Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

AJIB NDO BASI TENA VPL 2015-16

$
0
0
Mwamuzi Anthony Kayombo aliyechezesha mchezo kati ya Simba dhidi ya Mwadui FC akiuonesha kadi nyekundu Ibrahim Ajib
Mwamuzi Anthony Kayombo aliyechezesha mchezo kati ya Simba dhidi ya Mwadui FC akiuonesha kadi nyekundu Ibrahim Ajib

Kadi nyekundu aliyooneshwa mshambuliaji wa Simba Ibrahim Ajib inamfanya kukosa mechi zote (mbili) za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu huu pamoja na mchezo wa kwanza wa ligi ya msimu ujao.

Ajib-red card 2

Ajib alioneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja ‘straight red card’ baada ya kumchezea vibaya Hassan Kabunda wa Mwadui FC zikiwa zimesalia dakika chache pambano hilo kumalizika.

Ibrahim Ajib akielekea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo mara baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Hassan Kabunda
Ibrahim Ajib akielekea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo mara baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Hassan Kabunda

Kwa mujibu wa sheria na kanuni za mchezo wa soka, mchezaji anayeoneshwa  ‘straight red card’, analazimika kutumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu mfululizo.

Ajibu atakosa mechi mbili za mwisho ambazo Simba imebakiza kabla ya kufika tamati ya ligi baadaye mwezi huu, pamoja na mchezo wa kwanza wa ligi msimu ujao. Mechi ambazo Ajib atazikosa ni ule wa Majimaji vs Simba (11-05-2016) na mchezo wa mwisho wa kumaliza ligi ambapo Simba itakuwa ugenini kucheza na Mtibwa Sugar (15-05-2016).

Ajib-red card 4

Kwa maana hiyo, Ibrahim Ajib tayari amemaliza msimu wa ligi wa 2015-16.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9000

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>