Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Mourinho, Matic & Lindelof wanarejea nyumbani: United haijafungwa na Benfica tangu 2005

$
0
0

SL Benfica na Manchester United FC ni wapinzani wa muda mrefu katika soka la barani ulaya – wakati United wakiuwinda ushindi wa 3 katika kundi A huku Benfica wakiutafuta ushindi wa kwanza baada ya kupokea kipigo kizito katika mchezo wa mwisho dhidi ya Basel.

Mechi zilizopita

• United wameshinda mechi 6 katika mechi 9 walizokutana, mchezo wa kwanza ulikuwa ushindi wa robo fainali ya michuano ya ulaya msimu wa 1965/66 na baadae katika mchezo wa fainali ya ulaya msimu wa 1967/68 na United wakashinda ubingwa wa ulaya kwa mara ya kwanza.

• Ushindi pekee wa Benfica dhidi ya United kwa goli la ushindi wa Luisao kwenye ushindi wa 2-1 jijini Lisbon mnamo mwaka 2005, ushindi huo uliiondoa United kwenye makundi ya Champions League kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1994.

• United walilipa kisasi cha kipigo wakati Louis Saha alipofunga goli pekee katika mchezo uliopigwa September 2006 jijini Lisbon. Mchezo wa marudiano katika dimba la Old Trafford – Benfica walianza kufunga lakini wa mchezo United walishinda 3-1 na kuwaondoa Benfica kwenye hatua ya makundi.

• Timu hizi mbili zilipangwa kwenye makundi msimu wa 2011/12, walitoka sare ya 1-1 jijini Lisbon, Ryan Giggs akifunga goli dakika ya 42 na Cardozo Oscar akifunga dakika ya 24.

• Mchezo wa pili ulikuwa November 2011, goli la kujifunga la Phil Jones na goli la Pablo Aimar yaliipa Benfica sare ya 2-2 baada ya magoli ya Dimitar Berbatov na Darren Fletcher.

• Benfica, wakati huo wakiwa wanafundishwa Jorge Jesus, walishika nafasi ya kwanza kwenye kundi C msimu wa 2011/12, United wakamaliza wa 3 nyuma ya FC Basel

Benfica

• The Eagles walipata kipigo kizito zaidi katika UEFA Champions League baada ya kufungwa 5-0 na Basel.

• Benfica wameshacheza mechi 34 dhidi ya vilabu vya Uingereza; rekodi yao inaonyesha wameshinda mechi 11, sare 6 na wamefungwa 17. Walifungwa na United fainali ya ulaya 1968 na pia wakapoteza mchezo wa fainali ya Europa League dhidi ya Chelsea mwaka 2013 jijini Amsterdam

Manchester United

• Rekodi ya United katika michezo dhidi ya vilabu vya Ureno ugenini ni ushindi mechi 6, sare 2 na wamefungwa 4. Hawajapoteza mchezo hata mmoja katika mechi 5 zilizopita nchini humo – mara ya mwisho kufungwa ilikuwa 2005 vs Benfica.

• Huu ni msimu wa 21 katika UEFA Champions hatua ya makundi, ni mara ya 4 tu ndio wameshindwa kuvuka hatua hiyo. Mara 2 kati ya 4 walizotolewa ilikuwa katika misimu 4 iliyopita; United walimaliza nafasi ya 3 msimu wa 2011/12 na 2015/16, msimu wa mwisho katika UCL.

• Mourinho alianza kufundisha soka akiwa Benfica mnamo September 2000, lakini hakukaa sana zaidi ya miezi ya miwili tu. Misimu mitatu iliyofuata alikuwa UD Leiria na FC Porto, alikutana na Benfica mara 7 (Ushindi 4, sare 2, amepoteza 1). Kipigo pekee alipata katika mchezo wa fainali ya kombe la Ureno msimu wa 2003/04.

• Victor Lindelöf amejiunga United akitokea Benfica mwanzoni mwa msimu huu, akiwa ameitumikia Benfica mara 48 katika miaka mitano aliyokaa na klabu hiyo ya Ureno.

• Nemanja Matić alikuwa Benfica kuanzia mwaka 2011 mpaka 2014, alifunga magoli 7 katika mechi 56 za ligi.

• Rui Vitória akiwa UD Vilafranquense walifungwa 4-0 ugenini na Porto ya Jose Mourinho msimu wa 2003/04.

Taarifa za Vikosi

•Manchester United leo wamepata ahueni baada ya Luke Shaw na Marcos Rojo wamejumuishwa katika kikosi kilichosafiri kwenda Lisbon.

United bado itamkosa Paul Pogba, Maroune Fellaini na Michael Carrick.

•Benfica wao watamkosa André Almeida ambaye ana kadi nyekundu ya moja kwa moja aliyopata dhidi ya FC Basel.


Petr Cech ashindwa kuisaidia Gunners katika matuta tangu ajiunge nao

$
0
0

Huwezi kutaja magolikipa watatu wakubwa katika ligi kuu ya Epl ukamuacha mlinda mlango wa Arsenal Petr Cech ambaye tangu amefika Epl amekuwa na mafanikio makubwa akiidakia Chelsea na hatimaye Arsenal.

Lakini Cech pamoja na uhodari wake langoni ila tangu amejiunga na Gunners anaonekana kupwaya sana huku akiwa mlinda lango mwenye rekodi mbovu zaidi katika ligi kuu katika mikwaju ya penati.

Rekodi zinaonesha tangu Cech asaini Arsenal hajawahi kupangua wala kudaka mkwaju wa penati hata mmoja na penati zote 11 zilizopigwa langoni mwake tangu ajiunge na Arsenal zimekwenda nyavuni.

Hali hii ni tofauti na alipokuwa Chelsea ambapo alifanikiwa kuokoa mikwaju minne ya penati katika ligi ya Epl na huku akicheza mikwaju mitatu katika michuano mikubwa ya Champions League.

Wakati magolikipa wemgine kama David De Gea akiokoa penati mbili kati ya 17 zilizoelekezwa langoni mwake, golikipa wa Liverpool Simon Mignolet ni kinara wa kuokoa penati ambapo hadi sasa ameshacheza penati 7 kati ya 15.

Mwishoni mwa wiki Arsenal walijikuta wakipigwa bao mbili kwa moja na Watford huku bao la kwanza la Watford likiendeleza rekodi mbovu ya Petr Cech kuokoa matuta baada ya Trooy Deney kufunga kwa mkwaju wa penati.

Ujumbe wa mke wa Niyonzima kwa mumewe

$
0
0

Mke wa kiungo wa Simba Haruna Niyonzima amemwambia mumewake inabidi aongeze juhudi zaidi ili aendelee kuwafurahisha mashabiki wake.

Mama watoto huyo wa Niyonzima alizungumza na Jacob Mbuya wa Clouds Media Group baada ya mchezo wa Simba dhidi ya Mtibwa Sugar uliomalizika kwa sare ya kufungana 1-1.

“Nampongeza kwa sababu alicheza vizuri kwa namna nilivyoona, lakini naomba aongeze nguvu kwa ajili ya kuwafurahisha wanaompenda.”

Alipoulizwa kuhusu changamoto anazopata kufuatia mumewake kuhama kutoka Yanga kwenda Simba amesema hakuna ugumu anaopitia zaidi ya kubadili marafiki.

“Unajua Niyonzima alicheza kwa muda mrefu Yanga, nilipata marafiki wengi lakini baada ya kuhama sio wote waliokuwa marafiki wakati yupo kule wataendelea kuwepo hadi sasa baada ya kuhama.”

Idadi ya majeruhi yazidi kuongezeka Stamford Bridge

$
0
0

Wakati mashabiki wa Chelsea wakiendelea kuuguza kidonda cha kupokea kipigo cha mabao 2 kwa 1 kutoka kwa Crystal Palace klabu ya Chelsea imepokea habari mbaya nyingine baada ya idadinya majeruhi kuongezeka.

Victor Moses ameungana na Alvaro Morata na Ngolo Kante katika orodha ya majeruhi wa Chelsea baada ya Mnigeria huyo kuumia katika mchezo dhidi ya Crystal Palace.

Habari zinasema Moses atakuwa nje ya uwanja kwa wiki nne ambazo ni sawa na mwezi mmoja hali itakayompelekea kukosa mchezo kati ya Chelsea na Manchester United ambao utapigwa tarehe 5 mwezi ujao.

Kiujumla Moses atakosa michezo saba ikiwemo michezo miwili ya Champions League dhidi ya As Roma na pia Bournemouth, Watford, Everton,Manchester United na West Bromich Albion.

Habari hizi zinaweza kuwa njema kwa mchezaji mpya wa Chelsea Davide Zapaccosta kwani anaonekana anaweza kuwa mtu sahihi kuziba pengo la Victor Moses ambaye msimu huu ulianza vizuri kwake.

Chelsea watakuwa uwanja wa nyumbani wa Stamford Bridge siku ya Jumatano ambapo wataikaribisha As Roma katika muendelezo wa michuano ya Champions League.

Kapumzike Ricardo Izecson “Kaka” mcha mungu uliyejaa upako miguuni mwako hakika umewaachia vijana somo hili

$
0
0

Miaka ya 2006/2007 kulikuwa na mchezaji mmoja ambaye kila mtu aliamini kwamba mipira ilikuwa ikiisikiliza miguu yake, ilisemekana alikuwa na uwezo wa kuambia mpira toka hapa nenda pale na mpira ukatii.

Watu waliamini hivyo kutokana na uwezo wake mkubwa aliokuwa akiounesha uwanjani na sio siri alimfanya kila kijana atamani kucheza mpira kwani aliufanya mpira uonekana kazi rahisi sana ukiwa unatumia akili.

Ricardo Izecson Dos Santos Leite mzaliwa wa Gama mwaka 1982 almaarufu kama Kaka ni mchezaji ambaye wazi wazi ilionekana kwamba mungu alikuwa na mpango juu ya miguu yake na ndio maana pamoja na majeraha makubwa akiwa mtoto lakini bado alipiga soka.

Kaka alikuwa kama mtumwa wa mungu aliyekuja kuonesha alichonacho na ndio maana wakati akiwa mtoto na umri wa miaka 18 tu alivunjika mguu ajali ambayo hadi madaktari waliamini ataparalyse na hatarudi uwanjani lakini wiki kadhaa baadae Kaka alivaa njumu na kwenda kukipiga uwanjani.

Jina la Kaka lilianza kuwa maarufu wakati akiwa bado yuko Sao Paulo lakini umaarufu uliongezeka zaidi mwaka 2003 wakati anajiunga na Ac Millan kuchukua nafasi ya Rui Costa kwa ada ya £8.5m na hapo dunia nzima ikaanza kushangaa uwezo wa Mbrazil huyu.

Akicheza pamoja na Andriy Shevchenko, Pipo Inzaghi na John Dahl Thomason aliifanya Rossoneri waonekane kama klabu ambayo haikuwa na namna ya kuzilika kukufunga kwani uwepo wake nyuma ya mtu kama Shevchenko ilikuwa ndoto ya kutisha kwa wapinzani.

Mwaka 2007 Kaka alichukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia lakini hakutaka kupop champagne kama wachezaji wengine wafanyavyo bali aliichukua tuzo yake na kuipeleka nyumbani kwao Sao Paulo ambako watu walimshukuru mungu kwa tuzo hiyo.

Tofauti kabisa na nyota bora wa dunia wa sasa Cristiano Ronaldo na vijana wengi wanasoka, Kaka hakuwa na tabia za kufuata fuata wanawake na hajawahi kufanya tendo la ndoa hadi mwaka 2008 ambapo ndio mwaka aliomuoa mke wake na mpenzi wa muda mrefu Carolline Celico.

Ukiacha Ronaldinho mpiga chenga wa Brazil, Kaka ndiyo mchezaji creative zaidi kuwahi kumuona na Brazil, uwezo wake wa kudrible huku akicheza soka bila kusukumana kwa kipindi kile vilinifanya kuamini hakuta kuja kutokea kama Kaka.

Safari ya Real Madrid ndio ulikuwa mwanzo wa Ricardo Kaka kupotea mchezoni kwani tangu ajiunge nao majeruhi yamekuwa yakimuandama kila siku huku akizungukwa na washambuliaji wengi wakubwa Rafael Van De Vaart, Karim Benzema, Raul Gonzalez, Gutti na Gonzalo Higuain.

Kaka hakuwahi kuwa na tamaa za pesa kama ilivyo kwa nyota wengine wa ukanda wa America Kusini alikuwa special sana na kwa asili ya atokeako ilikuwa ngumu kukataa uhamisho ambao angepewa £500,000 kwa wiki tena mwaka 2009 lakini alikataa huku sababu za kiimani zikitajwa.

Kaka alikuwa akitoka mazoezini hurudi nyumbani kwake na kusikiliza kwaya na kundinalipendalo lilikuwa Four Bishops, Kaka kila bao alilofunga anaamini linatoka kwa mungu na ndio maana kila akifunga hunyoosha mikono angani.

Majeraha yalipopitiliza ndani ya Bernabeu huku Madrid wakimuongeza nyota mpya Cr7 kikosini vilimfanya Kaka mwaka 2013 kurejea Millan na kisha akarudi nyumbani kwao Sao Paulo kwa mkopo kucheza kwa muda kabla ya kwenda Orlando City alikomalizia soka lake.

Lioneil Messi na Cristiano Ronaldo wanatajwa sana kuwa bora kuwahi kutokea duniani lakini huwezi kuwa bora sana wakati kombe la dunia hujawahi kuligusa, Kaka alibeba Ballon D’or, alibeba Champions League na alibeba kombe la dunia na hii inamfanya kuwa bora zaidi.

Carlos Alberto Perreira alikuwa kocha wa kwanza kumuita Kaka katika timu ya taifa na pamoja na majeraha ya mara kwa mara lakini alifanikiwa kuichezea timu ya taifa michezo 92 idadi sawa na Pele na kubwa kuliko Rivaldo, Neymar, Dida na Dunga.

Kaka ambaye anasema kitabu akipendacho zaidi ni biblia alicheza mchezo wake wa mwisho akiwa na Orlando City na kuithibitishia dunia kwamba sasa anarudi nchini kwao kupumzika na mwili umechoka hawezi kuendelea tena, hakika mwili lazima uchoke kutokana na burudani kubwa uliyoionesha dunia, ASANTE KAKA.

Nina sababu za kuamini Mecky Maxime atainyanyua Kagera Sugar

$
0
0

Mechi sita za VPL zimeshapigwa, Kagera Sugar ipo mkiani ikiwa na pointi mbili ambazo imezipata katika mechi ambazo wametoka sare bado hawajapata ushindi hadi sasa.

Yameanza kuzungumzwa maneno mengi juu ya kufanya vibaya kwa Kagera Sugar huku kocha Mecky Maxime akiwa anatajwa kuwa sababu ya timu hiyo kufanya vibaya.

Binafsi bado ninaamini Kagera Sugar itanyanyuka na kufanya vizuri chini Maxime licha ya wachache kuanza kubeza uwezo wake.

Mashabiki wa timu hiyo walibeba mabango wakitaka Maxime aondoke Kagera Sugar kufuatia timu yao kufanya vibaya mwanzoni mwa ligi huku wakibamizwa 6-0 na Yanga kwenye uwanja wao wa Kaitaba.

Msimu uliopita vs msimu huu

Mechi za mwanzo wa ligi msimu uliopita, Kagera ilianza vibaya kwa kuchezea vichapo vya mara kwa mara sawa na msimu huu ambapo hadi sasa bado hawajafanya vizuri.

Msimu uliopita Kagera Sugar ilimaliza nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi nyuma ya Yanga na Simba huku wakiwa juu ya Azam ambao walimaliza katika nafasi ya nne. Hapo ni namna gani Maxime amedhihirisha alivyokuwa mpambanaji ndani ya kikosi cha ‘wanankurunkumbi.’

Katika mechi 30 za ligi msimu uliopita Kagera walishinda mechi 15, wakatoka sare katika mechi saba na kupoteza mechi tano.

Hadi sasa timu yake haijashinda katika mechi sita walizocheza msimu huu kibaya zaidi Kagera haifungi magoli mengi, wamefunga magoli mawili tu katika michezo hiyo sita.

Bado naamini Kagera Sugar itanyanyuka

Ligi yetu jinsi ilivyo bado Kagera Sugar ina nafasi ya kufanya vizuri ikiwa chini ya Maxime na kumaliza katika nafasi waliyomaliza msimu uliopita.

Licha ya kutoshinda hata mchezo mmoja, ina pointi mbili ikiwa mkiani mwa ligi, Simba wanaoongoza ligi wana pointi 12 sawa na timu nyingine tatu (Mtibwa Sugar, Yanga na Azam) Simba na Kagera zinatofautishwa na pointi 10.

Ukiachana na Simba, Mtibwa Sugar, Yanga, Azam, Singida United, timu nyingine bado pia hazijafanya vizuri kwa sababu bado mechi nyingi zimekuwa zikitawaliwa na matokeo ya sare.

Timu bado nzuri

Licha ya kuondokewa na mfungaji wao Mbaraka Yusuph Abeid aliyejiunga na Azam, bado hakumaanishi Kagera Sugar imekwisha.

Kikosi cha Maxime ni kizuri na kina weza kukaa sawa, uwepo wa wachezaji wazoefu kama Juma Kaseja, Juma Nyoso, George Kavila, Geoffrey Taita, Ame Ali ‘Zungu’ wakisaidiana na vijana wanahitaji ushindi wa kwanza ili kuendeleza fomu ya ushindi.

Baada ya kiongozi wa Yanga kuchaguliwa kuongoza TPLB , Hans Poppe kazungumza haya

$
0
0

Mwenyekiti wa usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe amesema mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara (TPLB) Clement Sanga atende haki katika uongozi wake bila kujali kuwa yeye ni kiongozi wa Yanga.

“Yeye kuipenda Yanga hatumzuii kwa sababu ni mpenzi wa Yanga na kiongozi kule lakini atende haki asijipendelee”-Hans.

“Sasa hivi tunataka maendeleo ya soka sio mambo ya longolongo. Clement Sanga ni mtu ambae namfahamu nimezungumza nae mara kwa mara kwa mtazamo wake ni mtu ambae anapenda maendeleo nina imani atatekeleza wajibu wake vizuri.”

“Nimshauri tu kama kuna mambo anatakiwa ayasikilize wao kama rufaa basi wafanye ndani ya muda na kusimamia ratiba isibadilishwe mara kwa mara.”

Sanga ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa klabu Yanga amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara akimwangusha Ahmed Yahaya aliyekuwa madarakani awali kabla ya uchaguzi kufanyika.

Taarifa rasmi kuhusu majeruhi 4 Simba na mechi watakazokosa VPL

$
0
0

Mchezo wa ligi kuu Tanzania bara Jumapili iliyopita kati ya Simba dhidi ya Mtibwa Sugar ulishuhudia wachezaji wawili wa Simba wakishindwa kuendelea mchezo baada ya kupata majeraha.

Leo Jumanne October 17, 2017, afisa habari wa Simba ametoa taarifa ya maendeleo ya wachezaji wate wanaosumbuliwa na majeruhi na muda watakao kaa nje ya uwanja.

John Bocco

John Bocco aliumia kisigino na kupata maumivu ambayo yatamweka nje kwa siku mbili tatu hali itakayomfanya akose mchezo dhidi ya Njombe Mji Jumamosi October 21, 2017.

Salim Mbonde

Beki wetu wa kati ambaye tunamtegemea sana Salim Mbonde ameumia goti maumivu ambayo yatamfanya akose mechi nne (Njombe Mji, Yanga, lakini pia anaweza akakosa menchi nyingine mbili dhidi ya Tanzania Prisons na Mbeya City.)

Ripoti ya madaktari inasema maumivu yake sio makubwa sana lakini anahitaji kukaa nje kwa ajili ya kutumia dawa lakini kama itakuwa vinginevyo basi tutawataarifu.

Said Mohamed ‘Nduda’

Amerejea nchini lakini tofauti na maumivu aliyoyapata Zanzibar ambayo yalipelekea apelekwe India kwa ajili ya upasuaji, alikutwa na tatizo jingine ambalo alikuwa nalo kwa muda mrefu, kwa hiyo madaktari wakamfanyia upasuaji ambapo kwa bahati nzuri wamefanikiwa kwa asilimia 100.

Nduda atakaa nje kwa wiki nane tangu siku aliyofanyiwa upasuaji, maana yake tutaanza kuwa na Nduda kwenye kikosi kuanzia mwezi December.

Shomari Kapombe

Madaktari wameendelea kusisitiza aendelee kupona taratibu matatizo yake ya nyonga inawezekena yalikuwa makubwa tunaamini muda ambao madaktari wamesema akae nje tuendelee kumpa muda na kumvumilia.


Precision Air yaongeza nguvu udhamini Rock City Marathon

$
0
0

SHIRIKA la ndege la Precision Air leo limetangaza udhamini wake wenye thamani ya  Sh 20 milioni kwa ajili ya mbio za Rock City Marathon zinazotarajiwa kufanyika Octoba 29 jijini Mwanza.

Kwa udhamini huo, shirika hilo sasa linatambulika rasmi kama shirika maalum la usafiri wa mbio hizo miongoni mwa wadhamini wengine zikiwemo kampuni za PUMA, Tiper, RedBull, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), New Mwanza Hotel, EF Out door, CF Hospital, KK Security, na kampuni ya uchapishaji ya SDS.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Meneja Masoko na Mahusiano wa Precision Air Bw. Hillary Mremi alisema udhamini huo kwa kiasi kikubwa umechagizwa na malengo ya mbio hizo yaliyojikita katika kutangaza utalii wa ndani kupitia mchezo wa riadha.

“Lakini pia kibiashara tunaona kwamba mara nyingi watu wanaopenda kushiriki riadha wamekuwa na ‘hobby’ pia kusafiri sehemu tofauti tofauti ndani na nje ya nchi hivyo ushiriki wetu kwenye mbio hizi utazidi kutukutanisha na kundi hili muhimu,’’ alibainisha.

Zaidi alionyesha imani kuwa mbio hizo zitakazofanyika jijini Mwanza zitakata kiu ya washiriki wake wakiwemo abiria wa shirika hilo kwa kuwa tofauti na mchezo huo, jiji hilo lina vivutio vingi vya kitalii ikiwemo fukwe za Ziwa Victoria, Hifadhi ya Kisiwa cha Saanane na makumbusho ya kabila la wasukuma (Bujora).

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mbio hizo, Bw. Zenno Ngowi alisema kwao ni heshima kubwa kushirikiana na shirika hilo lenye heshima kubwa kwenye usafiri wa anga hapa nchini.

“Tunaamini kwamba ushirikiano huu na shirika hili linalotambulika kimataifa kwa ubora wa huduma zake za usafiri wa anga utaziweka na mbio hizi pia katika ngazi ya kimataifa.’’ alisema.

Aliongeza kuwa udhamini huo unamaanisha kwamba uhusiano wa shirika hilo na wateja wake hautaishia ndani ya ndege bali utaendelea zaidi hadi kwenye mitaa, fukwe, viwanja vya michezo na sehemu zote za utalii katika jiji la Mwanza na Kanda ya Ziwa yote.

Kwa upande wake Mratibu wa mbio hizo kutoka Kampuni ya Capital Plus, Bw. Bidan Lugoe alisema maandalizi yanaendelea vizuri na kwamba wamejipanga kupokea washiriki zaidi ya 4,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakiwemo viongozi na watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino.

“Kiukweli muitikio ni mkubwa sana kutoka ndani na nje ya nchi! Tofauti na washiriki wa kawaida kuna idadi kubwa ya viongozi wa serikali na kisiasa ambao tayari wamethibitisha ushiriki wao,’’ alisema Lugoe.

Aliwataja baadhi ya waliothibitisha ushiriki wao kuwa ni pamoja na baadhi ya wakuu wa mikoa ya Kanda ya Ziwa, Makamanda wa Jeshi la Polisi pamoja na wale wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Akizungumzia usajili wa mbio hizo Bw. Bidan alisema kwa wakazi wa jiji la Mwanza na mikoa jirani wanaweza kujisajili kwa kuchukua fomu katika Ofisi za michezo wilaya zote za mkoa wa Mwanza, Ofisi za riadha mikoa ya Geita, Simiyu na Shinyanga.

Sehemu nyingine ni pamoja na  Uwanja wa Nyamagana,  Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino  Mwanza, Kituo cha michezo  Malya, Shule ya Kimataifa ya Isamilo, New Mwanza  Hotel na Ofisi za EF Out door zilizopo jingo la Rock City Mall.

“Kwa upande wa Dar es Salaam Fomu za ushiriki pia zinapatikana jengo la SHAMO Tower, Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam’’ alitaja.

Fukuza fukuza ya makocha yaendelea Epl

$
0
0

Baada ya mafanikio makubwa sana waliyopewa na kocha aloyepita Claudio Ranieri inadaiwa wachezaji walianza kumsaliti Ranieri na kuwafanya mabosi kusahau fadhila zake wakamtimua na akaja Craig Shakespeare.

Baada ya kupewa timu akaiongoza michezo 16 huku akifanikiwa kuipeleka Leicester City katika robo fainali ya Champions League msimu uliopita na kuwafanya Leicester kumaliza ligi nafasi ya 12.

Msimu huu ukaanza huku Shakespeare akionekana kati ya makocha ambao ni wazi walikuwa wakifundisha akiwa na presha kubwa sana kutokana na matokeo yalivyobadilika ndani ya timu.

Tangu msimu kuanza Leicester wamecheza jumla ya michezo 10 katika mashindano yote lakini katika michezo yote hiyo wefanikiwa kushinda michezo mitatu tu, wakisuluhu mara 3 na vipigo vinne.

Katika mechi 3 Leicester walizoshinda ni mechi moja tu ya Epl na ewko nafasi ya 18 ya ligi wakiwa na alama zao 6 huku tangu kocha huyo ajiunge nao wakikubali kupigwa jumla ya mabao 43.

Tayari makocha mbalimbali akiwemo Carlo Ancelotti, Sam Alladayce, Allan Pardew na David Moyes wanatajwa kwenda Leicester City kuchukua mikoba ya Shakespaere.

Mabao 7 ya Liverpool hii leo yavunja rekodi ya Manchester United na kuweka rekodi mpya, matokeo yote haya hapa

$
0
0

Hii leo ilikuwa mara ya kwanza kwa klabu ya Liverpool kufunga idadi ya mabao 5 katika mechi ya ugenini katika michuano ya Champions League, michezo yao 45 iliyopita ya Champioms League hawakuwahi kufanya hivyo.

Robert Firminho (4), Phellipe Coutinho (13) na Mohamed Salaah (19,40) waliufanya mchezo uende mapumziko huku Liverpool wakiongoza kwa mabao 4 kabla ya Firmninho kuweka la tano kipindi cha pili.

Lakini bao la 6 la Oxlade Chamberlain liliwafanya kuwa klabu ya pili Uingereza kuwahi kufunga mabao 6 katika mchezo wa ugenini ya Champions League rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Manchester United huku ikiwa timu ya 9 kufanya hivyo.

Na bao la 7 la Alexander Arnold likawafanya Liverpool kuwa timu ya nne kuwahi kufunga jumla ya mabao 7 na zaidi ambapo timu za Bayern Munich, Barcelona na Lyon zimewahi kufanya hivyo na isitoshe kwa usiku wa leo Liverpool ilikuwa timu pekee ambayo haikuruhusu bao.

Manchester City waliipiga Napoli bao 2 huku Gabriel Jesus akifunga moja ya bao linalomfanya kufunga mabao 15 ndani ya michezo 22 ikiwa ni mchezo mmoja nyuma ya Kun Aguero wakati anafunga mabao kama hayo alipofika Man City.

Real Madrid wakiwa Santiago Bernabeu almanusra waambulie kichapo baada ya bao la kujifunga la Rafael Varane lakini dakika ya 43 ya mchezo Cristiano Ronaldo aliwaokoa Madrid kwa mkwaju wa penati.

Kwa suluhu ya leo Tottenham Hotspur wanakuwa timu ya tatu kuwahi kupata alama katika uwanja wa Santiago Bernabeu katika michezo ya Madrid 24 iliyopita katika Champions League.

Bao la Papstathopoulos liliookoa Dortmund kutoka katika kipigo na kuwafanya kutoka sare ya moja kwa moja dhidi ya Apoel Nicosia, huku Monaco wakifungwa 2 kwa 1 na Bestikas katika uwanja wao wa nyumbani.

Sevilla walijikuta wakiaibika kwa bao 5 kwa 1 kutoka kwa Spartak Moscow huku mabao ya Moscow yakiwekwa kimiani na Luiz Adriano, Promez, Giushakov na Dzhkiya.

Msimu Mpya Wa NBA Waanza, Vita Ya Kyrie Irving Dhidi Ya Lebron James Yaingia Dosari.

$
0
0

Baada ya kusubiri kwa muda mrefu tangu Golden State Warriors wawe mabingwa wa msimu wa 2016-2017 hatimaye msimu mpya wa 2017-2018 umeanza rasmi alfajiri ya leo huku kukiwa na drama za hapa na hapa hasa kutokana na usajili wa msimu huu ulivyofanyika.

Tofauti na ilivyotegemewa na wengi, msimu huu Kyrie Irving alikuwa ndiye mchezaji wa kwanza kutangaza hadharani nia yake ya kutotaka kucheza na Lebron James na kuhitaji kwenda kwenye klabu nyingine ambapo timu iliyokuwa inaweza kutoa walichohitaji Cavaliers ikawa ni Boston Celtics kwa kuwatoa Jae Crowder na Isaiah Thomas.

Ukiwa na mchezo ambao ulitegemewa kuvuta hisia za wengi hasa kuongeza wigo wa watazamaji, Kyrie Irving kama ilivyotegemewa alizomewa kila pale ambapo aligusa mpira ndani ya uwanja wa Quicken Loans Arena, Ohio Cleveland. Lakini hisia za upinzani huu hazikudumu sana kwani mchezaji Gordon Hayward ambaye naye alikuwa mchezaji aliyesajiliwa na Boston Celtics alitua vibaya wakati akiruka na kupelekea kuvunjika mguu wake kwenye maeneo ya mfupa wa ugoko na kutengua Kifundo cha mguu.

Majeruhi haya yanayoweza kumweka nje kwa msimu huu wote yalipelekea mchezo kubadilika huku wachezaji wote wakionekana kuumizwa na tukio hilo lakini Cavaliers waliweza kuibuka na ushindi wa pointi 102-99. Lebron James alifunga pointi 29, Kevin Love akaongeza 15 na Derick Rose akafunga 14 kwa upande waCavs.

Kyrie Irving alimaliza mchezo na alama 22 na assist 10 huku mchezaji Jaylen Brown aliyeibuka na kuziba nafasi ya Hayward ndani ya mchezo akimaliza mchezo huo na alama 25.

HIGHLIGHTS

Golden State Warriors Chali Mechi Ya Kwanza Ya Msimu.

$
0
0

Wakiwa ni mabingwa watetezi huku pia wakiwa wametwaa ubingwa wa NBA mara mbili na kuingia fainali mara tatu mfululizo katika kipindi cha misimu mitatu iliyopita, klabu ya Golden State Warriors ikiendelea kuwa chini ya kocha Steve Kerr ilikuwa inafungua pazia la ligi ya NBA dhidi ya Houston Rockets, alfajiri ya leo kwenye uwanja wa Orcale Arena, huko Oakland San Fransisco.

Warriors walianza kwa kuwa na sherehe fupi ya kukabidhiwa pete zao ambazo ni zawadi ya kutwaa ubingwa wa NBA. Lakini huku kwenye michezo mingine ikiwa imezoeleka kuwa na medali kwenye NBA na michezo mingi ambayo asili yake ni Marekani hutumia pete kama zawadi rasmi.

Golden State Warriors ilianza mchezo huu bila ya kuwa na nyota wake Andre Iguodala ambaye ana majeraha, lakini pia ikiwakaribisha wachezaji wapya Nick Young, Jordan Bell ambaye ni kinda kutoka chuoni na Omri Casspi.

Mchezo huo ambao ulikuwa kama sherehe ya mitupo ya pointi 3, ilishuhudia Warriors wakimaliza mchezo kwa kupoteza dhidi ya James Harden na Chris Paul ambaye amejiunga na Houston Rockets akitokea Los Angeles Clippers kwa pointi 121-122. Harden aliiongoza Houston kwa kufunga pointi 27, Erick Gordon akifunga pointi 24 na PJ Tucker akimaliza na alama 20.

Warriors waliongozwa na Stephen Curry aliyefunga pointi 22, Klay Thompson akaongeza 16, Kevin Durant akafunga pointi 20 baada ya kutokuanza vyema mchezo, huku Nick Young akimaliza mchezo na alama 23 akitokea benchi akiwa amepata mitupo 6 ya pointi 3. Draymond Green alitoka katika robo ya tatu na hakuweza kurejea kutokana na kuumia goti.

HIGHLIGHTS

 

 

Huyu ndiye Yusuph Mgeta, aliyemficha Okwi pale Kirumba Mwanza

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

“Silaha yangu kubwa uwanjani napokabiliana na washambuliaji wa timu pinzani  ni kutumia akili nyingi panapotakiwa, na nguvu panapotumika,” anaanza kusema mlinzi wa kati wa Mbao FC, Yusuph Amos Mgeta nilipofanya naye mahojiano wiki hii akiwa jijini Mwanza wakijiandaa na mchezo wa raundi ya saba katika ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC siku ya Jumamosi ijayo.

Mlinzi huyo mwenye ‘mwili wa beki’ alikuwa wa kwanza msimu huu kuwaonyesha mabeki wa timu  nyingine jinsi ya kumzima mshambulizi wa Simba na kinara wa ufungaji katika VPL, Mganda, Emmanuel Okwi wakati Mbao FC ilipolazimishwa sare ya kufungana 2-2 na Simba SC katika uwanja wa Kirumba, Mwanza mwezi uliopita.

Mgeta ambaye huu ni msimu wake wa pili kucheza ligi kuu, amesajiliwa Mbao FC msimu huu kama mbadala wa Mghana, Ahsante Kwassi aliyejiunga na Lipuli FC ya Iringa msimu huu.

Mgeta alikuwa pacha wa Yusuph Mlipili katika beki ya Toto Africans msimu uliopita ameonekana kucheza vizuri na nahodha wa Mbao, Mrundi, Yusuph Ndikumana katika beki ya kati ya timu hiyo licha ya kwamba tayari wameruhusu magoli 9 katika michezo 6 msimu huu.

Akiwa tayari amecheza michezo minne kati ya sita ya kikosi cha Mbao FC, Mgeta alionyesha namna alivyo na uwezo wa kukimbia na kucheza vizuri na Okwi jambo ambalo lilimuondoa mchezoni mshambulizi huyo wa
Simba aliyefunga magoli 7 katika michezo mitano.

“Tunaenda kucheza na Azam FC na utakuwa mchezo mwingine mgumu. Bado tunapambana kujiweka sawa,” anasema Mgeta ambaye kikosi chake kitawavaa mabingwa hao wa msimu wa 2013/14 kikiwa nafasi ya tisa katika msimamo.

“Kwa sasa naomba uzima tu, nimejipanga kwa nguvu ya mwenyezi Mungu kufanya mambo makubwa msimu huu na kuisaidia klabu yangu.”

MAMBO MENGINE YA MUHIMU KUJUA KUHUSU MGETA

Amezaliwa, Mei 15, 1994 katika Hospitali ya Somanda, Bariadi. Amesoma Somanda Shule ya Msingi, Bariadina kuhitimu darasa la saba mwaka 2006.

Wazazi wake ni wenyeji wa Musoma na kwa sasa wanaishi huko. Baba yake mzazi alikuwa daktari katika Hospitali ya Somanda, Bariadi.

Yusuph ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia ya watoto wane ya Mzee Mgeta.

Mlinzi huyo wa kati anavaa jezi namba 16 katika kikosi cha Mbao FC, lakini anasema alichagua namba hiyo kwa sababu alikosa namba anayoipenda-namba 6.

Ni shabiki mkubwa wa mlinzi wa klabu ya Arsenal ya England na timu ya Taifa ya Ufaransa, Laurent Koscielny. Pia ni shasbiki wa mabingwa hao mara 13 wa kihistoria wa EPL.

Video: Kammpuni ya GF Trucks & Equipment wametekeleza ahadi yao kwa Mbao FC

$
0
0

Kampuni ya GF Trucks & Equipment leo October 18, 2017 imekabidhi basi kwa klabu ya Mbao FC ya jijini Mwanza litakalotumika katika shughuli za timu kufuatia kusaini mkataba wa kuidhamini timu hiyo August 25 mwaka huu.

Unaweza kuangalia story kamili kupitia Dauda TV kwa kubofya play kwenye video hapa chini.


Vipigo vikubwa kuwahi kutolewa Champions League

$
0
0

Siki ya jana tulishuhudia kalbu ya Liverpool ikitoa dozi ya mabao 7 kwa 0 dhidi ya Maribor, hii ilikuwa kwa mara ya kwanza kwa Liverpool kufanya hivyo katika uwanja wa ugenini kwenye Champions League.

Mabao 7 sio jambo la kushtuka sana lakinj mabao 7 ugenini ilikuwa kipigo kikubwa sana, Liverpool wameshawahi kufunga mabao zaidi ya matano katika Champions League lakini haikuwa ugenini, kwa haraka haraka hivi ni vipigo vikubwa kuwahi kutolewa Champions League.

Arsenal 7 Slavia Prague 0, hii ilikuwa October mwaka 2007 katika uwanja wa Emirates ambapo Gunners waliwakaribisha Slavia Prague, mabao mawili kutoka kwa Theo Walcott, mawili kutoka kwa Fabregas na mengine kutoka kwa Hubacek,Hleb na Bendtner wakailaza Prague bao 7.

Bayern Munich 7 Shaktar Donestki 0, huu ulikuwa msimu wa mwaka 2014/2015 pale Allianz Arena, Thomas Muller alifunga mara mbili,Boateng, Ribery, Badstuber,Lewandoski na Gotzw waliongoza kikosi cha maangamizi kuwaua Shaktar.

Bayern Munich 7 Fc Basle 0, Bayern hawa hawa walikutana na Fc Basle mwaka 2012 na kuwapiga bao 7 kwa nunge, Arjen Robben alifunga mara mbili, Thomas Muller akafunga mara moja huku Mario Gomez akifunga mabal manne katika dimba la Allianz Arena.

Real Madrid 8 Malmo 0, hii ilikuwa mwaka 2015 palw Santiago Bernabeu ambapo Cristiano Ronaldo alifunga mara nne, Karim Benzema akafunga mara tatu huku Kovacic akifunga moja na kuwaua Malmo kwa jumla ya mabao 8 kwa nunge.

Liverpool 8 Bestikas 0, mwaka 2007 ambapo Liverpool ilikuwa kati ya timu za kuogopwa Ulaya, Bestikas walikwenda Anfield na mabao ya Yossi Benayoun aliyefunga hat trick, Peter Crouch mawili,Ryan Babel mawili na  Steven Gerrad aliyefunga moja yaliwaaibisha Bestikas katika mchezo huo.

Picha: Mazoezi ya kwanza Simba bila Jackson Mayanja

$
0
0

Kikosi cha Simba leo October 18, 2017 kimefanya mazoezi chini ya kocha mkuu Joseph Omog bila uwepo wa kocha msaidizi Jackson Mayanja ambaye ametangaza kujiuzulu nafasi yake kwa sababu alizodai ni za kifamilia.

Wachezaji wote ambao wako fit Simba wamefanya mazoezi kwenye uwanja wa Uhuru, Dar ikiwa ni maandalizi kuelekea mchezo wao wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Njombe Mji siku ya Jumamosi October 21, 2017 kwenye uwanja huohuo.

Sababu kubwa iliyotajwa na Mayanja kujiuzulu ni kwamba, anahitaji muda wa kutatua matatizo ya kifamilia yanayoikabili familia yake iliyopo nchini Uganda. Mayanja pia amewashukuru mashabiki na wapenzi wa timu hiyo, wachezaji pamoja na benchi la ufundi bila kusahau uongozi wa klabu hiyo kongwe nchini.

Mayanja ameitumikia Simba kwa zaidi ya misimu miwili, alijiunga na klabu hiyo kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Selemani Matola ambaye pia alijiuzulu nafasi ya kocha msaidizi chini ya muingereza Dylan Kerr. Siku chache baada ya Mayanja kusaini mkataba wa kuifundisha Simba kama kocha msaidizi, klabu hiyo ilimtimua Kerr aliyekuwa kocha mkuu wakati huo na Mayanja akapewa jukumu la kuiongoza timu.

Antonio Conte aandika rekodi mbovu nyingine wakati wakibanwa mbavu darajani, matokeo ya CL Jumatano ya leo haya hapa

$
0
0

Eden Hazard alifunga mara mbili, idadi ambayo ni kubwa kuliko magoli yote aliyofunga katika mechi 14 za Chelsea zilizopita na David Luiz alifunga moja katika sare ya bao tatu tatu dhidi ya As Roma.

Mabao ya As Roma yeliwekwa kimiani na Aleksandre Kolarov na Eden Dzeko aliyefunga mara mbili na kumfanya Antonio Conte kwa mara ya kwanza kuruhusu mabao 3 katika mechi moja ya Champions League.

Lioneil Messi alifunga bao lake la 100 katika michuano ya soka Ulaya wakati Barcelona wakiifunga Olympiacos mabao 3 kwa 1 huku mabao mengine yakiwekwa kimiani na Nikolaou na Lucas Digne, huku Gerrad Pique akipewa kadi yake nyekundu ya kwanza katika Champions League.

Juventus walitoka nyuma ya bao moja na kuibuka na ushindi wa mabao 2 kwa 1 dhidi ya Sporting Cp huku mabao ya Juventus yakiwekwa kimiani na Stefanl Sturalo huku la ushindi likiwekwa kimiani na Mario Mandzukic.

Paris Saint German waliibuka kidedea kwa mabal 4 kwa nunge huku Kylian Mbappe, Edson Cavanni,Neymar na Di Maria wakifunga na goli la Cavanni likamfanya kuwa mchezaji wa 3 kufunga katika michezo 7 mfululizo katika Champions League baada ya Niestrooy na Cr7.

Matokeo mengine Manchester United waliichapa Benfica bao 1 kwa sifuri bao la Marcus Rashford, Bayern Munich wakawapiga Celtic 3 kwa nunge, Athletico Madrid na Quarabag Fk wakaenda sare ya bila kufungana.

Manchester United na Chelsea zazidi kuongeza majeruhi huku Conte na Mourinho wakitupiana vijembe

$
0
0

Marcus Rashford jana alifunga bao pekee katika mchezo wa Champions League dhidi ya Benfica na kuiweka United kileleni mwa kundi lao lakini Rashford huyo huyo anaingia kwenye kundi la majeruhi la Paul Pogba, Eric Bailly na Morouane Fellaini.

Chelsea nao jana walikuwa uwanjani wakishuhudia timu yao ikiongoza mabao mawili na baadaye yakarudi yote lakini wakafanikiwa kutoka suluhu ya mabao matatu kwa matatu dhidi ya As Roma.

Chelsea ambao walimkaribisha Alvaro Morata aliyetoka kuwa majeruhi bado wanamkosa kiungo wao mkabaji Ngolo Kante ambaye aliumia wakati akiwa katika majukumu kuitumikia timu yake ya taifa.

Nafasi ya Kante ilichukuliwa na Tiomoue Bakayoko ambaye taarifa zinasema na yeye ameumia baada ya mchezo wa jana huku mlinzi wa kati David Luiz naye akipata majeraha yatakayomuweka nje kwa muda.

Kocha wa klabu hiyo Antonio Conte amesema hawezi kuhatarisha afya za wachezaji wake na kwa kuwa wameumia kidogo atawaacha nje ya uwanja hadi pale watakapokuwa fiti kuanza kucheza.

Wakati huo huo Antonio Conte amemuambia kocha wa Manchester United Jose Mourinho kwamba aangalie timu yake na aache kufuatilia masuala ya klabu ya Chelsea na kushangazwa na kitendo cha Mou kuwafuatilia.

Kauli ya Antonio Conte inakuja baada ya Jose Mourinho kudai kwamba kuna makocha ambao wachezaji wao wakipata maejeraha huwa wanapiga sana kelele kauli ambayo ilionekana kama kijembe kwa Conte.

Chelsea imeambulia alama moja tu katika michezo yao mitatu iliyopita katika msimu huu na Jumamosi hii wataikabili Watford huku Ngolo Kante,Victor Moses,Tiomoue Bakayoko na David Luiz wakiwa mashakani kuukosa mchezo huu.

West Bromich Albion na laana ya kuwaachisha kazi makocha wa timu nyingine EPL, hata Ferguson walimsindikiza 

$
0
0

Hata haikuchukua zaidi ya masaa 24 kwa mabosi wa Leicester kumtimua Craig Shakespeare baada ya sare dhidi ya West Brom, na hii ulikuwa muendelezo wa West Brom kuwaachisha na kuwafukuzisha kazi makocha.

Rekodi zinaonesha katika ligi kuu Uingereza ukikutana na West Brom huku kocha akiwa katika presha kubwa baasi ujue upo uwezekano mkubwa sana afukuzwe akishindwa kuwafunga kama rekodi zinavyoonesha.

Andre Villas Boas,March mwaka 2012 Villas Boas hakuwa amefanya vizuri sana kwani alishinda mara mbili katika mechi 12, lakini alipokutana tu na West Bromich Albion walipomfunga bao moja siku hiyo hiyo Roman Abromovich akamfukuza AvB.

Roberto Di Matteo, sasa mwaka huo huo Chelsea wakawa na Roberto Di Matteo kocha ambaye aliwapa ubingwa wa Champions League, lakini Chelsea hawakuwa wanafanga vizuri sana na walipopigwa bao 2 kwa 1 na West Brom mwezi November 2012 Chelsea wakamtimua Di Matteo.

Roberto Mancini, tofauti na Di Matteo na Boas, huyu Mancini hakufungwa na West Brom bali walikuja pale Etihad wakala bao moja kiroho safi lakink mwenendo wa City haukuwaridhisha waarabu wa Man City baada ya ushindi huo wakamfukuza Mancini.

Paulo Di Canio, alitoka kushinda michezo 3 kati ya 13 katika Epl na mabosi waliendelea kumuamini na kumpa muda, walipoenda kuitembelea West Brom September 21 mwaka 2013 wakapigwa bao 3 kwa nunge na hapo hapo Sunderland wakamuondoa kikosini.

Chris Hughton, mwezi April mwaka 2014 Norwich walikuwa nyumbani kuwakaribisha West Bromich Albion na wakati huo Hughton alikuwa kwenye presha kubwa lakini alipopigwa tu bao 1 kwa nunge nyumbani ukawa mwisho wake kuifundisha Norwich.

Sir Alex Ferguson, May 19 2013 ni kati ya siku mashabiki wa United hawataki kuikumbuka kwa kuwa ndio siku SAF aliamua kustaafu, mechi yake ya mwisho ilikuwa dhidi ga West Brom ambapo walitoka sare ya bao 5 kwa 5 na tangu hapo Fergie akaachana na ukocha.

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>