Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Mfahamu mrithi wa nafasi ya Jackson Mayanja Simba

$
0
0

Baada ya aliyekuwa kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja kujiuzulu nafasi hiyo, kocha Masud Djuma raia wa Burundi anatajwa kuziba nafasi hiyo.

Djuma amepata mafanikio akiwa kama kocha na kuishawishi Simba kumsaini kuwa msaidizi wa Joseph Omog kwenye benchi la ufundi la Simba.

Msimu uliopita Djuma alikuwa kocha wa Rayon Sports ya Rwanda na kuisaidia timu hiyo kutwa aubingwa ligi kuu. Badae akachaguliwa kuwa kocha bora wa msimu 2016/2017.

Amewahi kuvichezra vilabu vya APR, Rayon Sport, Prince Louis, Inter Star pamoja na timu ya Taifa ya Burundi ‘Intambamurugamba’.

Alikuwa sehemu ya kikosi cha timu ya taifa ya Burundi kilichoshiriki mashindano ya FIFA ya vijana (FIFA World Yourth Championship) mwaka 1995 nchini Qatar. Alicheza mechi tatu katika mashindano hayo.

Inaelezwa Djuma ni kipenzi cha wachezaji kutokana na ukatibu wake na kuwafanya wachezaji marafiki zake, huwa anavaa jezi na kujumuika pamoja kwenye mazoezi na wachezaji.

Amezaliwa August 30, 1977 Bujumbura Burundi, kwa sasa ana miaka 40. Bado kijana mwenye nguvu za kuweza kukimbizana na wachezaji mazoezini.

Inategemewa akatambulishwa rasmi leo October 19, 2017 mbele ya waandishi wa habari kwenye mkutano maalum wa Simba na vyombo vya habari makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi, Dar.


Hivi unajua kama Okwi amefunga magoli mengi zaidi ya timu 12 za VPL?

$
0
0

Mchezaji wa Simba Emanuel Okwi amefunga magoli saba (7) hadi sasa katika mechi tano za ligi alizocheza msimu huu, magoli mengi zaidi ya timu 12 kati ya 16 za VPL.

Amefunga magoli hayo (7) dhidi ya Ruvu Shooting (4), Mwadui (2) na Mtibwa Sugar (1), magoli yote ameyafunga kwenye uwanja wa Uhuru, Dar. Hajafunga katika mechi mbili Mbao 2-2 Simba na Stand United 1-2 Simba huku akikosa mchezo mmoja wa ligi Azam 0-0 Simba.

Okwi ndio anaongoza mbio za wafungaji wa VPL msimu huu akiwa amemwacha kwa magoli matatu mtu anaemfuatia ambae ni Mohamed Rashid ea Tanzania Prisons mwenye magoli manne.

Okwi amevizidi vilabu hivyo ambavyo vimecheza mechi sita lakini havijafikia magoli saba. Mtibwa Sugar (6), Yanga (6), Azam (5), Singida United (6)  Ndanda (4), Lipuli (3), Njombe (3), Mwadui (6), Ruvu Shooting (3), Majimaji (4), Stand United (3) na Kagera Sugar (2).

Timu tatu pekee ndio zimefunga magoli mengi zaidi ya Okwi, Simba (15), Tanzania Prisons (8) na Mbao. Mbeya City imefunga magoli saba (7) sawa na magoli yote ya Okwi.

Lebron James apigania usawa wa weusi kwa weupe kwa staili yake

$
0
0

Ligi kuu ya NBA ya nchini Marekani, ilianza mzunguko wake mpya tarehe 17 Oktoba na huu ni msimu wa 72 wa ligi hii ambapo mchezo wa kwanza ulihusisha vilabu vya  Cleveland Cavaliers na Boston Celtics katika uwanja wa nyumbani wa Cavs’ unaofahamika kama Quicken Loans Arena. Tofauti na ligi za michezo mingine, hapakuwepo na matukio yoyote makubwa yaliyohusisha kwenda kinyume au kupinga wimbo wa Taifa ikiwa kama ishara ya kupigania umoja na mshikamano nchini Marekani.

Wachezaji wa Cavs wao walishikana mikono kama ilivyokuwa katika hatua ya michezo ya maandalizi huku Celtics wao wakisimama wima kama timu moja, wakifuatana kwa usawa wa mabega huku wachezaji kadhaa na makocha wakiwa wameweka mikono yao kifuani kipindi ambacho kamanda wa jeshi mstaafu, Generald Wilson alipowaongoza kuimba wimbo wa Taifa.

Hata hivyo baada ya taa kurejea na mwanga kutawala katika uwanja wa  Quicken Loans Arena, nyota wa Cavs  LeBron James aliacha miguu yake izungumze badala ya kinywa chake.

Lebron James alivaa viatu ikiwa ni staili mpya vinavyofahamika kama Lebron 15 vikiwa na maandishi yanayong’ara kwa nyuma yakiwa yameandikwa EQUALITY. Viatu vilikuwa vyeusi isipokuwa maneno hayo yenye maana ya USAWA yakiwa katika rangi inayong’ara ya dhahabu.

Wakati watu wote wakitizama namna ambavyo migomo ikiendelea kwenye ligi ya NFL ambayo inasimamia mchezo wa American Football, James aliamua kuwa kwenye siku ya ufunguzi angefanya kitu ambacho kingeweza kusaidia namna ya kuongeza uelewa wa yote yanayoendelea kuhusiana na watu weusi dhidi ya weupe wa Marekani.

“Nilitaka kufanya hili jambo liendelee kuzungumzwa katika hali chanya, liendelee kupigiwa kelele,,” James alikiambia kituo cha  ESPN baada ya timu yake ya Cavs’ kupata ushindi wa 102-99. “Tunafahamu ugumu tunaoupitia, tunafahamu tuliyopitia kama Taifa na kama dunia kwa ujumla. Hivyo nilipata nafasi ya kutumia jukwaa na fursa yangu na nikafanya hivyo.”

Nike, ambayo Lebron amesaini nao mkataba wa Maisha, walianzisha kampeni ya USAWA unayoweza kuisoma hapa (EQUALITY campaign) mwezi  February wakiwa na lengo la kutumia wachezaji wao kupaza sauti kwa kutumia nguvu ya michezo kuwataka watu kusimamia haki na usawa kwenye jamii walizomo.

Viatu alivyoviaa James havitouzwa na vyanzo mbalimbali vikiripoti kuwa hii itakuwa ni kwa ajili ya wachezaji pekee. Hata hivyo katika sehemu ya kampeni hii kutakuwa na kiwango cha dola milioni 5 zitakazotolewa na NIKE kwa mashirika mbalimbali ambayo yanasimamia na kusisitiza Amani, ambayo yanajenga mahusiano ya watu ndani ya jamii.

“Sijaja Simba kufanya maajabu”-Kocha mpya

$
0
0

Kocha msaidizi mpya ndani ya kikosi cha Simba Masud Djuma amesema hajaenda klabuni hapo kufanya maajabu bali ni kutoa mchango wa kile alichonacho kwa kushirikiana na benchi la ufundi lililopo sasa.

“Sijaja kufanya maajabu, nimekuja kuisaidia Simba kwa kidogo nilichonacho ili kuisogeza mbele zaidi”-Masud Djuma kocha msaidizi Simba.

Kuhusu ukali

Unaambiwa Djuma huwa ni mtata kwa wachezaji hasa pale wanapokuwa kinyume na maelekezo yake.

Amesema yeye ni mtu wa pande mbili, mkali na mpole lakini huwa mkali pale ambapo mchezaji anataka kuharibu kazi.

“Mimi ni kama kiganja cha mkono, kina pande mbili. Mimi ni mpole lakini kwa upande mwingine ni mkali. Nimekuja hapa kufanya kazi ili kuipeleka Simba mbele na mimi nisogee mbele.”

Kuhusu kutoka kuwa kocha mkuu hadi kocha msaidizi Simba.

Alikuwa kocha mkuu msimu uliopita wakati anaifundisha Rayon Sport ya Rwanda kabla ya mkataba wake kumalizika. Akashinda tuzo ya kocha bora wa msimu wa Azam Rwandan Premier League.

“Nilianzia chini, baafa ya kuwa kocha bora Rwanda nikasema sitaki tena kuwa kocha msaidizi ndani ya Rwanda nimekuja hapa kuwa chini ya kocha mkubwa ni kama mzazi kwangu nahitaji kujifunza kutoka kwake ili nipande.”

Anaijua vizuri mechi ya Simba na Yanga

“Nimezaliwa nimekuwa nazisikia Simba na Yanga, kila sehemu kuna mechi zenye presha kubwa siwezi kuahidi lolote kuhusu mechi ya Simba na Yanga kwa sababu mpira una matokeo matatu.”

Kuhusu kutimuliwa

Amesema makocha ni sawa na mabegi, hayapaswi kufunguliwa zipu hadi mwisho kwa sababu muda wowote unaweza ukafunga zipu na kuondoka.

“Sisi makocha ni kama mabegi, hupaswi kufungua zipu yote kwa sababu muda wowote unaweza kuondoka.”

Kyrie Irving Akumbwa Na Mkosi, Giannis Antentokounmpo Mchezaji Bora NBA?

$
0
0

Inawezekana jina la Giannis Antetokounmpo likawa maarufu kutokana na ugumu wake lakini tangu msimu uliopita amekuwa mchezaji anayetizamwa zaidi katika kundi la wachezaji vijana wanaoweza kuja kuitikisa NBA. Hii ndio sababu ambayo Kevin Durant alikiri kuwa Giannis ni mchezaji wa kipekee na anaweza kumaliza maisha ya NBA akiwa mchezaji bora zaidi kuwahi kutokea.

Alfajiri ya Leo, Giannis aliiongoza klabu yake ya Milwaukee Bucks kushinda mchezo wao wa kwanza dhidi ya Boston Celtics ambayo sasa itakuwa imepoteza michezo miwili mfululizo. Boston Celtics ambayo inaonekana kuwa na kikosi kipya kabisa kilichojaa vijana baada ya kuondokewa na nyota wake kama Isaiah Thomas, Avery Bradley, Jae Crowder na Kelly Olynyk imepoteza mchezo wake wa ili mfululizo huku ikiwa ni siku moja tangu kumpoteza nyota wao Gordon Hayward aliyevunjika vibaya dhidi ya Cleveland Cavaliers.

Giannis Antentokounmpo alifunga pointi 37 huku pia akidaka rebound 13, huku wenzie  Malcolm Brogdon akifunga pointi 19 na Khris Middleton akiongeza pointi 15 na kudaka rebounds 9 lakini pia Mathew Dellavedova alitoa mchango wake wa pointi 15 kwenye ushindi huo.

Kyrie Irving alikuwa na usiku atakaotaka kuusahau baada ya kumaliza mchezo na pointi 17 huku akipata mitupo 7 tu kati ya 25 aliyojaribu ikiwa ni mchezo wake wa kwanza nyumbani kwa Boston Celtics yaani TD Garden,  Jaylen Brown yeye aliongeza 18.

Kabla ya mchezo huo, kwenye screen maalumu ndani ya uwanja wa TD Garden, ilipita video ikimuonyesha Gordon akiwa hospitali akiwashukuru washabiki na wachezaji wenzie kwa kumtakia heri katika kuuguza majeraha.

HIGHLIGHTS

 

“Haijawahi kupita tar 2 Simba haijalipa mishahara”-Manara

$
0
0

Afisa habari wa Simba Haji Manara amesema klabu yao haijawahi kuzidisha zaidi ya tarehe mbili (baada ya mwezi kumalizika) kulipa mishahara ya wachezaji pamoja na benchi lake la ushindi.

Manara alikuwa akifafanua kuhusu kuhusu tuhuma za mitandao ya kijamii zilizoelekezwa kwa klabu ya Simba kwamba aliyekuwa kocha wao msaidizi Jackson Mayanja amekimbia njaa ndani ya klabu hiyo.

“Haijawahi kupita tarehe mbili Simba haijalipa mishahara wachezaji wala benchi la ufundi. Jana mlimsikia wenyewe kocha Mayanja”-Haji Manara.

“Omog bado ni kocha wa Simba hajaondoka kama baadhi ya mitandao ya kijamii ilivyoandika kwamba Omog ameandika barua ya kuomba kuondoka kwa sababu ya njaa.”

Jana Jumatano October 18, 2017 Mayanja alitangaza kujiuzulu nafasi yake ya ukocha msaidizi kwa sababu ya kukabiliwa na matatizo ya kifamilia.

BBC iko hoi, MSN  tayari imekufa, MCN haoo wanauchukua mpira La Liga wanaupeleka Ligue 1

$
0
0

Upi utatu uliokuwa ukikugusa sana katika soka? Ni ule utatu ambao Bale anakimbia na mpira toka goli lao hadi la wapinzani na kuusukuma kwa Benzema kisha anatupiwa Ronaldo kuwamaliza wapinzani(BBC) na wanabeba Champions League?

Au ule utatu wa wahuni kutoka America Kusini ambapo Neymar anakusanya kijiji chote kinamfuata anamsukumia Suarez ambaye anawaangusha mabeki kabla ya kumsukumia Lioneil Messi La Pulga awaumize timu pinzani? (MSN)

Hao sio wa kwanza, unakumbuka utatu wa Carlos Tevez, Wayne Rooney na Cristiano Ronaldo pale United? Je Pipo Inzaghi, Ricardo Kaka na Andrea Pirlo waliowaua Liverpool bao 2 kwa 1 pale Olympique Stadium 2007? 


Kila zama zina mwisho wake na ni wazi sasa zama za MSN zimekwisha, Neymar hayupo huku Suarez hayuko fiti amebaki Messi, BBC nako Bale majeraha kila kukicha, Benzema amekwisha huku Cristiano Ronaldo umri huooo unampa mkono na anafunga kwa kusua sua.

Ni muda wa MCN sasa kukiwasha, na kinachovutia kuhusa utatu huu ni kwamba unajengwa na vijana wadogo sana wakipata uzoefu kwa mkongwe mmoja huku kukiwa na mchanganyiko wa soka la Ulaya na America wote wakiwa na njaa ya kuiteka dunia.

Unapokuwa na mkusanya kijiji mwenye umri mdogo kama Mbappe mchezaji ambaye dunia kwa sasa inamzungumzia yeye na anataka kuonesha nini anacho, una Neymar anayepigiwa chapuo kubeba Ballon D’Or na Cavanni anayetaka kuonesha bado yupo yupo, unatarajia nini kama sio magoli tu?

Haishangazi hata kidogo kuona hadi sasa PSG weshaweka kambani mabao 43, ndio haishangazi na itashangazaje wakati katika kikosi chako una washambuliaji viwembe wa namna hii, kazi kubwa waliyonayo mashabiki wa PSG kwa sasa ni kuamka tu na kushangilia utatu huu.

Michezo sita MCN waliyocheza kwa pamoja wameweka kambani mabao 17, ikiwa ni wastani wa mabao matatu katika kila mchezo mmoja rekodi ambayo tayari imekuwa tishio kwa wapinzani wa PSG msimu huu na sio uongo wanatisha sana.

La kuvutia zaidi kuhusu MCN ni kwamba wote wanaonekana wana njaa sana ya kufunga na ndio sababu inayoleta ushindani wa kufunga katika timu yao, jambo ambalo linaongeza idadi ya mabao PSG.

Edison Cavanni ameshasema wao hawajaenda PSG kuwa marafiki, kwa maana nyingine hawajaenda PSG kuuza sura bali wameenda kupambana kwa ajili ya timu na wao kama wao MCN wako hapo kufunga tu na sio kingine.

Mabao 43 ambayo PSG wamefunga katika msimu huu, 58% yametoka kwa wanyama hawa na hii inamaanisha wachezaji wenhine wote wa PSG wamechangia 48% tu ya mabao ya PSG msimu huu, tuombe mungu atupe uhai lakini naamini MSN hawasimamishiki na watawasha moto zaidi.

Mesut Ozil awaambia rafiki zake atasaini Manchester United

$
0
0

Mesut Ozil bado hali yake katika klabu ya Arsenal imekuwa ya sintofahamj, kiungo huyo Mjerumani hadi sasa hajasaini mkataba mpya ndani ya klabu hiyo huku ule alio nao unakaribia kuisha.

Mesut Ozil anataka kulipwa mshahara wa £350,000 kwa wiki koasi ambacho Arsenal wamesema hawana na kutaka kumpa £280,000 pesa ambayo Mesut Ozil na wawakilishi wake wameikataa.

Kwa hali ilivyo ni wazi kwamba dirisha lijalo la usajili Mesut Ozil pamoja na Alexis Sanchez wanaweza kuondoka bure katika klabu hiyo kwani wote wawili mikataba yao inafikia ukingoni.

Manchester United wanaguatilia mienendo ya suala la Ozil na Sanchez kwa ukaribu lakini sasa inasemekana Manchester United wako katika nafasi nzuri kumchukua Mesut Ozil dirisha la January.

Mesut Ozil ana uhusiano mzuri sana na kocha wa United Jose Mourinho na walishawahi kufanya kazi pamoja jambo ambalo linaonekana linaweza kumvuta Mesut Ozil akakipige Old Traford.

Mesut ameshawaambia marafiki zake kuhusu kuungana tena na Jose Mourinho huku kocha Arsene Wenger naye akithibitisha kwamba Ozil na Sanchez wote wanaweza kuondoka katika dirisha lijalo la usajili.

Wenger amesema suala la Sanchez na Ozil wamejaribu kila kitu na kuna uwezekano wa lolote kutokea japo wachezaji hao wote wawili wanaonekana wana furaha katika kikosi cha Arsenal.


Burundi ndio taifa lenye makocha wengi VPL

$
0
0

Jana Alhamisi October 19, 2017 klabu ya Simba ilimtambulisha kocha msaidizi mpya Masud Djuma raia wa Burundi aliyechukua nafasi ya Jackson Mayanja ambaye alijiuzulu siku moja kabla ya Djuma kutambulishwa kuwa msaizi mpya wa Joseph Omog ambaye ndiye boss wa kikosi hicho cha mtaa wa Msimbazi.

Ujio wa Djuma ndani ya Simba unaongeza idadi ya makocha wa Burundi ndani ya ligi yetu na kufikia watatu. Nsanzurwimo Ramadhani (kocha mkuu Mbeya City), Etienne Ndayiragije (kocha mkuu Mbao FC) na Masud Djuma (kocha msaidizi Simba) hawa wote ni makocha wanaotoka taifa la Burundi.

Etienne Ndayiragije

Amefungua njia kwa makocha wa Burundi kuaminiwa katika kipindi hiki kutokana na mafaniko aliyoyapata akiwa na Mbao msiu uliopita, kwa mujibu wa mwenyekiti wa klabu hiyo Bw. Solly Njashi malengo ya klabu yao kwa msimu uliopita yalikuwa ni kubaki ligi kuu Tanzania bara na kufika hatua ya robo fainali ya Azam Sports Federation Cup.

Etienne alivuka malengo hayo baada ya kuifikisha Mbao fainali ya ASFC na kupoteza 2-1 kwa Simba May 2017 kwenye uwanja wa Jamhuri Dodoma, Mbao ilifanikiwa kusalia kwenye ligi licha ya kupambana hadi dakika za mwisho kukwepa mkasi wa kushuka daraja ambao mwisho wa siku uliwakumba wenzo wa jijini Mwanza Toto African pamoja na timu nyingine mbili ambazo ni JKT Ruvu na African Lyon.

Kocha wa Mbao amekuwa ni muumini wa vijana, tangu alipokuja Mbao hadi sasa bado msingi wa timu yake umejengwa na wachezaji vijana, msimu huu ana wachezaji wengi ambao wanacheza ligi kuu kwa mara ya kwanza aliowaunganisha na wazoefu wachache ambao pia hawana majina makubwa ndani ya nchi.

Mbao imekuwa ni timu ambayo inatoa ushindani mkubwa kwenye ligi wameifunga Yanga mara mbili msimu uliopita, mara ya kwanza ilikuwa ni mchezo wa nusu fainali ya ASFC kabla ya kuwachapa tena kwenye mechi ya mwisho msimu uliopita.

Nsanzurwimo Ramadhani

Ameanza kazi rasmi Mbeya City mwanzoni mwa mwezi huu baada ya kuondoka kwa Kinnah Phiri, bado hajaonesha cheche zake ameisimamia City kwenye kwa mara ya kwanza akiwa kocha mkuu ilipotoka sare ya kufungana 2-2 dhidi ya Mbao Ijumaa iliyopita uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Anabebwa na uzoefu wake katika soka la Afrika Mashariki pamoja na kusini mwa Afrika akiwa amefundisha vilabu vya mataifa mbalimbali Burundi, Rwanda, Botswana, Malawi, Uganda na Afrika Kusini. Amewahi kuwa mshauri wa benchi la ufundi kwenye timu ya taifa ya Burundi pia amewahi kuwa kocha wa muda wa timu ya taifa ya Malawi.

Masud Djuma

Alikuwa mchezaji katika vilabu tofauti vya Burundi na Rwanda lakini pia amewahi kucheza Seychelles kabla ya kuamua kuingia kwenye fani ya ukocha. Msimu uliopita (2016/2017) aliiwezesha Rayon Sport kushinda ubingwa wa ligi kuu ya Rwanda ‘Azam Rwanda Premier League’ ambapo pia alishinda tuzo ya kocha bora wa msimu huo.

Amejiunga na Simba kuwa kocha msaidizi chini ya Omog lakini tayari Burundi wameongeza idadi ya makocha kwenye ligi ya Tanzania. Burundi limekuwa taifa pekee lenye makocha wengi kwenye ligi ya Tanzania ukiachana na makocha wazawa.  Makocha wengine wa kigeni ni Joseph Omog-Simba (Cameroon), George Lwandamina-Yanga (Zambia),  Aristica Cioaba-Azam (Romania), Hans van Pluijm-Singida United (Netherland).

Mbao vs Azam: Vita ya ‘beki nyanya’ na ‘wafungaji butu’ nani ataepuka sare ya tatu mfululizo?

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

MABINGWA mara moja wa zamani, Azam FC inapaswa kupandisha kiwango chao kiufungaji msimu huu na mchezo wa raundi ya saba ugenini vs Mbao FC unapaswa kuambatana na tumakini mkubwa katika kujilinda kwani timu hiyo ya Mwanza inapenda kushambulia sana ikicheza katika uwanja wa Kirumba.

Mbao FC japokuwa haijapata ushindi wowote katika uwanja wao wa nyumbani lakini kiufungaji kikosi hicho cha kocha Mrundi, Etienne kimefanikiwa kufunga magoli manne katika uwanja wa Kirumba dhidi ya Simba SC na Mbeya City FC huku mshambulizi wake Habib Hajji akiwa tayari ameshafunga magoli matatu kati ya nane ya timu yake.

Beki ‘yanya’ ya Mbao, wafungaji butu Azam FC

Mlinzi wa kulia, Boniphace Maganga amefunga magoli mawili hadi sasa. Stahili yake ya kupanda kuongeza nguvu katika mashambulizi na umakini wake katika kupiga mashuti ya mbali yenye mwelekeo sahihi ulimfanya mlinzi huyo chipukizi wa Taifa Stars kufunga goli la ushindi wakati Mbao FC ilipopata ushindi pekee msimu huu vs Kagera Sugar FC (ugenini).

Mlinzi wa kati na nahodha wa kikosi hicho Mrundi, Yusuph Ndikuma amefunga goli moja na kufanya safu hiyo ya ulinzi kuwa na idadi kubwa zaidi ya magoli ya kufunga hadi sasa wakati ligi ikiwa imeshachezwa michezo sita kwa kila timu.

Kiuzuiaji, Mbao FC ni timu ya tatu iliyoruhusu magoli mengi katika ligi msimu huu (imefungwa magoli tisa.) Wakati safu hiyo ya ulinzi ya kikosi cha Etienne ikiruhusu magoli tisa, safu ya mashambulizi ya kikosi cha Mromania, Aristica imefunga magoli matano tu.

Mbaraka Yusuph ndiye kinara wa ufungaji wa Azam FC hadi sasa akiwa amefunga magoli mawili. Mghana, Yahaya Mohamed amefunga goli moja sawa na kijana Peter Paul ambaye alifunga goli la kusawazisha wakati Azam FC ilipolazimisha sare ya 1-1 dhidi ya Singida United. Huku nahodha wa kikosi, Himid Mao akifunga katika sare iliyopita Mwadui FC 1-1 Azam FC.

Kitendo cha washambuliaji hao kufunga magoli manne katika michezo sita kwa timu inayojengwa bado nasisitiza wako katika mwendo mzuri na kwa kutumia udhaifu wa Mbao FC katika kujilinda kikosi hicho kilichotwaa ubingwa msimu wa 2013/14 kinaweza ‘kunoa’ makali zaidi kwa kufunga walau magioli mawili katika mchezo mmoja kwa mara ya kwanza msimu huu.

Mbio za ubingwa ni sasa

Kuwa na pointi 12 sawa na viongozi wa ligi Simba SC, MtIbwa Sugar na mabingwa watetezi kunaonyesha kuwa ligi bado ‘mbichi’ nab ado hakuna tofauti kubwa kati ya timu na timu.

Kwa Azam FC ambao walianza maandalizi yao Juni na kuwa timu ya kwanza kufanya hivyo sasa wanapaswa kuanza kufunga kweli ili kuthibisha kuwa wako tayari kwa mbio za ubingwa na pengine kushinda taji hilo kwa mara ya pili mwishoni mwa msimu.

Kushindwa kupata matokeo ya ushindi katika michezo vs Singida United ( Jamhuri Stadium, Dodoma) na Mwadui FC (Mwadui Complex) bado hakupaswi kuwakatisha tama kwani wamekutana na timu ambazo pengine zingiweza kuwafunga bila Azam FC kukomboa goli katika kila mchezo.

Ila timu yenye dhamira ya ubingwa inapaswa kushinda walau mchezo mmoja na kutoa sare mbili katika viwanja vya ugenini. Lakini bahati mbaya kwa Azam FC wanaweza kushindwa kupata ushindi katika mchezo wa tatu mfululizo wakicheza ugenini kwa sababu wanakutana na Mbao ambao pia wanasaka ushindi wa kwanza nyumbani msimu huu.

Kumbuka Mbao FC nao wanaingia katika mchezo huu vs Azam FC Jumamosi hii wakipambana kuepeka sare ya tatu mfululizo katika uwanja wa nyumbani. Nani mshindi?

Muangalieni Xhaka vizuri ipo siku mtamuita Song

$
0
0

Na Privaldinho ABIUD

Mume wake Leonita Lekaj ndiye aliyeibuka kidedea mwaka 2011 kwa kuitoa Man utd kwenye michuano ya Uefa akiwa na Fc Basel. Huyu mume wake Lekaj ndiye Vieira mpya wa Arsenal. Viera huyu mpya alipewa kadi nyekundu 3 kwenye msimu wa maka 2015/16 akiwa na Borussia M’bach. 

Patrick Vieira wakati anambutua kiwiko Materrazi alipoulizwa kwanini alifanya vile alisema kuwa bila unafiki kuwa hampendi Materrazi. Ukiachilia mbali Richard Dunne kujifunga magoli (10) yeye na Patrick Vieira, pamoja Duncan Ferguson ndio wanaongoza kwa kadi nyekundu EPL wakiwa na kadi 8 kila mmoja.

Granit Xhaka ambaye wengi wanaamini ndiye mrithi wa Vieira mpaka sasa ana kadi nyekundu 2 ndani ya Arsenal akiwa amebakiza kadi 6 tu kuvunja rekodi ya Viera lakini akiwa tayari ameshapewa kadi nyekundu 9 ndani ya miaka mitatu tu uwanjani akiwa na miaka 24.

Kadi walizopewa akina Duncan na Vieira kwa miaka 10 na zaid, mdogo wao Xhaka tayari anazo na zaidi kwa miaka mitatu tu.

Licha ya kuwa na rekodi mbaya lakini bado anaonekana kuwa ni mpambanaji sahihi kwenye dimba la katikati. Wakati Granit Xhaka anavutwa jezi na Pogba hakujali sana, kwa sababu mwaka 1986, walikuwa wakiishi Kosovo, jimbo la huko Yugoslavia. Baba yake mzee Rajip Xhaka aliposikia mlangi wao unagongwa alitoka  kufungua mlango. Ghafla alikutana na polisi waliomvuta shati lake na kumtoa nje kama Pogba alivyomvuta jezi yake. 

Baba yake alikuwa mbishi sana kitendo kilichowakera polisi. Xhaka aliwahi kusema hawezi kuacha mpira wa kukaba kwa nguvu na kucheza takoling sana. Ndio asili yake. Baba yake hakuwahi kumwonea mtu aibu.

Ukorofi wa mzazi wake ulimfanya afungwe gerezani kwa miaka mitatu kwa kile kilichoitwa kuwa alihujumu serikali iliyokuwa madarakani. Xhaka amekuja na ladha aliyoondoka nayo Vieira. Nani ambaye hakumbuki tifua tifua la Vieira na Roy Keane? Basi kama hukumbuki hata hili  mbungi la Xhaka na Pogba hukuliona? 

Licha ya Xhaka kuanza msimu uliopita vibaya, Arsene Wenger aliamua kubadili mfumo, ambao ulimfanya Xhaka afanye vyema? Wenger aliamua kuachana na mfumo wa 4 4 2 na kuhamia mfumo wa 3 4 2 1. Hii ni baada ya Wenger kugundua udhaifu wa Xhaka. Alifahamu Xhaka ni nani, alikumbuka alivyokuwa akiteseka kwa Vieira. Ndio alibadilisha mfumo ili kumpa Xhaka uhuru zaidi. 

Kwa mfano mwepesi tu Wakati msimu unaanza xhaka alikuwa na 61% ya pasi zilizokamilika kwenye mfumo wa 4 4 2. Rekodi mbovu kabisa kwa mchezaji wa timu inayocheza pasi nyingi kama arsenal. Mfumo huo ulimfanya kuwa mkabaji zaidi jukumu ambalo sio lake. Lakini kwenye mfumo wa 3 4 2 1 ambapo Chamberlain na Coqlien walimsaidia kukaba alikuwa na ustadi wa pasi uliofikia asilimia 81. Ndio, Wenger hapa alilamba joka, na alijiamini. Kwani wewe hukuona alitwaa FA mbele ya Mabingwa?

Miezi minne ya awali Xhaka litengeneza nafasi 10 kwenye mfumo ule ule wa 4 4 2, hovyo kabisa, hapa tunasema mtoto alitumwa Mafuta ya taa akanunua ya kula, je hayo mafuta utapeleka wapi wakati yamewekwa kwenye chupa ya mafuta ya taa?  lakini kwenye mfumo wa 3 4 2 1 alitengeneza nafasi 25, pia alitengeneza magoli mawili kwenye mfumo huu 3 4 2 1 ilhali hapo awali kwenye 4 4 2 hakutengeneza goli lolote.

Baada ya Wenger kugundua Vieira hawezi kuhimili presha za kucheza kama kiungo mkabaji nyuma yake alimweka Gilbeto au Parlour. Hivyo ameamua kumweka Coquelin nyuma yake huku pemben akaamua kuwema mabeki watakaomfanya Xhaka asihaingaike sana.

Baba yake Xhaka alikuwa mtukutu, hakuwa muoga, alikuwa mpambanaji na huenda nae huko kwao aliitwa mchochezi. Xhaka ameiga maisha ya baba yake, haogopi kadi, amempa Wenger Presha kubwa  kiasi cha kubadili mfumo. Wenger ni mwoga, asingeweza kuweka Euro 35 benchi kwa sababu ya kadi nyekundu, imembidi amwekee wakabaji wengine mbavu za pembeni ili kazi yake iwe kuchezesha timu. Tunasema ni kama mikutano ya siasa imekatazwa, Xhaka anapaswa kuwa jimbon kwake tu (katikatiki ya uwanja). 

Msimu mpya huo umeanza Arsenal inatafuniwa hata maji. Hali mbaya. Nina wasiwasi miaka kadhaa ijayo nitamwona Xhaka kwenye jezi nyingine, Sumaye alikipenda sana Chama chake leo yuko wapi? Huwa naamini Ndoa ni tamu pale ukumbuni, lakini maisha yanayoendelea yanakuwa magumu. Mchezaji anaposajiliwa anakuwa na furaha kubwa sana ila maisha ya kuishi na kabati lenye Mende ndiyo yatakayomshinda Xhaka.  Kama Arsenal itazidi kuporomoka, basi huenda Xhaka kwa ubora wake huu asiendelee kubakia klabuni hapo. Alexandre Song alikuwa bonge la mchezani… kiujumlaa fundii… lakini hakupenda maisha ya dhiki.. aliondoka.. mwangalieni Xhaka vizuri. Atageuka Song muda sio mrefu.

Polisi waingilia kati fujo zilizoibuka katika mchezo wa Everton vs Lyon

$
0
0

Jana michezo mbali mbali ya ligi ya Europa ilipigwa na moja kati ya mchezo ambao umeongelewa sana ni mchezo kati ya Everton waliokuwa nyumbani kuikaribisha Lyon kutoka nchini Ufaransa.

Kwa tulioutazama mchezo haukuwa mchezo mkali sana lakini kilichozua gumzo ni fujo kati ya wachezaji wa Everton wakiongozwa na Ashley William dhidi ya wachezaji wa Lyon ambapo ilihusisha pia mashabiki.

Katila mchezo huo ambao uliisha kwa Eveton kufungwa bao 2 kwa 1 kulionekana kikundi cha mashabiki akiwemo baba mmoja aliyekuwa na mtoto wakijaribu kutaka kuwapiga wachezaji wa Lyon pembeni mwa uwanja.

Polisi mjini Marseyside ambao ndio mji wanaotokea Everton wametangaza rasmi kuanza kwa uchunguzi wa tukio hilo huku pia chama cha soka barani Ulaya UEFA wameanza kufanga uchunguzi wao kuhusiana na fujo hizo.

Endapo Everton watapatikana na hatia baasi watachukuliwa hatua kali haswa mlinzi wao Ashley Williams ambaye ndiye alionekana kinara katika mvutano huo.

Msuva, Samatta, ‘wapigana vikumbo’ mtandaoni

$
0
0

Na Arone Mpanduka (Tumaini Media)

BAADA ya kufanya vizuri katika timu yake ya Difaa El Jadida ya nchini Morocco pamoja na timu ya taifa Taifa Stars, winga mshambuliaji Simon Msuva amempiku mshambuliaji Mbwana Samatta kws kuwa na wafuasi wengi katika ukurasa wa video wa YouTube.

Mwezi Julai mwaka huu Msuva alijiunga na klabu hiyo ya Morocco akitokea Yanga huku Samatta akiwa tayari amekubalika ndani ya kikosi cha Genk ya Ubelgiji tangu alipojiunga nayo Januari mwaka jana.

Kwa ujumla wachezaji hao wamejizolea mashabiki lukuki wanaofuatilia matukio yao katika kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii hasa kufuatia kufanya vema wanapokuwa katika klabu zao pamoja na timu ya Taifa Stars.

Imebainika kwamba katika ukurasa wake wa video wa YouTube unaojulikana kama Msuva Simon, Msuva amepata zaidi ya wafuasi 3,000 huku Samatta akiwa na wafuasi zaidi ya 2,000.

Idadi hiyo ni ya watazamaji waliojitokeza kuwaunga mkono katika kurasa hizo ambapo kwa kufanya hivyo wanapata fursa ya kuona kila video mpya inayowekwa kwenye kurasa zao.

Kwa upande wa kurasa za instagram, Samatta ana zaidi ya wafuasi laki tano (500,000) na kumpiku Msuva ambaye kwenye ukurasa huo ana zaidi ya wafuasi laki mbili (200,000).

Kwa upande wa mtandao wa twitter, Samatta amemzidi kete Msuva kwani ana wafuasi zaidi ya elfu hamsini (50,000) huku Msuva akiwa na zaidi ya wafuasi elfu moja (1,000). Msuva alichelewa kufungua ukurasa wa twitter ukilinganisha na Samatta.

Wakati huohuo ukurasa huo wa Samatta umependwa na zaidi ya watazamaji 1,000 huku wa Msuva ukipendwa na zaidi ya watazamaji 200.

Anachokifanya Samatta YouTube licha ya kuweka matukio yake ya uwanjani hasa mabao anayofunga katika Ligi ya Ubelgiji, Samatta amekuwa akipendelea kuweka kazi nzuri za wachezaji wengine kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Ikumbukwe hivi karibuni aliwahi kuweka video ya mabao mawili ya Msuva ambayo aliwafunga Botswana katika mechi ya kirafiki ambayo Stars ilishinda 2-0.

Mbali la hilo Samatta alishawahi kuweka video ya Emmanuel Okwi wakati alipoipatia bao Uganda hivi karibuni kwenye mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Misri.

Pia Samatta huwa anaweka video za magoli mazuri ya wachezaji mahiri wa Ligi mbalimbali za Ulaya.

Faida za mitandao kwa Msuva, Samatta

Zipo faida mbalimbali za wachezaji hao katika matumizi ya mitandao ya kijamii hasa ikitokea wakaitumia kwa njia zilizo sahihi.

Faida ya kwanza ni kipato kupitia mitandao, kwa mfano YouTube humlipa muhusika pindi anapofikisha watazamaji milioni moja katika ukurasa wake.

Hiyo ina maana kwamba wachezaji hao wanapaswa kuendelea kujituma uwanjani ili kujizolea mashabiki wengi watakaokuwa na hamu ya kuperuzi kurasa zao na hatimaye kufanikiwa kutimiza idadi hiyo itakayowafanya wawe wanakinga kiasi cha pesa kila mwezi.

Faida nyingine ni kusaidia kuwajengea uwezekano wa kazi zao kuonekana sehemu kubwa zaidi duniani na hivyo kuwapa urahisi wa kucheza soka katika nchi yoyote bila kikwazo chochote.

Mawakala wengi wa mchezo wa soka pamoja na wasaka vipaji huwa wanatumia kurasa maalumu za mitandao ya kijamii kuangalia uwezo wa mchezaji husika kabla ya kuanza kumfuatilia na kumfanyia majaribio.

0786 160643

Safu butu ya ushambuliaji ya Atletico Madrid itawagharimu msimu huu

$
0
0

Ufungaji wa wa magoli ni tatizo ambalo limedhihirika kuwa ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya Atletico Madrid msimu huu na matokeo yake timu imekuwa ikipoteza sana msimu huu wa 2017/18 kama ambavyo ilionekana juzi katika mchezo dhidi ya Qarabag kwenye ligi ya mabingwa wa ulaya.

Baada ya michezo 11 msimu huu – mechi 8 kwenye La Liga na mechi 3 za Champions League – Atletico wamefunga magoli machache kuliko wakati wote ambao Simeone amekuwa kocha – wamefunga magoli 14 tu, magoli 5 kati ya hayo wameyafunga katika mchezo mmoja dhidi ya Las Palmas mwezi August.

Msimu uliopita, Atletico walikuwa wamefunga magoli 24 mpaka kufikia hatua kama hii ni Leganes tu ndio walifanikiwa kucheza nao bila nyavu zao kutikiswa na washambuliaji wa Simeone kwenye michezo 11 ya kwanza.

Msimu wa 2015/16 Antoine Griezmann akiwa na Jackson Martinez, Fernando Torres, Angel Corre na Luciano Vietto – Rojiblancos walikuwa wameshafunga magoli 18, 13 pekee yakifungwa na washambuliaji tu.

Msimu wa 2014/15, Griezmann akiwa na Mario Mandzukic katika ushambuliaji, walikiisaidia kikosi cha Simeone kufunga magoli 22 katika mechi 11 za mwanzo.

Falcao na Diego Costa waliongoza kwa kufunga magoli 25 kwenye mechi 11 za mwanzo msimu wa 2012/13, lakini msimu ambao Atletico Madrid walianza vizuri zaidi ulikuwa msimu wa 2013/14 ambapo walifunga magoli 26 kwenye idadi hiyo ya mechi – msimu huu walimaliza wakiwa mabingwa wa La Liga na wakafika fainali ya Championd League.

Atletico wanashika nafasi ya 4 kwenye ligi, kwenye kundi lao la Champions League wanashika nafasi 3 nyuma ya Chelsea na Roma. Wanahitaji kutafuta suluhisho kwenye safu yao ya ushambuliaji au wataishia kwenye Europa League na kuikosa top 3 ya La liga msimu huu.

Ukame wa mabao waikumba Santiago Bernabeu, haijawahi tokea tangu 2003/2004

$
0
0

Tangu msimu wa ligi kuu nchini Hispania La Liga kuanza, mabingwa watetezi wa ligi hiyo Real Madrid wanaonekana kusuasua sana huku kukiwa na ukame mkubwa wa mabao tofauti na msimu uliopita.

Msimu uliopita uwanja wa Santiago Bernabeu ulionekana kama machinjio makuu ya wapinzani lakini msimu huu pana hali ya ukame mkubwa wa mabao ambao haujawahi tokea kwa misimu saba iliyopita.

Real Madrid wamecheza michezo 7 katika uwanja huo wa Santiago Bernabeu lakini mabao waliyopata katika michezo hiyo ni mabao 11 ambayo ni idadi ndogo ya mabao na mara ya mwisho hali hii ilitokea msimu wa 2003/2004.

Upungufu wa  mabao Madrid unaashiria nini? Iko wazi kwamba majeraha ya Gareth Bale yanaitesa Madrid huku adhabu aliyopewa Cr7 kukosa mechi kadhaa za msimu pia ni tatizo lakini iko wazi kwamba Madrid eneo lao la ushambuliaji haliko vizuri.

Haliko vizuri kwa sababu viungo Toni Kroos na Luca Modric wameshapiga pasi 108 kwenye nusu ya tatu ya wapinzani lakini idadi ya mabao iliyopo ni pungufu mnoo tofauti na pasi zinazopigwa kwenye lango la wapinzani.

Zinedine Zidane anaweza kubeba lawama kwa upande mwingine kwa kumruhusu Alvaro Morata na James Rodriguez waondoke wakati kikosi chake hakikuwa na uhakika wa washambuliaji waliopo kuwa vizuri.

Wastani wa ufungaji wa Real Madrid katika Champions League ni 14% ambayo ni ndogo zaidi katika michuano hiyo huku wakiwa wamezidiwa mabao 9 na vinara wa La Liga klabu ya Barcelona.


Okwi atafunga tena?

$
0
0

Atafunga tena? Swali la kujiuliza kuhusu Emanuel Okwi ‘Muhenga’ ambaye anaongoza chati ya wafungaji wa ligi kuu Tanzania bara akiwa na magoli saba aliyofunga katika mechi tano alizocheza.

Amefunga katika mechi zote tatu ambazo Simba imecheza uwanja wa Uhuru, katika magoli hayo saba hakuna goli ambalo amefunga nje ya uwanja wa huo unaotumia kama uwanja wa nyumbani na Simba.

Magoli ya Okwi uwanja wa Uhuru

  • Simba 7-0 Ruvu Shooting (Okwi alifunga magoli manne, akawa mchezaji wa kwanza kufunga hat-trick msimu huu.)
  • Simba 3-0 Mwadui (alifunga magoli mawili na kufikisha magoli sita)
  • Simba 1-1 Mtibwa Sugar (akaendeleza rekodi ya kufunga mfululizo kwenye uwanja wa Uhuru na kufikisha magoli saba yote akiyafunga uwanja huohuo.)

Mechi ambazo Okwi hajafunga

  • Mbao 2-2 Simba (waliofunga kwa upande wa Simba ni Shiza Kichuya na James Kotei
  • Stand United 1-2 Simba (magoli ya Simba yalifungwa na Shiza Kichuya pamoja na Laudit Mavugo)
  • Azam 0-0 Simba (Okwi hakucheza)

Leo Jumamosi October 21, 2017 Simba inacheza dhidi ya Njombe Mji uwanja wa Uhuru, uwanja ambao Okwi amefunga mfululizo katika mechi tatu zilizopita, swali ni moja tu Okwi atafunga tena?

“Nataka kuvaa medali ya ubingwa, narejea kukata ‘kiu’ yangu na mashabiki Azam”-Wazir Junior

$
0
0

Na Baraka Molembole

KUREJEA kikosini kwa mshambulizi kijana, Wazir Junior katika kikosi cha Azam FC ni faraja kubwa kwa kocha Mromania, Aristica ambaye ameshuhudia safu yake ya mashambulizi ikifunga magoli manne tu kati ya matano ya timu yake katika michezo sita ya ligi kuu msimu huu.

Junior ambaye amesajiliwa Azam FC msimu huu akitokea Toto Africans ya Mwanza ameshindwa kuichezea Azam FC mchezo wowote ule msimu huu kutokana na majeraha ya ‘kuvilia damu’ chini ya kifundo chake cha mguu wa kushoto, majeraha ambayo aliyapata wakati timu yake ikiwa katika maandalizi ya mwishomwisho ya msimu nchini Uganda.

“Naweza kurudi rasmi katika michezo ya ligi kuu Jumamosi hii kama nitapata nafasi ya kucheza dhidi ya Mbao.” Anasema Junior nilipofanya naye mahojiano mafupi Alhamis hii akiwa jijini Mwanza na kikosi cha Azam FC ambacho kitacheza na Mbao FC katika uwanja wa Kirumba, Mwanza.

“Sijaonekana katika michezo sita ya mwanzo ambayo timu yangu imecheza msimu huu kutokana na kupata majeraha wakati wa maandalizi ya msimu nchini Uganda.

“Damu ilivilia chini ya kifundo cha mguu wangu wa kushoto lakini sasa naendelea vizuri na niko tayari kuichezea timu yangu mpya kwa mara ya kwanza katika ligi.”

Wazir Junior ni kati ya wachezaji vijana waliopata nafasi ya ‘kuruka’ na kufika ligi kuu moja kwa moja pasipo kucheza ligi daraja la kwanza wala lile la pili. Mwenyeji huyo wa Tanga alisajiliwa Toto Africans na kocha John Tegete mara baada ya timu hiyo kurejea VPL mwaka 2015.

“Sijawahi kucheza ligi daraja la kwanza wala la pili. Nakumbuka nilipata nafasi ya kucheza michuano ya Mei Mosi, 2015 ambayo ilifanyika Mwanza mwishoni mwa mwezi April. Mwaka huo Toto ilikuwa imepanda ligi kuu. Nilicheza michezo miwili katika michuano ile ndipo kocha Tegete akaniona, akanisajili na safari yangu ya ligi kuu ikaanzia hapo.”

Kwa mchezaji kijana ambaye hakuwahi kucheza ligi yoyote ile ya juu, kitendo cha kufunga magoli 16 katika misimu miwili ikiwemo ‘Hat trick’ moja katika uwanja wa Majimaji, Songea hakika si jambo dogo na kuna kila dalili njema kwa kijana huyu ambaye alifunga magoli nane katika msimu wake wa kwanza VPL 2015/16 na mengine nane msimu wa 2016/17 tena akiwa katika timu iliyokuwa chini ya msimamo huku ukata ukiwa mkali klabuni.

“Kwangu mimi kila kitu kimebadilika. Kutoka katika mashindano ya Mei Mosi 2015, Toto Africans hadi sasa Azam FC kwangu ni mabadiliko makubwa. Sasa naongeza jitihada ili kuhakikisha navaa medali ya ubingwa msimu huu. Nafahamu mashabiki wa Azam FC wananisubiri kwa hamu sana, lakini wasiwe na haraka wataniona hivi karibuni.”

Yugoslavia ilimzawadia mabomu, Old Traford ikamzawadia taulo

$
0
0

Na Priva ABIUD

Unapotaja mabeki bora kuwahi kutokea Katika ligi kuu ya England kwa miaka 20 iliyopita usipomtaja Nemanja Vidic basi unahitaji Maombi. Ndiye beki pekee katika ardhi ya England aliyetwaa tuzo ya mchezaji bora wa msimu. Tena ametwaa mara mbili (2009 na 2011) ikiwa ni wachezaji watatu tu wametwaa tuzo hizo mara mbili (Cristiano Ronaldo, Thiery Henry na Nemanja Vidic).

Huyu ni mwanajeshi ambaye haogopi uso wake kuumia, majeraha ya mwilini n.k. ni moja ya mashujaa waliotumia jasho na damu kuwapigania Mashetani wekundu. Aliwahi kupasuka pua mara kadhaa na kuvunjika kwa ajili ya timu yake.Vidic aliusaliti mwili wake kwa ajili ya Mioyo ya mashabiki milion 700 wa Man utd kote duniani.

Akiwa mtoto, nchini Yugoslavia palitawalia na vita vya muda mrefu. Aliishi kwa wasiwasi yeye na familia yake wakihofia kupigwa mabomu. Baadae kijana huyu kutoka kolomije ya Serbia alifanikiwa kisoka. Kwa kuwa alizoea mazingira ya vita, basi Vita ya Yuogoslavia aliihamishia Old Trafford. Kila mshambuliaji aliyekuja mbele yake alikuwa adui yake. Ni ngumu ukimuona anacheka wala kulia. Ukiona kamera imemuonesha basi ujue anapokea kadi au anafoka.

Alikuwa anakwenda uwanjani akiwa na anawaza ushindi tu. Hakujua masuala ya fasheni. Huenda alikuwa anajipaka baby care tu. Nywele zake nyekundu ziliashiria king’ora kwenye ukuta wa Man Utd. Aina yake ya uchezaji maarufu kama “blitzkrieg” kule Ujerumani ilimpa umaarufu mkubwa. 

Hakuzaliwa kwenye mali, alizaliwa vitani Alizaliwa kwenye umasikini mkubwa. Mwaka  2004 alipojiunga na Moscow alibadilisha hali ya hewa ya Urusi. Alijenga mnara mkubwa wa umaarufu kwenye Ardhi yenye sura za kibabe (warusi).  Aliifungia timu yake magoli 12 kwenye michezo 67.

Ukipita mitaa ya  Titovo ukawa unalitaja ovyo ovyo jina la Vidic unaweza ukapigwa kofi. Ni nembo sahihi ya ushujaa na Upambanaji. Haijalishi umezaliwa mazingira gani. Ila juhudi zako zitakufanya ufanikiwe. Mnamo mwaka 1989 alisajiliwa na klabu ya Jedinstvo Uzice akiwa na miaka 12 tu. Watoto wa umri ule wengi walipelekwa vitani. Ila unaambiaa kwa uwezo wake na upambanaji wake ulifanya wanajeshi waweke silaha chini wanamtazame mwanajeshi mwanzao akisakata kabumbu. 

Hakwenda vitani kuua alikwenda vitani kutwaa mataji. Je wewe jiulize unaelekea wapi? Vitani kuua au kupata mafanikio? Hakuna aliyemlazimisha kwenda vitani, walijua ana kipaji chenye umuhimu kuliko rasilimali za Balkan. Jiulize wewe watu wanakulazimisha kwenda wapi? Je watu wamegundua una kipaji gani? Kama bado waoneshe wewe una nini.

Vidic pia alifanya vyema akiwa na Timu yake ya taifa. Mnamo mwaka 2006 kwenye michuano ya kufuzu kombe la dunia, timu yake iliruhusu goli moja tu. Ni heri risasi iingie kuliko umfunge goli. Mashabiki 76,000 wa Old trafford waliwekeza imani yao kwa Mserbia huyu mwenye roho ya Khitler.

Wengi wanamfananisha Vidic na Steve Bruce lakini mimi naiona sura ya Adolf Hitler kwenye umbo La Vidic. Wakati Cristiano Ronaldo akiwa na chanuo lake pamoja na Kioo, Vidic alikuwa na taulo lake maalumu la kufutia damu.

Vidic alikuwa tayari kuweka mguu sehemu ya kichwa na kuweka kichwa sehemu ya mguu. Ni nahodha wa miaka ya hivi karibuni ambaye hawezi kusahaulika kirahisi. Kwenye michezo 221 ndani ya Man utd alijikusanyia kadi za njano 39 na kadi nyekundu 6, aliweza kuoiga pasi zaidi ya 8996 ikiwa ni sawa na pasi 42 kwa mechi. Alitelezea mipira mara 363, na kuondoa mipira ya juu mara 808 na kuondoa mipira mara 2231 na amejifunga goli moja tu licha ya kusababisha magoli matatu tu.

Leo ni tarehe 21 mwezi wa kumi tarehe ambayo Vidic alizaliwa. Happy birthday kwa shujaa.. alinunhliwa  euro milion 7 na ameisaidia Man utd kutaaa vikombe 15.

Okwi anaendelea kutesa uwanja wa Uhuru

$
0
0

Emanuel Okwi amefunga goli la nane katika mechi yake ya sita ya ligi kuu Tanzania bara msimu huu wakati Simba ikishinda 4-0 dhidi ya Njombe Mji.

Okwi ameendeleza utawala kwenye uwanja wa Uhuru, magoli yake yote (8) ameyafunga kwenye uwanja huo. Mchezaji pekee mwenye magoli mengi aliyofunga kwenye uwanja mmoja.

Amefunga mechi nne mfululizo ambazo Simba imecheza kwenye uwanja wa Uhuru, hajafunga katika mechi mbili ambazo amecheza nje ya uwanja wa Uhuru.

  • Simba 7-0 Ruvu Shooting (Okwi alifunga magoli manne, akawa mchezaji wa kwanza kufunga hat-trick msimu huu.)
  • Simba 3-0 Mwadui (alifunga magoli mawili na kufikisha magoli sita)
  • Simba 1-1 Mtibwa Sugar (akaendeleza rekodi ya kufunga mfululizo kwenye uwanja wa Uhuru na kufikisha magoli saba yote akiyafunga uwanja huohuo.)
  • Simba 4-0 Njombe Mji (Okwi alifunga goli (1) la kwanza katika mchezo huo. 

Raia huyo wa Uganda aliifungia Simba bao la kwanza kwa kichwa kipindi cha kwanza huku Mzamiru Yassin akipinga mbili naLaudit Mavugo akimaliza goli la nne.

Simba imefikisha pointi 15 sawa Mtibwa Sugar ambao wameshinda 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons lakini ‘mnyama’ anaongoza ligi kwa tofauti ya magoli.

Matokeo ya mechi nyingine zilizochezwa leo

  • Mtibwa Sugar 1-0 Tanzania Ptisons
  • Ndanda 0-0 Singida United
  • Mbao 0-0 Azam
  • Lipuli 1-0 Majimaji
  • Mbeya City 2-0 Ruvu Shooting

Bayern Munich waifikia BvB huku United akichezea kipigo

$
0
0

Katika mchezo wa mapema zaidi hii leo Chelsea waliepuka kipigo kutoka kwa Watford baada ya kutoka nyuma kwa bao 2 kwa 1 hadi kuibuka na ushindi wa mabao 4 kwa 2 katika mchezo uliokuwa wa kusisimua sana.

Walichofanya Chelsea leo inaonekana sio kigeni sana kwanj msimu uliopita pia katika michezo yote ambayo Chelsea waliwafunga Watford mabao yao yalipatika katika dakika kuanzia 87 na kuendelea.

Kabla ya siku ya leo Manchester United walikuwa hawajawahi kupoteza mchezo dhidi ya Huddersfield kwa miaka zaidi ya 46 iliyopita lakini hii leo kwa mara ya kwanza wamekubali kipigo  katika msimu huu wa ligi.

Manchester City wenyewe waliendelea kujichimbia kileleni mwa ligi huku Kun Aguero akiwela rekodi ya ufungaji kwa kufikisha mabao 177 katika klabu hiyo wakati wakiiua Burnley mabao 3 kwa 0.

Katika ligi kuu nchini Hispania Barcelona wamezidi kujikita kileleni mwa ligi ya La Liga baada ya hii leo kuibuka kidedea dhidi ya Mlaga kwa mabao mawili yaliyowekwa kimiani na Gerard Deulufoe na Andres Iniesta.

Ujerumani Bayern Munich wamefanikiwa kuziba tofauti ya alama kati yao na Dortmund baada ya hii leo kushinda bao moja dhidi ya Humburger kwa goli la Cerentin Tolliso huku Borussia Dortmund wakienda sare ya bao mbili kwa mbili na Eintracht.

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>