Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Mtanzania aliyetangaza fainali ya UEFA 2006 huku analia kwa sababu ya Arsenal

$
0
0

Mtangazaji mkongwe wa soka nchini Juma Nkamia mezitaja mechi tatu ambazo anazikumbuka zaidi katika kipindi chake chote alichokuwa akitangaza soka.

Kubwa kuliko zote ni mechi ya fainali ya michuano ya vilabu bingwa Ulaya mwaka 2006 kati ya Arsenal dhidi ya Barcelona ambapo alitangaza mchezo huo huku akitokwa na machozi baada ya kushuhudia timu anayoipenda (Arsenal) ikiwa nyuma kwa mabao 2-1 huku wachezaji wakiwa pungufu uwanjani kufuatia golikipa Jens Lehmann kuoneshwa kadi nyekundu.

“Mechi ambayo naikumbuka sana ilikuwa kati ya Arsenal na Barcelona iliyochezwa Stade de France Paris (fainali ya vilabu bingwa Ulaya 2006) mechi ambayo Arsenal walifungwa 2-1, nakumbuka goli la pili lilifungwa na Samuel Eto’o Fils.”

“Ni mechi ambayo Jens Lehmann alioneshwa kadi nyekundu, mimi ni shabiki wa Arsenal kwa hiyo mechi hiyo naikumbuka nilikuwa tangaza hadi machozi yananitoka, ni mambo ambayo nayakumbuka sana.”

Mchezo mwingine ambao bado upo kwenye kumbukumbu za Nkamia ni ule wa AFC Leopard vs Simba katika mashindano ya vilabu bingwa Afrika uliochezwa jijini Nairobi Kenya.

“Nakumbuka mchezo kati ya Simba dhidi ya AFC Leopards ilikuwa ni michuano ya East & Central Afrika pale Nairobi, ilikuwa ni mwezi wa Ramadhani (mwezi mtukufu0 nilikuwa natangaza mechi mbili kwa siku kwa sababu nilikuwa pekeangu.”

Mechi nyingine ambayo Nkamia anaikumbuka sana ni kati ya Express ya Uganda vs Yanga kwa sababu aliingiza mkwanja bila kutegemea kutoka kwa mtangazaji mwenzake.

“Nakumbuka nilikutana na mtangazaji mmoja wa Kenya anaitwa Leonard Mambo Mbotela alikuja akanikuta naandika majina ya wachezaji (lineups) akaniuliza, mtangazaji yupo wapi? kwa sababu nilikuwa bado kijana mdogo sana nikamwambia yupo chini anachukua majina ya wachezaji.”

“Badae akaja akanikuta natangaza hakuamini kama ni mimi akanipa shilingi 20,000 ya Kenya. hiyo mechi naikumbuka sana na Simba ilifungwa 2-1.”

“Naikumbuka mechi kati ya Yanga na Express, mechi ambayo ilichezwa uwanja wa Nakivubo pale Kampala ilimalizika kwa sare ilikuwa michuano ya kombe la klabu bingwa Afrika.”

Kama ulikuwa hujui basi chukua hii, Juma Nkamia ndio mtangazaji wa kwanza kutangaza ligi ya England (EPL) na ligi ya Ulaya (UEFA Champions League) kwa kiswahili pale BBC.

Kwa sasa Nkamia anajihusisha na mambo ya siasa akiwa ni mbunge wa jimbo la Chemba (CCM), hajasikika kwa muda mrefu katika fani yake ya utangazaji soka.


Alvaro Morata akaribia kuifikia rekodi ya Jose Mourinho

$
0
0

Hadi hivi sasa Jose Mourinho ndio kocha ambaye ana mafanikio katika ligi tatu kubwa barani Ulaya. Ligi za Serie A, La Liga na Epl ambazo Mourinho alifundisha alifanikiwa kubeba makombe.

Lakini hivi sasa mshambuliaji wa Chelsea na timu ya taifa ya Hispania Alvaro Morata anaonekana kutaka kufanya kile ambacho kocha Jose Mourinho ameshakifanya katika ligi alizozipitia.

Tayari Alvaro Morata ameshabeba ubingwa wa Serie A akiwa na Juventus na msimu uliopita alikuwepo katika kikosi cha Realadrid kilichotwaa ubingea wa michuano ya Champions League na La Liga.

Kwa sasa Alvaro Morata yuko Chelsea ambako nako kama akipata ubingwa wa Uingereza baasi atafikia rekodi ya Mourinho ya kubeba mataji katika ligi kuu tatu kubwa barani Ulaya.

Alvaro Morata mwenyewe amekiri kufurahia kuwa Chelsea na kusema kwamba hajutii uhamisho huo kwani unamfundisha kitu kipya huku pia akiwa na malengo ya kufanya alichofanya Hispania na Italia.

Morata sio mchezaji wa kwanza kucheza Serie A, La Liga na Epl kwani wapo wakina Pepe Reina, Fernando Torres, Gaizka Mandite na Michu lakini kati yao hakuna aliyefanikiwa kuchukua kombe kwenye nchi zote tatu.

Alvaro Morata alikuwa shujaa wiki iliyopita akifunga bao pekee lililoiua Manchester United na kuwafanya Chelsea kupunguza pengo la alama kati yao na Manchester United hadi kufikia tofauti ya alama moja.

Kwanini itakuwa Guardiola na Man City kumaliza msimu bila kufungwa

$
0
0

Hawazuiliki, hawashindiki, hawafungiki – hivi ndivyo wanavyoelezewa Manchester City msimu huu.

City wameanza msimu na moto wa gesi, wakiweka rekodi za kila aina. Wamekuwa timu ya pili kuanza ligi kwa mafanikio haya katika historia tangu Spurs walipoanza kwa kushinda mechi 11 msimu wa 1960-61. Kwa mwendo kama Utaendelea hivi mpaka mwishoni mwa msimu basi huenda wakamaliza na pointi 107 na magoli 133. Kiwango chap kimeleta maswali kama kuna timu yoyote itakayoweza kuwasimamisha ndani ya dakika 90 au ndani ya mechi 38.

“Kama wataendelea kupata upendeleo wa maamuzi katika uwanja wa nyumbani namna hii, basi hakuna atakayeweza kuwazuia,” alisema Arsene Wenger, akizungumza kwa hasira kuhusu goli la penati na lile alilofunga Jesus katika kipigo cha 3-1 Jumapili iliyopita.

Hata hivyo historia inatumbia kwamba kuna mahala City watakwama wakati msimu ukiendelea, sio tu kwasababu bado hawajakutanana wapinzani wao wakubwa kwenye mbio za ubingwa: Tottenham Hotspur na Manchester United lakini pia kadri msimu unavyoenda ipo siku watasimamishwa.

Kuna sababu maalum kwanini naamini watasimamishwa: Tayari wanamchezesha kiungo kwenye safu ya ulinzi wa kushoto kwasababu Benjamin Mendy amepata majeraha yatakayomuweka nje kwa muda mrefu, Fabian Delph anafanya kazi nzuri, lakini itatokea wakati wapinzani watautumia udhaifu wake.

Ikitokea akapata majeruhi kutokana na historia yake ya kuumia mara kwa mara basi Pep itabidi atafute mbadala wa 3.

Upande wa ulinzi wa kati – wana uimara wa kutosha? Huku Vincent Kompany akiwa nje kwa majeruhi, Nicolas Otamendi akiwa kifungobi katika mchezo ujao vs Leicester, Eliaquim Mangala anategemewa kuchukua nafasi. Endapo City watapata majeruhi mmoja katika safu ya kati ya ulinzi, mfaransa huyu ambaye alicheza hovyo vs Wolves katika Carabao Cup, ataanza kupewa nafasi mara nyingi zaidi kikosini. Hata Otamendi ambaye msimu huu ameimarika, bado ana makosa mengi. Alinyanyaswa mno na Mohamed Salah kwa dakika 45 mnamo September. Golini, endapo Ederson ataumia itabidi wamrudishe Bravo.

City wana uimara zaidi katika nafasi 6 za mbele ya uwanja, lakini hakuna mbadala sahihi wa Fernandinho katika kikosi chao. Hakuna anayeweza kuziba vizuri pengo la Kevin de Bruyne na mchango anaoutoa kwenye timu. Yoyote kati yao akipata majeruhi City watakuwa na udhaifu mkubwa katikati katika kuucheza mchezo ambao wameuzoea na unaowapa sifa kubwa katika dunia ya soka. Wakati City walipocheza na Wolves, De Bruyne na Fernandinho hawakuanza na City wakapoteza unyumbulifu wao na hawakucheza mchezo wao na matokeo yake mchezo ukaenda mpaka dakika ya 120.

Halafu kuna sababu za ujumla kwanini timu yoyote inaweza kupata taabu kupata matokeo: wanaweza kucheza dhidi ya wapinzani ambao golikipa wao anaweza kuwa kwenye kiwango cha aina yake, na pia wakati mwingine maamuzi ya refa au timu pinzani ikawa na bahati zaidi yao.

Na ndio maana ni ngumu sana kwa City kumaliza msimu bila kupoteza. “Ipo timu itakuja kutufunga,” Guardiola alisema Ijumaa iliyopita. Ukweli wa kwamba kikosi cha Wenger cha msimu wa 2003-04 ndio kikosi cha mwisho kumaliza ligi bila kupoteza inaonyesha wazi namna jambo hilo lilivyo gumu. Hii suala halikutakiwa kuanza kuongelewa kabla hata January.

Spurs walianza ligi kupoteza kwa muda mrefu msimu uliopita, Chelsea pia msimu wa 2014-15, City wenyewe pia msimu wa 2012-13 na Liverpool 2007-08. Ni timu moja kati ya hizo ndio ilienda kutwaa ubingwa. Kuna timu ambazo zilianza ligi bila kupoteza kwa muda mrefu huko nyuma na baadae wakaenda kuchukua ubingwa lakini hawakufanikiwa hata kusogelea kumaliza ligi bila kufungwa:

Manchester United hawakupoteza mechi 24 za mwanzo wa ligi msimu wa 2010-11, Liverpool katika mechi 29 za mwanzo 1987-88 au Leeds katika mechi 29 msimu wa 1973-74, wote wakaishia kufungwa mara 4 mpaka kufikia mwishoni mwa misimu hiyo.

Mpaka sasa City wapo mbele kwa pointi 8. Guardiola akasema bado kuna pointi 84 za kushindania, sasa zimepungua mpaka 81 baada ya ushindi wikiendi iliyopita. Lakini miaka 8 iliyopita, kikosi cha United ambacho kilishinda makombe ya ligi 4 katika misimu 5 ya nyuma, kilikuwa mbele kwa pointi 8 mbele huku mechi 6 zikiwa zimebakia. City wakaenda wakabeba ndoo.

Ndio maana haishangazi Jose Mourinho alisema Jumapili iliyopita faida ya kuongoza kwa pointi 8 katika EPL sio sawa na ile ya ligi kama za Ureno, La Liga, au Bundesliga. “Sio pengo ambalo huenda likashindikana kulifikia hapa England. Real Madrid hawajawahi kutoka nyuma kwa pointi na kwenda kushinda ubingwa; United walishawahi kutoka nyuma kwa tofauti ya pointi 12 nyuma ya Newcastle msimu wa 1995/96 na wakachukua ubingwa”. Miaka 3 iliyopita, Chelsea ya Mourinho walikuwa mbele kwa pengo la pointi 8 mbele ya City ya Pellegrini, City wakalifuta pengo hilo na kuwafikia Chelsea kabla ya The Blues kufanikiwa kuwazidi mwishoni na kutwaa ubingwa.

Yote haya hayawezi kuondoa ukweli kuhusu ubora wa City, wamekuwa ndio timu bora, yenye kufunga magoli mengi na inayocheza soka la kuvutia zaidi. Lakini kufanikiwa mwanzoni mwa msimu ni mbali sana na suala kutokufungika hasa kwenye ligi ya England.

City wameshawahi kuanza hivi ligi msimu wa 2011-12, wakishinda mechi 10 katika mechi 11 za kwanza na wakifunga goli 1 zaidi ya idadi ya sasa, lakini walienda mpaka mwishoni mwa msimu wakiwa wameshapoteza mechi 5. Walitegemea goli la maajabu la dakika ya 94 ya mchezo wa mwisho kufanikiwa kuwa mabingwa kwa tofauti ya magoli.

Ozil na Sanchez ni nafsi za usaliti kwenye ndoa ya mkeka

$
0
0

Na Priva ABIUD

Hivi mmesikia alichosema Lee Dixon? Amesema angekuwa yeye ndiye bosi wa Arsenal angeshawatimua Alex Sanchez na Mesut Ozil. Dixon anadai kuwa Fuku fuku hili la Ozil na Sanchez liliwahi kuitokea Arsenal miaka ile 1988 wakiwa Na Mshambuliaji Michael Thomas aliyeifungia Arsenal goli la ushindi kwenye mechi ya fainali dhidi ya liverpool. Inasadikika baada ya goli lile Michael alishikwa tamaa ya maslahi na mwisho wa siku aliuzwa Liverpool.

Lee Dixon anaamini ni bora kuishi na wanajeshi wadhaifu kuliko  mashujaa wanafiki na wenye roho za usaliti kwa sababu ya tamaa. Ozil yupo mbioni kutimka Arsenal kwa taarifa za Maguel Delaney wa The Guardian. Michael Laurence wa whoscored.com amesema Ozil amekuwa akilaumiwa kila mara hasa timu inapokosa matokeo. Mashabiki wa Arsenal wanaamini Ozil kaficha Chenza anawapa machungwa tu. Kwangu Mimi naona mfumo mzima wa Ndoa yake na Arsenal umejengwa na harusi ya mkeka. Ozil akiwa na timu ya taifa kufikia mwaka 2013 alifunga magoli 17 katika michezo 47 akiwa na idadi sawa na ya Karim benzema aliyekuwa na magoli 17 kwenye michezo zaidi ya 50. Kwa sasa ana magoli 22 michezo 86 huku Benzema akiwa na magoli 26 mechi 81. Angalia namna Ozil alifanya vizuri akiwa na timu nzuri.

Mimi bado anamini Ozil na Sanchez wana umuhimu mkubwa, kwa sababu Arsenal haijawahi kushindwa mchezo wowote wa ligi ambao aidha Sanchez na Ozil hawajanza.

Kuna jambo huwa naliwaza sana. Hivi ni kweli Mesut Ozil alikubali kuondoka Madrid na Kwenda Arsenal? Alikosa nini? Kipi kilimsukuma kutoka timu kubwa aliyobeba nayo La liga na kutwaa kikombe cha Copa De la Rey? Je hata kama Madrid ilikuwa hamhitaji je aliona nini Arsenal? Utagundua hapa palikuwepo na ndoa ya mkeka.

Kwa Upande wa Sanchez, akiwa barcelona alianza Michezo 65 huku akitokea benchi michezo 23, lakini alipotua Arsenal alianza michezo 104 na kuanzia benchi mechi 7 tu. Unapata picha gani hapa? Utagundua kilichomlazimisha Sanchez kukimbia nyumbani na kwenda kwenye Maisha ya ndoa ya Arsenal ni hakupata nafasi ya kutosha Barca. Barca waligundua kuwa walikuwa wakitumia kiwango cha Sanchez vibaya. Hivyo ilibidi tu wapate hela kuliko kumweka benchi. 

Ingekuwa uamuzi wa ajabu sana kama Sanchez angekataa kuja timu ambayo ingemfanya kuwa mfalme wao. Cha ajabu Sanchez amejikuta dhahabu jalalani. Hakuna ambaye amegundua kama kwenye jalala la Arsenal ipo lulu ndani yake. Jitihada zake zote zinaishia kupata kipigo cha nguruwe kuzaga zagaa nyumba ya shekh (Buyern 10 2 Arsenal).

Sanchez amegundua hii ni ndoa ya mkeka baada ya kuona kuwa kibosile wake wa zamani anamuhitaji kwa udi na uvumba (Pep Guardiola). Kwa huyu mwanaume wake wa sasa Ozil na mke mwenza Sanchez wanafanyishwa kazi kama Punda. Sanchez Anafanyishwa kazi zote ziwe chafu ana safi (amecheza mechi 104 na mechi 7 akitokea benchi). Hi inaonesha kuwa Sanchez hajioni kama mama mwenye nyumba bali anajikuta yeye ni beki tatu. Sura ya Sanchez inaongea kwa sauti kuliko hata mdomo wake. Sanchez sio mtu wa maneno sana hasa ukizingatia lugha n.k . Sanchez mara kadhaa ameonekana uso wake unakaribia kuchakaa kwa kuwa na huzuni ya vipigo vya ajabu ajabu kila mara licha ya jitihada zake. Kuna mechi dhidi ya Buyern Uzalendo ulimshinda ilibidi acheke, hata kama ni wewe ungefanyaje? Kumi kwa mbili?

Akiangalia Mashariki hamuoni shetani, Magharibi haoni malaika, kusini hamuon mwanadamu ila kaskazini  anaona giza.

Roho za Sanchez na Ozil zimeshaisaliti Arsenal lakini naamini ifikapo 2018 tutaona mashekh wa Man City wakienda kutoa talaka.

Tunahitaji kuona mabadiliko Challenge Cup 2017

$
0
0

Mashindano ya kombe la Chalenji yanatarajiwa kuendelea mwaka huu kuanzia November 25 hadi December 9, 2017 ambapo Tanzania imethibisha kushiriki mashindano hayo ambayo yalisimama kuchezwa kwa miaka miwili iliyopita.

Mashindano ya Chalenji yamepoteza mvuto na msisimko kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, kutofanyika kwa mashindano hayo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita mfululizo inaelezwa ni kutokana na chama mlezi (CECAFA) kutokuwa na pesa za kuendesha mashindanon hayo.

Michuano ya Chalenji kwa miaka ya hivi karibuni haijaonekana kupiga hatua kwenda mbele, kila kukicha iko palepale au wakati mwingine inaonekana kurudi nyuma. Michuano yote ya vilabu hata ile ya mataifa huwezi kutofautisha kwa ubora kutoka msimu mmoja hadi mwingine.

Wanaweka maslahi mbele kuliko mpira wenyewe na hilo linathibitika pale ambapo mashindano yalikuwa yanalazimishwa yafanyike Tanzania kwa kigezo kwamba mashabiki wanakwenda uwanjani kuangalia mechi huku Simba na Yanga zikiwekwa kwenye mashindano hata kama timu moja wapo haina sifa za kushiriki mashindano.

Inapotokea timu hizi zikashiriki (Simba na Yanga) hutengenezwa mazingira ya kuzikutanisha kwenye hatua ya nusu fainali au fainali kwa sababu wanaamini watapata pesa za viingilio kwa ajili ya kufidia gharama za uendeshaji. Kwa stahili hiyo mashindano yanapoteza mvuto na thamani .

Inabidi CECAFA watafute mbinu mbadala za kuywezesha mashindano kufanyika  kwa kutafuta wawekezaji, watafute mfumo mzuri pamoja na motivation kwa mfano msimu huu mashindano yatafanyikia Kenya, basi kuwe na utaratibu mzuri wa kuwasafirisha wachezaji na wapokelewe kwa muda, wafikie kwenye hotel nzuri, washindane kweli na timu inayostahili kupata matokeo ipate.

Ikienda hivyo ushindani utarudi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma enzi zile tunasikiliza kwenye radio kina Dominic Chilambo wanatutangazia, ushindani ulikuwepo wakati huo Zamoyoni, Majid Musisi, Jack Chamangwana wakiwa wanatesa kwenye soka la ukanda huu, mashindano yalikuwa yanamvuto.

Kina Musonye na wenzake wakikaa wakatengeneza mazingira ya timu kushindana kweli na kuweka pembeni siasa zilizozoeleka naamini kila kitu kitakuwa sawa kwa sababu lengo la mashindano haya ni zuri na ni miaongoni mwa mashindano ya muda mrefu lakini yamedumaa ukilinganisha na mashindano ya kanda nyingine za Afrika ambayo yamekuja baadae.

Goodnews: Upasuaji aliofanyiwa Samatta umemalizika salama

$
0
0

Ni taarifa njema kwa watanzania wote hususan wadau wa soka kwamba, nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta upasuaji wake wa goti umefanyika na kumalizika salama.

Samatta aliumia goti November 4, 2017 wakati akiitumikia klabu ya ya KRC Genk ya Ubelgiji na kushindwa kuendelea na mechi dhidi ya Lokeren mchezo ambao ulimalizika kwa suluhu.

Kupitia ukurasa wake rasmi wa wa instagram (samagoal77) ameandika ujumbe unaothibisha kwamba upasuaji umefanyika na kumalizika salama.

“Napenda kuwajulisha kuwa, upasuaji wangu umeenda vizuri. Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, timu ya madaktari pamoja na mashabiki wangu.”

“Nimepokea meseji nyingi sana kutoka sehemu tofauti duniani na napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru sana kwa meseji na Dua zenu.”

Baada ya kufanyiwa vipimo, madaktari walimwambia Samatta atakaa nje ya uwanja kwa takribani wiki sita kabla ya kuanza kucheza tena.

Mafundi wa soka waendelea kutundika daluga, sasa ni zamu ya Xavi

$
0
0

Mafundi wa soka wanazidi tu kutundika daluga, tayari tumeshuhudia mwaka huu wachezaji nyota akiwemo Pirlo, Ricardo Kaka na Xabi Alonso wakiachana na soka, sasa nyota wa zamani wa Barcelona naye anatundika daluga.

Ni Xavi Hernandez ambaye kwa sasa anacheza katika klabu ya Quatar ya Al Sadd. Xavi ametangaza rasmi ya kwamba baada ya msimu huu kuisha baasi atatundika daluga zake na kuamua kuanza kuangalia maisha mengine.

Xavi tangu ameanza kucheza soka ameshcheza jumla ya michezo 890 ambapo katika michezo hiyo amefanikiwa kufunga jumla ya mabao 103 huku akibeba makombe 8 ya ligi ya nchini Hispania La Liga.

Akiwa na Barcelona kiungo huyo amefanikiwa kushinda michuano ya Champions League mara 4, akashinda michuano ya Copa Del Rey mara 3 huku akiisaidia Hispania kubeba michuano ya Euro mara 1 na kombe la dunia mara 1.

Xavi amesema baada ya kuacha kucheza soka atakaa pembeni na kuanza kuwa kocha kwani mwakani anataraji kupata leseni yake ya ukocha huku akimshukuru mungu kwa kucheza soka kwa muda mrefu bila majeruhi makubwa.

Kocha Aliou Cisse awapa Senegal tiketi kuelekea Urusi 2018,mwaka 2002 aliwapeleka Japan akiwa kama mchezaji

$
0
0

Baada ya timu ya taifa ya Misri na Nigeria kutangulia kukata tiketi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia 2018, hii leo timu ya taifa ya Senegal nayo imekata tiketi kuelekea michuano hiyo.

Senegal wamekata tiketi hiyo baada ya kushinda mabao mawili kwa nunge dhidi ya timu ya taifa ya Afrika Kusini Bafana Bafana katika mchezo uliopigwa mjini Polokwane nchini Afrika Kusini jioni ya leo.

Alikuwa ni Diafra Sakho alieyanza kuwafungulia Senegal ukurasa wa mabao dakika ya 12 kabla ya Thamsanq Mkhize kujifunga dakika ya 36 na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa wageni kupata ushindi wa mabao mawili.

Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Sadio Mane alikuwa chachu ya ushindi wa leo wa Senegal kwani achilia mbali assist ya bao la kwanza pia alikuwa chanzo cha Afrika Kusini kujifunga katika mchezo huo.

Kocha wa timu ya taifa ya Senegal Aliou Cisse anaingia katika vitabu vya rekodi Senegal kwani mwaka 2002 aliipeleka Senegal kombe la dunia yaliyofanyika Korea/Japan kama mchezaji na mwaka huu anaipeleka tena akiwa kama kocha.

Sasa Afrika tayari kumeshapatikana wawakilishi watatu (Nigeria, Misri na Senegal) na sasa kunasubiriwa timu mbili ili kukamilisha idadi kamili ya wawakilishi 5 watakaotuwakilisha katika fainali za kombe la dunia.


Lukaku aondoa ukame wa mabao huku Italia wakiwa mashakani kuelekea Urusi 2018

$
0
0

Timu ya taifa ya Ubelgiji ilikuwa uwanjani usiku wa jana kukabiliana na timu ya taifa ya Mexico ambapo katika mchezo huo Romelu Lukaku alifunga mabao mawili kati ya matatu katika suluhu ya tatu tatu.

Eden Hazard alifunga lingine huku mabao ya Mexico yakipatikana kupitia kwa Andres Guardado aliyefunga kwa penati kabla ya Hirving Lozano kuongeza mengine mawili.

Ufaransa wenyewe walikuwa uwanjani na timu yao inayosadikiwa kuwa ni kizazi cha dhahabu na kuwafunga Wales 2 kwa nunge kupitia kwa Antoine Griezman na Olivier Guroud.

Timu ya taifa ya Ureno nao bila Cr7 walicheza na Saudi Arabia ambapo Ureno waliibuka kidedea kwa mabao 3 kwa nunge mabao ya Ureno yakifungwa na Fernandes, Guedes pamoja na lile la Mario.

Katika hatua ya mtoano kuelekea kombe la dunia timu ya taifa ya Sweden iliishtua Italia baada ya kuwafunga bao 1 kwa nunge na hivyo kuwaweka Italia mashakani kulekea kombe la dunia 2018.

Zimwi la majeruhi laendelea kuing’ang’ania Manchester United

$
0
0

Taarifa zinasema Paul Pogba na Marcos Rojo wako mbioni kurejea uwanjani na mwisho wa wiki hii wanaweza kuwepo uwanjani katika kikosi cha Manchester United.

Wakati mashabiki wa United wakifurahia kupona kwa wachezaji wao sasa kuna habari mpya kwamba Phil Jones anaweza kuwa nje ya uwanja baada ya kupata majeruhi.

Jones alikuwepo wakati timu ya taifa ya Uingereza ikikipiga mechi ya kirafiki dhidi ya Ujerumani hapo jana lakini alishindwa kumaliza mchezo huo baada ya kuumia.

Taarifa zinasema Jones hakuwa fiti kuelekea mchezo wa jana, na majeruhi aliyapata dakika ya 10 lakini kocha wa timu ya ya Uingereza aliendelea kumchezesha hadi dakika ya 24.

Phil Jones amekuwa na msimu mzuri na anaonekana kuanza kuaminiwa na kocha Jose Mourinho kwani amekuwa akimchezesha pamoja na Chriss Smalling kama mabeki wa kati siku za usoni.

Clouds, Shadaka, waibukia mashindano ya vyuo

$
0
0

Chama cha michezo cha vyuo vikuu Tanzania (Tanzania Universities Sports Asociation “TUSA”) kimeingia makubaliano na Shadaka Sports Management pamoja Clouds Media kwa ajili ya kuendesha mashindano yanayoandaliwa na chama hicho.

Mashindano ya TUSA mwaka huu yanatarajiwa kuanza December 14 hadi 20 mkoani Dodoma kwa kushirikisha vyuo wanachama pamoja vyuo vingine ambavyo vimealikwa.

Mwenyekiti wa TUSA Bw. Winston Mdegela

Mwenekiti wa TUSA Winston Mdegela amesema lengo la mashindano ya  vyuo vikuu ni kujenga afya za wanafunzi, kujenga nidhamu na utaifa likini ikiwa ni fursa kwa wachezaji kuonesha vipaji vyao na kutafuta soko.

Mashindano yanayoandaliwa na TUSA yanashirikisha michezo mbalimbali ikiwemo soka, netball, basketball, pooltable, karate, kukimbia na michezo mingine mingi.

“Tunawashukuru wenzetu wa Clouds na Shadaka Sports Management kwa kukubali kuungana nasi katika kuendesha mashundano ya mwaka huu. Tunaomba wadau wa michezo waje kuangalia na kuchukua wachezaji kutoka kwenye mashindano haya kuwapeleka kwenye timu zao”-Mdegela.

Kwa upande wa mwakilishi Shadaka Sports Management na Clouds Media, Issa Masoud amesema wameamua kuingia kwenye mashindano hayo ili kuendelea kuwapa fursa vijana ya kuonesha vipaji vyao.

Issa Masoud, Mwakilishi wa Clouds Media Group na Shadaka Sports Management

“Tunaendelea kuishi kauli mbiu yetu ‘tunakugungulia dunia kuwa unachotaka’ tumeingia kushirikiana na TUSA ili kuwafungulia dunia vijana wawe wanavyotaka”-Masoud.

“Ukiachana na kujenga afya, nidhamu na utaifa, michezo ni ajira inayoajiri vijana wengi. Tunataka vijana watoke kupitia sehemu rasmi sio kutoka vichochoroni. Marekani vijana wengi wanaocheza basketball wametoka vyuoni, tunataka ifike mahali wachezaji wetu watoke sehemu zinazotambulika.”

Mwenyekiti wa TUSA Winston Mdegela amewaomba wakuu wa vyuo kuwaruhusu wachezaji kushiriki mashindano hayo kwa sababu kuna faida nyingi watapata.

Wachezaji wanaocheza VPL hatarini kutemwa Zanzibar Heroes

$
0
0

Na Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Soka ya Zanzibar (Zanzibar Heroes), ambao wanacheza ligi kuu Tanzania bara huenda waachwa katika kikosi hicho kutokana na kutopewa ruhusa na vilabu vyao kujiunga na timu hiyo ya Taifa mpaka ligi kuu bara itakapokwenda mapumziko.

Kocha mkuu wa Zanzibar Heroes Hemed Suleiman ‘Morocco’ amesema kutokana na kutopewa ruhusa wachezaji hao huenda wakaachwa badala yake wakaitwa wachezaji wengine wanaocheza soka visiwani Zanzibar.

Morocco amesema ikifika Novemba 15 ikiwa bado wachezaji hao hawajawasili kambi ya Heroes watalazimika kuachana nao na kuongeza nguvu kwa vijana wanaocheza vilabu vya Zanzibar kwani hawawezi kuwaruhusu wachezaji hao kujiunga na kambi siku chache kabla ya kusafiri.

“Tumeshaanza mazoezi tangu juzi, lakini uhakika wa kuwapata wachezaji wanaocheza ligi ya bara ni ngumu, tumewasiliana na vilabu vyao lakini wametuambia wachezaji hawatowaruhusu kujiunga na sisi mpaka ligi isimame Novemba 19.”

“Sisi tunataka kuondoka Novemba 22, hawatopata mufa wa kukaa na wenzao kwa sababu huenda wakafika Zenj Novemba 20 au 21 sasa hapo bora tuwaache tuite wengine wanaocheza hapahapa Zanzibar.”

Wachezaji waliyoitwa awali katika kikosi cha Zanzibar Heroes ambao wanatoka ligi kuu Tanzania bara ni walinzi Abdallah Haji “Ninja” (Yanga), Adeyum Saleh ‘Machupa’ (Kagera Sugar), Haji Mwinyi Ngwali (Yanga), Abdulla Kheir ‘Sebo’ (Azam), Viungo Mudathir Yahya (Singida United), Mohd Issa ‘Banka’ (Mtibwa Sugar) na Suleiman Kassim ‘Seleembe’, (Majimaji) pamoja na washambuliaji Kassim Suleiman (Prisons), Matteo Anton (Yanga) na Seif Rashid Abdallah ‘Karihe’ (Lipuli).

Wakati huohuo Mlinzi kinda wa Zanzibar Heroes aliyeitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi hicho Ibrahim Abdallah wa Taifa ya Jang’ombe amepania kupigana kufa au kupona ili apate nafasi ya kwenda nchini Kenya katika Mashindano ya CECAFA Chalenji CUP yanayotarajiwa kufanyika Novemba 25 na kumalizika Disemba 9 mwaka huu.

Simba, Yanga, kurejea taifa

$
0
0

Leo November 11, 2017 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiambatana na kamati ya maandalizi ya fainali za Afrika (AFCON U17) amefanya ziara ya kutembelea uwanja wa taifa kukagua ukarabati unaoendelea katika eneo la kuchezea (pitch) na maeneo mengine.

Dkt. Mwakyembe ameishukuru kampuni ya SportPesa ambayo ndio imebeba jukumu la kukarabati uwanja huo.

“Nashukuru kuona nyasi za uwanjani zimeota vizuri na unapendeza, kikubwa nashukuru kwa vijana wetu sita ambao wamefundishwa namna ya kutunza viwanja”-Dkt. Mwakyembe.

Mkuu wa oparesheni SportPesa Luca Neghesti amethibitisha ukarabati wa uwanja utakamilika November 21 na utakabidhiwa November 24 mwaka huu ukiwa tayari kwa matumizi.

“Kazi ya kukarabati sehemu ya kuchezea imekamilika na nyasi zilizooteshwa zimeota vizuri na zimeshika hivyo upo tayari kutumika,” alisema Luca.

Vilabu vya Simba na Yanga ambavyo huutumia uwanja wa taifa kwa mechi zao za nyumbani huenda zikarejea kwenye uwanja huo kuanzia November 24 baada ya kukabidhiwa kwa serikali. Vilabu hivyo vililazimika kutumia uwanja wa Uhuru kwa mechi zao za nyumbani kupisha matengenezo yanayoendelea uwanja wa Taifa.

Julio kalazwa tena ligi daraja la kwanza

$
0
0

Dodoma FC imepoteza mechi yake ya pili mfululizo baada ya kufungwa 1-0 na Biashara Mara kwenye mchezo wa leo November 11, 2017 ligi daraja la kwanza Kundi C. Kikosi cha kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ kilipoteza mchezo uliopita dhidi ya Pamba ya Mwanza kabla ya kulazwa tena leo.

Matokeo hayo yanaibakisha Dodoma FC na pointi zake 18 ikiachia uongozi wa Kundi C kwa Alliance Schools ambvayo imefikisha pointi 19 baada ya ushindi wake wa leo mabao 4-1 dhidi ya Toto Africans.

Ushindi wa Biashara Mara unafufu matumaini yao ya kucheza ligi kuu Tanzania bara msimu ujao baada ya kufikisha pointi 17 na huku ikiendelea kubaki katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Kundi C pointi moja nyuma ya Dodoma FC yenye pointi 18 katika nafasi ya pili.

Matokeo yote ya mechi za ligi daraja la kwanza zilizochezwa leo November 11, 2017.

Kundi A

  • Mshikamano 3-0 African Lyon
  • Mgambo JKT 0-0 Friend Rangers

Kundi B

  • Mufindi United 0-2 Mbeya Kwanza
  • Polisi Tanzania 2-1 Mawenzi Market

Kundi C

  • Dodoma FC 0-1 Biashara Mara
  • Toto Africans 1-4 Alliance Schools
  • Transit Camp 2-1 Rhino Rangers

Misimamo ya makundi yote (A,B na C) ligi daraja la kwanza

Majina ya wanasoka 5 wanaowania tuzo ya mwanasoka bora Afrika(BBC) yawekwa hadharani

$
0
0

Jopo la wataalamu wa soka wakiongozwa na mkongwe wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Emmanuel Emunike wamekaa chini na kujadili majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika msimu huu.

1.Naby Keita. Amekuwa gumzo kubwa katika ligi ya Ujerumani Bundesliga kutokana na kiwango alichokionesha akiwa na Rb Leizpg na msimu huu alikuwepo katika kikosi cha Bundesliga. Keita pia anahusishwa na kujiunga na Liverpool.

2.Sadio Mane. Alikuwepo katika kikosi cha Epl cha waandishi wa habari za michezo, alichaguliwa mchezaji bora wa klabu ya Liverpool msimu uliopita huku pia hapo jana akiisaidia Senegal kufuzu kwa fainali za kombe la dunia.

3.Pierre Aubameyang. Msimu uliopita alifanya makubwa Ujerumani akifunga mabao 35 na kuweka rekodi kuwa mchezaji wa 4 kuwahi kufunga mabao 30 nchini Ujerumani huku akiwa Muafrika wa kwanza kufikisha mabao hayo katika Bundesliga.

4.Mo Salah. Ameiwezesha Misri kushiriki michuano ya kombe la dunia lakini msimu uliopita alikuwa na kiwango kizuri sana alipokuwa Fiorentina huku msimu huu akiwa amefunga mabao 7 katika ligi ya Epl.

5.Victor Moses. Kama ilivyo kwa Salah na Mane huyu naye tayari timu yake imefuzu kuelekea Urusi, Victor Moses tangu kocha Antonio Conte ajiunge na Chelsea amekuwa akimpa sana nafasi japokuwa msimu huu ameandamwa na majeraha yanayomuweka nje hadi sasa.


Miamba miwili ya kiarabu yakamilisha idadi ya wawakilishi wa Afrika kuelekea Urusi mwakani

$
0
0

Miamba miwili toka Afrika timu ya taifa ya Morocco na Tunisia imekata tiketi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia itakayofanyika nchini Urusi mwakani baada ya kupata alama katika michezo yao ya leo.

Tunisia walihitaji alama moja tu ili kwenda kushiriki michuano hiyo na wamefanikiwa kupata alama moja baada ya hii leo kulazimisha suluhu ya bila kufungana dhidi ya timu ya taifa ya Libya.

Suluhu ya leo ya Tunisia imewafanya kufikisha idadi ya alama 14, alama ambazo Dr Congo wameshindwa kuzifikia huku leo wakilazimishwa suluhu ya bao moja kwa moja dhidi ya timu ya taifa ya Guinea.

Morocco kwa upande wao wamekata tiketi kuelekea kombe la dunia baada ya kuwafunga Ivory Coast kwa jumla ya mabao 2 kwa nunge katika mchezo uliokua wakuamua nani wakwenda kombe la dunia kutoka Grouop C.

Alianza Nabir Dirar dakika ya 25 kuwapa wageni bao la kuongoza, wakati Ivory Coast wakijipanga kusawazisha dakika 5 baadae Medhi Benatia aliwapa wageni bao la pili lililowahakikishia tiketi kuelekea Urusi.

Kwa matokeo hayo sasa yanaifanya Afrika kukamilisha idadi ya washiriki 5 katika kombe la dunia ambao ni Misri, Nigeria, Senegal, Tunisia na Morocco.

Maskini Neymar, aangua kilio mbele ya waandishi wa habari

$
0
0

Baada ya Brazil kuibuka kidedea kwa ushindi wa bao 3 dhidi ya Japan kulikuwa na mkutano baada ya mechi kati ya waandishi wa habari na nahodha wa Brazil Neymar pamoja na kocha mkuu wa timu hiyo Tite.

Katika mkutano huo jambo lililovuta hisia na kusikitisha mashabiki wa Brazil na PSG ni kitendo cha Mbrazil Neymar Dos Santos kuangua kilio na kisha kuamua kuondoka katika chumba cha mkutano.

Neymar aliangua kilio wakati kocha wake Tite akimzungumzia na akimtetea kuhusu habari zinazoandikwa siku za usoni kwamba hana furaha na maisha ya PSG na uhusiano wake na kocha wa klabu hiyo sio mzuri.

Tite amesema anakerwa sana na habari anazozishiwa Neymar ikiwemo kuwa na mahusiano mabaya na yeye kwani hajawahi kugombana na Neymar, wakati Tite akiendelea kumtetea Neymar ndipo alianza kulia.

Neymar mwenyewe kabla ya Tite kuongea alisisitiza kwamba ana furaha kuwa katika klabu ya PSG na kusema kwamba hana tatizo na mchezaji yoyote katika klabu hiyo, na yuko vizuri tu na Edison Cavani.

Alisisitiza kwamba kitu pekee kinamsumbua kwa sasa na kuambiwa hayuko vizuri na Edison Cavanni na amewataka waandishi wa habari kuacha kutunga story na kuandika vitu wasivyovijua.

Neymar alisajiliwa na PSG akitokea Barcelona  kwa ada iliyovunja rekodi ya dunia ya £198m lakini tangu atue PSG amekuwa akitengeneza vichwa vingi vya habari na vingi vikiwa sio vizuri.

Maguri kakabidhiwa majukumu ya Samatta

$
0
0

Baada ya mshabuliaji Mbwana Samatta kukosekana kwenye kikosi Stars kitakachocheza mchezo wa kirafiki dhidi Benin, kocha mkuu wa timu hiyo Salum Mayanga amesema majukumu yote ya Samatta yatabebwa na mshambuliaji Elias Maguri.

“Kutokuwepo kwa captain (Samatta) kutokana na tatizo alilolipata la maumivu, nafasi yake atacheza Elias Maguri na baadhi ya maeneo ya Erasto Nyoni na Mzamiru Yassin tumeweza kuangalia kwa macho mawili nafasi zao na tumeziziba”.

“Kwa kifupi tutacheza vizuri mcherzo wetu dhidi ya Benin na matumaini ya kufanya vizuri yapo kwa sababu vijana wetu wapo kwenye ari na kuona tunaendelea kucheza vizuri na timu yetu kuimarika kiufundi.”

Wachezaji ambao hawapo kwenye kikosi cha Stars utokana na sababu mbalimbali ni Mbwana Samatta na Farid Mussa (wanauguza majeraha) Mzamiru Yassin na Erasto Nyoni (wanatumikia adhabu ya kadi nyekundu.)

Mechi 13 za Taifa Stars chini ya Salum Mayanga tangu March 2017

$
0
0

Leo November 12, 2017 kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinacheza ugenini dhidi ya Benin mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA, ni mchezo wa kwanza wa kirafiki kwa Stars chini ya Salum Mayanga kucheza nje ya Tanzania. Kabla ya hapo mechi zote za kirafiki zilikuwa zikichezwa uwanja wa nyumbani.

Stars inaingia kwenye mchezo huo chini ya Mayanga ikiwa imecheza mechi 13, imeshinda michezo 6, sare 6 huku ikiwa imepoteza mchezo mmoja tu. Katika mechi hizo Stars imefunga jumla ya magoli 15 na kuruhusu kufunga magoli 9 na kufanya wastani wa magoli kuwa 6.

Mechi 13 ambazo kocha Salum Mayanga ameiongoza Stars tangu alipokabidhiwa juku hilo kutoka kwa Charles Boniface Mkwasa

  • Tanzania 2-0 Botswana (mechi ya kirafiki ya kimataifa)
  • Tanzania 2-1 Burundi (mechi ya kirafiki ya kimataifa)
  • Tanzania 1-1 Lesotho (kufuzu AFCON)
  • Tanzania 2-0 Malawi (COSAFA)
  • Angola 0-0 Tanzania (COSAFA)
  • Tanzania 1-1 Mauritius (COSAFA)
  • Afrika Kusini 0-1 Tanzania (COSAFA)
  • Zambia 4-2 Tanzania (COSAFA)
  • Tanzania 0-0 Lesotho (Stars ilishinda kwa penati 4-2 COSAFA)
  • Tanzania 1-1 Rwanda (kufuzu CHAN)
  • Rwanda 0-0 Tanzania (kufuzu CHAN)
  • Tanzania 2-0 Botswana (mechi ya kirafiki ya kimataifa)
  • Tanzania 1-1 Malawi

Mrembo ajitokeza na kusema alitembea na Cr7 wakati mpenzi wake ni mjamzito

$
0
0

Cristiano Ronaldo anasifika kwa kiwango chake uwanjani na ufungaji wake wa mabao lakini nje ya uwanja pia Mreno huyo ana sifa nyingine kubwa ambayo ni kutembea na warembo kila kukicha.

Wakati dunia ikisubiria mtoto wa Cr7 wa nne ambaye aatakuwa mtoto wake wa kwanza kuzaliwa na mama anayefahamika(Georgina Rodriguez), kumeibuka mrembo mwingine na kudai alilala na Cristiano Ronaldo.

Natacha ni mrembo ambaye ni mtangazaji wa runinga amejitokeza na kuongea na jarida moja la michezo kwamba Ronaldo alitembea naye na baada ya muda aliamua kumblock na kumpotezea.

Natacha amedai kwamba yeye na Cr7 walikuwa marafiki sana na muda mwingi waliutumia kuwasiliana na ndipo usiku mmoja walilala pamoja kisha binti huyo alimuambia Ronaldo mpango wake kwenda nchini Ureno.

Binti huyo anasema Cristiano hakupenda yeye aende Ureno na siku hiyo hiyo baada ya kulala naye ndipo Ronaldo akamblock na sasa Natacha anaamini kwamba Ronaldo alimuhitaji tu ili kumtumia.

Pamoja na kupotezewa na Cristiano Ronaldo lakini mlimbwende huyo amesisitiza kwamba hajutii kitendo alichofanyiwa na mwansoka huyo bora wa dunia bali anaona ndoto zake zimekuwa kweli.

Ronaldo alionekana kutulia sana kimapenzi tangu aanze uhusiano na Georgina lakini habari hizi huenda zikaanza kuchafua hali ya hewa katika uhusiano wa wapenzi hao.

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>