Quantcast
Channel: ShaffihDauda
Viewing all 9000 articles
Browse latest View live

Baada ya kukosekana kwa miaka 2, Mudathir amerejea Stars kwa kishindo

$
0
0

Kiungo wa Singida United Mudathir Yahya amecheza kwa kiwango cha juu kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Taifa Stars dhidi ya Benin uliomalizika kwa sare ya 1-1 huko nchini Benin.

Mudathir hakuitwa kwa muda mrefu kwenye kikosi cha Stars, mara ya mwisho kuitumikia timu ya Taifa ilikuwa November 2015 ambapo Stars ilifungwa 7-0 ugenini na Algeria kwenye mechi za awali kuwania kufuzu michuano ya kombe la Dunia hiyo ni baada ya kutoka sare ya 2-2 kwenye mechi ya kwanza iliyochezwa uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo (Algeria 7-0 Tanzania) Mudathir Yahya hakumaliza dakika 90 kufuatia kuoneshwa kadi nyekundu na mwamuzi

Imepita takribani miaka miwili tangu Mudathir alipocheza mechi ya mwisho kabla ya mchezo wa leo, kiwango chake katika mchezo wa leo dhidi ya Benin kilikuwa ni cha juu kutokana na kutimiza majukumu yake kwa asilimia nyingi.

Kwa sasa Mudathir anacheza kwa mkopo katika kikosi cha Singida United akitokea Azam, amekuwa na mchango mkubwa kwenye klabu yake huku akivaa kitambaa cha unahodha kutokana na nahodha mkuu wa timu hiyo (Nizar Khalfani) kukaa benchi kwenye mechi nyingi tangu kuanza kwa msimu huu.

Mudathir Yahya pamoja na Jonas Mkude walirejeshwa kwenye kikosi cha Stars kuziba nafasi ya kiungo Mzamiru Yassin na ‘kiraka’ Erasto Nyoni ambao kwa pamoja wanatumikia kadi nyekundu walizooneshwa kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Tanzania dhidi ya Malawi uliochezwa uwanja wa Uhuru.

Kwa upande wangu, Mudathir ndio mchezaji bora wa mchezo (man of the match) kati ya Benin dhidi ya Tanzania.

  • Katika mchezo wa leo, Benin ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kwa mkwaju wa penati bao likifungwa na nyota wa nchi hiyo Stephano Sessegnon dakika ya 30.
  • Elias Maguli akaisawazishia Stars dakika ya 50 kipindi cha pili akiunganisha krosi ya Shiza Kichuya.
  • Ni sare ya pili mfululizo kwa Stars baada ya kupata sare kama hiyo (Tanzania 1-1 Malawi) ikiwa ni mechi ya kwanza ya kirafiki ya kalenda ya FIFA Stars kucheza ugenini (tangu timu iwe chini ya Salum Mayanga) baada ya kucheza nyumbani mechi zake zilizopita.

Cr7 autangazia ulimwengu ujio wa Alana Martina

$
0
0

Wiki chache zilizopita Ctistiano Ronaldo katika mtandao wa Instagram alitangaza ujio wa mtoto wake wa nne ambaye tayari alishampatia jina kwamba akiazaliwa ataitwa Alan Martina.

Baasi usiku wa leo Cristiano Ronaldo akiwa jijini Atlaanta nchini Marekani ameitangazia dunia ujio wa Alana ambaye ni mtoto wa nne wa mwanasoka bora huyo wa dunia.

Alana ndio mtoto pekee wa Cristiano Ronaldo ambaye mama yake anafahamika kwanj watoto watatu waliotangulia wa mwanasoka huyo mama zao hawajulikani.

Ronaldo alikuwa na mwanae wa kwanza Cr7 Junior ambaye ndio waliongozana hadi hospitalu aliyokuwepo Georgina kwa ajili ya kumpokea ndugu yao huyo mpya katika familia yao.

Katika post yake Cristiano aliandika “Alana amezaliwa, tuna furaha sana kwani Georgina na Alana wote wako salama,tuna furaha mno” aliandika Cr7.

Xhaka na Modric nao wakata tiketi ya Urusi 2018

$
0
0

Timu zilizofuzu kuelekea kombe la dunia zinazidi kuongezeka baada ya usiku wa leo mataifa mawili ya Crotia na Switzrrland kukata tiketi kwa ajili ya michuano hiyo.

Walianza Switzerland ambao suluhu yao ya bila bila dhidi ya Northern Ireland iliwafanya kufuzu kuelekea kombe la dunia na hii ikiwa mara yao ya 4 mfululizo.

Switzerland wakiongozwa na kiungo wa Arsenal Granit Xhaka wanafuzu katika michuano hiyo kwani mchezo wa kwanza uliopigwa nchini N Ireland waliibuka kidedea kwa bao 1.

Crotia nao baada ya ushindi wa bao 4 kwa 1 vs Ugiriki siku chache zilizopita, leo wamepata suluhu ya bila kufungana iliyowapeleka michuano ya kombe la dunia mwakani

Crotia inakuwa timu ya 28 kufuzu kwa fainali za michuano hiyo na sasa kumebakia timh 4 tu kwa ajili ya kukamilisha idadi kamili ya wanaokwenda kushiriki kombe la dunia.

Mayanga ametaja sababu za kumchezesha Himid kama beki

$
0
0

Yameibuka maswali mengi baada ya kocha wa Stars Salum Mayanga kumchezesha Himid Mao katika nafasi ya ulinzi wa kulia wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya Benin tofauti na ilivyozoeleka kumuona nahodha huyo msaidizi akicheza katika eneo la kiungo wa ulinzi.

Kocha wa Stars Salum Mayanga ametoa sababu za kiufundi zilizopelekea kumpa Himid majukumu ya kucheza kama beki wa kulia wakati kwenye benchi kukiwa na mchezaji Boniface Maganga (Mbao FC) ambaye katika klabu yake anacheza katika nafasi ya ulinzi wa kulia lakini katika mchezo dhidi ya Rwanda kuwania kufuzu michuano ya CHAN uliochezwa CCM Kirumba Mwanza, Maganga aliingia kuchukua nafasi ya Kapombe aliyeumia.

“Baada ya kupata tatizo la Erasto Nyoni nililazimika kuangalia tufanye nini kwenye mechi hii tuliyocheza ugenini, nikaamua ni bora kuongeza viungo wawili lakini nikaweka tahadhali upande wetu wa kulia kwa kumuanzisha Himid kwa kuwa nilikuwa na idadi kubwa ya viungo lakini Himid anaimudu vizuri hiyo nafasi.”

“Kiufundi ni kitu cha kawaida, nimefanya hivyo kwa sababu nilikuwa na uhakika uwezo huo anao na pia kutokana na idadi kubwa ya viungo niliokuwa nao unaweza kuwapangua kulingana na mahitaji ya mechi na timu ikacheza salama.”

“Tumecheza ugenini dhidi ya timu yenye idadi kubwa ya wachezaji wa kimataifa, nililazimika kucheza na watu wenye uzoefu mkubwa ili kuwa salama zaidi katika kuzuia lakini pia katika uwezo wa kumiliki mpira na kushambulia.”

“Kiufundi nilifikia maamuzi hayo kwa faida ya timu na niliyaamini maamuzi yangu ndio maana nikafanya hivyo.”

Afya ya Kapombe yazua ‘kizaazaa’ Simba

$
0
0

Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Zacharia Hans Poppe ameibuka na kusema beki wao wa kulia Shomari Kapombe anatakiwa kuchagua kucheza au kutocheza lakini wao hawawezi kuendelea kumlipa mshahara wakati hafanyi kazi anayotakiwa kuifanya.

Poppe amekiri kwamba, walimsajili Kapombe kwa sababu walikuwa wanamhutaji lakini kama bado hajapona majeruhi yake inabidi wakae na kuzungumza kuona wanafanyaje kuhusu hilo.

Kuhusu tetesi za beki kutemwa katika kirisha dogo la usajili, Poppe amesema, hiyo itakuwa ni juu yake mwenyewe (Kapombe) kama amepona acheze kama hawezi basi.

“Hiyo itakuwa juu yake mwenyewe, kama amepona acheze kama hawezi basi, huwezi kumlipa mtu mshahara wakati hafanyi kazi inayotakiwa kufanywa.”

“Inategemea nay eye mwenyewe, kama anataka kucheza acheze, hataki ahame sio anakula hela bure. Majeruhi gani yasiyopona muda wote huo? Kama majeruhi basi akae pembeni hadi apone kwa sababu hii ni kazi ambayo mtu unahitaji kutumia mwili wako kama mwili hauwezi sasa utamlipa mshahara wa kazi gazi.”

“Vipimo vinaonesha amepona vizuri tu, lakini yeye anaweza kuwa anaogopa ataumia, sasa ni yeye mwenye aamue anacheza au hachezi.”

Kapombe alisajiliwa na Simba kabla ya kuanza kwa msimu huu baada ya kumaliza mkataba wake na Azam lakini ameshindwa kucheza mechi yoyote kutokana na kuuguza majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kwanza kuwania kucheza michuano ya CHAN dhidi ya Rwanda uliochezwa July 15, 2017 uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

July 18, 2017 www.shaffihdauda.co.tz ilizungumza na daktari mkuu wa Taifa Stars Richard Yomba ambaye alisema, Kapombe alihitaji uchunguzi kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili na hakuwa miongoni mwa wachezaji waliosafiri kwenda Rwanda kwa ajili ya mchezo wa marudiano July 23, 2017.

“Kapombe yupo kwenye matibabu ya awali ya saa 72, kutokana na hali yake ya sasa hatoweza kushiriki mazoezi na wenzake. Tukifika Dar tutamkabidhi kwa mwenyekiti wetu wa tiba ili aweze kupata uchunguzi zaidi MOI Muhimbili” – Richard Yomba, daktari wa timu ya taifa ‘Taifa Stars. (July 18, 2017)

Ibrahim MO au Domayo utakuwa usajili bab-kubwa Yanga si Mohamed Issa ‘Banka’

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

MABINGWA mara tatu mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara, timu ya Yanga inapaswa kurejea sokoni wakati huu wa usajili wa dirisha dogo na kusaini mchezaji mmoja wa kiwango cha juu ama wawili. Yanga inahitaji mfungaji mpya kuelekea michuano ya Caf mwezi Februari, 2018 na pengine kocha Mzambia George Lwandamina anaweza kusaini kiungo mmoja wa kati mwenye uzoefu kama atalazimika kufanya hivyo.

Kukosekana kwa washambuliaji wa kigeni Mrundi, Amis Tambwe ambaye hajacheza mchezo wowote msimu huu kutokana na majeraha ya goti, Mzimbabwe, Donald Ngoma ambaye alicheza michezo minne tu na kupata maumivu yanayosemekana kuwa ya nyama za  paja na namna wachezaji hao wanavyoendelea kupona napata wasiwasi mkubwa kama Yanga inaweza kufikia malengo bila nyongeza ya mfungaji.

Matheo Anthony ameshindwa kupenya katika kikosi, Emmanuel Martin si mfungaji na kuendelea kutegemea magoli ya Ibrahim Ajib na Obrey Chirwa pekee katika VPL na michuano ya Caf na ile ya FA ni jambo ambalo linaweza kuwayumbisha hasa nikichukulia mfano wa kile kilichowatokea msimu uliopita waliposhindwa kuiondoa timu ya kawaida Zanaco FC kutoka Zambia katika Caf Champions league.

Yanga ilishindwa kuwaondoa Wazambia na kufuzu kwa hatua ya makundi kwa sababu haikuwa na safu imara ya ushambuliaji kutokana na majeraha ambayo yalikuwa yakiwaandama Tambwe, Ngoma, Chirwa. Licha ya kufanikiwa kuhifadhi ubingwa wa ligi kuu kwa mara ya tatu mfululizo Mei, 2017 lakini bado michezo yao saba ya mwisho katika ligi ilikuwa migumu na hilo lilichangiwa na idadi ya chini ya magoli waliyokuwa wakifunga.

Stamili Mbonde

Lwandamina anaweza kutazama mbali zaidi na kusaini mfungaji wa kutoka nje ya nchi, lakini anaweza kumtazama mshambulizi wa Mtibwa Sugar FC, Stamili Mbonde ambaye si tu anaweza kucheza vizuri mbele ya lango la timu pinzani, bali ana uwezo wa kudhibiti mpira, kutoa pasi  na kutengeneza nafasi za kufunga.

Mbonde amefunga magoli mawili tu msimu huu, lakini anacheza katika kikosi ambacho hakitengenezi nafasi  nyingi za kufunga. Msimu mmoja uliopita Yanga ilimsaini, Paul Nonga kutoka Mwadui FC kwa kuamini mshambuliaji huyo angeweza kuwa msaidizi mzuri wa kina Tambwe na Ngoma lakini hakufanya vizuri.

Mbonde si Nonga kwa sababu kwanza ni kijana anayeanza kukomaa katika soka wakati Nonga ni mchezaji aliyepanga kustaafu soka ndani ya misimu miwili ijayo. Wanaweza kuongeza mfungaji toka ng’ambo ya nchi kama atapatikana lakini ‘mtu huyu’ mwenye mwili mkubwa anaweza kufanya vizuri sasa na baadae.

Frank Domayo

Kumrudisha Frank Domayo katika kikosi cha Yanga wakati huu ni bora zaidi kuliko kumsaini Mohamed Issa ‘Banka’ kutoka Mtibwa Sugar. Domayo anaweza kukosa nafasi katika timu ya kwanza pale Azam FC lakini ni mchezaji ambaye anaweza kutumia uzoefu wake kutengeneza muunganiko mzuri sambamba na Mcongoman, Papy Tshishimbi na Mzimbabwe, Thabani Kamusoko.

Sioni kitu kipya kutoka kwa Mohamed Issa ikiwa atasajiliwa kwa sababu Rafael Daud, Pius Buswita wamesajiliwa kwa ajili ya kuunganisha timu kutoka kati mwa uwanja hadi kwa washambuliaji. Hawajafanya vibaya hadi sasa na naona wakienda kujiamini zaidi na itakapotokea hivyo watakuwa
msaada mkubwa katika utengenezaji wa magoli.

Kama jaribio la kuwasaini Said Ndemla, Mohamed Ibrahim kutoka Simba litafanikiwa itakuwa jambo zuri sana kwa kocha Lwandamina lakini akishindwa kuwapata wachezesha timu hao anaweza kumtazama Domayo ambaye alifanya mambo makubwa wakati angali kinda katika timu hiyo. Sasa amepevuka, na Yanga inahitaji mchezaji bora mwenye uzoefu katika kiungo na si chipukizi.

Muandishi wa kwanza kugundua Neymar ataondoka Barcelona aibuka na jipya kuhusu Mbrazil huyo ikiwemo uhamisho kwenda Real Madrid

$
0
0

Hali haieleweki kwa mshambuliajiwa Kibrazil Neymar ndani ya PSG, zipo habari zinazodai kwamba Neymar anafurahia maisha yake PSG lakini zipo habari nyingi zinazosema Neymar hana furaha tangu aondoke Barcelona.

Marcelo Bechler alikuwa muandishi wa kwanza kufahamu kwamba Neymar anaondoka Barcelona na ni kati ya waandishi wanaoaminika sana katika masuala ya michezo nchini Brazil.

Bechler ameibuka na mpya ambapo anasema Neymar alipokutana na Luis Suarez na Gerrad Pique aliwaambia kwamba kati ya vitu vinavyomuumiza hivi sasa ni tukio la yeye kuondoka Barcelona.

Bechler amesisitiza kwamba Neymar hapati kile alichotegemea kukipata akiwa PSG kwani uwepo wa wachezaji mastar kama Edison Cavanni, Angel Di Maria unamfanya Neymar akose hashima kama aliyoitarajia.

Lakini pia muandishi huyo ameweka wazi kwamba ni kweli Neynar hana mahusiano mazuri na kocha mkuu wa PSG Unai Emery na hilo pia linamnyima sana Neymar ndani ya timu ya PSG.

Kuhusu tetesi za uhamisho wa Neymar kwenda Real Madrid Bechler amesema ni rahisi sana kwa Neymar kurudi Barcelona kuliko kwenda Real Madrid na kusisitiza kwamba uhamisho wake kwenda Madrid hauwezi tokea kirahisi.

United hawamtaki Bale wala Griezman bali huyu ndio nyota wanayejipanga kuvunja kibubu kwa ajili yake

$
0
0

Manchester United walikosa amani sana baada ya dili la uhamisho wa nyota wa Ufaransa Antoine Griezman ambalo walipambana kwa muda mrefu sana lakini ikashindikana dakika za mwisho.

Baada ya hapo United walimnunua Lukaku lakini ikatajwa kwamba bado wanatega kuhusu Griezman na pia wanaangalia kwa ukaribu maendeleo ya nyota wa Real Madrid Gareth Bale ambaye anaandwamwa na majeruhi.

Lakini sasa yameibuka mengine kwani United wanaonekana wako serious kwenye uhamisho wa nyota kinda wa Real Madrid ambaye siku za karibuni amekuwa gumzo kubwa katika ulimwengu wa soka Marco Asensio.

Inasemekana kwamba United wanataka kuvunja rekodi ya usajili tena klabuni hapo kwa kutoa kiasi cha £170m na mshahara wa £461,000 kwa ajili ya kumnunua Asensio katika dirisha lijalo la usajili.

Habari zaidi zinadai kwamba Asensio na Mourinho wameshawahi kufanya mazungumzo na kama dili hilo likifanikiwa baasi Asensio anaweza kusaini mkataba wa miaka 5 kuitumikia United.

Manchester United wanajipanga kutumka tena kiasi kikubwa zaidi cha pesa katika dirisha kubwa la usajili mwakani na sasa Asensio naye anaingia kwenye rada za Mashetani hao wekundu.


Kikosi bora cha Waafrika waliokosa kombe la dunua

$
0
0

Tayari nafasi 5 za kwenda kombe la dunia Urusi zimeshapatina huku Nigeria, Tunisia, Senegal, Misri na Morocco wakizichukua, wapo wachezaji hatari kwa sasa ambao wamekwama kwenda kombe la dunia.

1.Dennis Onyango. Onyango amekuwa na kiwango kizuri sana siku za karibuni na ndio maana haikuwa ajabu kwake kupewa tuzo ya mchezaji bora Afrika mapema mwaka huu.

2.Serge Aurier. Alishuhudia nafasi yao ya kufudhu kombe la dunia ikienda kwa Morocco, Aurier amekuwa katika kiwango kizuri kuanzia timu ya taifa  hadi Tottenham Hotspur.

3.Fouzi Ghoulam. Wengi wanamkumbuka katika mechi kati ya Napoli vs Chelsea alionesha kiwango kikubwa sana, lakini pamoja na kiwango bora anachoonesha Napoli ameshindwa kuisaidia Algeria kwenda kombe la dunua.

4.Eric Bailly. Mlinzi wa kati wa Manchester United, Bailly ni kipenzi cha mashabiki wengi wa United lakini naye kama ilivyo Aurier wameshindwa kuisaidia Ivory Coast kwenda kombe la dunia.

5.Joel Matip. Mlinzi kisiki wa Liverpool, hana maelewano mazuri sana na timu yake ya taifa na pia hii inaweza kuwa sababu kwa Matip kutoisaidia Cameroon kwenda kombe la dunia.

6.Jean Seri. Kiungo anayekipiga katika klabu ya OGC Nice ambako tayari vilabu vikubwa vinatajwa kumuwinda ikiwemo Barcelona lakini yeye naye na Ivory Coast watabaki nyumbani kombe la dunia likipigwa.

7.Franck Kassie. Orodha ya mastar kutoka Ivory Coast watakaokosa michuano ya kombe la dunia inazidi kukua, Kassie amekuwa akifanya vizuri nchini Italia tangu alipokuwa Atlanta na sasa Ac Millan

8.Naby Keita. Amekuwa gumzo kubwa katika msimu uliopita wa usajili, bado hakijaeleweka kuhusu uhamisho wake kutoka Rb Leizpg kwenda Liverpool lakimi Keita ameshindwa kuibeba Guinea kwenda kombe la dunia.

9.Yacine Brahime. Kati ya washambualiaji hatari wa Afrika walioko Ulaya ni Brahime, Kwa sasa Brahime anakipiga katika klabu ya Fc Porto lakini ubora wake haukutosha kuibeleka Algeria kombe la dunia.

10.PierreAubemayang. Kwa sasa ndio Muafrika anayecheka na nyavu zaidi barani Ulaya akiwa katika klabu ya Borussia Dortmund lakini hiyo haikusaidia kwake kuipeleka Gabon kombe la dunia.

11.Ryad Mahrez. Winga hatari zaodo katika bara la Afrika, alikiwepo katika kikosi kilichoipa Leicester ubingwa wa Uingereza lakini ameshindwa kuipa Alageria tiketi ya kwenda Urusi.

Sweden watafanikiwa kumstaafisha Buffon bila kombe la dunia machinjoni San Sirro?

$
0
0

Italy wapo katika hatari ya kukosa kucheza kombe la dunia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1958 ikiwa tu watashindaa kuifunga Sweden katika mchezo wa usiku wa leo utakaopigwa katika dimba la San Siro.

Kikosi cha Giampiero Ventura kilishindwa kupindua matokeo ya 1-0 dhidi ya Sweden pamoja na kucheza vizuri katika kipindi cha pili jijini Stockhlom na leo watakuwa wanahitaji ushindi mkubwa ili kuweza kukata tiketi ya kwenda Russia 2018.

Sweden wao wanajua wakipata goli jijini Milan itawabidi waitaliano wafunge magoli 3 ili waweze kufuzu.

Wasweden waliuanza mchezo wa kwanza kwa kasi katika dimba la Friends Arena, wakishangiliwa na umati wa mashabiki wao. Kikosi cha Janne Andersson kilipata nafasi nyingi katika kipindi cha kwanza, huku washambuliaji Ola Toivonen na Emil Forsberg walikaribia kufunga mara kadhaa. Dakika

Ya 60 wakapata goli la kuongoza kupitia Jakob Johansson.

Italy walijaribu kusawazisha mara kadhaa, na beki wa Manchester United Matteo Darmian alipiga shuti lilogonga mwamba.

Mchezo wa leo katika dimba la San Sirro unaweza kuwa mchezo wa mwisho wa Gianluigi Buffon kuitumikia Italia katika mechi za mashindano, ikiwa tu Azzuri watashindwa kufuzu. Golikipa wa Juventus ameshathibitisha kwamba ataastafu soka mwishoni mwa msimu, akiombea Italy wafuzu kwenda Russia 2018, na hayo yatakuwa mashindano yake ya 5 ya kombe la dunia kwake.

Mchezaji muhimu wa kikosi cha Ventura – Marco Veratti ataukosa mchezo huu. Kiungo huyo wa Paris Saint Germain amesimamishwa kutokana na kupata kadi ya njano katika mchezo uliopita kwa kumfanyia madhambi mshambuliaji wa Sweden Marcus Berg. Hivyo kiungo wa Napoli Lorenzo Insigne atachukua nafasi yake.

Kikosi cha Ventura kinahitaji magoli na huenda Simone Zaza akaongoza safu ya ushambuliaji. Mshambuliaji huyo wa Valencia aliukosa mchezo uliopita kutokana na majeruhi ya goti na mpaka sasa hakujakuwa na uhakika wa kucheza kwake.

Upande wa Sweden, Janne Andersson tayari amethibitisha kuwa fiti kwa mchezo na huenda kaanza. Mchezaji wa RB Leipzig Emil Forsberg anatarajiwa kuanza upande wa kulia na anategemewa kuwa mchezaji muhimu zaidi kwa timu yake dhidi ya Azzuri.

Wakati Sweden wakiisaka tiketi ya kwenda Russia 2018 wakiwa wameikosa michuano hiyo tangu 2006, Italy wao hawajawahi kuikosa michuano hii tangu 1958 – zaidi ya miaka 59 iliyopita.

Takwimu za Azzuri katika uwanja wa San Sirro zinaonyesha wamecheza mechi 42 bila kupoteza, wameshinda 31 na sare 11.

Hili linawapa nguvu vijana wa Ventura kuelekea mchezo huu utakaopigwa majira ya saa 4:45.

Kun Aguero apoteza fahamu wakati akiikabili Nigeria

$
0
0

Striker wa Manchester City alipoteza fahamh katika vyumba vya kubadilishia nguo wakati wa mapumziko ya mchezo wa kirafiki kati ya timu yake ya taifa ya Argetina zidi ya timu ya taifa ya Nigeria.

Aguero ambaye alifunga moja kati ya mabao mawili wakati timu yake ikifungea bao 4 kea 3 hapo ja a ilimlazimu kubebea ndani ya gari la wagonjwa kwa ajili ya kwenda hospitali kufanyiwa vipimo zaidi.

Wataalamu wa mambo wamehusisha kuzimia kwa Aguero na ajali ya gari aliyoipata siku chache zilizopita na kusema kwamba huenda mwanasoka huyo bado hajapona vizuri majeraha yake ya mbavu.

Manchester City wenyewe wamekanusha taarifa hiyo wakisisitiza kwamba hakuzimia bali alichoka tu huku shirikisho la soka nchini Argetina hadi sasa likishindwa kutoa taarifa yoyote kuhusu tukio hilo.

Tayari Aguero amepewa ruhusu kurudi nchini Uingereza kwa ajili ya matibabu zaidi na hakuna uhakika kama atakuwepo mwishoni mwa wiki hii ambapo Manchester City watashuka dimbani kuikabili Leicester City.

Aliyekuwa mume wa Irene Uwoya amefariki

$
0
0

Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Rwanda Hamad Ndikumana akifahamika na mashabiki wa Rwanda kwa jina maarufu la Kataut amefariki usiku wa kuamkia leo.

Ndikumana alikuwa kocha msaidizi wa Rayon Sports ya Rwanda, kocha mkuu wa timu hiyo Olivir Karekezi amethibitisha kifo cha Ndikumana.

“Ni kweli amefariki jana usiku kama saa sita” amesema Karekezi ambaye alikuwa akizungumza kwa shida kutokana na msiba huo.

Ndikumana alikuwa mume wa zamani wa msanii wa Bongo Movies nchini Irene Uwoya na walibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.

Katika kipindi cha uhai wake, Ndikumana alicheza soka la kulipwa kwa muda mrefu nchini Cyprus lakini pia aliwahi kucheza Tanzania katika kikosi cha Stand United mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa Gwakaya Olivier ambaye ni afisa habari wa Rayon Sports, amesema ugonjwa wa moyo unatajwa kuwa chanzo cha kifo cha Ndikumana.

“Alisikia maumivu makali kifuani akaomba soda ya baridi wakamletea na alipomaliza tu kunywa akatapika na akaishiwa pumzi ndipo akakata kauli”-amesema Olivier lakini akasisitiza bado wanasubiri uchunguzi zaidi wa kitabibu.

Pogba muhimu zaidi United: Majeraha yake yalivyowagharimu Lukaku & Mhikitaryan

$
0
0

Baada ya mwanzo mzuri katika msimu huu akifunga magoli 11 katika mechi 10 za kwanza, Romelu Lukaku alitegemewa kuendeleza moto wa ufungaji, hata hivyo tangu alipofunga goli lake la 7 katika Premier League mnamo September 30, Lukaku amepatwa na ukame mkubwa, akicheza mechi 7 mfululizo katika mashindano yote bila kufunga goli.

Wakati suala la ukame ni jambo la kawaida ambalo linawakuta washambuliaji wengi – Robin Van Persoe alicheza mechi 13 chini ya Sir Alex Ferguson bila kufunga – jambo linalompa wakati mgumu Jose Mourinho kuhusu hali ya uchezaji kiujumla ya Lukaku, hasa tangu Paul Pogba alipopata majeruhi.

Katika mchezo wa mwisho wa Manchester United katika EPL, dhidi ya Chelsea, Lukaku aligusa mpira mara 24 tu. Alishindwa kujihusisha zaidi na mchezo na alikuwa amepotezwa kabisa. Sio ya makosa yake yote, sapoti kutoka kwa viungo wake haikuwa inayojitosheleza, kwa kifupi haukuwa mchezo mzuri kwake.

Ukiangalia upande wa Bluu Alvaro Morata, aligusa mpira mara 51, hapa utaona mshambuliaji huyu Kibelgiji hakuwa na influence ya kutosha mchezo na hii imekuwa kawaida katika michezo mikubwa yote msimu huu.

Dhidi ya Liverpool, katika dimba la

Anfield, Lukaku aligusa mpira mara 22 tu, wakati Robert Firminho aligusa mpira mara 58 katika dakika 87 alizocheza. Tofauti kubwa baina ya washambuliaji hawa wa timu mbili – takwimu zinazotia mashaka kwa Lukaku.

Mourinho amekuwa akimtetea Lukaku kutokana na kiwango chake, lakini kuna mambo ya kuangalia kwanini kiwango kimeshuka. Hakuna shaka kutokuwepo kwa Pogba kumechangia sana kuporomoka kwa nguvu kwenye mashambulizi kiujumla ya timu.

Pogba ndio “nuklia” ya timu kwenye kuunganisha safu ya kiungo na ushambuliaji. Hakuna mchezaji kwenye timu ambaye anafikia unyumbulifu na ubunifu wa Pogba na ndio maana kutokuwepo kwake kumeiathiri saba timu.

Ander Herrera sasa ndio mbadala wake kwenye kiungo, lakini mchezaji huyo wa zamani wa Athletic Bilbao hana uwezo wa Pogba. Hana nguvu, wala ufundi, achilia mbali kimo chake. Kuna vingi vya kuongelea kuhusu mchezaji kiungo na sifa zake, viungo wengi wa kati waliofanikiwa ni wale wenye nguvu na ubunifu.

Tatizo lingine linaloiagharimu United, ni Henrikh Mikhitaryan. Ingawa amecheza kwenye timu kwa muda wote, kiwango chake kimeporomoka kwa kiasi kikubwa na anastahili kukaa benchi kwa sasa, pamoja na kwamba alianza ligi vizuri akitoa assists 5.

Wakati Manchester United ilipocheza na Stoke City ugenini katika sare 2-2, alipiga pasi 106, 93 kati ya hizo zilifika. Katika mchezo huo huo Mhikitaryan ambaye alicheza mbele ya Pogba alikamilisha pasi 48.

Dhidi ya Chelsea katika uwanja wa Stamford Bridge, Mhiki alikamilisha pasi 19 tu.

Hilo linakuonyesha wazi namna Pogba alivyo muhimu katika kuunganisha safu ya kiungo na ushambuliaji ya timu na kuzisababishia matatizo timu pinzani.

Ni kweli kuna utofauti wa ubora kati ya Chelsea ba Stoke, lakini hapa pointi inabaki kwenye ukweli kwamba Pogba anaweza kuumiliki mpira na pindi anapokuwa na mpira kunakuwa na urahidi wa wachezaji wengine kuhuusika zaidi na mchezo na kuleta matatizo kwenye lango la wapinzani. Mkhitaryan anaonekana amekosa muelekeo bila Pogba, jambo ambalo linapelekea Lukaku kukosa usaidizi mbele.

Lukaku jana ametimiza magoli 31 katika mechi 64 alizoitumikia nchi yake na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa nchi hiyo, lakini kiwango chake akiwa na Uzi mwekundu wa United imekuwa hakiridhishi.

Kifuatacho ni kipindi cha Christmas, kipindi muhimu ambacho mechi zinakuwa ngumu na nyingi. Habari nzuri kwa United Pogba atakuwa fiti kuanzia mchezo ujao dhid ya Newcastle, wakati atahitaji muda ili kurudi kwenye kasi yake – uwepo wake utaisadia kuirudisha United ambayo ilianza msimu huu kwa soka zuri na linalozalisja magoli mengi.

Historia, maisha na mafanikio ya soka la Ndikumana Afrika na Ulaya

$
0
0

Jumatano November 15, 2017 soka la Afrika Mashariki limepokea taarifa za simanzi kufuatia kifo cha mchezaji wa zamani Hamad Ndikumana ambaye hadi anafikwa na mauti alikuwa akihudumu kama kocha msaidizi wa klabu ya Rayon Sports ya Rwanda.

Kifo cha Ndikumana kinaelezwa kusababishwa na matatizo ya moyo lakini hadi sasa bado taarifa za kitabibu hazijatufikia ambazo zinafafanua kwa kina sababu iliyopelekea kifo cha nyota huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Rwanda.

Usichanganye Selemani Ndikumana na Hamad Ndikumana

Watu wengine wanachanganya kati ya Hamad Ndikumana na Selemani Ndikumana, Selemani ni mzaliwa wa Bujumbura Burundi na aliwahi kucheza soka kwenye klabu ya Simba kati ya mwaka 2006-2007, hawa ni watu wawili tofauti kabisa.

Sifa kubwa ya Ndikumana kwenye soka

Alisifika kwa uwezo wake mkubwa wa kufanya tackling, ndio ulikuwa utambulisho wake ukimuuliza mtu yeyote aliyemfahamu vyema Ndikumana lazima atakugusia kuhusu hilo.

Historia fupi ya masiha ya Hamad Ndikumana  

Hamad Ndikumana maarufu kwa jina la ‘Katouti’ alizaliwa October 5, 1978 (39) Kigali, Rwanda. Alikuwa na urefu wa mita 1.81 ambazo ni sawa na futi 5 na inchi 11, alikuwa na uwezo wa kucheza kama beki wa pembeni (kulia na kushoto).

Alianza kucheza soka la ushindani mwaka 1998 akiwa na klabu ya Rayon Sports FC  ya nyumbani kwao Rwanda ambapo alidumu kwa msimu mmoja tu (1998-99) kabla ya kutimkia  Ulaya kucheza soka la kulipwa.

Ndikumana kama Samatta tu

Mwaka 2000 alijiunga na klabu ya  K.F.C. Turnhout ya Ubelgiji taifa ambalo nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta ameanzia kucheza soka barani Ulaya akiwa na klabu ya KRC Genk.

Amecheza Ubelgiji kwa miaka mitano (2000-2005) akiwa na vilabu vine tofauti ambavyo ni K.F.C. Turnhout 2000-2001, RSC Anderlecht 2001-2002, KV Mechelen 2002-2003, KAA Ghent (Ubelgiji) 2003-2005.

Maisha mapya Cyprus

Mwaka 2006 Ndikumana aliondoka nchini Ubelgiji na kuelekea zake Cyprus ambako pia aliendelea kucheza soka hadi mwaka 2011, akiwa Cyprus alicheza katika vilabu sita kwa misimu sita tofauti (2006-2011).

Vilabu ambavyo amecheza Ndikumana akiwa Cyprus ni APOP Kinyras Peyias 2005-2006, Nea Salamis Famagusta FC 2006-2007, Αnorthosis Famagusta FC 2007-2008, AC Omonia 2008-2009, AEL Lemesou 2009-2010, APOP Kinyras Peyias 2011.

Atakumbukwa Rwanda na Afrika

Aliisaidia Rwanda kufuzu kucheza michuano ya mataifa ya Afrika mwaka 2004 ikiwa ni mara ya kwanza kwa The Amavubi kushiriki michuano hiyo katika historia ya soka la Rwanda kimataifa. Jina lake litaendelea kubaki kwenye vitabu vya soka la Rwanda na Afrika kutokana na kuwa miongoni mwa wachezaji walioshiriki AFCON 2014.

Alicheza Stand United ya Shinyanga

Alijiunga na Stand United msimu wa 2015-2016 lakini hakucheza kwa muda mrefu mechi za VPL na baadae akaondoka zake kufuatia migogoro iliyokuwa ikiiandama klabu hiyo changa kwenye ligi ya Tanzania bara.

Ndikumana alikuwa  shemeji yetu

July 2009 Ndikumana alifunga ndoa na mrembo Irene Uwoya ambaye ni staa wa Bongo movies, ndoa hiyo ilifungwa kwenye kanisa la Mt. Joseph Dar es Salaam Tanzania. Wawili hao walijaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume (Krish), baadaye ndoa yao ilivunjika na kila mmoja akaendelea na maisha yake.

FIFA waikataa rekodi ya Romelu Lukaku na kupunguza mabao yake

$
0
0

Mashabiki wa Ubelgiji na Manchester United jana walijawa na furaha baada ya kusikia kwamba mshambuliaji wao Romelu Lukaku amevunja rekodi ya ufungaji katika timu yao ya taifa.

Romelu Lukaku alitajwa kuvunja rekodi hiyo kwa kuwapita Bernard Voorhoof na Paul Van Himst ambao wana mabao 30 huku goli dhidi ya Japan likimfanya yeye kufikisha 31 idadi ambayo hata Lukaku mwenyewe alijinasibu kuifikia.

Lakini sasa shirikisho la soka duniani FIFA limeibuka na kutoitambua rekodi hiyo ya Romelu Lukaku kwa kusema kwamba moja kati ya michezo ambayo Lukaku alifunga hautambuliki na shirikisho hilo.

Mechi hiyo ilikuwa mwaka 2014 ambapo Ubelgiji walicheza dhidi ya timu ya taifa ya Luxembourg ambapo Ubelgiji waliibuka kidedea kwa mabao 5 huku Romelu Lukaku akifunga mabao 3 kati ya hayo 5.

Kinachowafanya FIFA kuundoa mchezo huo kwenye rekodi zao ni kitendo cha Ubelgiji kufanya sub 7 badala ya 6 katika mchezo huo suala ambalo lilikuwa kinyume na sheria katika mechi hiyo.

Hii sasa inamaanisha Lukaku ana mabao 28 tu na kama anahitaji kuwa mfungaji bora wa muda wote nchini Ubelgiji itambidi kufunga mabo matatu ili kufikisha 31.


Mahakama yaelezwa kiasi alichohongwa makamu wa raisi wa Blatter

$
0
0

Bado kesi ya kutumia vibaya ofisi za FIFA inaunguruma na hii leo mashahidi kadhaa walipanda kizimbani kutoa ushahidi wao juu ya masuala ya rushwa yanayotajwa kuligubika shirika hilo wakati wa utawala wa Sepp Blatter.

Kubwa lililojiri ni taarifa mpya kuhusu makamau wa zamani wa Sepp Blatter bwana Julio Grondona ambaye imetajwa mahakamani hapo kwamba alipewa kiasi cha $1m kwa ajili ya kuipigia kura Quatar.

Akiongea mahakamani hapo Julio Curzao ambaye ni mkurugenzi wa kampuni moja inayohusika na masuala ya masoko katika michezo alisema Grondona alimuambia kuhusu kiasi hicho.

Curzao anasema mwanzoni hakufahamu kiasi hicho cha pesa kinatokea katika nchi gani lakini baada ya Grondona kubadili mawazo na kusema anaipigia kura Quatar ndipo akafahamu pesa hiyo inakotoka.

Grondona anatajwa kuwa alikuwa akicontrol mchakato huo wa rushwa huku yeye na mjumbe mwingine aitwaye Teixeira ambaye naye aliipigia kura Quatar huku mjumbe mwingine toka Paraguay akikataa suala hilo na kuamua kuipigia kura Japan.

Grondona pia alijaribu kwenda hadi kwa maofisa wa FIFA katika nchini nyingine ikiwemo nfani ya Urusi kujaribu kuwashawishi kupiga kura kwa ajili ya Quatar kuandaa michuano hiyo mikubwa mwaka 2022.

Quatar wameshakana kwa mara kadhaa tuhuma hizi zinazoelekezwa juu yao huku wakisisitiza kwamba mchakato ulikuwa wa haki, Quatar ndio waandaaji wa michuano ya kombe la dunia 2022.

Sakata la Kakolanya kuidai Yanga lachukua sura mpya, Meneja, Mkwasa, wafunguka

$
0
0

Sakata la golikipa wa Yanga Beno Kakolanya kuidai klabu yake limezidi kuchukua sura mpya baada ya meneja wake Suleiman Haroub kukiri mteja wake kushindwa kulipwa pesa ya usajili na klabu yake kinyume na makubaliano yao ya kimkataba kati ya pande mbili.

Meneja huyo amesema kinachowasikitisha ni kwamba, hakuna juhudi za makusudi zinazooneshwa na Yanga ili mteja wake aweze kupata kile anachostahili.

“Kakolanya aliingia mkataba wa miaka miwili na Yanga ambapo kwa sasa anatumikia mwaka wa mwisho wa mkataba wake. Katika mkataba huo kulikuwa na makubaliano ya fedha ampayo nusu alichukuwa na nusu iliyobaki alitakiwa apate mwezi July mwaka huu wakati msimu mpya unaanza lakini kwa bahati mbaya mpaka leo hii hajapata”-Suleiman Haroub meneja wa Kakolanya.

“Tunapokumbushia suala hilo majibu yanakuwa “hali ni mbaya kifedha, kesho, keshokutwa” mpaka tumefikia leo. Kweli tunajua hali ya kiuchumi kwa klabu ya Yanga inawezekana ikawa si nzuri kwa mazingira yalivyo na majukumu ni makubwa lakini jitihada za kuonesha kweli wanania zimekuwa haziridhishi kwa sababu hawaoneshi dhamira ya kumpa kijana hela yake jambo hilo linatusikisha.”

Zilisikika tetesi kwamba huenda mkataba wa Kakolanya ukavunjwa lakini meneja Haroub amesema kwa upande wao hawana na hawawezi kufanya hivyo lakini kama itaonekana ni ngumu kwa golikipa huyo kulipwa hiyo itakuwa ni hatua nyingine.

“Taarifa za Yanga kuvunja mkataba na Kokolanya mimi sina na Beno hawezi kuvunja mkataba ndio maana nimesema tunafanya mazungumzo kwanza kuona anapata haki yake lakini pale itakapoonekana ni ngumu kupata haki yake sasa hiyo itakuwa ni hatua nyingine.”

Alipoulizwa kuhusu kiasi ambacho Kakolanya anachoidai Yanga, meneja alisema hilo linabaki kuwa siri kati ya Yanga na wao na asingependa kuweka wazi lakini alisema ni kiasi kidogo cha pesa ambacho anshangaa kwa nini wadaiwa wanashindwa kulipa.

“Hilo nisingependa kulizungumzia sana, lakini si hela nyingi sana ni hela kidogo tu ndio maana nasema sioni dhamira yao ya kumlipa, kwa sababu kama kuna watu wanasajiliwa kwa milioni 50 au 40 lakini mtu ambaye anadai kiasi kidogo wanashindwa kumlipa inaonekana hakuna dhamira au uhitaji wa huyo kijana au labda hana umuhimu katika timu. Sasa kama hana umuhimu basi ni vizuri wakaonesha namna nzuri ya kuachana nae au wamtimizie chake kuliko kumnyanyasa.”

Katibu mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa amekiri kuwa Kakolanya anaidai klabu hiyo, lakini ameongeza kuwa si Kakolanya pekeyake anaedai bali wapo wachezaji wengi wenye mada na klabu inaandaa utaratibu wa kuwalipa hivyo Kkolanya awe mvumilivu atapata haki yake.

“Ni kweli, lakini wengi bado hawajapata hela zao kwa hiyo anatakiwa kusubiri. Sio peke yake kuna wenzie pia bado hawajalipwa, sasa cha kulalamika ni kitu gani, waulize hao waliopata kidogokidogo wamepewa na nani, mimi ndio mtendaji mkuu ninaeijua bajeti, hao waliopata wametoa kwa nani? Mimi ndio mwandikaji barua hayo yote unayo sema ni maneno ya mtaani tu”-Charles Boniface Mkwasa, Katibu mkuu Yanga.

“Watu wote ambao wanatudai tunaandaa utaratibu wa kuwalipa wala hakuna tatizo lolote, wala sio mtu mmoja pekeake na hakuna sababu ya kumnyima, haki yake ataipata anatakiwa avute subira tu.”

Banka azikaribisha Simba, Yanga

$
0
0

Na Abubakar Khatib ‘Kisandu’, Zanzibar

Dirisha dogo la usajili kwa msimu wa 2017-18 limefunguliwa Jumatano ya November 15, 2017 kwa ajili ya vilabu vya madaraja mbalimbali kufanya maboresho ya vikosi vyao kwa kusajili au kupunguza wachezaji. Kumekuwa na tetesi za chini kwa chini zikimhusu kiungo chipuki wa Mtibwa Sugar Mohamed Issa ‘Banka’ akitajwa kuonwa na jicho la Yanga baada ya kufanya vyema kwenye klabu yake na mabingwa hao watetezi wa taji la VPL wanatajwa kutaka kusajili katika kipindi hiki.

Shaffidauda.co.tz imefanikiwa kumnasa Banka kwenye exclusive akiwa Zenj na timu ya taifa ya Zanzibar Heroes ambapo kiungo huyo amesema, hadi sasa hakuna klabu yoyote iliyomfata kufanya nae mazungumzo kuhusu kumsajili lakini amesema atakuwa tayari kujiunga na timu yoyote itakayohitaji huduma yake.

“Hadi sasa hivi sijatafutwa na mtu yeyote, mimi bado ni mchezaji halali wa Mtibwa. Timu yoyote ambayo itanihitaji nikafanye kazi kwao nitakuwa tayari”-Mohamed Issa ‘Banka’.

Banka amekuwa mchezaji wa pili kutoka ligi kuu Tanzania bara kujiunga na kikosi cha Zanzibar Heroes akitanguliwa na mshambuliaji wa Majimaji Suleiman Kassim ‘Seleembe’.

Kiungo huyo amesema atapigana ili awe miongoni mwa wachezaji watakaoiwakilisha Zanzibar kwenye michuano ya kombe la Chalenji itakayofanyika nchini Kenya kuanzia mwezi December mwaka huu.

“Hii ni mara yangu ya nne kuitwa Zanzibar Heroes lakini miaka yote huwa nachujwa sibahatiki kusafiri na timu kwenda kwenye mashindano, lakini mwaka huu nataka kupigana ili nipate nafasi kwa sababu kila ninaemuangalia kwenye timu ana uwezo mkubwa.

Sababu kubwa ya Banka kujiunga mapema na Zanzibar Heroes ni kutokana na kadi tatu za njano alizooneshwa kwenye michezo mitatu mfululizo iliyopita ya VPL wakati akiitimukia timu yake ya Mtibwa Sugar hivyo mchezo wao ujao wa Jumapili Nov 19 dhidi ya Kagera Sugar hatokuwa sehemu ya kikosi cha Mtibwa.

Wachezaji ambao wanatokea ligi kuu Tanzania bara ambao bado hawajajumuika na Zanzibar Heroes ni Walinzi Abdallah Haji ‘Ninja’ na Haji Mwinyi Ngwali (Yanga), Adeyum Saleh ‘Machupa’ (Kagera Sugar), Abdulla Kheir ‘Sebo’ (Azam), Viungo Mudathir Yahya (Singida United), pamoja na washambuliaji Kassim Suleiman (Prisons), Matheo Antony (Yanga) na Seif Rashid Abdallah ‘Karihe’ (Lipuli).

Beki wa Prisons aikana Simba

$
0
0

Tetesi kwamba klabu ya Simba inahitaji huduma ya beki wa pembeni wa Tanzania Prisons Salum Kimenya zimemfikia mwenyewe (Kimenya) ambaye kwa sasa yupo kwenye maandalizi makali kuelekea game inayozikutanisha klabu yake ya sasa (Tanzania Prisons) na wanaotajwa kuwa mabosi wake watarajiwa.

Majibu ya Kimenya kuhusu kutajwa kujiunga na Simba yanapishana na taarifa zilizopo ambapo inaelezwa mambo yameshakamilika kinachosubiriwa ni muda tu ili beki huyo kuhamia Msimbazi.

“Sijui chochote, hata mimi nasikia tu hizo habari. Yote ni mipango ya Mungu lakini sijui chochote”, amesema Kimenya ambaye amekuwa katika kiwango kizuri katika misimu ya hivi karibuni.

Ikitokea Simba wakamfuata kwa dhamira ya kutaka kumsajili, Kimenya alijibu hivi: “Hilo siwezi kulizungumzia mpaka nifuatwe”.

Baada ya kuulizwa maswali mengi kuhusiana na tetesi za usajili wake kwenda Simba, Kimenya alisema: Kwa sasa najiandaa kwa game ya Simba sitaki kuongelea sana masuala haya.”

Kabla ya kuanza kwa msimu huu, beki huyo wa kikosi cha maaskari wa jeshi  la Magereza alihusishwa kujiunga na klabu ya Azam lakini dili hilo halikufanikiwa dakika za mwisho kabisa.

Simba ipo mkoani Mbeya ikisubiri kucheza dhidi ya Tanzania Prisons siku ya Jumamosi Nov 18, 2017 kwenye uwanja wa Sokoine, kama Kimenya akiwa fit atakuwa kwenye kikosi cha Prison kitakachoikabili Simba huku ‘mnyama’ akiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza 2-1 katika mechi ya msimu uliopita kwenye uwanja huo.

Ugomvi wa hadharani wa Ramos vs Ronaldo, nani mwamba Bernabeu?

$
0
0

Kumekuwepo na hali ya kutokubaliana na kutoa zinazotoa kutoelewana kwa wachezaji wawili wakubwa wa Real Madrid: Cristiano Ronaldo na Sergio Ramos.

Huku matokeo ya uwanjani yakiwa ya kusuasua kwa ‘Los Merengues’ mwanzoni mwa msimu, wote wawili wamekuwa wakiulizwa nini kilichosababisha hali ya kutokuelewana, na imeripotiwa kwamba Nahodha wa Ureno ndio aliyeanza kutoa kauli zilizozalisha vita hiyo baridi waliyonayo.

Kufuatia matokeo ya kipigo dhidi ya Tottenham katika Champions League, Ronaldo alitoa kauli ambayo iliyoonyesha hakupendezwa na suala la kuuzwa kwa baadhi ya wachezaji muhimu wenye uzoefu katika timu hiyo, wachezaji kama James Rodriguez, Pepe, na Alvaro Morata.

Wakati maoni ya Ronaldo yakionekana ya msingi na yaliyopokewa na mashabiki na wachambuzi, Ramos alionekana wazi kukerwa na gazeti la El Chiringuito limeripoti nahodha huyo wa Madrid alikerwa sana na maneno ya Ronaldo.

Ramos ameeleza kwamba Madrid ilishinda mataji mawili mwanzoni mwa msimu bila uwepo wa hao wachezaji wanaolalamikiwa kuuzwa ambao CR7 anasema wamechangia kiwango chao kuporomoka, na baada ya hapo maelewano baina ya wawili hawa yakaendelea kupoteza muelekeo mpaka sasa.

Baada ya kipindi cha kiangazi kumetokea mabadiliko katika chumba cha kubadilishia nguo hasa baada ya wachezaji waliondoka kuwa ni marafiki wa Ronaldo. Wakiwemo wareno wenzie, Pepe na Fabio Coentrao na rafiki yake mwingine James Rodriguez.

Upande wa Ramos yeye amezidi kuwa na nguvu, hasa baada ya sera ya Zidane ya kuongeza vijana kikosi cha kwanza: wachezaji wengine kama Nacho, Dani Carvajal, Marco Asensio, Isco na Dani Ceballos – hawa wote ni wafuasi wa Ramos na hawawezi kusema chochote dhidi yake – kitu ambacho ni tofauti kwa Ronaldo.

Kingine kilichoongeza chumvi kwenye kidonda – ni maoni ya Ramos ya hivi karibuni – kwanza alipoanza kumzungumzia Neymar na suala la kuhamia Madrid, jambo ambalo kwa upande wa Ronaldo halikwenda vizuri, na kingine ni pale alipoulizwa kuhusu hatma ya uwepo wa Ronaldo Madrid.

“Cristiano anaondoka? Muulizeni mwenyewe, sifahamu lolote kuhusu yeye.” Alijibu Ramos baada ya sare ya Spain vs Russia – kauli ambayo inaelezww imezidi kuchangia ugomvi wake dhidi ya Ronaldo kuelekea mchezo muhimu wa wikiendi hii dhidi mahasimu wao Atletico Madrid.

Viewing all 9000 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>