Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Poleni sana mashabiki wa Arsenal kwa hili.

$
0
0

Hakika ni neno “pole” tu ndilo linalofaa kuwapa mashabiki wa Arsenal kwani pamoja na vita waliyojaribu kupigana na kupiga kelele mtandaoni kwa muda mrefu lakini mambo yameenda tofauti na walivyotaka.

Kila mshabiki wa Arsenal alikuwa na kauli moja tu “Wenger Out” lakini sasa ni “Wenger In” kwani kocha huyo haendi popote na atabaki katika klabu hiyo kwa miaka miwili zaidi hata kama mashabiki hawapendi.

Kuna wengine walidhani labda ili kulinda heshima yake Wenger angekataa mkataba mpya na kuondoka bila kutimuliwa, lakini mzee huyo wala hajasikia na amekubali ofa ya mkataba mpya wa miaka miwili.

Taarifa zinadai siku ya Jumanne mmiliki wa klabu ya Arsenal bwana Stan Kroenke alikutana na Arsene Wenger na kukubaliana juu ya mkataba huo ambapo taarifa rasmi kutoka klabuni zilipangwa kutolewa siku ya Jumatano.

Wenger anapewa mkataba mpya baada ya Arsenal kubeba ubingwa wa FA lakini wakimaliza nje ya top four kwa mara ya kwanza toka mwaka 1996 na wamiliki wa klabu hiyo wanaamini Wenger ndio mtu pekee ambaye atawarudisha juu.

 


Klabu za Epl zajazana kumi bora ya klabu zenye thamani kibiashara Duniani.

$
0
0

Utafiti uliofanywa na wataalamu wa masula ya kibiashara katika soka,umegundua kwamba japokuwa klabu ya Manchester United haikuwepo katika michuano ya Champions League msimu uliopita lakini thamani ya klabu hiyo kibiashara ni kubwa kuliko timu yoyote duniani.

Thamani ya mabingwa hao wa Europa League ni £3.07bn ikiwa ni juu ya mabingwa wa Champions League ambao thamani yao kibiashara ni £2.97bn, Real Madrid nao wako juu ya Barcelona walioko nafasi ya tatu wakiwa na thamani ya £2.76bn.

Nafasi ya nne ni klabu ya Bayern Munich ambao wenyewe ni mabingwa wa soka wa nchini Ujerumani na wana thamani ya £2.44bn wakifuatiwa na Manchester City wenye thamani ya £1.97bn.

Arsenal wako nafasi ya sita wakiwa na thamani ya £1.95bn wakifuatiwa na mabingwa wapya wa soka nchini Uingereza Chelsea ambao wenyewe wana thamani ya £1.59bn.

Liverpool wenyewe wako nafasi ya nane wakiwa na thamani ya £1.33bn na Juventus wako nafasi ya tisa na thamni ya £1.21bn huku Tottenham wakimaliza 10 bora wakiwa na thamani ya £1b.

 

Real Madrid na Manchester United waoneshana ubabe kifedha.

$
0
0

Hiki ni kiburi kikubwa ambacho United wameamua kuwaonesha Real Madrid, ni sawa na kusema United hawataki chochote kile toka kwa Real Madrid bali wanataka waachane na wachezaji wao.

Dau la £60m ambalo Real Madrid wamelituma kwa Manchester United kumtaka David De Gea ni kubwa sana haswa kwa nafasi anayocheza David De Gea na ni wazi hii ilikuja kama bahati.

Lakini huwezi kuamini kwani Manchester United wamesema hapana na hawako tayari kupokea kiasi hicho cha fedha kwani David De Gea hauzwi kwa kiasi chochote kile na mpango wao ni abaki klabuni hapo.

Haitakuwa rahisi kwa Real Madrid kukubali kushindwa kwani ni timu ambayo mara zote imekuwa kama inahitaji mchezaji yoyote yule huwa wanamchukua hata kwa gharama kiasi gani.

Na David De Gea amekuwa mchezaji ambaye wanamtaka sana na kwa hakika watarudi tena na ofa mpya ambayo wanahisi inaweza kuishawishi United kumuuza De Gea.

 

Tetesi za usajili: Mastaa wa kimataifa kutemwa Simba

$
0
0

Na Zainabu Rajabu

KLABU ya Simba inatarajia kuwatema baadhi ya mastaa wake wa kimataifa ili nafasi zao kuchukuliwa na wachezaji wa Yanga, Donald Ngoma na Haruna Niyonzima.

Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa wachezaji hao wanakaribi kuanguka wino wa miaka miwili kwenye klabu hiyo yenye makao yake Msimbazi, Dar es Salaam.

Shaffihdauda.co.tz. imezungumza na kiongozi wa ya Simba kwa sharti la kutotajwa jina, ambaye amesema klabu hiyo inatarajia kuwanasa Haruna Niyonzima na Donald Ngoma kabla ya mwezi Julai mwaka huu.

“Tuko mbioni kukamilisha usajili wa Ngoma na Niyonzima ambao wanaweza kusaini miaka miwili, tunaendelea kupambana na kama wakisaini itabidi tupunguze wachezaji wakimataifa tuliokuwa nao msimu uliopita.”

Simba imekuwa ikiwawania Ngoma na Niyonzima tangu msimu uliopita ambapo sasa imeonekana kukaribia kuwanasa wote wawili kutokana na mikataba yao kufikia ukingoni.

Wekundu wa msimbazi hao wamemaliza Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu wakiwa nafasi ya pili nyuma ya Yanga baada ya kuvuna pointi 68 kwenye michezo 30 waliyocheza.

Sheria za Ligi Kuu ya Tanzania Bara zilizowekwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zinaruhusu klabu za Ligi Kuu kusajili mwisho wachezaji saba wa kigeni. Hadi sasa timu hiyo ina wachezaji saba wa kigeni iliyowatumia kwenye msimu uliopita ambao ni kipa Daniel Agyei (Ghana), Method Mwanjale (Zimbabwe), James Kotei (Ghana), Janvier Bokungu (Congo DRC), Juuko Murshid (Uganda), Fredrick Blagnon (Ivory Coast) na Laudit Mavugo (Burundi).

Himid Mao kuhusu majaribio aliyofanya Ulaya na mkataba wake na Azam

$
0
0

Kiungo wa ulinzi wa Azam FC na timu ya taifa Himid Mao amesema alifanya majaribio aliyokwenda kufanya Denmark kwenye klabu ya Randers yalikwenda vizuri na anachosubiri sasa ni pande mbili za vilabu kufikia makubaliano ili kufanya maamuzi.

“Nilikuwa nafanya mazoezi na timu na nilifanikiwa kucheza mechi pia, wameshaniona kilichobaki ni wao kumalizana na uongozi wa Azam ili niweze kujiunga nao.”

“Mawasiliano na majadiliano bado ya yanaendelea wakala wangu ananipa ripoti kwa kila hatua inayopigwa watanzania wawe na subira chochote kinaweza kutokea.”

“Walikuwa wananifuatilia kwa muda mrefu haikuwa kama bahati, sports director wao alikuwa ananifuatilia kuanzia kwenye mechi za Azam na timu ya taifa kwa hiyo ni watu ambao wananifahamu vizuri.”

“Mkataba wangu na Azam unamalizika mwezi Novermber mwaka huu, bado tunaendelea na mazungumzo lakini kuna ofa zipo kutoka vilabu mbalimbali, naangalia ofa za nje halafu nitalinganisha na Azam halafu nitachagua niende wapi.”

Himid amekuwa katika kiwango cha juu katika misimu ya hivi karibuni kitu kinachovivutia vilabu vingi vya ndani na vya nje ya nchi kutaka kumsajili nyota huyo aliyejenga jina lake akiwa na Azam.

‘Uwezekano wa kuondoka au kubaki Azam upo’– Kawemba

$
0
0

Kufuatia tetesi za kuondoka kwa mtendaji mkuu wa klabu ya Azam FC Saad Kawemba, amevunja ukimya na kusema hadi sasa yeye bado ni mtendaji wa klabu hiyo licha ya mkataba wake kuelekea ukingoni.

Kawemba amesema wapo kwenye mazungumzo kuhusu mkataba mpya kwa hiyo chochote kinaweza kutokea kubaki au kuondoka Azam.

“Mkataba wangu unaenda mwisho lakini sijapokea barua kutoka kwa mwajiri wangu ya kuniambia hawataendelea na mimi. Tupo kwenye mazungumzo, matumaini ya kuendelea yanaweza yakawepo na yasiwepo vilevile kwa sababu bado hatujamaliza mazungumzo”.

“Matokeo msimu huu hayakuwa mazuri sana kwa upande wetu kwa hiyo ndio maana presha imekuwa kubwa pengine labda CEO aondoke.”

Hivi karibuni zilisambaa taarifa kwenye mitandao ya kijamii kwamba, Kawemba ameachana na klabu ya Azam.

UCL Final: Kwanini Madrid italipa zaidi ya billion 200 kwa kutwaa Champions League vs Juve

$
0
0

Yamebaki masaa takribani 48 kabla ya referee wa kijerumani Felix Brynch hajapuliza kipenga cha kuashiria kuanza kuanza kwa mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya msimu wa 2016/17. 


Jijini Cardiff, Real Madrid watakuwa wanautafuta ubingwa wa 12 wa ulaya wakati watakapopambana na Juventus – lakini pia ubingwa huu wataigharimu klabu zaidi ya billioni 200 za kitanzania kwa ajili ya bonasi za kulipa wafanyakazi wao. 

Haijawahi kutokea katika historia ya kizazi hiki kwa timu yoyote kuweza kutetea ubingwa wa ulaya, lakini vijana wa Los Blancos sasa wana sababu zaidi ya moja kuiweka rekodi mpya. 

Nahodha Sergio Ramos na wachezaji wenzake wakubwa katika klabu hiyo walicheza kamari wakati walipojadili juu ya maombi ya bonasi, na klabu ilikubali maombi yao na sasa wanahitaji kuifunga Juve ili warudi Madrid wakienda bank wanacheka.

Wakati ilipoonekana kuna uwezekano wa Real kushinda makombe mawili msimu huu, ilkubaliwa kwamba kila mchezaji atapokea 1.5 millioni euros kwa kufanikisha mafanikio hayo. 

Msimu uliopita, klabu ililipa jumla ya 32 million euros kwenye bonasi za wachezaji na benchi la ufundi, hii ilitokana na ushindi wa Champions League na kila mmoja alivuta takribani kiasi cha  700,000 euros per na 100,000 euros kwa kuifunga Barcelona pale Camp Nou katika El Clasico.

Wakati huu, Los Blancos chini Florentino Perez wanatarajiwa kulipa kiasi cha zaidi ya 80 million euros ambazo kwa pesa ya madafu ni zaidi ya 208 billion – lakini tu endapo wataifunga Juventus katika mchezo wa fainali ya Mabingwa wa ulaya usiku wa Jumamosi ya tarehe 3 June. 

Rasmi: Azam wametangaza kuachana na C.E.O wao Saad Kawemba

$
0
0

Azam FC imetangaza rasmi kuachana na Afisa Mtendaji Mkuu wake, Saad Kawemba, baada ya kumaliza mkataba wake.

Azam FC pia imefanya mabadiliko ya mfumo wa kiuongozi, Cheo cha C.E.O kimefutwa, badala yake atabaki General Manager.

Aidha, sera ya usajili inabadilika ambapo watatumia zaidi njia kuwapandisha wachezaji kutoka kikosi B kinacholelewa kwenye Akademi ya klabu hiyo.


Tetesi za usajili: Barthez, Oscar Joshua, safari imeiva Yanga

$
0
0

KIPA mkongwe wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ na beki wa pembeni wa timu hiyo, Oscar Joshua ni kati ya wachezaji watakaokuwepo kwenye kikosi cha Singida United katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara, kama hawatakuwa katika kikosi hicho basi safari yao kwa upande wa Yanga itakuwa imeishia hapo.

Barthez na Joshua ni kati ya wachezaji ambao hawakuwa na nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza cha kocha Mzambia, George Lwandamina katika msimu uliopita wa ligi kuu, wachezaji hao wote bado wana mikataba ya mwaka mmoja wa kuichezea Yanga kwenye msimu ujao wa ligi.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu hiyo, wachezaji hao wataondolewa Yanga na kupelekwa Singida inayofundishwa na Hans van Pluijm aliyekuwa anaifundisha Yanga kabla ya nafasi yake kuchukuliwa na George Lwandamina.

Mtoa taarifa huyo amesema, wachezaji hao walikuwepo kwenye orodha ya wachezaji watakaochwa katika msimu ujao, lakini kutokana na mikataba yao kutomalizika watatolewa kwa mkopo.

“Barthez na Joshua hawana nafasi ya kucheza katika kikosi cha Lwandamina na pia hana mipango nao, hivyo kama uongozi tumeona tuwatoa kwa mkopo.

“Tutawatoa baada ya kufanya mazungumzo na uongozi wa Singida na kukubali kuwachukua, hivyo tumeona tuwaachie waende huko wakacheze,”alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa Barthez kuzungumzia hilo alisema kuwa: “Bado sijapata taarifa rasmi ya kupelekwa kwa mkopo, ni tetesi ninazozisikia pekee kama ulivyosikia wewe ni vema tukasubiria kwanza kabla ya mimi kuongea chochote.

Exclusive: Dauda TV imemnasa mchezaji wa zamani wa Everton

$
0
0

Dauda TV imemnasa mchezaji wa zamani wa Everton Leon Osman ambaye kwa sasa ni balozi wa klabu hiyo, Osman kwa sasa yupo nchini ikiwa ni utangulizi kabla ya ujio wa klabu ya Everton nchini mwezi July, 2017.

Amezungumza mambo mengi kuhusu wakati wake akiwa kama mchezaji wa Everton lakini pia hakuacha kugusia kuhusu ziara ya klabu hiyo nchini na Afrika kwa ujumla.

Amesema ujio wao Tanzania utawasaidia katika kujitangaza na kutengeneza mashabiki wengi katika bara la Afrika.

“Ni hatua nzuri kwa klabu kujitangaza duniani hususan kwenye bara la Afrika na miaka michache ijayo Everton itakuwa ni miongoni mwa vilabu maarufu duniani.”

Kuhusu klabu ambayo ilimpa wakati mgumu kipindi anacheza EPL, Osman amesema alikuwa anafurahia zaidi kucheza dhidi ya West Ham United.

“Kuna vilabu vingi ndani ya Premier League ambavyo vinaupinzani mkubwa sana mkicheza dhidi yao lakini nilikuwa nina-enjoy kucheza na West Ham United kwenye uwanja wao wa nyumbani kwa sababu nilikuwa nafunga magoli dhidi yao.”

 

“Nilikuwa pia napenda kucheza kwenye uwanja wa White Hart Lane, lakini nilikuwa napenda ushindani uliokuwepo dhidi ya West Ham.”

Balozi huyo wa Azam amesema, wakati wa uchezaji wake Ashley Cole alikuwa anampa changamoto ukilinganisha na wachezaji wengine aliokuwa anakutana nao.

“Mlinzi wa zamani wa kushoto wa England na vilabu vya EPL vya Arsenal na Chelsea Ashley Cole ni mchezaji ambaye alikuwa ananipa changamoto nilipokuwa nikikutana nae, alikuwa ana nguvu na kasi.”


‘Simba inapaswa kuachana na Omog na kumtazama mkali huyu wa mbinu’

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

NAAMINI moja kati ya mabadiliko muhimu katika kikosi cha Simba SC ni kuachana na kocha wake Mcameroon, Joseph Omog.

Licha ya kuisaidia Simba kushida ubingwa wa kombe la FA na kushindwa kwa tofauti ya magoli na mabingwa Yanga SC katika ligi kuu Tanzania Bara 2016/17, makosa binafsi ya Omog yaliigharimu sana timu hiyo na yalikaribia kuwaangusha katika fainali ya FA vs Mbao FC.

Omog inawezekana alifanikiwa kama kocha wakati alipoisaidia AFC Leopard ya Congo Brazaville kushinda ubingwa wa Caf Confederation Cup 2012, na akashinda ubingwa wa VPL 2013/14 akiwa kocha wa Azam FC, lakini Mcameroon huyo ameonyesha wazi udhaifu wa kimbinu huku suala la ufundi likinipa shaka mara kwa mara.

Kupoteza uongozi wa 2-0 walioupata Azam FC vs El Merreikh ya Sudan katika uwanja wa Azam Complex kisha kuondolewa katika Caf Champions League kwa jumla ya magoli 3-2 baada ya pambano la marejeano jijini, Khartoon Machi, 2015 nitaendelea kuamini kulisababishwa na mabadiliko ya kocha huyo ambaye alimtoa mshambulizi Kipre Tchetche katika kipindi cha pili.

Kipre aliwamiliki walinzi wa El Merreikh ambao waliogopa kusogea mbele wakimuhofu Muivory Coast huyo ambaye alipotolewa Azam FC wakapigwa presha kisha wakapoteza mwelekeo na kuchapwa 3-0 na kuondolewa katika michuano.

Mapambano matatu vs Hans, Lwandamina 

Ndiyo, Simba haikupoteza mchezo wowote dhidi ya ‘watani’ wao wa jadi Yanga katika michezo miwili waliyokutana katika ligi kuu na mmoja wa Mapinduzi Cup 2017  lakini kuna sababu kadhaa za kimsingi zinazonifanya niamini kocha huyo hana uwezo wa kuifanya Simba ipate ubingwa wa VPL na kuleta changamoto katika michuano ya Caf Confederation Cup mwaka ujao.

Mfano, katika mchezo wa Oktoba Mosi, 2016 ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana 1-1 vs Yanga. Watu wanaweza kuendelea kumlaumu aliyekuwa mwamuzi wa mchezo huo Martin Saanya lakini kwa namna Simba ilivyocheza katika eneo la ulinzi na jinsi walivyopanga mashambulizi ni wazi hawakuwa bora kuliko Yanga.

Upangaji mbovu wa kikosi 

Kuwaacha nje ya kikosi walinzi kama Abdi Banda, Mganda, Juuko Murishid na kumuanzisha Novaty Lufunga lilikuwa ni kosa la kiufundi na liliwagharimu.

Kilichowanusuru Simba na kichapo ni kuwahi kuchoka kwa viungo wa kati wa Yanga lakini bado mbinu zao ndogo zilishindwa kuwapatia nafasi ya kutengeneza magoli na wakasubiri hadi dakika tatu za mwisho kusawazisha kwa mpira wa kona ya moja kwa moja iliyopigwa na Shiza Kichuya.

Kikosi cha Mholland, Hans van der Pluijm kilikuwa katika uchovu baada ya kucheza mfululizo kwa miezi zaidi ya 24 (kuanzia Kagame Cup, Julai, 2015 hadi Makundi Caf Confederation Cup , Septemba, 2016.) Hivyo wachezaji wake wengi walikuwa wakicheza huku wamechoka.

Mashabiki wa Simba waling’oa viti wakati ule na kusahau mapungufu muhimu katika timu yao. Waliamini wana timu iliyokamilika. Game ya nusu fainali Mapinduzi Cup 2017 ilimalizika kwa suluhu-tasa.

Yanga ilikuwa chini ya Mzambia, George Lwandamina tena akiwa ndani ya mwezi wake wa kwanza tangu alipopewa kibarua kilichokuwa kimeachwa na Hans.

Lwandamina hakuwa na kikosi imara kutokana na wachezaji wake wengi kuwa na majeraha lakini aliweza kumtoa jasho Omog na kustahimili pambano ambalo wengi waliamiani Simba ingeshinda rundo la magoli hasa ukizingatia Yanga ilikuwa imetoka kuchapwa 4-0 na Azam FC siku mbili nyuma.

Ushindi wa Mbinde 2-1 Februari, 2017 dhidi ya mahasimu  wao Yanga bado hauwezi kuficha madhaifu ya kocha Omog. Yanga haikuwa na makali lakini walimudu pambano kwa robo tatu ya mchezo.

Makosa yaleyale aliyofanya Omog katika mchezo wa mzunguzo wa kwanza akayarudia tena. Licha ya kucheza kwa dakika zaidi ya 50, Lufunga alionekana wazi kwenye nafasi ya beki wa kati hucheza akiwa na mashaka makubwa.

Lufunga si mzuri katika kucheza ‘tackle’ na anapojaribu kufanya hivyo hucheza faulo. Kasi yake pia ya kukimbia si nzuri ndiyo maana alionekana ‘kumilikiwa’ na Mzambia, Obrey Chirwa. Wakati mechi ikiendelea, Omog akamtoa Lufunga nafasi yake ikachukuliwa na kiungo wa kati nahodha wa timu, Jonas Mkude.

Mcongoman Besala Bokungu akaenda kucheza kati na Banda yalikuwa ni mabadiliko mazuri hasa ukizingatia Lufunga alikuwa na kadi ya njano. Kutokana na kiwango bora kabisa cha Muzamiru Yassin alichokionyesha kabla ya mchezo huo vs Yanga, uamuzi wa Omog kumpeleka Muzamiru katika beki namba 2 ulikuwa ni wa ajabu sana kwa maana aliwaacha Mghana, James Kotei na Mkude katika dimba la kati.

Viungo hao wawili si watengenezaji wa nafasi za kufunga. Kama ni ‘bahati’ basi ilikuwa kwa Omog ila mabadiliko yake ya kumtoa Lufunga na kumpa nafasi Mkude yalipaswa kumbakisha Muzamiru katika eneo la kiungo na si kumpeleka katika beki ya kulia.

Omog alinufaika sana na mbinu ya kushambulia pembeni, lakini mabadiliko yake ya kiufundi mara kwa mara yamekuwa si sahihi. Kwa namna walivyokuwa kikosi cha Omog kisingeweza kufunga magoli mengi kwa sababu alishindwa kutengeneza safu ya kwanza na ile ya pili ya washambuliaji kati ya Ibrahim Ajib, Mrundi, Mavugo, Muivory Coast, Blagnon na Juma Liuzio.

Vs Mbao FC

Kwenye mchezo wa fainali ya FA Cup, Omog aliamtumia Kotei na Mganda, Juuko Murshid katika beki ya kati. Jambo hilo liliwafanya Simba kuwa na nguvu ya ziada na ufundi katika safu yake ya ulinzi.

Mbinu hiyo ya kiufundi iliweza kuleta matunda kwa sababu mwisho wa dakika 90′, Omog aliweza kupata matokeo aliyostahili-kikosi chake kutoruhusu goli. Kotei aliweza kuwaonyesha watazamaji ni jinsi alivyokuwa bora katika beki ya kati, huku akiwa kiunganishi kizuri cha safu ya ulinzi na kuwa msaada mkubwa katika ngome ya mabeki wanne.

Lakini kama kocha angekuwa amejipanga vyema angempanga Kotei katika eneo la kiungo na kumpa nafasi Abdi Banda kucheza na Juuko katika beki ya kati kwa sababu kujipanga vyema katika safu ya ulinzi ni vizuri zaidi kama timu itamtumia Kotei kwenye sehemu ya kiungo kama kweli Omog alitaka kuona timu yake ikienda mbele kushambulia, na hili litamfanya Mkude kupoteza nafasi yake kikosini.

Kwa mechi kama ile ya fainali ambayo timu inahitaji kufunga japo goli moja, Kotei angeweza kuipatia Simba nguvu kubwa ya kushambulia ikianzia kwenye idara ya kiungo. Omog alishindwa kimbinu na kocha wa Mbao, Mrundi, Ettiene Ndayiragije.

Lakini kama kocha angekuwa amejipanga vyema angempanga Kotei katika eneo la kiungo na kumpa nafasi Abdi Banda kucheza na Juuko katika beki ya kati kwa sababu kujipanga vyema katika safu ya ulinzi ni vizuri zaidi kama timu itamtumia Kotei kwenye sehemu ya kiungo kama kweli Omog alitaka kuona timu yake ikienda mbele kushambulia, na hili litamfanya Mkude kupoteza nafasi yake kikosini.

Kocha huyo wa Mbao aliingiza timu yake kuanza mchezo kwa stahili ya kujilinda huku wakishambulia kwa kustukiza. Aliwapanga walinzi wanne, viungo watano na kumuacha mshambulizi mmoja mbele.

Omog ambaye aliwapanga washambuliaji watatu mbele, viungo watatu na walinzi wanne alishuhudia timu yake ikimiliki mpira kwa kiasi kikubwa lakini hawakuwa na mbinu za kupeleka mipira sahihi kwa washambuliaji.

Mbao walikuwa wagumu katikati ya uwanja na ili Simba ipitishe mipira walimuhitaji kiungo kama Kotei ambaye ni mchangamfu, mwenye ubunifu na pasi za uhakika. Mkude ni mzuri lakini stahili yake ya uchezaji inachelewesha sana ushindi huku akihatarisha usalama wa timu yake kutokana na upigaji wake wa ‘pasi mkaa.’

Ettiene alipogundua Simba haina makali akawaruhusu wachezaji wake kushambulia mara baada ya kuanza kwa kipindi cha pili. Jambo hilo liliwafanya Simba kuwa katika presha. Kilichowaangusha Mbao ni kutokuwa na wachezaji wengi wenye maarifa binafsi. Ettiene ameijenga timu yake kucheza kitimu huku ikiongozwa na mbinu zake ndiyo maana walipoona zimesalia dakika 15 kabla ya kumalizika kwa dakika 90′ akairudisha timu yake kucheza mchezo wa kujilinda kwa tahadhari ya hali ya juu.

Akafanikiwa kumaliza dakika 90 kwa suluhu-tasa. Alikuwa makini pia katika ufanyaji wake wa mabadiliko na hakupoteza heshima kwa wapinzani licha ya kuonekana kuwamudu.

Blagnon alipofunga goli la uongozi upande wa Simba dakika ya 109′, Etienne akaamua kuwapa uhuru wachezaji wake kushambulia na baada ya kusawazisha goli hilo wakarudi kujilinda kwa lengo la kuivusha mechi hadi katika hatua ya mikwaju ya penalti.

Kama kocha huyo wa Mbao FC angekuwa na kikosi chenye ubora mpana angefanikiwa zaidi lakini Omog ameendelea kudhihirisha si kocha mwenye mbinu bora zaidi hasa katika michezo muhimu.

Nadhani Simba inahitaji nyongeza ya wachezaji lakini kabla  inapaswa kumuondoa Omog na kumpa kazi mmoja kati ya makocha Mecky Mexime ama Etienne ili kuungana na Mganda, Jaclson Mayanja makocha ambao wana mbinu na ufundi huku vikosi vyao vikicheza vile wanavyotaka.

Shaffih Dauda vs Edgar Kibwana kuhusu Azam kumtema Saad Kawemba

$
0
0

Juni 1, 2017 Azam ilitoa taarifa rasmi kuhusu kuachana na mtendaji wao mkuu Saad Kawemba baada ya mkataba wake kumalizika na uongozi kuamua kuachana nae pamoja na kuifuta nafasi ya mtendaji mkuu (C.E.O) kwenye klabu yao.

Mijadala imekuwa mingi na mikali kuhusu hatua ya Azam kuachana na Kawemba na kuifuta nafasi aliyokuwa anaitumikia, ndani ya Sports Extra kulikuwa na mjadala mkali ambapo wachambuzi wa kituo hicho Shaffih Dauda na Edgar Kibwana nao walipishana mitazamo kuhusu hatua ya Azam.

Kibwana yeye bado anaona kuna ukakasi katika uamuzi uliofanywa na Azam kuhusu kuifuta nafasi ya mtendaji mkuu huku pointi yake ya msingi ikiwa ni kwamba, wakati Azam wanamwajiri Abdul Mohamed kama General Manager  hawakujua kama tayari walikuwa na C.E.O? Hakuna tofauti ya kiutendaji kati ya C.E.O na General Manager? Majukumu aliyokuwa anayatekeleza Kawemba yatafanywa na nani?

“Napata mashaka na utendaji wa Azam FC, sijui wanata nini. Wamemuondoa Saad Kawemba kama C.E.O wa Azam FC na kukifuta kabisa cheo hicho, wakati wanamuajiri Abdul Mohamed kama General Manager hawakutambua kuwa kulikuwa na C.E.O? Walihitaji nini kutoka kwa Kawemba na Abdul?, “ amesema Edgar Kibwana.

Kwa upande wake Shaffih Dauda yeye hakuwa tofauti na uamuzi uliofanywa na Azam, amesema kuondoka kwa Kawemba ni sawa na kumpa meno Abdul Mohamed kwa sababu awali majukumu ya wawili hao yalifanana na kulazimika kugawana ili tu kila mmoja aonekane anawajibika.

“Mimi nimewaelewa sana Azam kwa kumuondoa Saad Kawemba pamoja na kuifuta nafasi ya C.E.O ndani ya klabu yao kwa sababu Kawemba na Abdul Mohamed majukumu yao yalikuwa yanafanana.”

“Ilibidi wagawane majukumu ili kila mmoja aonekane anafanya kazi, Kawemba akawa yupo zaidi kwenye mambo ya kiutawala halafu Abdul akabaki kupambana na mambo yanayoihusu timu tu lakini kiuhalisia ni majukumu ambayo yangeza kufanywa na mtu mmoja.”

“Kuondoka kwa Saad Kawemba ni sawa na kumpa meno Abdul Mohamed ambaye awali alikuwa anatembea juu ya kivuli cha Kawemba.”

Kwenye mitandao ya kijamii kumekuwa na mitazamo mingi kuhusu jambo hili, naomba comment yako kuhusu mtazamo wako juu ya Azam kuachana na Kawemba na kuifuta nafasi ya C.E.O. Je wako sahihi na watafanikiwa au wamechemka?

Tetesi za usajili: Striker wa Stand United yupo sokoni

$
0
0

Mshambuliaji wa Stand United Chidiebere Abasirim amesema mkataba wake na klabu yake umemalizika rasmi Juni 1, 2017 na kuanzia sasa yeye ni mcheziji huru.

Chidiebere amesema, bado anasubiri kuona kama uongozi wa Stand United utamuongeza mkataba mwingine kwa ajili ya kuendelea kubaki katika timu hiyo lakini pia anakaribisha vilabu vingine vinavyovutiwa na huduma yake na yeye kama mchezaji yupo tayari kufanya kazi mahali popote kwa sababu mpira ni kazi yake.

“Mkataba wangu wa Stand United umemalizika Juni 1, 2017 kuanzia sasa mimi ni mchezaji huru. Hadi sasa bado hakuna mazungumzo yoyote kati yangu na Stand lakini bado muda upo nasubiri kusikia kutoka kwa viongozi wangu kama wataniambia chochote.”

“Kwa sababu mimi ni mchezaji huru, nakaribisha vilabu vingine ambavyo vinavutiwa na mimi tuzungumze kama tukifikia makubaliano nipo tayari kucheza sehemu yoyote kwa sababu soka ndio kazi yangu.”

Mshambuliaji huyo hakufanya vizuri sana msimu uliopita kutokana na jeraha la kuvunjika taya alilipopata wakati timu yake ikicheza na Azam FC kwenye uwanja wa Kambarage, Shinyanga. Jeraha hilo lilimuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu na aliporejea hakupata muda mwingi wa kucheza kutokana na kukaa nje kwa muda mrefu.

Chidiebere amesema kwa sasa yuko fiti na anaendelea kujifua kwa mazoezi binafsi licha ya ligi kumalizika lakini yeye anahitaji kurudisha uwezo wake uliopungua kutokana na kukaa nje ya uwanja kwa muda.

UCL Final: CR7 atamfikia Messi? Je ataendelea kumuonea Buffon?

$
0
0

Mpaka wakati michuano ya UEFA Champions League ikiwa inaingia kwenye hatua ya robo fainali – ilionekana wazi kwamba rekodi ya Cristiano Ronaldo kuendelea kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo kwa msimu wa 5 mfululizo ilikuwa imeshindikana.  –

Lakini magoli matano vs Bayern na matatu dhidi ya Atletico yamemrudisha CR7 katika uelekeo wa kwenda kuifikia rekodi hiyo – sasa ana magoli 10 na anahitaji goli mmoja kumfikia Lionel Messi mwenye magoli 11. 

Ronaldo ataingia kwenye mchezo wa kesho akiwa na rekodi ya kufunga katika fainali kufunga katika fainali 3 kati ya 4 alizocheza za michuano ya ulaya.

Wafungaji bora wa 2016/17 UEFA Champions League 

Ronaldo alikuwa amefunga magoli mawili tu katika michezo 8 ya kwanza Champions League, kuelekea robo fainali alikuwa amepigwa magoli 8 na Messi, lakini akarudi kwenye form na kuandika rekodi ya kuwa mwanadamu wa kwanza kutimiza magoli 100 katika michuano ya ulaya. Pia akafanikiwa kuifikia rekodi ya Messi ya kufunga hat trick 7 katika michuano hiyo ya ulaya. 

Huku Messi akiwa tayari nje ya michuano, mchezo wa kesho unaweza ukawa nafasi nyingine kwa Ronaldo kumaliza msimu wa ulaya akiwa mfungaji bora tena. Ikiwa atafanikiwa kufunga basi ataweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa UCL kwa misimu mitano mfululizo.  
Kesho itakuwa ni mara ya 5 kwa Cristiano Ronaldo kukutana na Guinluigi Buffon katika michuano ya ulaya, katika mara 4 walizokutana tayari Ronaldo amemfunga Buffon katika kila mchezo – lakini pamoja na kumfunga ni mara 1 tu timu yake ilifanikiwa kuondoka na ushindi dhidi ya timu ya kipa huyo muitaliano.

-*Buffon na Ronaldo pia wameshawahi kukutana na katika mechi za kimataifa, ilikuwa mnamo March 2004, katika mchezo wa kirafiki ambao uliisha kwa Italy kuifunga 2-1 Ureno, CR7 alikuwa akiitumikia nchi katika mchezo wa 4 akitokea benchi katika kipindi cha pili. 

UCL Final: Benzema anaisaka rekodi ya mtoto wa mkimbizi Raymond Kopa ndani ya Madrid

$
0
0

Kwa zaidi ya miaka 100 ya historia ya klabu ya Real Madrid, Raymond Kopa ndio alikuwa mchezaji mwenye mafanikio zaidi ya kifaransa katika kikodi cha Real Madrid, lakini hivi sasa Karim Benzema anakaribia kuungana nae katika kundi hilo la upekee. 


Kopa alishinda makombe mawili ya ya ligi mnamo mwaka 1957 na 1958 na kisha akashinda vikombe vitatu mfululizo vya michuano ya ulaya (1957, 1958 and 1959) akiwa na akina Alfredo Di Stefano, kikosi hatari ambacho kinatajwa kuwa moja ya timu bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya mchezo wa soka. 

Miaka zaidi ya 50 baadae, Benzema anakaribia kufikia level za Kopa. 

Tayari ameshashinda ubingwa wa ligi mara 2 na keshO Jumamosi huenda akafanikiwa kutwa ubingwa wake wa 3 wa ulaya na kuifikia rekodi ya Raymond Kopa.  

March 3, Kopa, mmoja wa washindi wa tuzo ya Ballon d’Or alipoteza maisha, lakini Benzema ana nia ya kumuenzi kwa ushindi wa fainali ya UEFA Champions League vs Juventus. 

Kopa na Benzema – wana historia ya kufanana – wote ni watoto wa wahamiaji waliozamia Ufaransa kwa miaka tofauti. Mabwana hawa wawili wote wana medali nne kila mmoja za ubingwa wa Ligue 1, Kopa akishinda na Stade de Reims na Karim akishinda na Lyon, moja vilabu  vyenye mafanikio zaidi katika soka la Ufaransa..

Wote wawili Benzema na Kopa wamevitumikia vilabu viwili kila mmoja katika maisha ya soka la ushindani, The Little Napoleon ‘Kopa’ aliitumikia Stade de Reims na Madrid tu, wakati Benzema alianza maisha ya soka la ushindani na  Lyon na mpaka sasa yupo Madrid – na inaonekana itakuwa ngumu kuitumikia klabu nyingine ya Ufaransa labda arejee katika klabu yake ya utotoni au kwenda kucheza soka nchi nyingine. 

Kopa alishinda kila kitu katika misimu mitatu tu aliyoitumikia Los Blancos, akicheza mechi 103 tu wakati Benzema mpaka sasa amecheza mechi 364. 

Benzema ana magoli 183 wakati Kopa akiwa na magoli 30 tu.  


‘Manula haendi timu yoyote Tanzania’– Azam

$
0
0

Wakati kukiwa na taarifa kwamba golikipa tegemeo wa Azam FC Aishi Manula ameshamwaga wino kuitumikia klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili, afisa habari wa Azam Jafar Idd amesema golikipa huyo ataendelea kubaki Azam.

Jafar amesema, mazungumzo kati ya manula na uongozi wa Azam yanakwenda vizuri na kinachosubiriwa ni kukamilisha baadhi ya taratibu baada ya golikipa huyo wa Stars kurejea nchini kutoka Misri ambako yupo kambini na timu ya taifa.

“Aishi Manula na Shomari Kapombe mazungumzo yao na Azam yapo katika dakika za mwisho na yanakwenda vizuri, Aishi Manula ataendelea kuwepo Azam FC. Kilichobaki tunasubiri wakirudi kutoka Misri waje wakamilishe taratibu na uongozi. nawatoa shaka mashabiki wa Azam kuhusu suala la Manula kwamba bado ataendelea kuwepo Azam.”

Video: Jafar Idd amewataja wachezaji waliotemwa Azam

$
0
0

Klabu ya Azam mbali na kukanusha kuhusu Manuala kuiacha klabu hiyo na kujiunga na Simba, wamezungumzia mambo mengine matatu yanayoihusu klabu yao.

Mambo yaliyozunguzwa na Azam ni pamoja na kutoa orodha ya wachezaji walioachwa na klabu hiyo baada ya kumaliza mikataba, wachezaji wa timu ya vijana waliopandishwa kucheza timu ya wakubwa pamoja na mipango ya usajili.

Ame Ally ‘Zungu’, Hamisi Mcha ni miongoni mwa wachezaji waliotemwa katika awamu ya kwanza lakini Jafar Idd amesema kuna awamu nyingine ambayo pia huenda wachezaji kadhaa wakatoswa na klabu hiyo.

Jafar amewataja wachezaji watano waliopandishwa timu ya wakubwa wakitokea timu ya vijana (U20).

Amezungumzia pia kuhusu mipango ya usajili na nafasi ambazo wataziangalia kutokana na mapendekezo ya kocha.

Griezman agongelea msumari wa moto katika kidonda cha Manchester United.

$
0
0

Yametimia, hakika unaweza kusema tu hivyo japokuwa hujui ni nini kitatokea kesho kwani lolote linaweza kutokea haswa pale palipo na pesa.

Antoine Griezman tetesi zimekuwa ndefu sana,huyu akisema lile na yule akisema hili kuhusiana na uhamisho wake wa kwenda Manchester United.

Griezman mwenyewe alisema wazi kwamba kuna alama 6 kati ya 10 kwamba yeye anakwenda United na kuifanya dunia iamini kwamba kweli Griezman anatua Old Trafford.

Lakini tweet ya mchezaji huyo imebadilisha kabisa upepo wa habari yake na kuanza kuipeleka katika upande mpya kwani Griezman anaonekana kubaki Atletico Madrid.

Griezman aliandika “now more then ever” na kuweka hashtags ambazo zilionesha umoja alionao yeye na klabu yake ya sasa ya Atletico Madrid.

Taarifa toka ndani ya klabu ya Manchester United zinasema United tayari wameona dili hilo ni gumu kwa sasa na wameanza kuangalia uwezekano wa nyota mwingine mkubwa.

Leon Osman humuambii kitu kwa wachezaji hawa Waafrika.

$
0
0

Baada ya Leon Osman kuja nchini Tanzani aliulizwa maswali mengi, lakini kati ya swali alikumbana nalo ni mchezaji gani wa Afrika bora kuwahi kucheza naye.

Osman alisema Steven Piener ni mchezaji baye alikuwa akishangaa jinsi alivyokuwa na uwezo wa kuchezea mpira na ujuzi wake uwanjani ulikuwa unamfanya awe anamshangaa.

Lakini Osman pia amesema kati ya simulizi ambazo atawadithia watoto wake siku moja ni hadithi za kumhusu Samuel Etoo kwani yeye kama Osmane anajivuni sana kucheza na Samuel Etoo.

Osman amesema pia hadi sasa alimuona Mnigeria Yakububkama striker ambaye alikuwa akiifanya kazi ya ufungaji kuonekana kuwa rahisi sana kutokana na uwezo wa Mnigeria huyo kucheka na nyavu.

Osman ameitabiria Afrika kuhusu kombe la dunia na kusema anahisi hivi karibuni tu taifa moja kutoka bara la Afrika litabeba kombe hilo la dunia.

 

Ni Juventus vs Real Madrid,tambua haya yafuatayo.

$
0
0

Ni Juventus na Real Madrid huku Real Madrid akijaribu kutafuta rekodi mpya ya kubeba kombe la Champions League mara tatu mfululizo tangu michuano hiyo kuanzishwa.

Vijana wa Real Madrid wataingia katika mchezo huo wakihitaji bao moja tu ili kuweza kuwa timu ya kwanza kufunga idadi ya mabao 500 katika michuano ya Champions League.

Lakini haitakuwa rahisi kwa Real Madrid kufanya hivyo kwani Juventus hawajafungwa hadi sasa na wanataka kumaliza msimu huu wa champions league bila nyavu zao kuguswa.

Endapo Juventus wataifunga Real Madrid na kubeba ndoo itawafanya kuwa timu ya kwanza baada ya United ya mwaka 2008 kumaliza msimu wa champions league bila kufungwa.

Na Juventus wanakisasi na Real Madrid cha mwaka 1998 nchini Uholanzi ambapo Jeventus “The Biaconeri” walifungwa na Los Blancos katika fainali ya Uefa ya mwaka huo.

Hadi sasa hakuna mchezaji aliyefikia rekodi ya Paulo Maldini ya kufunga bao la mapema katika fainali ya champions league ambapo Maldini alitumia sekunde 51 kufunga katika mechi dhidi ya Liverpool mwaka 2005.

Lakini Massimiliano Allegri ameshashinda Coppa Italia na Serie A anahitaji Champions League ili kuwa sawa na Jose Mourinho,Pep Gurdiola,Jup Heyckens,Luis Enrique na Sir Alex Ferguson ambao wamewahi kubeba makombe matatu makubwa ndani ya msimu mmoja.

Endelea kusbscribe channel yetu ya YOU TUBE ya Dauda Tv kupata kwa ukaribu kabisa uchambuzi na takwimu muhimu kuelekea mchezo huu mkubwa kabisa.

 

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>