Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

‘Goli la Amis Tambwe lilinitia aibu’– Casillas

$
0
0

Na Zainabu Rajabu

MLINDA mlango wa Kagera Sugar, Hussein Sharif ‘Casillas’ ameibuka na kusema kuwa alikuwa akimuogopa straika wa Yanga, Amissi Tambwe raia wa Burundi kila alipokutana naye uwanjani.

Casillas ambaye msimu huu alipata majanga ya kusimamishwa na klabu yake ya Kagera Sugar kwa madai ya rushwa, amesema alikuwa akimuogopa Tambwe ili asimfunge.

Shaffihdauda.co.tzilizungumza na Hussein Sharrif ‘Cassillas’ amesema: “Ni straika ambae ni mjanja na pia msumbufu akiwa na mpira ni lazima akufunge tu.”

“Msimu uliopita nilipokuwa Mtibwa Sugar sikutaka hata siku moja Tambwe
anifunge,lakini walivyokuja kucheza na sisi Morogoro akanifunga nilijisikia aibu kwa sababu kabla ya mpira kuanza nilimwambia leo hunifungi,”amesema Casillas.

Mchezaji huyo ambae kwa sasa anakipiga katika timu ya Burudani FC inayoshiliki michuano ya Sport Extra Ndondo Cup ambayo yapo chini ya   Cloud Media Group.


Mkude, Agrey, Mwinyi, waachwa kwenye kikosi cha Stars

$
0
0

Kikosi cha wachezaji 21 wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinachodhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti, kinatarajiwa kuondoka kesho Jumanne saa 10.45 jioni kwenda Misri.

Taifa Stars ambayo itakuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa kesho saa 7. 45 mchana inakwenda Misri kufanya kambi ya siku nane kujindaa na mchezo dhidi ya Lesotho utakaofanyika Juni 10, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wachezaji hao 21 kutoka hapa Tanzania wataungana na na wengine wawili, Nahodha Mbwana Samatta na Faridi Mussa wanaocheza ughaibuni katika kikosi hicho na kufanya jumla ya wachezaji kuwa 23 watakaokuwa nchini Misri.

Nahodha Msaidizi, Jonas Mkude hatakuwako kwenye msafara huo kutokana na ushauri wa madaktari walioelekeza kwamba nyota huyo wa Simba apate mapumziko ya angalau siku nne.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga ameridhia na kusema kuwa Mkude ataungana na wenzake Juni 8, mwaka huu timu itakaporejea kutoka Misri. Mayanga hajajaza nafasi ya Mkude.

Wachezaji ambao hawatakuwako kwenye kikosi hicho ni pamoja na Haji Mwinyi  (Yanga SC) na Aggrey Morris  (Azam FC) ambao wanaweza kuingia kwenye timu ya Taifa ya Zanzibar baada ya kuwa mwanachama mpya wa CAF kama kocha akiwahitaji.

Mchezo dhidi ya Lesotho ni muhimu kwa Tanzania ikiwa ni mechi ya kwanza kwa Taifa Stars katika Kundi ‘L’ kuwania nafasi muhimu ya kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika nchini Cameroon.

Mbali ya Lesotho na Tanzania, mataifa mengine katika Kundi ‘L’ ni Uganda na Cape Verde ambao pia wikiendi ya Juni 9, 10 na 11, mwaka huu watakuwa katika mchezo wa kwanza pia kuwania nafasi hiyo.

Kikosi cha Taifa Stars kinachofundishwa na Kocha Salum Mayanga kinaundwa na makipa Aishi Manula  (Azam FC), Benno Kakolanya  (Yanga SC) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar).

Walinzi wa pembeni upande wa kulia ni Shomari Kapombe (Azam FC) na Hassan Kessy (Yanga SC) wakati upande wa kushoto wapo Mohammed Hussein (Simba) na Gadiel Michael.

Walinzi wa kati Erasto Nyoni  (Azam FC), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba SC) na Nurdin Chona (Tanzania Prisons) ilihali viungo wa kuzuia ni Himid Mao (Azam FC) na Jonas Mkude kutoka Simba SC ambaye hatasafiri na timu kwa sasa.

Viungo wa kushambulia Salum Abubakar (Azam FC), Said Ndemla  (Simba SC) na Mzamiru Yassin (Simba) wakati viungo wa pembeni ni Simon Msuva (Yanga SC), Shiza Kichuya (Simba SC) na Farid Mussa (Teneriffe, Hispania).

Washambuliaji wapo Mbwana Samatta (KRC Genk- Ubelgiji), Ulimwengu (AFC Eskilstuna – Sweden), Ibrahim Ajib (Simba SC), Mbaraka Yusufu (Kagera Sugar) na Abdurahman Mussa (Ruvu Shooting).

Wasaidizi wa Mayanga katika benchi la ufundi ni Novatus Fulgence ambaye ni kocha msaidizi Patrick Mwangata – kocha wa makipa pia yumo Meneja wa timu, Danny Msangi; Mtunza Vifaa, Ally Ruvu, Daktari wa timu ni Richard Yomba na Daktari wa viungo ni Gilbert Kigadya.

Timu hiyo iliingia kambini Machi 23, 2017 kwenye Hoteli ya Urban Rose, Dar es Salaam kabla ya kesho kwenda Misri na baadaye itarejea Tanzania kucheza na Lesotho, Juni 10, mwaka.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

Video: Tshabalala amezungumzia tuzo ya mchezaji bora na ubingwa wa ASFC

$
0
0

Mchezaji bora wa VPL 2016/17 Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ amesema, ni ndoto ya kila mchezaji kushinda tuzo ya mchezaji bora, kwa vile yeye ameshinda tuzo hiyo msimu huu, anamshukuru Mungu.

Dauda TV ilimnasa Tshabalala mara baada ya mechi ya fainali ya ASFC dhidi ya Mbao FC ambapo Simba ilishinda kwa mabao 2-1 na kukata tiketi ya kushiriki michuano ya CAF Confederation Cup.

Tshabalala amesema kombe la ASFC ni zawadi kwa wanasimba ambao walikuwa na kiu ya kuiona timu yao ikishiriki mashindano ya kimataifa.

Ernesto Valvarde ateuliwa kuwa kocha mpya Barca, ni nani huyu?

$
0
0

Ernesto ni mzaliwa wa nchini Hispania ambako alizaliwa miaka 53 iliyopita nchini Hispania na amewahi kuichezea timu yake ya taifa huku pia akipita katika vilabu mbalimbali nchini Hispania.

Ernesto Valverde amevichezea vilabu vya Alaves, Sestao, Espanyol,Atletic Bilbao lakini pia alikuwepo katika kikosi cha Barcelona kilichoshinda kombe la Cup Winners Cup na Copa Del Rey chini ya Johan Cruyf.

Mwaka 1997 ndipo Valverde aliamua kuacha kucheza soka na kuanza kujihusisha na masula ya soka ambapo alifundisha timu kama vile Espanyol,Olympiakos,Villareal,Valencia na hatimaye Bilbao.

Uwezo wa Ernesto Valrade ulionekana mkubwa sana haswa walipochukua kombe la Super Cup mwaka 2014 baada ya kuifunga Barcelona mabao 4 kwa nunge hapo ndipo alianza kufahamika sana.

Lakini pia Valvarde sio mgeni sana wa makombe kwani alipokuwa akiinoa Olympiakos alifanikiwa kubeba makombe matano ya michuano mbali mbali nchini Ugiriki.

Valvarde anakwenda kuchukua kazi ya Luis Enrique aliyeamua kustaafu, lakini atakuwa na kibarua kigumu kuirudishia Barca ubingwa wa La Liga na Champions league ambayo yote msimu huu wameikosa.

‘Kama waamuzi watatenda haki, timu yoyote inaweza kuchukua ubingwa’– Aishi Manula

$
0
0

Golikipa wa Azm FC na Taifa Stars Aishi Manula amesvunja ukimya na kusema, endapo waamuzi wa Tanzania watachezesha mechi za mashindano mbalimbali basi timu yoyote inaweza kuibuka bingwa mbali na timu zenye majina makubwa kama Azam, Simba na Yanga.

“Kama waamuzi wa ligi yetu watatenda haki, timu yoyote inaweza kuchukua ubingwa,” amesema Manula ambaye ni mshindi wa tuzo ya golikipa bora VPL 2016/2017.

Manula amesema, Azam, Yanga na Simba hazifanyi vizuri kimataifa kwa sababu ya upendeleo zinaopewa na baadhi ya waamuzi wa ndani.

“Azam, Simba na Yanga hazifanyi vizuri kimataifa kwa sababu zinapata ‘favor’ kwenye ligi ya ndani.”

Manula ameamua kung’oa kabisa mzizi wa fitina kuhusu soka la Bongo hakuacha kumpongeza mwamuzi bora wa VPL 2016/2017 Elly Sasii.

“Tukipata waamuzi kama aliyeshinda tuzo ya mwamuzi bora msimu huu (Elly Sasii) tutafika mbali.”

Golikipa huyo anaekuja kwa kasi hakuacha kusema kwamba, wadau wengi wanafatilia timu chache za ligi na kugundua makosa machache ya waamuzi lakini zinapocheza timu zenye majina madogo ndipo yanapofanyika madudu lakini watu hawaoni kwa sababu hawafatilii.

“Watu wanafatilia timu chache tu zinazocheza ligi, lakini zinapocheza timu ambazo hazina majina ndio yanafanyika ‘madudu’ mengi lakini watu hawajui kwa sababu hawafatilii.”

“Ukisikia mwamuzi kafungiwa basi itakuwa kwa sababa ameharibu kwenye mechi inayozihusisha timu za Azam, Yanga au Simba. Huwezi kusikia mwamuzi kafungiwa kwenye mechi ya Ndanda na African Lyon, lakini huku ndio kwenye madudu mengi.”

Mbaraka hana tatizo na Simba, kamilisheni mahitaji yake

$
0
0

Mshambuliaji wa Kagera Sugar na timu ya taifa Mbaraka Yusuph amesema yupo tayari kurudi Simba endapo klabu hiyo itatimiza mahitaji yake kabla ya kusaini mkataba wa kuitumikia.

“Nipo tayari kurudi Simba endapo watakidhi mahitaji yangu,” amesema Mbaraka wakati akizungumza na Sports Extra ya Clouds FM.

Mbaraka alitolewa kwa mkopo kwenda Kagera Sugar, lakini baada ya mkataba wake na Simba kumalizika akajiunga na Kagera Sugar ambayo inammiliki kama mchezaji wao halali tofauti na Simba wanavyodai kwamba bado ni mchezaji wao halali.

“Mimi ni mchezaji halali wa Kagera Sugar, makataba wangu na Simba ulishamalizika kwa hiyo kama wananihitaji inabidi tukae chini na kuzungumza.”

Mbaraka amesema malengo yake katika msimu uliopita yalikuwa ni kuwa mfungaji bora lakini hakufanikiwa badala yake akaishia kufunga magoli 12 magoli mawili nyuma ya Simon Msuva na Abdulrahman Musa walioshinda tuzo hiyo kwa kufunga magoli 12 kwa msimu mzima.

“Nilipanga niwe mfungaji bora msimu huu lakini kwa bahati mbaya malengo yangu hayajatimia, nashukuru kwa hii tuzo niliyoshinda ya mchezaji bora chipukizi.”

Mino Raiola atunga hadithi ya uongo kuzichonganisha Man City na United.

$
0
0

Kati ya majina ya mawakala maarufu katika soka hivi sasa ni Mino Raiola, Raiola ni mjanja mjanja sana katika kuuza wachezaji na ana mbinu nyingi za kumfanya mteja wake auzwe kwa bei ya gharama kubwa.

Mwishoni mwa wiko hii magazeti ya Italia pamoja na klabu ya Napoli yalitoa taarifa inayodai Raiola amekuwa akivujisha habari za uongo kwa vyombo vya habari ili kujaribu wateja wake wauzwe kwa bei kubwa.

Raiola ameona klabu mbili tajiri za jiji la Manchester zilivyo na shida na golikipa, baada ya kuliona hilo akaingia kazini kujaribu kuzifanyia mchezo ili awatafutie golikipa wa bei ghali na yeye apate faida kubwa.

Mino Raiola ndio wakala Gianluigi Donnaruma golikipa wa Ac Millan ambaye amekuwa akiwindwa na Manchester United pamoja na Manchester City.

Mwishoni mwa wiki habari kubwa ya vyombo vya habari mchini Italia ilikuwa Donnaruma kukaribia kusaini katika klabu ya Napoli ya nchini humo humo Italia, katika habari hiyo ilisema Napoli wamezipiku United na City.

Siku moja tu baada ya taarifa hiyo kutoka, Napoli walitoa taarifa za kukanusha habari hizo na wakisema waziwazi kwamba chanzo cha taarifa hiyo ni wakala wa mchezaji huyo bwana Mino Raiola.

Napoli hawajakana kumfuata Donnaruma lakini wamekanusha kwamba wanakaribia kumchukua na kuweka wazi kuhusu chanzo cha habari hiyo, Raiola anafanya hivyo ili kujaribu kuchukia kiasi kikibwa cha fedha toka kwa United na City.

 

Je, Huddersfield wataleta njaa EPL au ni vibonde wapya.

$
0
0

Jumla ya mikwaju 10 ilipigwa ili kumpata mbabe ambapo Huddersfield waliibuka kidedea dhidi ya Reading na kufanikiwa kupanda ligi kuu nchini Uingereza kwa mara ya kwanza tangia mwaka 1972.

Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bila kwa bila na ndipo muamuzi alipoamua mikwaju ya penati ambapo hadi ilipofika mkwaju wa penati wa 10 ndipo mshindi alipatikana.

Kocha wa Reading ambaye pia alikuwa mchezaji wa zamani wa Manchester United Jap Stam amekiri kusononeshwa sana na matokeo hayo kwani vijana wake walijiamini mno na waliamini wangeifunga Huddersfield.

“Ni ngumu sana kwetu hatujashinda mchezo huu na hii inamaanisha hatutacheza Epl msimu ujao, hili ni suala gumu sana kwangu mimi na kwa wachezaji lakini ndio maisha ya soka” alisema Stam.

Katika mchezo huo, Aaron Mooy raia wa Australia ambaye yuko Huddersfield akitokea Man City aliibuka kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Kocha wa Huddersfield Wegner anaibuka kuwa shujaa wa klabu hiyo kwani kabla ya majira ya Xmass kocha huyo alikuwa akitakiwa na vilabu vya Aston Villa na Wolfburg lakini akaamua kubaki katika timu hiyo.

 


‘Bocco ni mchezaji wa klabu moja, inashangaza ‘mfalme wa Azam FC’ anavyoondolewa’

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

NAAMINI John Bocco ni mfungaji hatari zaidi ya Doland Ngoma, lakini ni kwa nini ‘mfalme’ huyu wa klabu moja anaondolewa katika ‘himaya’ yake? Umeamini Azam FC ni ‘figa la Tatu’ katika soka la Tanzania baada ya Yanga na Simba? Upande wangu niliamini hivyo mara tu baada ya Saad Kawemba kupewa nafasi ya utendaji mkuu wa klabu hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007.

Sikuwahi kuamini Azam FC ni ‘washindani wenye mabadiliko’ kwa sababu ‘palipo na pesa ndipo pajaapo watu.’ ‘Majungu’ ni sehemu ya maisha ya mwanadamu, chuki ni visasi visivyo na mwisho na ndani ya klabu hiyo ‘Majungu ndiyo Mtaji.’

Achana na namna walivyoondolewa ‘wapambanaji’ kama Habib Kondo, Mohamed Seif ‘King’-makocha ambao walitengeneza historia ya kuipandisha ligi kuu Azam FC mwaka 2008, lakini walikuja kupuuzwa na kudharauliwa mara tu ya klabu kubadilika ghafla ‘kutoka klabu ya kawaida hadi kuwa klabu tajiri’ katika soka la Tanzania na pengine Afrika Mashariki yote.

Matatizo yalianza kitambo 

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kuandika makala nikimshauri  mmiliki wa Azam FC kuachana na watendaji wa ndani na kujaribu kuwaajiri raia wa kigeni katika idara nyeti za kiuongozi klabuni hapo. Naamini mmiliki wa klabu hiyo anahitaji kuona timu yake ikipiga hatua ndani na nje ya uwanja na baada ya kuona mambo hayaendi vile anavyotaraji chini ya watendaji wazawa.

Mmiliki naamini ana uwezo wa kuajiri watendaji wa kimataifa ambao wanaweza kumtengenezea ‘mwanga’ wa kule klabu itakapokuwa baada ya muda fulani. Kuendelea kuwaajiri wazawa ni tatizo ambalo leo hii linaifanya Azam FC kupita katika matarajio niliyowahi kuyasema miaka kadhaa iliyopita-klabu kukosa ‘dira’ ambayo ingetuonesha muelekeo wa klabu hata kama timu isingekuwa ikishinda mataji.

Taji la VPL 2013/14 na lile la klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati-Kagame Cup 2015 ni mafanikio kwa klabu iliyo na miaka kumi tu tangu kuanzishwa kwake lakini bado nilisema Azam FC si ‘changamoto mpya’ katika soka la Tanzania kwa sababu hadi sasa sifahamu Azam FC inakwenda katika mwelekeo gani.

Mtibwa Sugar FC ilipanda ligi kuu mwaka 1997 na kufikia mwaka 2000 walikuwa na mataji mawili ya ligi kuu na ikumbukwe wakati huo mpira ulikuwa ukichezwa kwa kiwango cha juu na timu yenye ubora ilikuwa na nafasi ya kushinda ubingwa si kama ilivyo sasa-timu yenye pesa zaidi ndiyo hushinda taji.

Azam FC inaelekea walipo Mtibwa Sugar na wanaoipeleka shimoni klabu hiyo ni wamiliki wenyewe kwa kuwaajiri watu ‘wabinafsi’ wenye ‘mapenzi na klabu za Simba na Yanga.’ Kwa nini wasiwaajiri watendaji wa kimataifa katika idara ya utendaji?

Wanajidanganya sana na kudanganywa kuhusu ‘wapiga majungu’ na wanaotaka kuonekana ‘miungu-watu.’ Hawa ndiyo waliwaondoa kina King na Kondo bila thamani, ni hawa waliwaondoa rundo la wachezaji bora na kuwasaini ‘magarasa wa kimataifa’ kwa gharama ya juu.

Wakati wanawaondoa kina King na kuwaajiri Wabrazil mwaka 2009 walisema watengeneza ‘utambulisho wao’.

Walipokuwa wakiwaondoa kina Boniface Pawasa, Shaaban Kisiga, Shekhan Rashid na kuwasaini Wakenya Ibrahim Shikanda, Osborn Monday, Francis Ouma na Mganda, Peter Shenyonjo naamini ilikuwa ni sehemu ya kuimarisha timu kinidhamu, kiubora, na kiufundi hasa ukizingatia vijana kama Himid Mao, Bocco, Salum Abubakary, Salum Machaku wakipandishwa katika timu.

Wapo walioamini Azam  FC itafanikiwa haraka na kusahau watendaji wao walikuwa-ama wanachama wa Simba au Yanga.

 Kuondolewa kwa Bocco

Nilimsikia msemaji wa klabu ya Azam FC akielezea kuachana na Bocco aliyemaliza mkataba wake. Wakati akizungumza nilikuwa makini kusikiliza sababu hasa ya kuondolewa kwa mfungaji huyo wa muda wote wa klabu na baadae nikagundua hakukuwa na sababu yoyote ile ya maana pale aliposema, “Tumeshamtaarifu mwalimu kuwa hatutokuwa na Bocco msimu ujao.”

Kwa maneno ya Jafar Idd ni kwamba Bocco ameachwa na uongozi si kocha ndiyo maana uongozi umemtaarifu kocha kuachana na Bocco na si kocha kuwataarifu viongozi. Hivi ndivyo sajili za watu wa Simba au Yanga hufanyika na sasa Azam FC imeshika hatamu katika hilo.

Kuondolewa kwa Bocco ni muendelezo tu wa viongozi wa klabu hiyo kuwaacha wachezaji bora. Jabir Aziz, Malika Ndeule, Kipre na ndugu yake wote waliondolewa huku mchango wao ukiwa bado unahitajika klabuni hapo lakini kwa sababu zisizo za kimpira wachezaji hao wakaachwa waondoke.

Naamini mchezaji kama Bocco alistahili kuendelea kuthaminiwa ndani ya Azam FC na namtazama kama mchezaji wa klabu moja tu kama ilivyo kwa nyota wa kimataifa kama Francesco Totti ‘King of Rome’, Ryan Giggs, Phillip Lamh na wengineo ambao walizitumikia klabu moja kwa maisha yao yote ya soka.

Bocco akiwa na umri wa miaka 27 tu ameondolewa Azam FC kwa sababu kuna baadhi ya watendaji hawakutaka kuona mchezaji huyo akiendelea kuboresha rekodi zake. Unaachaje kumsaini Bocco na kuwasaini wachezaji ‘magarasa’ kutoka nje kwa zaidi ya dola 60, 000?

Nasikia kuna viongozi walitaka ‘kupiga 10%’ lakini Bocco akakataa matakwa yao, tatizo likaanzia hapo na kwa vile wao ndio wameshikilia ‘mpini’ wakaamua walichoamua. Kumuondoa Bocco ni sehemu tu ya ‘hujuma’ ambazo watendaji wa klabu hiyo wamekuwa wakizifanya lakini wanasahau kuwa kufanya hivyo ni kuendelea kuiumiza klabu.

 Miezi 10 iliyopita

Niliandika makala, ‘Waambieni Wahispaniola wa Azam FC, Bocco hagusiki Azam FC…’ niliandika kwa sababu sikuona sababu ya kuachwa kwake ambazo zilitolewa na kocha Zeben Hernandez na kwa jinsi wawili hao walivyofanya kazi kwa miezi 6 ni wazi tamko lile halikuwa limetolewa na kocha yule raia wa Hispania zaidi lilitolewa na uongozi wake wa juu.

 Hii ndiyo sehemu ya makala hiyo…

Una akili kweli wewe, utoke kwenu afu uje utuambie ‘Mr. AzamFC’ hana hadhi ya kuichezea Azam!! Pumbavu zenu. Ujio wenu tu mimi niliuchukia, na mnaanza kunipa sababu za kuwachukia zaidi… Waambie kuhusu Bocco, Himid na Sure Boy. Kwanza, waambie kuwa Bocco ndiye aliyeipandisha ligi kuu timu ya Azam FC mwaka 2008. Ni shujaa wa kukumbukwa wa timu.

Pili, waambie kuwa Bocco huyuhuyu ndiye mfungaji bora wa Ligi kuu Tanzania Bara wakati Azam FC ilipomaliza ‘TOP 2’ kwa mara ya kwanza msimu wa 2011/12. Ni shujaa wa timu. Tatu, Waambie kuwa Bocco ndiye mchezaji aliyefunga goli la ubingwa wakati Azam FC iliposhinda taji lake la kwanza na la pekee katika VPL msimu wa 2013/14. Hagusiki.

Waambie kuwa ‘hirizi’ yenu hiyo ya bahati ndiye mchezaji aliyeipa  Azam FC taji la kwanza la kimataifa (Kagame Cup 2015.) Zaidi waambieni ukweli tu kuwa Azam FC inaweza kucheza bila Bocco uwanjani lakini si kumuondoa katika timu. Hagusiki!

Mwisho wa kunukuu makala yale…

Video: Dakika 1 ya ushauri wa Masao Bwire kwa Yanga

$
0
0

Yanga wataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika msimu ujao kufuatia kuwa mabingwa wa VPL 2016/2917.

Msemaji wa Ruvu Shooting Mao Mwire ametoa ushauri kwa klabu hiyo ili kuhakikisha inafanya vizuri kwenye michuano hiyo na kuitangaza vyema Tanzania kisoka kwenye anga za kimataifa na kuacha kuwa wasindikizaji.

Huyu hapa Masao Bwire akitoa ushauri huo, angalia video hapa chini kujua hasa alichokizungumza Bwire.

Video: Ripoti ya Daktari wa Stars kuhusu hali ya Jonas Mkude

$
0
0

Daktari wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ ameelezea hali ya afya ya kiungo wa timu hiyo Jonas Mkude ambaye alipata ajali siku ya Jumapili Mei 28, 2017 wakati anatoka Dodoma kuelekea Dar kujiunga na kambi ya Stars.

Amesema Mkude kwa sasa yupo kwenye uangalizi wa wiki moja na baada ya hapo ataungana na timu kama hali yake itakuwa nzuri wakati huo Stars itakuwa imesharudi kutoka Misri ambako inaenda leo Mei 30, 2017 kwa ajili ya kambi ya wiki moja kujiandaa na mechi dhidi ya Lesotho Juni 10 kuwania kufuzu michuano ya AFCON.

Mkude atabaki Dar es Salaam ili kuendelea kuangalia hali yake ya afya ambapo kwa sasa anaendelea kutumia dawa za maumivu.

Kuelekea UCL Final: Takwimu 10 za mchezo wa Real vs juve

$
0
0

Zimebaki takribani siku 4 kabla ya ulimwengu wa soka kushuhudia mtanange wa fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya kati ya miamba ya Italia na Spain – Juventus na Real Madrid. 

Kuelekea mchezo huo wa fainali naendelea na mfululizo wa mambo mbalimbali yanayohusiana na mchezo huo.

TAKWIMU 10

• Real Madrid wanahitaji kufunga goli moja zaidi ili kuwa timu ya kwanza kutimiza magoli 500 katika historia ya UEFA Champions League, kuanzia hatua ya makundi mpaka fainali. 
• Dani Alves alicheza mchezo wake wa 99 wa UEFA Champions League vs Monaco. Jumamosi ijayo atakuwa mchezaji wa 31 kutimiza mechi 100 katika mashindano hayo. 

• Kipigo cha Real Madrid vs Atletico katika nusu fainali ya kimewaacha Juventus kuwa timu pekee ambayo haijapoteza mchezo hata mpaka sasa katika michuano hiyo. The Bianconeri wanaiwinda rekofi ya kushinda ubingwa UEFA Champions League bila kupoteza mchezo hata mmoja – na kuifikia rekodi ya Manchester United ya 2008. 

• Madrid na Juve wote watakuwa wanacheza fainali zao za 6 za UEFA Champions League, wanaifikia rekodi ya AC Milan. 

• Madrid wameshinda mechi zao zote 5 za fainali za UEFA Champions League, wana rekodi nzuri kwenye michuano hiyo wakati Juventus wamepoteza mchezo wa fainali za UCL kuliko timu yoyote – mara 4. Ushindi wao pekee ulikuja dhidi ya Ajax kwa mikwaju ya penati mnamo mwaka 1996. 

• Ukiiondoa Madrid ambao wana rekodi 💯 ya kushinda fainali za UEFA Champions League –  Marseille (1993), Porto (2004) na Internazionale (2010) ambao wamecheza fainali ya UCL mara 1 nao wana rekodi hiyo pia. 

• Madrid wana lengo la kuwa timu ya kwanza kutetea ubingwa UEFA Champions League. AC Milan (1989, 1990) chini Ariggo Sacchi walikuwa timu ya mwisho kutwaa ubingwa wa Kombe la Ulaya mfululizo, timu nyingine ziliwahi kusogelea kuivunja rekodi hiyo ni Milan (1994, 1995), Ajax (1995, 1996), Juve (1996, 1997) and Man. United (2008, 2009) – wote hawa walifika fainali baada ya kutwaa ubingwa msimu uliopita lakini walifungwa – Je Madrid atauvunja mwiko huu. 

• Zinédine Zidane anaitafuta rekodi ya kwanza kubeba ubingwa wa UEFA Champions League mara mbili mfululizo – wakati Ramos anaitaka rekodi ya kuwa nahodha wa kwanza kubeba taji hilo mara mbili..

• Bila kuhesabu mwaka 2017, Italy na Spain ndio nchi ambazo vilabu vyake vimeingia fainali mara nyingi zaidi – kila nchi mara 27; Spain wameshinda mara 16 katika hizo mara 27 na Italy wamebeba mara 12 na kupoteza mara 15. 

• Hii itakuwa mara ya 4 kwa vilabu vya nchi hizi mbili kukutana na UEFA Champions League – mara nyingi zaidi kuliko pair nyingine ya vilabu vya nchi nyinginezo – vilabu vya England v .

Wamekanusha Kaseke kumalizana na Singida United

$
0
0

Na Zainabu Rajabu

BENCHI la Ufundi la klabu ya Yanga limesema halifahamu kama kiungo wake Deus Kaseke ametimka klabuni humo.

Taarifa za ndani kutoka kwenye klabu hiyo zinasema kuwa mchezaji huyo yupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili kwenye klabu ya Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu huu.

Singida imeanza usajili kwa kasi baada ya kumsajili kocha wa zamani wa Yanga na mkurugenzi wa Ufundi, Hans van der Pluijm na wachezaji watano wa kimataifa, mbali na hao, Singida imehakikishia inaimarisha vyema kikosi chake baada ya kumsajili kiungo mahiri wa Mbeya City, Kenny Ally.

Shaffihdauda.co.tz imezungumza na kocha msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi amesema bado wanaamini Kaseke ataendelea kubaki Yanga kwa ajili ya msimu ujao.

“Tunachofahamu kuwa Kaseke bado ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuwa katika mipango ya kocha, tunamuamini Kaseke na tunaamini ataendelea kuitumikia Yanga msimu ujao,” alisema Mwambusi.

Kocha huyo wa zamani wa Mbeya City amesema Kaseke bado yupo kwenye mipango ya kocha George Lwandamina kwa ajili ya msimu ujao kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa.

Kaseke alisajiliwa na Yanga kipindi cha Pluijm ambaye anatarajia kumsajili ili kuwa naye Singida United kwa ajili ya msimu ujao, mchezaji huyo anaonekana kutamani kwenda Singida United kwa ajili ya kuungana na kocha wake wa zamani.

Video: Ulimwengu amejibu kuhusu kutaka kujiunga Yanga na malengo yake Sweden

$
0
0

Mshambuliaji wa AFC Eskilstuna ya Sweden na Taifa Stars amesema, Sweden kama sokoni kuelekea kucheza soka kwenye ligi kubwa kama yalivyo malengo yake.

Ulimwengu amesema majeraha ndio yalimrudisha nyuma na kumfanya asionekane uwanjani kwa muda, lakini kwa sasa yupo fiti na watanzania watasikia vitu vizuri kutoka kwake.

mchezaji huyo ambaye hajawahi kucheza ligi ya Tanzania amekanusha taarifa zilizowahi kumhusisha kutaka kujiunga na Yanga baada ya kuachana na TP Mazembe ya Congo DR.

‘Bora niondoke kuliko kutolewa kwa mkopo’– Juma Mahadhi

$
0
0

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Yanga Juma Mahadhi amesema, hayuko tayari kutolewa kwa mkopo kwenda timu nyingine, kama itatokea klabu yake inataka kumtoa kwa mkopo ataomba imuache ili akatafute maisha sehemu nyingine.

Hiyo inatokana na tetesi ambazo zimekuwa zikienea kwamba, klabu ya Yanga huenda ikamtoa nyota huyo kwa mkopo kwenda klabu ya Singida United ambayo imepanda kucheza ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.

“Sipo tayari kutolewa kwa mkopo, kama itatokea hivyo nitaomba waniache niende kutafuta maisha sehemu nyingine. Mimi sijui lolote kuhusu hilo, klabu yangu haijaniambia chochote na kama wataniambia, msimamo wangu ndio huo,” amesema Juma Mahadhi alipozungumza na Sports Extra.

Mahadhi pia amesema alitamani kucheza mechi nyingi katika klabu yake lakini imekuwa tofauti na mipango pamoja na matarajio yake.

“Nilijipanga nicheze mechi nyingi na kuisaidia klabu yangu zaidi ya hapo lakini malengo yangu hayakutimia. Kulikuwa na ushindani mkubwa kwenye kikosi na kila mchezaji aliyepata nafasi alitaka kuonesha anapaswa kucheza kila mechi.”

“Najipanga kwa ajili ya kufanya vizuri katika msimu ujao ili nipate nafasi ya kucheza mechi nyingi tofauti na msimu huu.”

Kuhusu klabu ambazo zinahitaji huduma yake kwa ajili ya msimu ujao Mahadhi amesema zipo klabu kadhaa za ndani na nje lakini kwa sasa hawezi kuzitaja kwa sababu bado yupo ndani ya mkataba na Yanga.

“Nimepokea ofa kutoka vilabu mbalimbali ndani na nje ya nchi, kwa sasa siwezi kuzungumzia lolote kwa sababu nipo ndani ya mkataba. Waende wakaonane na manager wangu na viongozi wa klabu wakikubaliana nitafanya maamuzi kwa sababu mpira ni kazi yangu.”


Kapombe kuhusu Bocco kuondoka Azam na tetesi za kurudi Simba

$
0
0

Kumekuwa na mitazamo tofauti kuhusu kuondoka kwa nahodha na mchezaji wa muda mrefu wa Azam FC John Bocco ‘Adebayor’ ndani ya kikosi hicho chenye maskani yake Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Shomari Kapombe ni mchezaji mwenzake Bocco waliyepata kucheza pamoja kwa muda mrefu kwenye kikosi cha Azam na timu ya taifa, Kapombe amesema kuondoka kwa Bocco ndani ya Azam ni kitu cha kaiwaida kwenye maisha ya soka.

Kuondoka kwa Bocco ndani ya Azam ni kita cha kawaida kwenye maisha ya soka, tumeona hata Ulaya wachezaji wenye heshima kama Bocco wameondoka kwenye vilabu vyao na maisha yameendelea.

“Bocco alikuwa bado ni mchezaji muhimu ndani ya Azam kutokana na uwezo wake lakini ameshaondoka anaenda sehemu nyingine kuangalia maisha yake kwa hiyo hilo limeshapita tuache maisha mengine yaendelee.”

Kapombe amezungumzia pia kuhusu tetesi ambazo zinamhusisha yeye kurudi kwenye klabu yake ya zamani Simba kwa ajili ya kuitumikia kuanzia msimu ujao.

“Nikitoka Azam nataka niende kucheza nje ya nchi, kwa sasa bao nafanya mazungumzo na Azam kwa ajili ya kuongeza mkataba mpya.”

“Azam ni klabu yangu hadi sasa kwa hiyo wananafasi kubwa ya kufanya mazungumzo na mimi kuliko klabu nyingine tukifikia makubaliano nitasalia hapa. Mazungumzo yanakwenda vizuri hadi sasa.”

‘Bocco alikuwa bado anahitajika Azam’– Aishi Manula

$
0
0

Golikipa namba moja wa Azam FC Aishi Manula amesema, John Bocco ‘Adebayor’ bado alikuwa anahitajika ndani ya kikosi cha Azam.

Manula amesema, licha ya timu yake kusajili wachezaji wengi wa kigeni miaka ya hivi karibuni bado Bocco amekuwa mhimili muhimu ndani ya timu yao kutoka na uwezo wake wa kutupia kambani.

“Unapokuwa na mtu kama Bocco katika timu ni kitu kikubwa sana kwa sababu ametoka mbali na Azam na amefanya mengi makubwa, makombe mengi yaliyopatikana ndani ya Azam FC  nadhani ni katika uongozi wake yeye kama nahodha, ni mtu muhimu sana.

“Bocco ni mchezaji ambaye bado alikuwa anahitajika katika klabu ya Azam, kwa sababu unaweza ukaona wachezaji wengi wanaokuja Azam katika nafasi yake hawafanyi vizuri. Wamesajiliwa wachezaji wengi professional waje waisaidie klabu na hawaisaidii mara zote Bocco anakuwa mkombozi na tegemeo.”

“Kitu cha kufikiria ni kwamba, leo Bocco anaondoka nani anakuja? Tunamuona Shabani Idd anakuja vizuri lakini bado ni kijana mdogo anahitaji support kubwa kutoka Bocco kama alivyokuwa anapewa awali. Nilikuwa nawaona wanakaa pamoja na kuzungumza, tukiwa mazoezini anajaribu kumuelewesha kwahiyo walikuwa ni marafiki.”

“Kuondoka kwa Bocco yule kijana anabaki pekeake kusimama mwenyewe itamuwia vigumu. Bocco anaondoka akiwa anategemewa kama top striker na utaona hata wakati yupo nje anasumbuliwa na majeraha timu ilikuwa inayumba.”

“Bocco kaondoka Azam kwa sababu ya maslahi yake hajaondoka kwa sababu Azam wamemchoka au hawahitaji tena kuwa na yeye kwa sababu uwezo wake umeshuka, uwezo wake haujashuka licha ya kusumbuliwa na mejeruhi.”

“Namtakia maisha mema huko anapokwenda na hata tukikutana nadhani hakutakuwa na uadui kwa sababu soka si uadui.”

Juma lililopita afisa habari wa Azam FC Jafar Idd alithibitisha klabu hiyo kuachana rasmi na Bocco baada ya mshambuliaji huyo kudumu kwa muda mrefu ndani ya Azam.

Tetesi za usajili: Mghana wa Mbao kaichomolea Singida United

$
0
0

Na Zainabu Rajabu

BEKI wa Mbao FC Asante Kwasi, raia wa Ghana amekataa ofa ya kujiunga klabu ya Singida United inayofundishwa na kocha Hans van der Pluijm, iliyotaka kumsajili kwa ajili ya kumtumia msimu ujao katika Ligi Kuu Bara, badala yake amesema angependa kujiunga na Azam FC.

Shaffidauda.co.tz ilizungumza beki huyo ambaye alisema anaamini Azam FC ni klabu sahihi kwake kujiunga nayo kutokana na kuvutiwa na namna yauendeshwaji wake na hata pia mazingira yake ya kazi.

“Baada ya ligi kuu Tanzania msimu uliopita kumalizika, nilifuatwa na wadau wa klabu ya Singida United wakinishawishi nijiunge nao lakini niliwagomea nikitaka wanipewe muda wa kutafakari ili niweze kuchagua wapi kwangu ni mahali sahihi kucheza soka langu.”

Asante kwasi (jezi namba 14) ni miongoni mwa wachezaji waliofanya vizuri kwenye msimu uliopita wa VPL 2016/2017 akiitumikia klabu ya Mbao FC

Beki huyo ambae uchezaji wake ulionekana kuwa vutia wengi kwenye fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup amesema: “Kuna timu nyingi hapa Tanzania lakini navutiwa zaidi na Azam jinsi inavyojiendesha, ni klabu inayofanya mambo yake kisasa sana.”

Hadithi hii ya Gabriel Jesus ikutie moyo kufikia malengo yako

$
0
0

Maisha ni juhudi na kupamban, bahati katika maisha haipo kwani hata mungu alitupa maarifa na vipaji ili tuvitumie katika kufanikisha malengo yetu ya kila siku, na hata hiyo “bahati” huwatembelea wanaopenda kujaribu.

Maneno hayo katika aya ya kwanza yanalandana na historia ya mwanasoka tishio katika klabu ya Manchester City Gabriel Jesus ambaye sasa sio tu ni tajiri bali ni kati ya wacheza na nyavu wanaozungumziwa sana Uingereza.

Jesus ambaye amesajiliwa kwenda Manchester City kwa ada ya £32m miaka mitatu iliyopita hakuna hata mtu mmoja ambaye alidhani anaweza kuwa na maisha aliyonayo hivi sasa ya kuendesha magari mazuri na kuishi katika nyumba nzuri.

Miaka mitatu iliyopita akiwa na umri wa miaka 17 tu ilimbidi afanye kazi ya ziada ili kupata kipato, Jesus aliamua kuwa mpaka rangi mitaani mjini Sao Paulo ambapo alifanya kazi hiyo katika mida wa ziada akitoka mazoezini.

Lakini hii haikumzuia Jesus kufukuzia ndoto zake kwani katika muda wake wa ziada alikwenda mazoezini kama kawaida na kuoambana uwanjani ili kutimiza ndoto zake ambazo zilikuwa katika soka.

Miaka mitatu sasa Jesus yuko kwenye kilele cha ndoto zake, hii inatufunza nini?kesho yako bora inaanza na leo,haijalishi ni mangapi unayoyapitia hupaswi kukata tamaa,pambana na amini katika ndoto zako na kila kitu kitakuwa sawa.

 

Hizi anazofanya Pep Gurdiola sokoni sasa ni fujo

$
0
0

Baada ya msimu wa ligi kuisha kulitembea ufagio katika klabu ya Manchester City na wachezaji kadhaa kuoneshwa mlango wa kutokea, hii ilimaanisha City wanaenda kujijenga upya kwa kuleta wachezaji mpya.

Baada ya dirisha la usajili tu kuanza Gurdiola akawapiga bao Real Madrid na Manchester United kwa kumnunua kiungo wa Monaco Bernardo Silva kwa dau la £43m.

Baada ya kumnunua Bernardo Silva siku kadhaa baadae ndani ya wiki moja Gurdiola kahamia kwa golikipa wa Benfica Ederson ambapo anatarajia kuwa golikipa ghali katika ulimwengu huu wa soka.

Gurdiola amepewa jina jipya la “Mr Cheque Book” jina ambalo amelipewa siku za hivi karibuni kutokana na pesa anazomwaga tu kwa kila mchezaji ambaye anamtaka.

Wakati suala la golikipa Ederson likikamilika tayari habari mpya kutoka familia za mwanasoka anayekipiga katika klabu ya Monaco Benjamin Mendy amekubali kujiunga na klabu ya Manchester City.

Picha za Mendy akiwa katika ndege binafsi siku ya Junapili inahisiwa alikuwa akienda Uingereza ili kukamilisha taratibu za mwisho za usajili wake kwenda Manchester City.

 

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>