Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

PICHA: SEKTA YA MICHEZO YAJIVUNIA KUPATA WASOMI WA ELIMU YA JUU

$
0
0
Mwandi wa habari za michezo kutoka kampuni ya The Guardian Limited Lasteck Alfred (kushoto) pamoja na golikipa wa Toto Africans Erick Ngwegwe kwenye mahafali ya kumaliza masters degree zao kwenye chuo kikuu cha St. Augustine, Mwanza
Mwandi wa habari za michezo kutoka kampuni ya The Guardian Limited Lasteck Alfred (kushoto) pamoja na golikipa wa Toto Africans Erick Ngwegwe kwenye mahafali ya kumaliza masters degree zao kwenye chuo kikuu cha St. Augustine, Mwanza

Nahodha na golikipa namba moja wa kikosi cha Toto Africans Erick Ngwegwe ame-graduate masters degree Jumamosi iliyopita siku ambayo kikosi cha Toto kilichezea kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Tanzania Prisons kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Ngwegwe na Lasteck wakiwa kwenye picha ya pamoja na ndugu, jamaa na marafiki
Ngwegwe na Lasteck wakiwa kwenye picha ya pamoja na ndugu, jamaa na marafiki

Ngwegwe amehitimu masters ya History kwenye Chuo Kikuu cha St. Augustine cha jijini Mwanza na huenda golikipa huyo ndiye mchezaji mwenye elimu ya juu kuzidi wachezaji wengine wanaocheza soka kwenye ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kwa sasa.

Golikipa wa Toto Africans Erick Ngwegwe pamoja na makocha wake
Golikipa wa Toto Africans Erick Ngwegwe pamoja na makocha wake

Golikipa huyo alipata degree yake ya kwanza ya Education lakini akaona bado anahitaji kusonga mbele kwenye elimu ya darasani na kuamua kupiga book zaidi na hatimaye amemaliza mastars yake ya History.

Golikipa wa Toto Africans ya Mwanza Erick Ngwegwe (kulia) pamoja na mwandishi wa habari za michezo Lasteck Alfred kutoka kapuni ya The Guardian Limited wakiwa kwenye picha ya pamoja siku ya mahafali yao
Golikipa wa Toto Africans ya Mwanza Erick Ngwegwe (kulia) pamoja na mwandishi wa habari za michezo Lasteck Alfred kutoka kapuni ya The Guardian Limited wakiwa kwenye picha ya pamoja siku ya mahafali yao

Mbali na golikipa huyo kuhitimu masters degree, mwandishi wa habari za michezo Lasteck Alfred kutoka kampuni ya The Guardian Limited wachapishaji wa magazeti ya The Guardian, Nipashe na Lete Raha pia alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliohitimu masters siku hiyo.

IMG-20160117-WA0022

Lasteck amehitimu masters degree ya Mass Communications pamoja na Erick Ngwegwe kwenye mahafali ya Chuo Kikuu cha St. Augustine Mwanza yaliyofanyika January 16, 2016.

Ngwewe akiwa kwenye majukumu yake, hapa ameweka vitabu pembeni analinda goli lake
Ngwewe akiwa kwenye majukumu yake, hapa ameweka vitabu pembeni analinda goli lake
Erick Ngwegwe akiwa kikazi zaidi anapokuwa anaitumikia klabu yake ya Toto Africans
Erick Ngwegwe akiwa kikazi zaidi anapokuwa anaitumikia klabu yake ya Toto Africans

Mtandao huu (shaffihdauda.co.tz) kwa niaba ya wafanyakazi wote unwapongeza Erick Ngwegwe na Lasteck Alfred kwa hatua kubwa waliyopiga katika elimu. Tunaamini elimu waliyoipata itakuwa na tija katika sekta ya michezo Tanzania na wao watakuwa mfano wa kuigwa kwa wanamichezo wengine ambao wako shuleni au wanaotaka kurudi shule kujiendeleza.

Kwa pamoja tunasema Hongereni sana!!


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles