Na Privaldinho ABIUD
Mume wake Leonita Lekaj ndiye aliyeibuka kidedea mwaka 2011 kwa kuitoa Man utd kwenye michuano ya Uefa akiwa na Fc Basel. Huyu mume wake Lekaj ndiye Vieira mpya wa Arsenal. Viera huyu mpya alipewa kadi nyekundu 3 kwenye msimu wa maka 2015/16 akiwa na Borussia M’bach.
Patrick Vieira wakati anambutua kiwiko Materrazi alipoulizwa kwanini alifanya vile alisema kuwa bila unafiki kuwa hampendi Materrazi. Ukiachilia mbali Richard Dunne kujifunga magoli (10) yeye na Patrick Vieira, pamoja Duncan Ferguson ndio wanaongoza kwa kadi nyekundu EPL wakiwa na kadi 8 kila mmoja.
Granit Xhaka ambaye wengi wanaamini ndiye mrithi wa Vieira mpaka sasa ana kadi nyekundu 2 ndani ya Arsenal akiwa amebakiza kadi 6 tu kuvunja rekodi ya Viera lakini akiwa tayari ameshapewa kadi nyekundu 9 ndani ya miaka mitatu tu uwanjani akiwa na miaka 24.
Kadi walizopewa akina Duncan na Vieira kwa miaka 10 na zaid, mdogo wao Xhaka tayari anazo na zaidi kwa miaka mitatu tu.
Licha ya kuwa na rekodi mbaya lakini bado anaonekana kuwa ni mpambanaji sahihi kwenye dimba la katikati. Wakati Granit Xhaka anavutwa jezi na Pogba hakujali sana, kwa sababu mwaka 1986, walikuwa wakiishi Kosovo, jimbo la huko Yugoslavia. Baba yake mzee Rajip Xhaka aliposikia mlangi wao unagongwa alitoka kufungua mlango. Ghafla alikutana na polisi waliomvuta shati lake na kumtoa nje kama Pogba alivyomvuta jezi yake.
Baba yake alikuwa mbishi sana kitendo kilichowakera polisi. Xhaka aliwahi kusema hawezi kuacha mpira wa kukaba kwa nguvu na kucheza takoling sana. Ndio asili yake. Baba yake hakuwahi kumwonea mtu aibu.
Ukorofi wa mzazi wake ulimfanya afungwe gerezani kwa miaka mitatu kwa kile kilichoitwa kuwa alihujumu serikali iliyokuwa madarakani. Xhaka amekuja na ladha aliyoondoka nayo Vieira. Nani ambaye hakumbuki tifua tifua la Vieira na Roy Keane? Basi kama hukumbuki hata hili mbungi la Xhaka na Pogba hukuliona?
Licha ya Xhaka kuanza msimu uliopita vibaya, Arsene Wenger aliamua kubadili mfumo, ambao ulimfanya Xhaka afanye vyema? Wenger aliamua kuachana na mfumo wa 4 4 2 na kuhamia mfumo wa 3 4 2 1. Hii ni baada ya Wenger kugundua udhaifu wa Xhaka. Alifahamu Xhaka ni nani, alikumbuka alivyokuwa akiteseka kwa Vieira. Ndio alibadilisha mfumo ili kumpa Xhaka uhuru zaidi.
Kwa mfano mwepesi tu Wakati msimu unaanza xhaka alikuwa na 61% ya pasi zilizokamilika kwenye mfumo wa 4 4 2. Rekodi mbovu kabisa kwa mchezaji wa timu inayocheza pasi nyingi kama arsenal. Mfumo huo ulimfanya kuwa mkabaji zaidi jukumu ambalo sio lake. Lakini kwenye mfumo wa 3 4 2 1 ambapo Chamberlain na Coqlien walimsaidia kukaba alikuwa na ustadi wa pasi uliofikia asilimia 81. Ndio, Wenger hapa alilamba joka, na alijiamini. Kwani wewe hukuona alitwaa FA mbele ya Mabingwa?
Miezi minne ya awali Xhaka litengeneza nafasi 10 kwenye mfumo ule ule wa 4 4 2, hovyo kabisa, hapa tunasema mtoto alitumwa Mafuta ya taa akanunua ya kula, je hayo mafuta utapeleka wapi wakati yamewekwa kwenye chupa ya mafuta ya taa? lakini kwenye mfumo wa 3 4 2 1 alitengeneza nafasi 25, pia alitengeneza magoli mawili kwenye mfumo huu 3 4 2 1 ilhali hapo awali kwenye 4 4 2 hakutengeneza goli lolote.
Baada ya Wenger kugundua Vieira hawezi kuhimili presha za kucheza kama kiungo mkabaji nyuma yake alimweka Gilbeto au Parlour. Hivyo ameamua kumweka Coquelin nyuma yake huku pemben akaamua kuwema mabeki watakaomfanya Xhaka asihaingaike sana.
Baba yake Xhaka alikuwa mtukutu, hakuwa muoga, alikuwa mpambanaji na huenda nae huko kwao aliitwa mchochezi. Xhaka ameiga maisha ya baba yake, haogopi kadi, amempa Wenger Presha kubwa kiasi cha kubadili mfumo. Wenger ni mwoga, asingeweza kuweka Euro 35 benchi kwa sababu ya kadi nyekundu, imembidi amwekee wakabaji wengine mbavu za pembeni ili kazi yake iwe kuchezesha timu. Tunasema ni kama mikutano ya siasa imekatazwa, Xhaka anapaswa kuwa jimbon kwake tu (katikatiki ya uwanja).
Msimu mpya huo umeanza Arsenal inatafuniwa hata maji. Hali mbaya. Nina wasiwasi miaka kadhaa ijayo nitamwona Xhaka kwenye jezi nyingine, Sumaye alikipenda sana Chama chake leo yuko wapi? Huwa naamini Ndoa ni tamu pale ukumbuni, lakini maisha yanayoendelea yanakuwa magumu. Mchezaji anaposajiliwa anakuwa na furaha kubwa sana ila maisha ya kuishi na kabati lenye Mende ndiyo yatakayomshinda Xhaka. Kama Arsenal itazidi kuporomoka, basi huenda Xhaka kwa ubora wake huu asiendelee kubakia klabuni hapo. Alexandre Song alikuwa bonge la mchezani… kiujumlaa fundii… lakini hakupenda maisha ya dhiki.. aliondoka.. mwangalieni Xhaka vizuri. Atageuka Song muda sio mrefu.