Zikiwa zimebaki siku 7 ligi kuu ya England, kutimbua vumbi ligi kuu ya England, ndo ligi ambayo imeongeza kutumia pesa za usajili mpaka sasa imetumia kiasi cha Euro billion 1 huku klabu ya Liverpool, ndo ikiongoza kutumia pesa nyingi katika usajili.
Liverpool, wametumia kiasi cha paundi million 195 kwenye usajili huku wakiweka rekodi ya kumchukua goli kipa wa klabu ya As Roma, Allison Becker, kwa kitita cha paundi million 75 na wamemsajili kiungo kutoka klabu ya Leizpg, Naby Keita, kwa kitita cha paundi million 60 huwo ndo ukiwa usajili ghali zaidi wa Liverpool.
![]()
Nafasi ya pili inashilikiwa na ligi kuu ya Itali, wametumia kiasi cha Euro million 927 kufanya usajili huku mchezaji ghali akiwa Cristiano Ronaldo, akitokea klabu ya Real Madrid, kwa uhamisho wa paundi million 100.
Nafasi ya tatu inashikiliwa na Ligi kuu ya Hispania, imetumia kiasi cha Euro million 643. Nafasi ya nne ikishika ligi kuu ya Ujerumani, ikiwa imetumia pesa kiasi cha Euro million 415.
Nafasi ya tano ikishika ligi kuu ya Ufaransa, ikiwa imetumia kiasi cha Euro million 376.
Kocha wa klabu ya Manchester City, amesema kuwa anahitaji kusajili mchezaji moja kabla ya dirisha la usajili halijafungwa. Guardiola, ambaye hivi karibuni alikuwa akimuhitaji kiungo wa klabu ya Napoli, Jorginho, ambaye amesajiliwa na klabu ya Chelsea, hivi karibuni. Guardiola, amesema kuwa anahitaji kiungo moja mwengine katika eneo la kiungo.
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Africa Lyon, Mbeya city, Tiko Okello,amerejea nyumbani Uganda, na kusaini mkataba na klabu ya Vipers Fc, akitokea klabu ya Benefica, De Macau.
![]()
Kiungo wa klabu ya Bayern Munich, Arturo Vidal, amefikia makubaliano na klabu ya Barcelona, na atafanyiwa vipimo na kusaini mkataba wa miaka mitatu utakaomfanya abaki klabuni hapo mpaka mwaka 2021.
Arturo, atukuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na klabu ya Barcelona, tayari wameshawasajili Arthur, Malcom, Lenglet.
Mchezaji wa Zamani wa West ham, Lionel Scalion ameteuliwa kuwa kocha wa muda wa timu ya taifa ya Argentina, baada ya aliyekuwa kocha wa Argentina Jorge Sampaoli kuondoka.
![]()
Beki wa klabu ya Arsenal, Sead Kolasnic, anatarajiwa kuwa nje ya uwanjani kwa muda usiopungua wiki 8 mpaka 10 baada ya kupata majeraha ya goti katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Chelsea. Kolasnic, alitolewa nje dakika ya 70 baada ya kupata maumivu ya goti .
![]()
Taarifa zote na Aziz Mtambo
Lampard azidi kutisha klabu yake ya Derby Country imeitwanga Reeding
![]()