Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

BAADA YA USHINDI KWENYE MECHI YA UEFA, MOURINHO ATEMA CHECHE HIZI…

$
0
0

SPT_GCK_160915_Football Champions league Group G Stamford Bridge, London.Chelsea v Maccabi Tel Aviv FC. Picture Graham Chadwick. Jose Mourinho

Baada ya jana usiku kuwafunga Maccabi Tel Aviv, goli 4-0 katika michuano ya klabu bingwa Ulaya, kocha wa Chelsea Jose Mourinho ametamba kwamba yeye ni moja kati ya makocha bora zaidi ulimwenguni.

Mourinho anasema kwenye maisha kuna kupanda na kushuka. Anasema siku zote yeye ni kocha mzuri bila matokeo na pia ni mzuri tu hata akipata matokeo.

Akifananisha suala lake na yaliyomkuta Wayne Rooney majuma kadhaa yaliyopita, Mourinho anasema, “mlimuona Rooney kaisha, siku chache baadae baada ya kuweka rekodi ya mabao na timu ya taifa, mnamuona kuwa ni moja kati ya wachezaji bora katika soka la kiingereza”.

Kocha huyo anasema hafikilii kama kupata ama kukosa matokeo kuna ondoa ubora wake kama kocha ama kunaondoa ubora wa Wayne Rooney, bali kama binadamu kuna kupanda na kushuka.

Mourinho amekua katika wakati mgumu tangu kuanza kwa ligi kuu nchini England msimu huu kutokana na kuanza vibaya katika michezo mitano ya awali ambapo hadi sasa wameambulia points 4 pekee. Weekend hii watarudi tena dimbani kumenyana na Arsenal katika uwanja wa Stamford Bridge.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>