao siku hizi unaitwa Principality Stadium kutokana na sababu za masuala ya wadhamini, una uwezo wa kuingiza mashabiki 74,500.
Uwanja huu ulianza kujengwa mwaka 1997 na ni uwanja wa nyumbani wa timu ya rugby ya Wales, na ilipofika mwaka 1999 uwanja huu ulikamilika na mchezo wake wa kwanza kuchezwa ulikuwa ni kati ya Wales na South Africa.
Uwanja wa Millenium Stadium sio mgeni sana katika masuala ya soka kwani wakati flani uwanja wa Wembley ulipokuwa ukifanyiwa matemgenezo, Millenium Stadium ulitumika kuchezea fainali za FA.
Miezi mitatu kabla ya fainali hii ya champions league tayari hotel za mji wa Cardiff ambako ndipo uwanja huu zilipo zilishajaa na watu walishaweka vyumba kwa ajili ya mchezo huu.
Real Madrid sio wageni katika mji huu wa Cardiff kwani mwaka 2014 walishawahi kucheza fainali ya super cup katika mji wa Cardiff na kubeba kombe hilo wakiifunga Sevilla ya nchini Hispania kwa mabao ya Cristiano Ronaldo.
Kutokana na tishio la ugaidi linaloendelea kuitesa dunia,wasimamizi wa Millenium Stadium wameoma ni vyema uwanja huo ukachezwa huku paa lake likiwa limefungwa.
Hii inatokana na mbinu mpya ambayo magaidi wamekuwa wakitumia kulipua sehemu zenye msongamano wa watu kwa kutumia ndege zilikazo bila rubani.
Kwa video na kuona jinsi Millenium Stadium unavyojifunga unaweza kuingia katika YOU TUBE na kusbscribe channel.yetu ya Dauda Tv na kuangalia page yetu ya Instagram.