Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

AZAM YAENDELEA KUIANDALIA DOZI NYINGINE BIDVEST

$
0
0
Kiungo wa Azam FC Michael Balou akimtoka kiungo mwenzake Mudathir Yahya huku Sure Boy akishuhudia wakati wa mazoezi leo asubuhi
Kiungo wa Azam FC Michael Balou akimtoka kiungo mwenzake Mudathir Yahya huku Sure Boy akishuhudia wakati wa mazoezi leo asubuhi

Azam FC leo asubuhi imeendelea na maandalizi ya kuikabili Bidvest Wits ya Afrika Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Jumapili kwenye uwanja wa Azam Complex kuanzia saa 9:00 alasiri.

Kiungo wa Azam FC Himid Mao akiuwahi mpira dhidi ya mshambuliaji wa timu hiyo Didier Kavumbagu
Kiungo wa Azam FC Himid Mao akiuwahi mpira dhidi ya mshambuliaji wa timu hiyo Didier Kavumbagu

Azam FC ilipata ushindi wa mabao 3-0 kwenye mchezo wa kwanza uliofanyika uwanja wa Bidvest jijini Johannesburg Afrika Kusini, inahitaji ushindi wowote au sare ya aia yoyote ili kuweza kusonga mbele kwa raundi ya pili ya michuano hiyo.

Magolikipa wa Azam FC wakisikiliza maelekezo kutoka kwa kocha wao
Magolikipa wa Azam FC wakisikiliza maelekezo kutoka kwa kocha wao

Endapo Azam wakiingia raundi pili, watakutana na timu kati ya Esperance ya Tunisia au Renaissance ya Chad, ambayo imefungwa mabao 2-0 na waarabu hao kwenye mechi ya kwanza wakiwa nyumbani jijini N’Djamena.

Vijana wa Stewart Hall wakimsikiliza kwa makini maelekezo ya kocha mkuu wa timu hiyo
Vijana wa Stewart Hall wakimsikiliza kwa makini kocha mkuu wa timu hiyo

Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>