Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Man City yatisha kombe la dunia

$
0
0

Na: DANIEL S.FUTE

ZIKIWA zimesalia takribani siku kumi kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia, tayari tumeweza kuona vikosi mbali mbali ambavyo vitaenda kuwakilisha vyema mataifa yao katika mchezo wa Soka.

Lakini kupitia vikosi hivyo wapo wachezaji kadha wa kadha ambao wanacheza Soka la kulipwa katika klabu mbali mbali ambao ni waajiri wao.

Wachezaji wengi wanaoitwa katika timu zao za taifa na makocha wao, huwa wanaangaliwa sana katika ubora ambao wanaonesha katika klabu zao.

Klabu ya Manchester City kutoka katika Ligi kuu England, ndio imekuwa klabu pekee kupeleka wachezaji wengi katika fainali za Kombe la Dunia 2018.

Man City imeweza kutoa wachezaji 16, ambao wameenda kuungana na mataifa yao kwaajili ya fainali hizo zitakazoanza wiki ijayo.

Hii inaonyesha ni jinsi gani klabu hii ilivyoundwa vyema katika msimu wa Ligi kuu uliopita kupitia kocha wao mkuu, Pep Guardiola.

Na hawa ndio wachezaji 16 ambao watasafiri na mataifa yao katika fainali hizi za Kombe la Dunia:

Vincent Kompany, Danilo, Ederson, Stones, Sterling, Walker, Clichy, Benardo Silva, David Silva, De Bruyne, Otamendi, Fernandinho, Gundogan, Gabriel Jesus, Kun Aguero na Benjamin Mendy.


Filamu ya usajili wa magumashi VPL ipo madukani

$
0
0
Juzi Alex Lwambano aliuliza kuhusu usajili wa Singida.

Je wale wachezaji walisajiliwa kwa mbinu za mwalimu yupi? Jibu inaonekana ni kama Wanasema Hans ndiye aliyeandaa mipango hiyo tayari.
Vipi Hemed Morocco kocha mpya alishirikishwa katika sajili hizo? Mimi sijui.

Ina wezekana kabisa mchezaji kusajiliwa bila ruhusa au maelekezo ya mwalimu. Si Unakumbuka Usajili wa Ander Herrera? Yule alishasajiliwa kipindi cha Fergie.

Ni kweli kila timu ina mipango yake na namna ya kufanya usajili. Sio kwamba kila mchezaji lazima asajiliwe na mwalimu. Ingekuwa hivyo basi makocha wangekuwa na timu zao kila saa wakisajiliwa wanaenda nazo.

Kuna malengo ya kibiashara ya timu kwa mfano usajili wa Fernando Torres, Usajili wa Gareth Bale. Inawezekana kweli Makocha wetu wa bongo hawana nguvu, lakini pia hata huko ulaya kuna wakati waalimu sio waamuzi wa mwisho wa usajili.

Tofauti yetu sisi na wale wa ulaya ni ipi?

Kwanza, nakubaliana na Yahya Njenge. Njenge anasema hivi, “ni vyema mchezaji au tuseme ni lazima mchezaji asajiliwe na falsafa za mwalimu. Mwalimu anapaswa kushirikishwa usajili wa mchezaji kabla ya yote”

(Bila shaka tuamini kuwa Hemed Morocco alipigiwa simu na akakubali sajili zote kwa mujibu wa Njenge).

Lakini Issa Maeda ana wazo tofauti.

Issa Ametoa sababu kubwa mbili za usajili hapa bongo kisha Lwambano akaongeza Moja.

Sababu ya 3 ya Issa ni kwamba, Usajili wa Tanzania ni wa roho mbaya wivu au kuzuia riziki za wengine.

Nilipomsikia Issa, nikakumbuka Sakata la Mzaliwa wa Kakole Shinyanga mdogo wangu Adam Salamba. Salamba ni rafiki yangu sana. Hivi majuzi niliongea nae kuhusu sakata lake la uhamisho kwenda Yanga. Hakunipa jibu la moja kwa moja lakini alikubali kwamba Yanga inamhitaji. Leo hii Salamba anatarajia kuvaa jezi nyekundu msimu ujao.

Hapo hapo nimekumbuka lile sakata la John Obi Mikel kwenda Man United kisha kuibiwa na Jose Mourinho.

Lakini Lwambano akauliza je wivu huu una faida kwa nani?

Njenge akajibu akasema mchezaji anapaswa kuangalia kama kuna uwezekano wa kucheza hiyo nafasi. Swali likaibuka kati yao, Je Salamba alihitajika Simba?
Binafsi kwa kuwa mimi nimjuaji nikajisemea moyoni kwamba wanataka kutengeneza kikosi kipana.

Hakuna kitu kibaya duniani kama kuiga usichokiweza.

Nani kawaambia kwamba mafanikio ya timu ni kuwa na kikosi kipana? Kikosi kipana ni kusajili ovyo bila mipango? Mbona timu kubwa kama Barcelona hawana huo mfumo wa kusajili wachezaji hovyo kwa ajili ya kupanua kikosi?

Mwisho wa siku Issa akatoa la moyoni

“kuna kijana mmoja bwana mdogo alinifuata akaniuliza, kaka, timu fulani wamekuja je niwakubalie? Nikamuuliza wametoa hela nzuri? Akaniji ndiyo kaka”

Kabla Issa hajamaliza kusimulia Lwambano akadakia na kusema
“wadogo Zangu maisha ndiyo haya haya, hizi ndoto za ulaya ni hadhithi za juma na uledi, maisha yenyewe magumu haya, pigeni hizo hela wakija na Milion 40 zao usikatae pigeni helaaa”

Issa akapigilia msumari kwa kudai kuwa hawa wachezaji wakihitajika Simba na Yanga wasikatae kabisa. Sasa hapa ndipo akili yangu ikakaa sawa. Kumbe lengo hapa sio timu ni hela/fursa.

Issa anasema
“Hakuna mchezaji wa kitanzania mwenye ufanisi wa muda mrefu. Mwaka huu atakuwa na msimu bora mwaka mwingine anapoteana hivyo linapokuja suala la Simba na Yanga ni Fursa ukiringa kwa lengo la kutaka kuendelea kuichezea klabu yako soka litaisha utakaribishwa mtaani na umasikini”

Katika sababu hii ya Issa ndipo sababu yake ya pili kuhusiana na usajili wa bongo ikaibuka.

Timu nyingi zinafanya usajili kwa sababu tu huyo mchezaji anatajwatajwa.

Kidogo hapa tunapaswa kukuna kichwa kabla hatujakubaliana nae

Nimekiangalia kikosi cha Yanga. Kuna wachezaji wengi binafsi yangu hawakupaswa kucheza klabu ile. Wengi wao walisajiliwa kwa sababu walitajwa tajwa sana. Na wengine walisajiliwa kwa sababu ile ile ya awali ya wivu (Buswita). Kuna wachezaji wanaonunuliwa bila timu kuangalia kama wanamhitaji au lah. Kwa mfano Simba ina mchezaji kama Said Ndemla, Ina Mzamiru Yasin ina Mo Ibrahim hawa wote wanachoma mahindi sasa jiulize Niyonzima alisajiliwa wa nini?
Leo hii Marcel baada ya kung’aa msimu paaap kavalishwa jezi nyekundu. Mo Rashid nae kaambiwa chagua moja, uendelee kula ndizi Mbeya au uje unywe juisi za Mo. Akasema usintanie maisha ndiyo haya haya.

Tena Mo anakwambia Okwi na Bocco hawamwambii kitu wajiandae kisaikolojia tu kukaa benchi. Unacheza na maisha mazuri nini?

Sababu ya mwisho ilikuwa ya Lwambano akasema “mchezaji kweli ana uwezo lakini wahusika wanatumia kigezo cha yeye kuwa na njaa kama sehemu ya kumpata bila kuangalia je atacheza wapi kivipi na kwanini”.
Issa Maeda akamtaja Jamal Mwambeleko ambaye alitokea Mbao Fc na kujiunga Simba, kama kielelezo cha wachezaji wazuri wanaozea benchi. Jamal anakumbana na na ushindani mkubwa sana kutoka kwa Erasto Nyoni, Tshabalala pamoja na Asante Kwasi.

Katika sababu hizi hakuna hata moja inayokwenda sawa na mawazo ya Njenge kwamba kocha anapaswa kushirikishwa kuhusiana na usajili wa mchezaji. Tena katika fukuafukua yangu nimekumbana na Fununu kwamba Omog aliondoka Simba kwa kuwa alikuwa analazimishwa wachezaji fulani wacheze au fulani asajiliwe.

Nimewaza sana sasa anayehusika na usajili ni nani?
Juzi juzi katika pita pita zangu nikakutana na kibonzo. Ulaya ukienda kuomba kazi unaombwa cheti, ujuzi wako na ueleze mipango yako, Lakini ukiingia Tanzania kuomba kazi unaulizwa hapa umeagizwa na nani? Kwa hiyo hata kwenye soka letu kuna uwezekano mkubwa usajili unafanywa maajumbani na sio maofisini.

Hatuna maskauti hatuna mawakawala hatuna wathaminishaji wa ufanisi wa mchezaji ila tuna namba za simu. Inapigwa tu oyaa dogo eeeh njoo Leaders Club hapa bosi anataka kuongea na wewe.

Inapigwa tu oyaa dogo eeeh njoo Leaders Club hapa bosi anataka kuongea na wewe.Makala hii imeandaliwa na Privaldinho (Instagram)

Maisha ya Yanga kabla na baada ya kuondoka Manji

$
0
0

Kwenye kipindi cha Sports Xtra cha Jumanne Juni 4, 2018, kaimu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga alizungumza mambo mengi yanayohusu klabu hiyo.

Miongoni mwa mambo ambayo aliyadadavua upana ni maisha ya Yanga kabla na baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji.

Tunashukuru kwa alichofanya Manji katika kipindi chote ambacho alikuwa madarakani na kabla ya kuwa madarakani wakati huo akiwa mdhamini wa klabu, amekuwa ni msaada mkubwa.

Kila mwanachama na mpenzi wa Yanga anajua maisha tuliyokuwa nayo wakati huo, Manji alikuwa mpiganaji na timu iliweza kufanya vizuri kwa kipindi chote ambacho alikuwepo.

Katika kipindi cha hivi karibuni wakati Manji yupo Yanga tuliweza kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya kambi mbalimbali hakukuwa na tatizo la kulipa mishara, ilikuwa inalipwa kwa wakati.

Aina ya wachezaji na benchi la ufundi lilikuwa ni zuri sana katika vipindi vyote ambavyo alikuwepo na hakukuwa na dosari.

Tulikuwa na kipindi cha neema kipindi hicho Manji yupo. Alikuwa analipa mishahara ya wachezaji, benchi la ufundi na secreriat kiasi kisichopungua Tsh. 125M kwa mwezi.

Ishu za usajili kwa wastani tulikuwa tunaweza kusajili wachezaji kwa kiasi cha Tsh. 500 hadi 600M.

Kwa hiyo unaweza kuona ni gape kubwa kwa yeye kutokuwepo ndani ya uongozi na kama mfadhili wa klabu ya Yanga.

Alipotangaza kujiuzuli ilikuwa kama mshtuko  na katika hali ya kawaida huwezi kutafuta njia ya kukimbia badadala yake unajipanga na kutulia ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Tunashirikiana na kamati ya utendaji kwa pamoja na mazingira yaliyoliyopo, tangu Manji ameondoka tulikuwa na deni kama miezi mitatu mapaka leo ni wastani wa miezi 18 ambayo pia nimekuwa nikikaimu nafasi yake.

Katika miezi hiyo 18 uongozi huu uliobaki umeweza kulipa mishahara kwa miezi 16, tuna deni la mishahara ya miezi miwili ambalo tunaendelea kulifanyia kazi kuhakikisha tunakamilisha. Changamoto ni moja, kwamba mishahara ilikuwa haiji kwa wakati katika kipindi chetu lakini kwa kifupi tuna deni la mishahara ya miezi miwili.

Sanga amesema wakati Manji yupo kulikuwa na mfumo kwanza yeye kama Mwenyekiti na mfadhili wa timu alikuwa anaweza kuchangia kwa atakavyoona inafaa kwa wakati huo kwa hiyo alikuwa anasimama kama mwenyekiti na mfadhili wa timu kwa wakati mmoja.

Ndiyo maana waliokuwa wanabeza mpango wa mabadiliko ya uendeshaji alipojaribu kuomba akodishwe nembo ya Yanga wakasema aondoke atakuja mwekezaji mwingine, tangu ameondoka hajaja mtu zaidi ya watu kukimbia.

Badada ya Manji kuondoka, Yanga ilikopa 500M

$
0
0

Kaimu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga baada ya kusema wakati Manji yupo ndani ya uongozi wa klabu hiyo alikuwa anachangia pesa kama mfadhili, inawezekana swali linalokuja akilini mwako sasa hivi Yanga inapata pesa kutoka wapi?

“Wanachama na wapenzi wa Yanga lazima watambue nguvu na mchango wa uongozi ambao upo madarakani, katika kipindi cha miezi 18 tumeweza kulipa mishahara ya miezi 16.”

“Wakati tunaingia tulijikuta tuna changamoto nyingi sana kuhusu suala la mishahara, tayari kulikuwa na madeni wakati huo tulikuwa tunatakiwa kushiriki michuano ya SportPesa. Tulichokifanya tuliwaambia hatuwezi kushiriki mashindano hayo kwa sababu wachezaji wengi walikuwa wamefikia mwishoni mwa mikataba yao.”

“Baada ya kuzungumza nao (SportPesa) walikubali kutukopesha pesa ambazo zipo kwenye mkataba wetu kiasi cha shilingi 500M tukaweza kulipa mishahara ya nyuma na hela nyingine tukaingiza kwenyr usajili.”

“Baada ya hapo tumekuwa tunatumia mbinu mbalimbali za kupata pesa za kulipa mishahara mbinu ambazo si vizuri sana kuzizungumzia kwenye vyombo vya habari lakini nitawaeleza wenye timu ambao ni wanachama siku ya mkutano.”

Sanga kuhusu wanaojiuzulu Yanga “hatutakiwi kukimbia mapambano”

$
0
0

Hivi karibuni kuna baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga wameamua kujiuzulu kutokana na sababu mbalimbali.

Salum Mkemi ni miongoni mwa wajumbe waliojiuzulu na kusema matokeo mabovu ya Yanga ndio sababu ya yeye kujiuzulu.

Ukiachana na Mkemi, Hashim Abdallah pia alitangaza kujiuzulu hivi karibuni na kusema aliingia kwenye uongozi akiwa na lengo la kuitoa Yanga sehemu moja kwenda nyingine ikiwa ni kubeba vikombe, kujiendesha yenyewe bila kutembeza bakuli lakini kwa muda wa miaka miwili aliokuwepo kwenye uongozi amefeli ndio maana amekaa pembeni.

Sanga amesema ukiwa vitani hutakiwi kukimbia mapambano, unatakiwa kupambana hadi mwisho.

“Tupo kwenye vita hatutakiwi kukimbia mapambano, tunatakiwa kupambana hadi mwisho halafu tuwaambie waliotuchagua tumefikia hapa, wao ndio watakuwa na maamuzi tufanye nini baada ya kufika hapo na baada ya hapo kitatokea hicho kinachotakiwa kutokea kwa maslahi mapana ya Yanga.”

“Ukiangalia sababu ambazo zimetolewa ambazo zimekuwa wazi na naweza kuzizungumzia, kuna mjumbe amejiuzulu na amesema ameona kwamba tumeishia nafasi ya tatu kwenye ligi kwa hiyo anawajibika.”

“Nimeangalia nimeona kila mwaka hata vilabu vingine vingekuwa vinafanya mabadiliko ya uongozi kwa sababu havijamaliza katika nafasi ambazo walijiwekea malengo.”

“Waliowachagua wanajua kwa nini wamesema vile lakini wao ndio watakuwa na hoja nyingi za kuhoji kwa nini viongozi wao wamejiuzulu.”

Yanga ina mpango kuziba nafasi ya Manji?

$
0
0

Hivi karibuni Yanga itafanya mkutano mkuu lakini wanachama na wapenzi wa klabu hiyo wanatamani kujua kupitia mkutano huo watapata viongozi wapya kuziba nafasi ya aliyekuwa mwenyekiti wao Yusuf Manji ambaye alijiuzulu tangu mwezi Mei 2017.

Nafasi nyingine ambazo zipo wazi ni za wajumbe wa kamati ya utendaji (Hashim Abdalla na Salum Mkemi) ambao wamejiuzulu hivi karibuni.

Kaimu mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga amesema mkutano mkuu ujao utakuwa na lengo la kuwaeleza wanachama matatizo yanayoikabili timu, kuhusu uchaguzi wa kuzipa nafasi zililizo wazi utatangazwa baadaye.

“Ukiangalia katiba yetu inapozungumzia mwenyekiti anapokuwa ameondoka madarakani kwa kujiuzulu, katiba inasema makamu atachukua nafasi hiyo mpaka mkutano mkuu unaofuata kwa ajili ya kujaza nafasi hiyo.”

“Pamoja na hayo, katiba ina mapungufu mengi sana. Ukizungumzia mkutano unaofuata maana yake kwenye mkutano huu ujao wa Juni 10 tufanye uchaguzi, lakini nadhani malengo yalikuwa ni kwa ajili ya nafasi nyingine ndogondogo kwa sababu unawezaje kufanya uchaguzi kwa nafasi kubwa na siku hiyo ukafanya mkutano mkuu wa wanachama?

“Kwa hiyo sisi tumeona ni afya kufanya mkutano mkuu wa wanachama ili tuwaeleze matatizo yaliyojitokeza, hata kama kuna kiongozi yoyote anaingia kwenye nafasi hiyo awe anajua nini kinatakiwa kufanyika baada ya kuchaguliwa, vinginevyo hatakuwa na taarifa yoyote.”

“Tutaenda kwenye mkutano mkuu wa wanachama, tutajadili baada ya hapo maelekezo ya kuja kujaza nafasi ya mwenyekiti tutatangaza muda ambao pia upo ndani kwa mujibu wa katiba na tutajitahidi kufanya muda mfupi ili ushiriki wa ligi kuu wa msimu ujao usiwe na matatizo hasa katika masuala ya usajili.”

Simba, Yanga chungu kimoja

$
0
0

Simba na Yanga zimepangwa kundi moja kwenye michuano ya CECAFA Kagame Cup 2018 michuano inayotarajia kuanza Juni 28-Julai 13, 2018.

Kundi A: Azam (Tanzania), JKU (Zanzibar), Uganda Reps (Uganda) Kator FC (S. Sudan).

Kundi B: Rayon Sports (Rwanda), Gor Mahia (Kenya), Lydian Ludic (Burundi), Ports (Djibouti)

Kundi C: Yanga (Tanzania), Simba (Tanzania), St. George (Ethiopia),  Dakadaha (Somalia).

Nicholas Musonye amesema ratiba ya mashindano ya mwaka huu yataanza Juni 28 hadi Julai 13, 2018 lakini ratiba ya mashindano imezingatia ratiba ya kombe la dunia. “Tumezingatia ratiba ya kombe la dunia hivyo mechi hizi hazitaingiliana na ratiba za kombe la dunia.”

Mashindano ya CECAFA Kagame Cup yatachezwa katika viwanja viwili, uwanja wa taifa na uwanja wa Azam Complex.

Bingwa wa mashindano hayo atapata dola 30,000 za kimarekani, mshindi wa pili dola 20,000 na mshindi wa tatu dola 10,000.

Mashindano ya Kagame yanadhaminiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame (mdhamini mkuu) lakini Azam TV ndio warushaji rasmi wa mechi zote za mashindano haya.

Orodha kamili ya makocha wa kombe la dunia hii hapa

$
0
0

Kocha: Óscar Tabárez
Timu: Uruguay
Miaka: 71

Kocha: Joachim Löw
Timu: Germany
Miaka: 58

Kocha: Carlos Queiroz
Timu: Iran
Miaka: 65

Kocha: José Néstor Pékerman
Timu: Colombia
Miaka: 68

Kocha: Didier Deschamps
Timu France
Miaka: 49

Kocha: Adam Nawalka
Timu: Poland
Miaka: 60

Kocha: Heimir Hallgrímsson
Timu Iceland
Miaka: 50

Kocha: Hernán Gómez
Timu: Panama
Miaka: 62

Kochq: Vladimir Petkovic
Timu Switzerland
Miaka: 54

Kocha: Fernando Santos
Timu: Portugal
Miaka: 63

Kocha: Ricardo Gareca
Timu: Peru
Miaka: 60

Kocha: Héctor Cúper
Timu: Egypt
Miaka: 62

Kocha: Aliou Cissé
Timu: Senegal
Miaka: 42

Kocha: Óscar Ramírez
Timu: Costa Rica
Miaka: 53

Kocha: Age Hareide
Timu: Denmark
Miaka: 64

Kocha: Juan Carlos Osorio
Timu: Mexico
Miaka 56

Kocha: Hervé Renard
Timu: Morocco
Age: 49

Kocha: Tite
TiMu: Brazil
Miaka: 57

Kocha: Janne Andersson
Timu: Sweden
Miak: 55

Kocha: Julen Lopetegui
Team: Spain
Age: 51

Coach: Roberto Martínez
Team: Belgium
Age: 44

Coach: Gernot Rohr
Team: Nigeria
Age: 64

Coach: Stanislav Cherchesov
Team: Russia
Age: 54

Coach: Gareth Southgate
Team: England
Age: 47

Coach: Nabil Maaloul
Team: Tunisia
Age: 55

Coach: Jorge Sampaoli
Team: Argentina
Age: 58

Coach: Tae-Yong Shin
Team: South Korea
Age: 47

Coach: Zlatko Dalic
Team: Croatia
Age: 51

Coach: Juan Antonio Pizzi
Team: Saudi Arabia
Age: 49

Coach: Bert van Marwijk
Team: Australia
Age: 66

Coach: Mladen Krstajic
Team: Serbia
Age: 44

Coach: Akira Nishino
Team: Japan
Age: 63

Unandhani ni kocha yupi ataopoa hapo


Wajue makinda wasioimbwa watakaosumbua kombe la dunia

$
0
0

Elizabeth lyavule

zimesalia siku tisa tu mataifa 32 yakianza kuoneshana ubabe kombe la dunia, huku macho ya wengi wakingojea kumuona Marcus Rashford na Uingereza, Marco Asensio na Hispania, Paul Dybala wa Argentina na wengine wengi, jaribu kuwafumbia macho hawa tuliowazoea na uwacheki makinda hawa tusiowajua sana na kuwasifu uwezo wao kule Urusi.

Hirving Lozano raia wa Mexico. Alianza maisha yake ya soka kama mshambuliaji nchini kwao Mexico akiwa na klabu ya Pachuka, msimu wake wa kwanza alifunga magoli 18 ndani ya michezo 37 aliochezea klabu yake hivyo maskauti wa timu ya PSV nchini Uholanzi walimuona wakamsajili na akiwa PSV amemaliza msimu akiwa ni mfungaji bora wa klabu magoli 17 na mfungaji namba tano wa ligi ya uholanzi pia alifanikiwa kutoa pasi za mwisho zilizozaa magoli 9 kubwa zaidi kaisaidia PSV kuwa mabingwa wa uholanzi (eredvisie).

Ana uwezo mkubwa wa kupiga mipira iliyokufa, ana krosi nzuri na katika umri wake wa miaka 22 aliitwa timu ya taifa Mexico na mchezo wake wa kwanza ilikua mwezi wa pili mwaka 2016 dhidi ya Senegal alifanikiwa kutoa pasi ya goli katika mechi hiyo. Ana magoli 7 katika michezo 26 aliyoichezea nchi yake moja akiifunga timu ngumu ya ubeligiji mwezi wa 11 mwaka 2017 katika sare ya goli 3-3. Ana uhakika wa namba Mexico tuone ataunda vipi ushirikiano na wenzie kuifanya nchi yao ifike mbali mwaka huu kule Urusi.

Lucas Torreira wa Uruguay ni kinda mwenye miaka 22 anaetizamiwa kuwa na mashindano mazuri ya kombe la dunia Urusi. Anacheza kama kiungo mkabaji na sasa yupo katika klabu ya Sampdoria nchini Italia, msimu uliokwisha amecheza michezo 33 ya ligi ya Italia “seria a” ametengeneza nafasi 33 za kufunga, akiingilia mpira kwa mpinzani (interception) mara 67 pia akifanikiwa kumpora mpira mpinzani (tackling) mara 66 si kitu kidogo kwa umri wake. Kwa takwimu hizo haitakua ajabu kumuona akiunda kikosi cha kwanza na wakali wengine kama Diego Godin, Suarez, Edson Cavan nakuifikisha mbali nchi yake katika mashindano hayo.

Aleksandr Golovin wa Urusi. Akiwa ni mwenyeji kinda huyu mwenye miaka 22 atapambana vilivyo kuiokoa nchi yake kukwepa aibu yakutoka mapema, anacheza katika klabu ya CSKA Moscow ya urusi na ni mmoja kati ya wachezaji waliobeba kombe la Ulaya la vijana chini ya miaka 17 mwaka 2013,

kinda huyu ni kiungo wa kati anaeweza kuunganisha timu kati ya ulinzi na ushambuliaji (box to box midfielder) huku akisifika kwa uwezo mkubwa wa kukokota mpira, kutoa pasi nzuri na kukaa na mpira bila adui kumpokonya.

Amecheza mechi 38 mashindano yote msimu wa 2017-2018 akafunga magoli 7, akatoa pasi za kufunga 4 si kitu cha kubeza kwa umri wake.

Ismaila Sarr raia wa Senegal. Kinda huyu wengi wanamlinganisha na Sadio Mane na wanamtabiria kufanya vizuri kuliko Sadio Mane akikomaa mana ndio kwanza ana miaka 22 tu.

Anacheza nafasi ya ushambuliaji kutokea pembeni huko Ufaransa katika klabu ya Rennes na msimu wake wa kwanza alikua na goli 5 pasi za mwisho zilizozaa magoli 5 katika michezo 22 aliyoanza huku 2 akitokea benchi. Akiwa na Senegal mwezi wa 9 mwaka 2016 alicheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Namibia akitokea benchi kuchukua nafasi ya Sadio Mane.

Kwasasa kashacheza michezo 10 nakufanikiwa kupata magoli 2. Ataungana na washambuliaji wengine kama Mame Biram Diouf, Maussa Sow, Diafra Sakho na Sadio Mane kuhakikisha wanaiwakilisha vizuri Senegal na Africa kiujumla wafike mbali.

Cristian Pavon kinda kutoka Argentina. Winga huyu hategemewi sana kupata nafasi kutokana na upinzani wa nafasi anayocheza kujaa wachezaji wazuri wenye vipaji kama Angel Di Maria, Paul Dybala na mfalme Leonel Messi.

Anacheza nchini kwao Argentina katika klabu ya Boca Junior,kawa na msimu bora ulopita akiifungia klabu yake magoli 6 nakutoa pasi 11 za mwisho zilizozaa mabao nakumfanya kocha Sampaoli kumuita kikosi cha wachezaji 23 watakaoiwakilisha nchi kombe la dunia,

aliichezea Argentina dhidi ya Urusi mwaka uliopita na kufanikiwa kutoa pasi iliozaa goli pekee lililofungwa na Sergio Kun Aguero katika ushindi wa 1-0 waloupata pia alitoa pasi kati ya magoli mawili katika mchezo wa kirafiki waliopoteza dhidi ya Nigeria.

Macho ya vilabu vyote vikubwa barani Ulaya yatakua Urusi kucheki vipaji kama hivi na haitakua ajabu kusikia wameenda timu kama Manchester utd, Arseno na Napoli pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa majira haya ya kiangazi.

Kocha wa Mtibwa kuhusu ubora wa Dilunga msimu huu

$
0
0

Hassan Dilinga alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mashindano ya Azam Federation Cup 2018 baada ya kuisaidia timu yake kushinda ubingwa wa mashindano hayo.

Dilinga amewahi kucheza Yanga, Ruvu Shooting amefanya vizuri msimu huu akiwa na Mtibwa Sugar kwa kuisaidia kumaliza ligi katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi kuu.

Kocha wa Mtibwa Sugar Zubery Katwila amezungumzia kilichombadilisha Dilunga na kuonekana bora msimu huu.

“Dilunga ni mchezaji anaeweza kubadili matokeo uwanjani wakati wowote, mbunifu anaweza kufanya chochote na anaunganisha mbele na katikati. Ni mchezaji wa aina yake na kwenye timu yangu namtumia kama mchezaji muhimu ambaye huwa namfanya awe huru afanye anachotaka.”

“Ni mchezaji mzuri, hapo katikati alipokuwa kwenye timu nyingine alikuwa anajitahidi kurudisha kiwango chake lakini hakukifikia.”

“Kuna wakati nilimuhitaji lakinisl sikufanikiwa kumpata, wakati huo nilikuwa kocha msaidizi Meck ndio alikuwa kocha mkuu. Sasa hivi mimi ndio kocha mkuu nimejitahidi hadi nimempata kwa sababu nilikuwa najua ana kitu gani na Mtibwa tunaweza kunufaika nae.”

“Nilimwambia wewe utatusaidia badae na kweli mafanikio anayaona hana jibu la kunipa zaidi ananipa tu pongezi kwa mafanikio anayopata.”

Dilunga amekuwa mfungaji bora kwa upande wa Mtibwa Sugar kwenye kombe la ASFC akiwa na magoli manne magoli mawili nyuma ya mungaji bora wa mashindano Habib Kyombo aliyefunga magoli sita.

Lechantre kabakiza siku 43 Simba

$
0
0

Kocha mfaransa wa Simba Pierre Lechatre amebakiza siku 43 kwenye mkataba wake wa kuifundisha Simba.

Mkataba wa Lechatre utamalizika June 18, 2018 ambapo atakuwa huru kuondoka au kubaki Simba kama watahitaji kuendelea nae.

Haji Manara akiwa Kenya amethibitisha kwamba mkataba wa kocha wao unaelekea ukingoni na amewaomba wanasimba kuwa watulivu na wavumilivu wakisubiri uongozi uamue kama utaendelea au utaachana na kocha huyo.

“Kocha Lechantre mkataba wake unamalizika mwezi June 18, 2018 uongozi utakaa nae utaona kama ipo haja ya kuendelea nae au la”-Haji Manara.

Lechantre alisaini mkataba wa kuifundisha Simba katikati ya msimu akichukua nafasi ya Joseph Omog ambaye alitimuliwa.

Masoud Djuma kuhusu ishu ya kujiuzulu Simba

$
0
0

Kocha msaidizi wa Simba Masoud Djuma amekanusha taarifa inayosambaa kwenye social media kwamba amejiuzulu kuifundisha klabu hiyo ambayo kwa sasa ipo nchini Kenya ikiendelea na mashindano.

Kocha huyo amesema hawezi kuondoka Simba hadi akamilishe kilichompeleka.

“Sijajiuzulu, maneno hayo siyajui ninamkataba Simba na nimepanga kumaliza mkataba wangu kwa amani, mimi nipo hadi nihakikishe nimefanya kilichonileta Simba”-Masoud Djuma.

Click ‘play’ hapa chini usikilize sauti ya Masoud Djuma alivyokanusha story inayo-trend kwenye social media kwamba ameikacha Simba.

Kwanini mashabiki wa Man Utd wanaipenda sana Real Madrid.

$
0
0

Na Elizabeth Lyavule

Ilianza tarehe 2 February mwaka 1958 ambapo wachezaji wa Manchester United walipata ajali ya ndege na kupoteza maisha. Liverpool walileta kejeli sana baada ya huu msiba mpaka wakaamua kutengeneza nyimbo ya kuwakejeli Manchester United na wakiimba “Your players have turned manure” Wakimaanisha wachezaji wenu waliokufa wamegeuka mbolea.

Watu wanapenda sana kuwakejeli mashabiki wa Manchester United kwa kupitia hili neno “MANURE”Kila mtu anayekejeli Manchester United kwa kupitia hili neno huwa anawakumbusha ajali ya ndege maana chimbuko la hili neno lilianzia huko.

Ilikuwa ni huzuni sana kipindi hicho lakini Liverpool hawakujali waliendelea kushangilia kwa furaha huu msiba. Na kwanini mashabiki wengi wa Manchester United duniani huwa wanaipenda Real Madrid kama timu yao ya pili?

Ni kwa sababu baada ya ajali ya ndege mwaka 1958 mwaka huo huo Real madrid walikuwa mabingwa wa Uefa champions league na waliomba kombe hilo wapewe Manchester United kama kuwafariji na Manchester United walikataa kupewa kitu cha bure ambacho hawajakitolea jasho.

Real madrid hawakuishia hapo wakati ligi imeisha na likizo imeanza waliwaalika Manchester United nchini Hispania na gharama zote waligharamia wao.

Kule nchini Hispania Real madrid waliandaa mechi za kirafiki nyingi tu na waliomba hayo mapato yote wapewe Manchester United ili yawasaidie kujijenga upya.

Real madrid hawakuishia hapo waliamua kumtoa mchezaji wao bora Alfredo De Steffano bure achezee Manchester United. Alfredo De Stefano alikuwa mmoja wa wachezaji waliotoa mchango mkubwa kwa Manchester United mpaka wakachukua kombe lao la kwanza la Uefa champion league akiwa anakaribia kustaafu.

Kwa hiyo uhusiano wa Manchester United na Real madrid ni mkubwa na hauwezi kuvunjwa hata kama Ramos angeng’oa bega la Salah fainali ama kumuua Karius.

Timu ya kwanza kufika Urusi kwa ajili ya World Cup hii hapa

$
0
0

Kuna kale kamsemo waswahili husema kutangulia bar sio kulewa. Lakini huwa waswahili hawa hawa mimi wananichanganya akili. Wakishakwambia hivyo ukizuga zuga wanakwambia chelewa chelewa utakuta mwana si wako.

Tena wapo wale wanaojiita Wahenga wanasema kwamba haraka haraka haina baraka, lakini ukijifanya mtaratibu saa watakung’ong’a kwa kebehi kwamba ngoja ngoja huumiza matumbo.

Wapersia wa Iran wao wameona wasizungukeeee sanaaa. Wao mapemaa washatimba Urusi. Hawana mambo mengi. Wao wamefuata kombe lao tu. Hawana tatizo na mtu.

Naam.. Timu ya taifa ya Iran wao tayari washatia maguu katika ardhi ya Putin kwa ajili ya mtanange wa Kombe la dunia.

Wao wameona hakuna haja ya kupoteza muda na wamefika mapemaaa kabisa ili kuisoma hali ya hewa halafu hapo baadae wausome mchezo. Wanajiamini na wanajua fainali ina wahussu na hawaachi kitu kabisa. Wametumwa ubingwa . Hawajenda kuuza sura au kushiriki. Wapo kazini. Hawarembirembi mambo. Wao wanachokijua ni kwamba Nyota njema huonekana asubuhi.

Wameawaacha wajerumaani waendelee kujadili kwanini Sane ameachwa na Wabrazil waendelee kumpongeza Fred kwenda Man United lakini waomkifika tu wakabidhiwe ubingwa wao.

Kocha mkuu wa taifa hilo Bwana Carlos Queroz ametoa tahadhari mapemaa. Amesema wapinzani wao watakiona cha mtema kuni. Afe mfugaji lakini lazima ng’ombe afike mnadanai. Ndio. wamesema sahauni kabisa kuhusu alama za bwerere.

Kocha huyo amesema wao watagawa dozi wala haakuna masihara kabisa. Wamefika mapema ili warilaksi na kuwaondoa wenge wachezaji wao.

Iran walikuwa timu ya kwanza ya Asia kukata tiketi ya bombadia kwenda Urusi. Hata hivyo hii ni kwa mara yao ya 5 wanakwenda katika mashindano ya Kombe la dunia.

Iran walifikia uwanja wa Ndege wa Vnukovo mapema hivi leo huku wakijiandaa na Mpambano wao wa kwanza dhidi ya Morocco june 15 katika uwanja wa St Petersburg.

Iran wamefikia katika kambi ya Lokomotiv Bakovka ambapo ndipo watapumzikia na kupanga mipango yao.

Mwiisho kabisa Kocha wao mkuu amewatakia kila mshiriki Kombe la Dunia Jema.

Mambo yapo mbio mbio ndugu zangu. Bado siku 8 tu. Ushajipatia king’amuzi cha Dstv mapema? Hebu changamkia fursa kama ndugu zako wa Iran. Usibabaishwe mambo yote yapo Dstv, kama Sio Dstv POTEZEA TU.

Floyd “Money” Mayweather aendelea kuwapoteza Messi na Cr7

$
0
0

Jariba maarufu la masuala ya biasha na kipato la Forbes limetoa orodha mpya ya wanamichezo ambao wanalipwa pesa nyingi, tathmini hii imefanywa kwa siku za karibuni kuanzia June 2017 hadi June 2018.

Jina la mwanamasumbwi Floyd Mayweather bado linaendelea kushika namba moja katika orodha ya wanamichezo walioingiza mkwanja mrefu kwa kipindi hiki akiwa amepewa kiasi cha $285m.

Sababu kubwa ambayo imemfanya Mayweather kuwa tajiri kiasi hiki ni pambano lake na Conor McGregor ambalo lilimfanya kuwa mwanamichezo wa 3 kuwahi kutengeneza $1b katika mchezo mmoja huku akilipwa karibia $275m katika pambano hilo.

Manguli wawili katika soka Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ndio wanaomfuatia Mayweather, ambapo Messi yuko nafasi ya pili akiwa amelipwa $111m katika muda huu wa miezi 12.

Baada ya Messi yupo Cristiano Ronaldo ambaye hadi sasa anawaza mkataba mpya ndani ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo kwa kipindi hiki cha June 2017 hadi June 2018 amepokea $108m ikiwa ni pungufu ya $3m kutoka alipo Messi.

Aliyekuwa mpinzani mkubwa wa Mayweather, bondia Conor McGregor anashikilia nafasi ya nns akiwa na $99m, huku mchezaji ghali zaidi duniani Neymar akiwa katika nafasi ya 5 na kiasi cha $90m.

LeBron James yuko nafasi ya 6 na $85.5m, huku mcheza tennis Rodger Federer akiwa nafasi ya saba na $77.2m, Stephen Curry yuko nafasi ya nane na $76.9m, huku nafasi ya 9 ikienda kwa mcheza baseball Matt Ryan $67.3m na ya 10 ni Matthew Stafford $59.5m


“Tulibeza mipango ya Manji”-Sanga

$
0
0

Kaimu mwenyekiti wa Yanga Bw. Frank Sanga ameweka wazi baadhi ya mipango ya aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji lakini mipango hiyo ilipigwa chini na wanachama na kuonekana haifai.

Sanga ameeleza pia namna Manji alivyoingia kwenye uongozi wa Yanga na malengo yake matokeo yake aliishia kujiuzulu baada ya kuona mipango yake haiendi sawa.

“Manji aliingia Yanga kama mtu aliyekuja kutatua migogoro ambayo ilikuwepo kwa muda mrefu, alituunganisha tukawa kitu kimoja.”

“Hatua ya pili alihisi hajaona mafanikio akiwa nje kama mfadhili wa kawaida, akaona ni vyema awe kiongozi, alipokuwa kiongozi ndiyo tukaingia pamoja.”

“Moja ya mkakati mkubwa ilikuwa ni kuona na kuendesha lakini kulikuwa na changamoto za uendeshaji uongozi kupitia kamati ya utendaji ya watu ambao wamechaguliwa kwa aina ya watu ambao wanaingia pale kwa utashi wa Yanga.”

“Baada ya kuingia kama mwenyekiti wa Yanga na mimi makamu, tulikuwa na kamati ya utendaji kwa ujumla tunafanya kazi pamoja lakini kulikuwa na changamoto zake ambazo nyingine sio za kuzizungumza.”

“Akaona kuna njia nyingine ya kwenda kwenye mabadiliko ya katiba ya kufanya mwenyekiti na makamu kuwa kwenye kapu moja na wao kuunda kamati ya utendaji, mabadiliko hayo yaliridhiwa na mkutano mkuu ambapo tulipelekea kuunda kamati ya utendaji ya kuteua ambayo nadhani ndiyo kamati ya utendaji iliyofanya kazi vizuri katika kipindi chote.”

“Tulikuwa na mfumo sahihi wa mawasiliano lakini pia tulikuwa na watu ambao tuliwahitaji kwa ajili ya maendeleo ya Yanga lakini pamoja na hayo tulipomaliza kipindi chetu cha miaka miwili ndani ya miaka minne tulilazimika kufanya uchaguzi. Maelekezo yakatoka TFF na BMT kwamba tufuate katiba ya zamani kwa sababu mabadiliko hayakuwa yamesajiliwa.”

“Tukakubaliana kutofanya uchaguzi ule, lakini tukakutana na changamoto zilezile tulizokutana nazo mwanzoni nadhani ndiyo maana mwenyekiti alikuja na njia nyingine ya kuendesha timu kwa njia kuikodisha.”

“Yalikuwa ni mawazo yake ya kutaka kuikodi timu, alikuwa tayari kutoa shilingi 100M kila mwaka kwa ajili ya kuendeleza matawi, faida zote za ubingwa na zawadi inachukua timu, usajili anafanya yeye, mishahara analipa yeye, biashara zote ambazo zingeanzishwa katika kipindi hicho 25% ya faida ingechukua Yanga.”

“Baada ya miaka 10 klabu ingerudi kwa wanachama lakini tukaona haifai na tukabeza lakini hatukuwa na njia mbadala, ametoka tunaanza kulalamika tunataka arudi.”

Luis Monti, mwanadamu pekee aliyecheza kombe la dunia mataifa mawili tofauti

$
0
0

Hakuna bahati kubwa kama kucheza michuano ya kombe la dunia, ndio maana Diego Maradona amekiri kwamba jasho la zile siku 30 katika michuano hiyo ni jasho tamu zaidi katika soka kwa mwanaume.

Lakini kama kuna bahati katika kombe la dunia baasi Muargentina mwenzake Maradona aitwaye Luis Monti alibahatika zaidi kwani huyu ndio alikuwa mwanadamu pekee kuwahi kushiriki kombe la dunia kwenye mataifa mawili tofauti.

Monti ana asili ya Argentina ambako alizaliwa huko mwaka 1901 na kuanza soka lake katika vilabu vya Huracan, Boca Juniors na baadae San Lorenzo akitajwa kama kati ya kiungo mkabaji bora kuwahi kutokea Argentina.

Mashindano ya kombe la dunia 1930 pale nchini Uruguay yalimpa heshima Monti katika hatua za mwanzo, aliisaidia Argentina kuifunga Ufaransa kabla ya kuwapiga bao 6-1 Mexico na kisha wakaipiga Chile bao 3-1.

Nusu fainali alifunga moja ya bao walipoifunga USA mabao 6-1, lakini fainali walikutana na Uruguay na half time tu Argentina akala 2-1, na hadi baada ya dakika 90 Argentina walikufa kwa bao 4-2.

Baada ya mchezo huu inadaiwa kwamba Monti pamoja na wachezaji wengine walianza kupokea vitisho kutoka kwa mashabiki mbalimbali wa Argentina wakitishia maisha yao na hii ikawafanya waishi kwa mashaka.

Wakati jambo hili linatokea ikaja ofa kutoka nchini Italia, ambako aliahidiwa $5000 kwa mwezi pamoja na gari. Ofa hii ndio ilihitimisha uraia wa Monti katika nchi ya Argentina kwani aliamua kusepa.

Alipofika Italia Monti aliichezea Juventus na uhamisho huu ukiwa na ushawishi mkubwa kutoka kwa mtawala wa Italia kipindi hicho Benito Mussolini na lengo lake haswa ni Monti kuwasaidia kutwaa kombe la dunia 1934 ambalo Italia walikuwa waandaaji.

1934 Argentina ambako ndiko aliondoka Monti waliondolewa na Sweden katika siku ambayo Monti alikuwa akilichezea taifa lake jipya la Italia na kuifunga USA kwa mabao 7-1.

Robo fainali Italia akakutana na Hispania na kutoka sare ya 1-1 na mchezo kuamuliwa kurudiwa ambapo baada ya marudiano Italia walifudhu kwenda nusu fainali kwa bao la Guissepe Meaza.

Inadaiwa mchango mkubwa wa Mussolini na figisu ziliifanya Italia kuingia fainali na wachezaji wa timu ya taifa ya Italia walipewa onyo na Mussolini akiwaambia inabidi washinde mchezo huo ama wafe.

Italia walikutana na Czechoslovakia katika fainali huku Italia wakipewa nafasi kubwa kushinda lakini hadi dakika ya 75 walikuwa nyuma kwa bao moja kwa nunge mbele ya wapinzani wao walioonekana vibonde.

Dakika ya 81 Italia walisawazisha bao hilo kupitia kwa Raimundo Orsi kabla ya Angelo Schiavo kuipatia Italia bao la pili ambalo lilimfanha Monti kubeba kombe la dunia akiwa katika taifa lake lingine.

Messi apata vitisho, mchezo wao wapigwa chini

$
0
0

Inasemekana timu ya taifa ya Argentine imefutilia mbali mchezo wao wa kirafiki dhidi ya taifa la Israel. Taifa hilo lilipata ripoti kwamba Lionel Messi na mke wake walipokea vitisho kutoka kwa wapalestine wakiwataka kuahirisha mchezo huo mara moja.

Katibu mkuu wa chama cha soka cha Palestina Jibril Rajoub aliuomba uongozi wa chama soka cha argentine kufuta mchezo huo mara moja

Baadhi ya mashabiki wa Messi nchini Palestina walichoma jezi za nyota huyo mara baada ya kikosi hicho kuwasili Jerusalem kwa muda.

Rajoub amesema anafahamu wazi kuwa mchezo huo ulikuwa ni wa kusheherekea Miaka 70 ya shirikissho la soka nchini humo.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliwasiliana na Rasi wa Argentine Mh Mauricio Macri. Netanyahu alimsihi Sana Macri kuwahimiza uongozi na wachezaji kutokufutilia mbali mchezo huo siku ya jumanne. Macri alimjibu waziri huyo kuwa yeye hawezi kuingilia maamuzi ya mwisho ya chama cha soka cha taifa hilo.

Raisi Macri aliwasiliana na uongozi wa chama cha soka kujua msimamo wao. Viongozi walimwambia kuwa kila mchezaji ana hofu na hakuna mchezaji ambaye yupo tayati kucheza pambano hilo. Macri alimpigia simu waziri wa Israel na kumuomba radhi kwamba hakuna mchezaji ambaye atakubali kucheza pambano hilo.

Macri mwenyewe alikuwa tayari kwenda katika mpambano baada ya kualikwa na matajiri wa kiyahudi wanaofanya kazi.

Mchezaji wao Gonzalo ” Nashukuru kwa maamuzi hayo Kwa ajili afya zetu na maisha yetu. Hakukua na haja ya kucheza na wayahudi.

Hata hivyo Uongozi wa chama cha soka cha Israel kimishtumu sana maamuzi ya Rajoub na kusema amevunja mipaka.

Waziri wa Ulinzi wa israel Avigdor Lieberman amelaani kitendo hicho na kudai kuwa Wapalestina wamejaa chuki na wivu.

Msemaji wa wizara ya ulinzi Gilad Erdan alionhelea suala hilo na kusema kwamba

wamekuza jambo hilo kwa makusudi ili kumtisha Messi. Amesema kitendo cha kuchoma jezi za nyota huyo ni mipango ya taifa hilo kutaka kuondoa amani.

Mchezaji kulipwa 150,000 kila mechi Ndondo Cup

$
0
0

Mabibo Market kupitia kwa kiongozi wake imeweka wazi kiasi ambacho atalipwa kila mchezaji kwa kila mechi atakayocheza kwenye mashindano ya Ndondo Cup msimu huu.

Naomi Kibago ambaye ni mweka hazina wa Mabibo Market amesema, msimu huu wa Ndondo Cup wamejipanga kulipa ‘kilo na nusu’ kila mchezaji kwa mechi moja.

“Mapato yanaendelea vizuri kama unavyojua hapa sokoni wafanyabiashara wapo wengi hawasumbui kwenye michango kwa hiyo hela ipo.”

“Kila mchezaji atakaechezea Mabibo Market msimu huu tutamlipa Tsh. 150,000 kwa kila mechi na inaweza kupanda zaidi ya hapo.”

Babu wa Keko kaanza mipango kuwania tuzo Ndondo Cup 2018

$
0
0

Shabiki wa Keko Furniture Abdul Pius maarufu kama Babu wa Keko ameshaanza maandalizi mapemaaa kuhakikisha anakamata tuzo ya shabiki bora wa Ndondo Cup msimu huu.

Babu wa Keko anakwambia tayari ameshaanza mazoezi kabla hata hatua ya makundi (32 bora) haijaanza kisa tu anataka kulamba tuzo ambayo amekuwa akiikosa kwa misimu kadhaa.

“Mwaka huu kitu cha kwanza nilichojifunza ni kwamba, huwezi kufanya jambo lolote ukafanikiwa bila kufanya mazoezi kwa hiyo mimi na crew yangu tunafanya mazoezi.”

“Ndondo Cup imenisaidia sasa hivi nimekuwa msanii na kuna vitu vyangu vingi navifanya kwa hiyo watu wasubiri. Nimeshafanya kazi kuhusu Ndondo ya msimu huu nimeelezea kisanii maana ya #Wastuewana.”

“Mwaka huuzawadi ya shabiki borabwa Ndondo Cup inanihusu.”

Keko Furniture ipo Kundi A pamoja na Boom FC, Makongo Sec na Mabibo Market. Game ya ufunguzi itaikutanisha Keko Ferniture dhidi ya Mabibo Market siku ya Ijumaa Juni 8, 2018.

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>