Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

HII NDIYO VIDEO AMBAYO OLUNGA ALIMTUMIA ARSENE WENGER AKIMUOMBA AMSAJILI

$
0
0

Michael Olunga

Amini usiamini kuna watu wanajiongeza kwenye huu ulimwengu hasa pale wanapotafuta namna ya kutimiza malengo na ndoto zao katika maisha.

Michael Olunga alirekodi video akimwomba kocha wa Arsenal mzee Arsene Wenger amsajili kwenye kikosi cha The Gunners huku akimuahidi hatomuangusha na atakuwa ametimiza ndoto zake za kutaka kuitumikia klabu hiyo ya London.

Olunga ambaye alikuwa ni striker wa Gor Mahia inayocheza ligi ya Kenya (Kenyan Premier League) pia anasema ameshafunga magoli 38 katika msimu huu.

Michael Olunga katikati akiwa kwenye majaribio kwenye klabu ya Djurgardens IF, Sweden
Michael Olunga katikati akiwa kwenye majaribio kwenye klabu ya Djurgardens IF, Sweden

Mchezaji huyo bora wa Kenya kwa sasa amejiunga na klabu yabaada ya kuonesha kiwango kizuri wakati wa majaribio aliyofanya kwa kipindi cha mwezi mmoja. Mkenya huyo amepewa mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu hiyo ya Sweden.

Olunga alikaa kwa msimu mmoja tu kwenye klabu ya Gor Mahia akitokea Thika United pia alikuwa mchango mkubwa kwa Gor Mahia kutwaa ubingwa wa KPL kwa mara ya15 bila kupoteza mchezo hata mmoja.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>